Jifunze Jinsi ya kufanya Manunuzi kwa Ebay mtandaoni

Jifunze Jinsi ya kufanya Manunuzi kwa Ebay mtandaoni

Nilijipeleka mwenyewe ila kufika pale walidai mzigo bado haujafika niende kuchukua J4 baada ya sikukuu.
Niliwauliza mbona tracking inaonyesha umefika tokea jana yake wakajibu kwamba bado upo GPO utafika mchana.
Sikuwa na jinsi nikaondoka ila baada ya nusu saa hivi wakani pigia simu nikachukue mzigo.
Yaonyesha ulikuwapo ila sijaelewa sababu za kuchelewesha kuutoa.
Kuhusu ushuru hawakunidai
Sometimes wanakuambia hivyo wakucheki ukoje. Na wewe ukiwalima na kadi ya "mbona tracking number inasema umefika?/nna tracking number na inaonesha mzigo uko bongo tayari" wanajua unajua unachokifanya. Pale dawa ni kuwa na "besti"/"msela" ambaye atakuwa anasimamia show zako.
 
Naomba nitoe mrejesho...

Niliagiza mzigo tarehe 28/03 na ukafika tarehe 11/04 nikapigiwa simu kuwa mzigo umefika.

Sikuweka Sanduku la Posta, niliandika namba ya simu na mtaa, so mzigo ukaletwa kwenye posta iliyo karibu nami.
 
Ahsanteni sana wakuu kwa mirejesho tarajali.. Nna mpango wa kuagiza mobile house from China. Maombi yenu muhimu 😉
 
Ahsanteni sana wakuu kwa mirejesho tarajali.. Nna mpango wa kuagiza mobile house from China. Maombi yenu muhimu 😉
Angalia kama Kuna seller wa Hong Kong ana hiyo bidhaa uagize toka kwake maana parcel toka China zinachelewa mnò kufika.
Kuna mzigo nimemuagiza kule karibu mwezi sasa sijautia mikononi
 
17track.PNG
everything ok
 
Naomba niulize je Mimi nika weka sanduku la posta ruvuma mzigo uta fika kwasaba najuwa ina shushwa dar je ? Huku kwetu utafikeje plz msaada
 
Naomba niulize je Mimi nika weka sanduku la posta ruvuma mzigo uta fika kwasaba najuwa ina shushwa dar je ? Huku kwetu utafikeje plz msaada
Mzigo utakufikia mahala opote Tanzania.
Kinachotakiwa ni taarifa sahihi katika anwani husika, ikiwa ni pamoja na
- Mkoa
- Wilaya
- S.L.P
- Namba ya simu
 
Mimi sina sanduku la posta je kuna ulazima wa kua nalo na je kama sina nifanyaje wakuu
 
Mimi sina sanduku la posta je kuna ulazima wa kua nalo na je kama sina nifanyaje wakuu
Kuna njia mbili za usafirishaji

Njia ya Kwanza: Inakuhitaji lazima uwe na sanduku la posta
Nja ya Pili: Utatumia physical address yako na namba ya simu tu

Ni vyema kufanya mawasiliano na muuzaji ili ujue ni njia ipi ya usafirishaji itakayotumika.

"Mimi sina sanduku la posta je kuna ulazima wa kua nalo?" - Sio lazama, Ila ni muhimu iwapo unafanya manunuzi mara kwamara mtandaoni.
 
Habari wana board!!

Nahitaji ufafanuzi wa haraka kwa aliyewahi kuagiza bidhaa toka Made in China (e commerce platform)

1. Wengi wao njia zao za malipo ni kupitia western union au T/T, je wana aminika kwa kiasi gani!?

2. Ntatambuaje kama ninayefanya naye biashara sio tapeli!?

3. Nili request latest price for certain product, cha ajabu napata email nyingi sana toka kwa wauzaji ambao siku request toka kwao!??

4. Mwisho kabisa, mbona bidhaa zao nyingi, hasa laptop zinakuwa na bei ndogo.

Kubwa zaidi, ni namna ya kutambua kama muuzaji ni tapeli au lah!!

Msaada please
 
Ukiacha Aliexpress, ebay, Amazon, Gearbest, Alibaba, ni online gani zingine tunaweza kununua online?
 
Habari wana board!!

Nahitaji ufafanuzi wa haraka kwa aliyewahi kuagiza bidhaa toka Made in China (e commerce platform)

1. Wengi wao njia zao za malipo ni kupitia western union au T/T, je wana aminika kwa kiasi gani!?

2. Ntatambuaje kama ninayefanya naye biashara sio tapeli!?

3. Nili request latest price for certain product, cha ajabu napata email nyingi sana toka kwa wauzaji ambao siku request toka kwao!??

4. Mwisho kabisa, mbona bidhaa zao nyingi, hasa laptop zinakuwa na bei ndogo.

Kubwa zaidi, ni namna ya kutambua kama muuzaji ni tapeli au lah!!

Msaada please
Binafsi sina uzoefu nao.
 
Samahanini ndugu zangu wa jf niko nje ya topic:, nauliza kama kuna mtu anajua chochote kuhusu kampuni inayoitwa teletrade wananishauri niwekeze kwenye kampuni yao hiyo na mfano nikiweka laki napata 30% ya iyo pesa wanadai wapo uswizi msaada tafadhali kama yupo mdau aliyebahatika kufanya investiment nao
 
Samahanini ndugu zangu wa jf niko nje ya topic:, nauliza kama kuna mtu anajua chochote kuhusu kampuni inayoitwa teletrade wananishauri niwekeze kwenye kampuni yao hiyo na mfano nikiweka laki napata 30% ya iyo pesa wanadai wapo uswizi msaada tafadhali kama yupo mdau aliyebahatika kufanya investiment nao
Google them, son!
 
Back
Top Bottom