Jinsi nilivyolazwa nje na wachawi mkoani Njombe

Jinsi nilivyolazwa nje na wachawi mkoani Njombe

Mkuu hii hali ipo Sana huku nyanda za juu kusini,miaka kadhaa nyuma,kipindi Cha Jiwe Kuna DC aliletwa Moja ya wilaya maarufu nyanda hizi,ila kilichomponza ni mdomo,na kusema mbovu Kwa wazee wa mji,siunakumbuka viherehere wa Jiwe kipindi kile??Siku ya siku kajichanganya kasema yeye ni raisi wa wilaya na haogopi mtu,wazee wakaona usitutanie,Asubuhi yake Dc anaamka na boksa makaburini.Na tangu kipindi hicho jamaa Kawa mpole balaa.
 
Shalom wapendwa,

Leo nimekumbuka kisa hiki, kilichonitokea mwenyewe nikiwa katika harakati Mkoa wa Njombe. Narudia tena hii sio stori ya kufikirika imenitokea mwenyewe.

Uchawi hauna faida yoyote ni ujinga uliokomaa, ni utumwa. Walio wachawi wanamani kutoka ila there is no way out there. Ninamiliki maduka ya dawa za binadamu yaliyopo maeneo ya vijijini huko, kazi yangu hua ni kuzunguka na kutafuta watu wa kuuza tu na kufunga mahesabu mwisho wa mwezi.

Siku Moja kuna dada wa ADDO aliyekuwa akiuza moja kati ya maduka alipata dharura na kwakua nilikuwa na nafasi nilimruhusu aende nami nikaenda kumpokea kuuza dawa Ili clients wasikose huduma mpaka atakaporejea. Sasa hapo ndipo tatizo lilipoanzia.

Hiyo siku nimeamka vizuri kabisa nikashinda vema jioni imefika nikafunga hesabu na kulikua na pesa kwenye draw nilizibeba na kwenda nazo nyumbani kwa sababu za kiusalama, nikaacha kiasi kadhaa pia kwenye draw. Baada ya kufikia nyumbani nikaweka pesa vizuri nikawasha data niperuzi kidogo Kisha nikalala.

Naamka asubuhi nimelala nje😂😂😂 kwenye shimo Moja lilikua jirani na nyumba. Kitu kilichonishangaza nililala na boksa nikaamka nje nikiwa na nguo zangu nilizovaa jana😨

Kitendo cha kutaka kurudi ndani nakuta mlango umefungwa kwa ndani, nikawa najiuliza nilitokea wapi? Nikajaribu kupush mlango ukafunguka kuingia ndani nakuta panya sita kitandani wametulia wananiangalia tu😂😂😂 nikarusha kiatu wakapanda darini na kupotea ghafla kukawa kimya.

Impact za tukio lile, pesa nilizorudi nazo jana hakukua na hata kumi iliyokuepo😬 (zilipotea)

Sikuweza kukaa tena kule, nikafunga duka mpaka yule dada aliporudi kusongesa gurudumu. Kwa Sasa nikienda huwa silali kabisa hata iwe late kiasi gani nitarudi mjini.

Kama hujapita Njombe hujaona uchawi bado.
Mm nimekaa Njombe miaka 10 ,sijawahi sikia huo mchezo.Ila Nasikia tu ,kuwa wanafanyiziana wao kwa wao sio wagen.Au na ww ni mjinga au mbena?
 
Mm nimekaa Njombe miaka 10 ,sijawahi sikia huo mchezo.Ila Nasikia tu ,kuwa wanafanyiziana wao kwa wao sio wagen.Au na ww ni mjinga au mbena?
Sio mkinga Wala mbena
 
Isije kuwa ni vijiji vya Mahaha,Shishani,Kabila n.k vya Wilayani Magu, Mwanza. Mwaka fulani pale kijijini wananchi waliua fisi kadhaa waliokuwa wanafanya matuko kwa wananchi na mifugo, cha ajabu fisi hao walikuwa wamevaa hirizi.

Sasa kuna watu ukiwaambia mambo haya wanakataa. Wamezaliwa hapa hapa Africa na wanavijua vituko vya Afrika, ila wanajifanya wamezaliwa na kukulia Australia, Canada au sijui wapi mbele huko. Mimi nasema hivi: kama hawaamini kama hayo mambo yapo, waende hapo kijijini Mahaha, wilaya ya Magu, mkoa wa Mwanza kisha wawaambie wakazi wa hapo kuwa wao hawaamini uwepo wa uchawi na wawatake wawathibitishie, majibu watayapata.
Uchawi upo mazee
 
First lady wa awamu ya .....
Kijijini kwetu hukoo Lindi kaenda msibani na mabodigadi wake Nini na Nini mke wa presidaa bwana analala ndaniii,kitandani nyie nyie nyieeee....[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]wamwera nyokooo sanaaaa....asubuhi kajikuta njee Mabodigadi wako Mlangoni wanalinda empty room...
Ilikua balaaaa kiranga komoo!!!
Unlock hio code
 
Back
Top Bottom