Jeshi la Israel Limelipua makao makuu ya Hezbollah Beirut wakati Netanyahu anaendelea kutoa speech umoja wa mataifa

Jeshi lipo lakini halijihusishi na vita. Israel anapigana na kikundi kidogo tu kama vile alshabab ya Somalia au bokoharam ya Nigeria.

Wafarisayo wa yombo sasa..... Israel taifa kubwa..... IDF inawashambulia vibaya.....

Kiuhalisia Israel na nyenzo na vyombo vyake vyote ni failure. Huwezi kuhangaika na wanamgambo tu miaka kibao huku ukiua wanawake na watoto wasio na hatia.
 
Baada ya Israel kuusambalatisha mji wa Gaza na sasa anaonekana kuanza kuushambulia Lebanon huku Iran akiwa mtazamani wa haya yote yanayotokea je Iran anaogopa naogopa uingilia kati kuwaokoa maswahiba wake ambao kila siku amekuwa anajinasibu kuwasaidia lakini kipindi hiki naona amekuwa mtazamani....akiacha wenzie Lebanon na Gaza wakiambulia kipigo kibaya....je huu ndo ni mwisho wa ushawishi wa Iran kwa maswahiba zak mashariki ya kati?
 
Hezbollah naona ni wepesi mno kuliko HAMAS
Hezbollah sio wepesi, wako vizuri sana kuliko Hamas na wanawazidi mbali. Tofauti zao ni kubwa.

Lebanon ni nchi ina eneo kubwa kuliko Gaza, Hezbollah wana eneo wako huru na wanatishia uwepo wa jeshi la serikali. Raia wa Gaza wanakubaliana na Hamas hata kama si direct ila raia wa Lebanon wengi hawaipendi Hezbollah na siri zao ni wepesi kuzitoa.
Gaza ni kama Kariakoo kubwa wamebanana hata ukitaka kuua gaidi mmoja lazima raia wengine wafe, ni ama uwahamishe kwanza au upunguze madhara kwao. Jambo lililofanya Israel iende taratibu sana. Ila kwa Hezbollah makombora mengi tu yalikuwa porini na sehemu zisizo na raia wengi. Machache ndio yako kwenye basements na majumba.

Hamas silaha zote waliweka hospitalini, shuleni, msikitini. Ikawa vigumu kuzisambaratisha bila kelele za kimataifa.

Hezbollah iliwahi pigana na Israel ikaachiwa ikajitapa ina uwezo, Israel isingekuja kuipiga kwa kubembeleza kama ilivyofanya kwa Hamas. Israel imetumia siku 10 kufanya matukio mfurulizo kwa Hezbollah na yote ni magumu, wakati kwa Hamas ilikuwa inaonekana ni kama Israel ina udhaifu.

Israel ilikwepa lawama tu ila Hamas wangepigwa kwa haraka na raia wengi zaidi wakafa. Kwa vile Hamas hawana nguvu tena, serious threat ni Hezb na Israel inatumia approach ya kuondoa viongozi waandamizi kwa pagers na mashambulizi, kisha sasa kuondoa viongozi wakuu. Wapiganaji wa Hezbollah watashuka morali na hawatakuwa na command structure, uongozi wenye uzoefu na ujasiri, wala mbinu. Watapigana desperate bila mpangilio na au wataacha kabisa kupigana. Approach hii isingetumika kwa Hamas.

Hata hivyo Hamas wanawazidi Hezbollah kitu kimoja, usiri.
 

Kimsboy: Unauliza swali hilo Kimsboy...Unanipa mshangao mkubwa maana wewe ndio umekuwa Mtaalamu wa Middle East....Unashindwa kweli kujua Israel haipigani na serikali ya Lebanon, bali na Hezbollah ndani ya Lebanon! Hezbolah imekuwa na nguvu nchini Lebanon, ina jeshi lake na inaiendesha serikali ya Lebanon! Hiki ni kikundi TU
cha Washia ambao wana support ya Iran.

Mkuu swali lako limenishangaza sana! Jaribu kuwa unafanya utafiti kidogo kabla hujaandika, hata kama una mapenzi na Iran/Hamas/ Hezbolah....wakati mwingine weka pembeni ushabiki. Itakusaidia sana.
 
Makao makuu ya Hezbollah mjini Beirut yamechakazwa vibaya kwa ndege za kivita za Israel na kuharibu eneo lote kabisa, shambulio Hilo lilimlenga kiongozi wa Hezbollah Hassan nasrallah ambaye haijulikani alipo mpaka sasa


View attachment 3108670
Rumors are swirling "she's gone" to be one of the 72 virgins
Huyo hapo in smoke
 
Kwa nchi hizi kalunguyeye,ni muhimu kuheshimu nchi zilizoendelea na kuziogopa kama tuogopavyo kuchungilia tulikoyokea
Mana olewake amchungiliaye mamaye aliyekaa vibaya
 
Bro acha kukariri hadithi za kwenu. Yaan unajidanganya jews wanaogopa kifo uko serious?
 
Pumbafu! Netanyau alishatangaza raia wasepe ili wamtoe nyoka hapo pangoni zen badae watarudishwa kwaio wacha moto uwake
 
Mtaalam , embu wafundishe hao Israel namna sahihi ya kupambana na hayo magaidi.

Wapo hapa wanakusoma.
 
Myahudi bana level nyingine!! Ona jinsi anavyo locate hayo makombora ambayo Hezbollah wameyaficha kwanye ma bunkers ya nyumba za raia

View: https://x.com/JewishWarrior13/status/1839782424131318224
 
Ila mashariki ya kati imegawanywa vipande vipande..divide and rule.....Dola Ile wangeungana hakuna wa kuwagusa
 
Kwani siku walipoishambulia Israel walichagua cha kupiga?

Kama walivyofagia ndivyo walivyofagiliwa. Na bado.

Nyie mabwege sana. Mlishangilia sana ile October mwaka jana. Tuliwaambia kuichokoza Israel kisasi chake ni kikali. Mkasema hana lolote na kuweka hesabu zenu za nguvu ya kijeshi hapa. Leo kiko wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…