Jirani anajenga Msingi wa ukuta katikati ya jiwe la mpaka la manispaa, Sheria ya Ardhi inaruhusu hii?

Jirani anajenga Msingi wa ukuta katikati ya jiwe la mpaka la manispaa, Sheria ya Ardhi inaruhusu hii?

Wewe Una bahati hujamegewa pakubwa.

Mtaani kwetu kuna Mswahili kafanya hivi na ameweka kigeti kwenye ukuta wa nyuma.
JamiiForums-2049917807_189x252~2.jpg
 
Kapata mseleleko hana gharama tena
Tena hapo amwambie aweke msingi wa mawe sio tofari. Amshauri na jirani wa upande wa pili nae aweke ukuta ili yeye aje amalizie kuzoba nyuma na mbele tu
 
Huku nimeomba ushauri kwa kuuliza kwanza kwa wataalamu na wazoefu.

Kabla sijaenda kusema kokote ama kufungua kesi?

Toa jibu ama ushauri kama yupo sahihi ama anakosea
Kweli hata zile mita mbili kila upande wa kiwanja kuachwa hajaacha
 
Hapana.Kuacha nafasi kati ya nyumba ya kiwanja kimoja na kiwanja kingine ni lazima kisheria za ujenzi.Na kuna vipimo vyake.Kila mmoja ataacha mita moja na nusu kutoka katika jiwe/bikoni yake.Akileta ubishi atabanwa kwa kuombwa yafuatayo kisheria za mipangomiji/halmashauri;-
1-Uhalali wa umiliki eneo(nyaraka halali),
2-kibali cha ujenzi kinachoenenda na muda(expire date)
3-Na kama amehamia/nyumba ipo,ataombwa leseni/kibali/ruhusa ya kisheria ya kuishi hapo,
4-Hana hivyo vitu;a,atapigwa faini kimojakimoja-b,atasimamishwa ujenzi-c,atavunja ukuta kwa muda atakaopewa kwa gharama zake-d,atapewa onyo kali aache ungedere.[emoji120][emoji120][emoji120][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hiyo Sheria utekelezaji wake unahitaji busara kama si kuitazama vizuri, maana Kuna baadhi ya maeneo, hivyo vichochoro vinavyozaliwa baada ya watu kujenga kuta zao, huwavutia sana vibaka na wavuta bangi, mwisho wa siku mtajuta kuwatengenezea ofisi.
 
Habari wadau,

Nina kiwanja changu kimepimwa na manispaa ya Ubungo.

Jirani yangu naepakana nae ameamua kujenga msingi wa ukuta wake kati kati ya jiwe linalotutenganisha..

Je, yupo sahihi? Sheria ya Ardhi inaruhusu hili kutokea?

Wataalamu na wazoefu naombeni ushauri

Tazama picha. Kiwanja changu ni upande wa kushoto na cha jirani ni upande wa kulia wa beacon

Beacon iliyowekwa na manispaa ndiyo hiyo pembeni ya mti (mti ameuweka ndani ya upande wa kiwanja changu) na hayo nyuma ndio matofali ya jirani

View attachment 2371564
Hairuhusiwi
 
Huku nimeomba ushauri kwa kuuliza kwanza kwa wataalamu na wazoefu.

Kabla sijaenda kusema kokote ama kufungua kesi?

Toa jibu ama ushauri kama yupo sahihi ama anakosea
...Sasa tukupe Ushauri Gani Hapo. Wee Sema ulitaka TU kutujulisha kwamba una kiwanja!
Nikuulize wewe swali la kawaida Hapo la kutumia TU Akili... Jirani akamua kujenga Hapo, Maji ya Mvua ya Bati lake yataangukia Wapi???[emoji35]
 
Yes amemsaidia upande mmoja..........Kuna wengine wana bahati anasaidiwa pande tatu zote yeye anabakiza kufunga mbele tu na kuweka geti....Ukinunua viwanja vya kupimwa ndio advantages zake hizo.
....Akiamua Kujenga Fensi....akiamua ndio atakapojenga nyumba yake ya Kuishi, je??
 
Amekengeuka.Kuna umbali maalum/kipimo katika mita alipaswa kuingia kwa upande wake ndiyo ajenge.Hiyo ni ili aache nafasi kati yake na jirani.Pia aache uchochoro/nafasi kwa ajili ya huduma za jamii kama maji,umeme na hata njia ya kupita.Mumuwahi kabla hajaziba kabisa eneo kwa kuwapa taarifa viongozi wa mtaa au Mipangomiji/Ardhi wilayani waje wampe elimu.
Huo ndio ushauri! Hapo juu, jamaa hawajui chochote, badala ya kupiga kimya, wao wameamua kujivua nguo!
 
Hapana.Kuacha nafasi kati ya nyumba ya kiwanja kimoja na kiwanja kingine ni lazima kisheria za ujenzi.Na kuna vipimo vyake.Kila mmoja ataacha mita moja na nusu kutoka katika jiwe/bikoni yake.Akileta ubishi atabanwa kwa kuombwa yafuatayo kisheria za mipangomiji/halmashauri;-
1-Uhalali wa umiliki eneo(nyaraka halali),
2-kibali cha ujenzi kinachoenenda na muda(expire date)
3-Na kama amehamia/nyumba ipo,ataombwa leseni/kibali/ruhusa ya kisheria ya kuishi hapo,
4-Hana hivyo vitu;a,atapigwa faini kimojakimoja-b,atasimamishwa ujenzi-c,atavunja ukuta kwa muda atakaopewa kwa gharama zake-d,atapewa onyo kali aache ungedere.[emoji120][emoji120][emoji120][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ingekuwa ndio hivyo nyumba zote zingekuwa zina vichochoro pande zote ndio hicho unamaanisha?
 
...Sasa tukupe Ushauri Gani Hapo. Wee Sema ulitaka TU kutujulisha kwamba una kiwanja!
Nikuulize wewe swali la kawaida Hapo la kutumia TU Akili... Jirani akamua kujenga Hapo, Maji ya Mvua ya Bati lake yataangukia Wapi???[emoji35]

Punguza makasiriko mzee mbona kiwanja kitu cha kawaida tuu, mpe ushauri bila kumtolea maneno ya shombo, ukizingatia ID za humu nyingi ni feki wala hata hatufahamiani.
 
Back
Top Bottom