TANZIA Joel Misesemo afariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofani jengo la Derm eneo la Makumbusho, Dar

TANZIA Joel Misesemo afariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofani jengo la Derm eneo la Makumbusho, Dar

Pale Mwanga Tower, Makumbusho limetokea tukio la mtu asiyefamika kujirusha kutoka gorofani, ambapo inasemekana tukio hilo limetokea mapema leo majira ya saa kumi na moja asubuhi.

Mpaka majira ya saa mbili asubuhi bado mwili wa mtu huyo ulikuwa eneo hilo. Taarifa zaidi zitakujia kadri zitakavyopatikana.

View attachment 2632805
Joel Misesemo enzi za uhai wake​

=====

Kijana asiyefahamika aliyekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 hadi 35 amefariki baada ya kujirusha kutoka gorofa ya 15 katika jengo la Derm lililopo Makumbusho, Dar es Salaam.


UPDATE: Polisi yathibitisha aliyejiua, kufanya uchunguzi


POLISI: KAMERA ZIMEONESHA JOEL MISESEMO AKIJIRUSHA MAKUSUDI KUTOKA GHOROFA YA 7
Kufuatia tukio la kifo cha Joel Misesemo mwenye umri kati ya miaka 35 hadi 40, Mkazi wa Mwananyamala, Jeshi la Polisi limesema chanzo cha awali ni mhusika kujirusha kutoka ghorofani kwenye jengo la Derm Plaza lililopo Makumbusho Kijitonyama.

Imeelezwa kuwa Joel alifika eneo hilo akiwa na gari aina ya Suzuki rangi ya silver (T142 DRM) na kuonekana katika jengo hilo Saa 11 Alfajiri ya Mei 23, 2023, akamwambia Mlinzi wa zamu kuwa anaenda kufanya ibada kwenye Msikiti uliopo ghorofa ya 15 ndani ya jengo hilo, muda mfupi baadaye alijirusha.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne amesema kamera za jengo hilo zimemuonesha akijirusha kwa makusudi kutoka ghorofa ya 7 kupitia dirishani na mwili wake umepelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala kwa uchunguzi Zaidi
Polisi wanawezaje kuendelea na uchunguzi wakati mtu ameshakufa?
 
Mwili wa binadamu ni delicate sana ,kitendo cha kudondoka kimechekecha viungo vya ndani ,mapolisi wanatumia sana style ya kuchekecha , polisi wakiona unawasumbua wanakuchekecha tu hauchukui mwezi lazima ukate moto.
Mmmh nikiwahi sikia hiyo ishu kule pwani. Mwizi baada ya kuiba akakimbilia msikitini.
Sasa mlangoni kuna watu wakawa wanashaliana kuwa wamtoe njee huyo mwizi alafu wamchekeche sasa hapo ndo napata maana halisi..
Duuh yaani vitu tumboni vimekaa kimtego kumbe 🤓🤓🙌🙌
 
Mmmh nikiwahi sikia hiyo ishu kule pwani. Mwizi baada ya kuiba akakimbilia msikitini.
Sasa mlangoni kuna watu wakawa wanashaliana kuwa wamtoe njee huyo mwizi alafu wamchekeche sasa hapo ndo napata maana halisi..
Duuh yaani vitu tumboni vimekaa kimtego kumbe 🤓🤓🙌🙌

Hatari sana mkuu ,ukichekechwa hauchukui round lazima ukate moto.
 
Wanaume tuwe na utaratibu wa kulia,inapunguza machungu yaliyo moyoni. Kulia siyo udhaifu.

unaingia zako chumbani na kuangusha kilio Kama nusu saa,ukitoka hapo kila kitu kinakuwa fresh. Jamaa kafa kifo kibaya Sana,si Ni heri tu angejioverdose dawa ya usingizi,akilala angelala moja kwa moja.

Hiyo unaweza ukalala na usife ila ukizinduka unakuwa mwehu
 
Wanachunguza mengi chanzo kwa undani zaidi..
Pia hata mwili pia je huyo mtu before ajajirisha mybe alitumia vitu vikali nk
Okay, maana nimekumbukia tukio la Tundu Lissu ambalo walisema hawawezi kuendelea na uchunguzi kwa kuwa hayupo nchini.
Na aliporudi wakadai hawawezi kuchunguza kwa kuwa hajaenda kutoa taarifa Polisi kuwa alimiminiwa risasi.
 
Okay, maana nimekumbukia tukio la Tundu Lissu ambalo walisema hawawezi kuendelea na uchunguzi kwa kuwa hayupo nchini.
Na aliporudi wakadai hawawezi kuchunguza kwa kuwa hajaenda kutoa taarifa Polisi kuwa alimiminiwa risasi.
Daah hapo sina neno...
Ila kwa huku uswahilini ukisikia kuchunguza ndo mambo yanakuaga hivo
 
Mwaka Jana kuna kijana aliwahi kujiua pembeni na hilo Jengo alikua mkaanga chips jpili inayofuata mchungaji kimaro akamtetea sana kua anamjua na alikua mtu poa ila sijui nini kilitokea baadae mchungaji kimaro akamgeuka Vibaya sana marehemu. Usikute wameamia apo. Nkipata thread iliyoongelea swala hilo ntaieka
 
Back
Top Bottom