TANZIA Joel Misesemo afariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofani jengo la Derm eneo la Makumbusho, Dar

TANZIA Joel Misesemo afariki dunia kwa kujirusha kutoka ghorofani jengo la Derm eneo la Makumbusho, Dar

Joel alipooza upande wa kushoto wa uso wake, hii Hali ya kupooza hakukubaliana nayo na tuliokuwa karibu nae aliacha kupost status kama awali takribani mwezi .
Hii hali minor stroke, inatibika. Dawa za hospitali, massage ya mafuta habatsoda na kutafuna jojo upande uliopata tatizo kwa muda wa miezi walau 4. Bila kusahau Maombi. Mtu anarudia hali yake vizuri tu.
 
Pale Mwanga Tower, Makumbusho limetokea tukio la mtu asiyefamika kujirusha kutoka gorofani, ambapo inasemekana tukio hilo limetokea mapema leo majira ya saa kumi na moja asubuhi.

Mpaka majira ya saa mbili asubuhi bado mwili wa mtu huyo ulikuwa eneo hilo. Taarifa zaidi zitakujia kadri zitakavyopatikana.

View attachment 2632805
Joel Misesemo enzi za uhai wake​

=====

Kijana asiyefahamika aliyekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 hadi 35 amefariki baada ya kujirusha kutoka gorofa ya 15 katika jengo la Derm lililopo Makumbusho, Dar es Salaam.


UPDATE: Polisi yathibitisha aliyejiua, kufanya uchunguzi


POLISI: KAMERA ZIMEONESHA JOEL MISESEMO AKIJIRUSHA MAKUSUDI KUTOKA GHOROFA YA 7
Kufuatia tukio la kifo cha Joel Misesemo Chizi mwenye umri kati ya miaka 35 hadi 40, Mkazi wa Mwananyamala, Jeshi la Polisi limesema chanzo cha awali ni mhusika kujirusha kutoka ghorofani kwenye jengo la Derm Plaza lililopo Makumbusho Kijitonyama.

Imeelezwa kuwa Joel alifika eneo hilo akiwa na gari aina ya Suzuki rangi ya silver (T142 DRM) na kuonekana katika jengo hilo Saa 11 Alfajiri ya Mei 23, 2023, akamwambia Mlinzi wa zamu kuwa anaenda kufanya ibada kwenye Msikiti uliopo ghorofa ya 15 ndani ya jengo hilo, muda mfupi baadaye alijirusha.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne amesema kamera za jengo hilo zimemuonesha akijirusha kwa makusudi kutoka ghorofa ya 7 kupitia dirishani na mwili wake umepelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala kwa uchunguzi Zaidi
Mnatuchanganya bwana. Mbona taarifa zingine zinasema alijirusha toka ghorofa ya 7 kwenye jengo lenye ghorofa 15? Nani mkweli sasa?
 
... lengo lake halikuwa kuswali bali kwenda kujirusha; angeruhusiwaje kupanda juu? Ni kujifanya anaenda kuswali (msikiti uko juu) ili aruhusiwe na mlinzi kupanda juu kutimiza nia yake ovu.
Ila bora kajihudumia mwenyewe maana vinginevyo labda angekua mteja wa gunia la mkaa.
Au jela hii hapa.
 
Huyo jamaa mkisimama wawili kwenye pared wewe mwenye biashara unaonekana una stress kumzidi na yupo sawa yeye anakwambia kikubwa anapumua mengine yataji-set.

Hapa utagundua namna nafsi zetu zilivyo tofauti.
Watu tunatofautiana kwenye kupokea na kuhimili matatizo
Wengine mioyo yao ni laini jambo fulani tu akilipata anafikiria kujiua

Ova
 
Hivi ukijirusha ukapona halafu miguu ikavunjika inakuwaje hapo?
Kama unataka kijirusha lazima uhakikishe unakwenda ghorofa ya juu zaidi,kama alivyofanya rafiki yetu Joel kwa.... er,hekima yake.
Hii stori haijakwisha bado. Hapa siyo America,ambapo watu wanaacha gari kando wanaenda kujiua.
I hope to God siyo matatizo ya wivu wa mapenzi tena.
 
Kama aliongea na simu kwa muda mrefu kisha akajirusha , aliongea na nani ?
Alioa toka 2014 , je maelewano na mke wake yalikuwaje ?
 
Kuna jamaa alijirusha pale magomeni kwenye ghorofa za Watumishi House alafu akafikia kwenye pipa la maji maarufu kama Sim tank na kufa baadae
Hakufa palepale alikimbizwa hospital. Huenda alifia njiani au hospital
Mbaya zaidi tukio lilikuwa linarushwa live na ITV wakakatisha matangazo. Yule njomba kut0ka Ntwara ilikuwa kazi yake michezo ya kupanda majengo marefu na kujirusha ndani ya tank za maji huku akiongozwa(guided) na kamba asidondokee nje ya tank.
Pale alifeli kukokotoa urefu wa jengo, uzito wake, na kina cha maji ili kutambua atakuwa submerged urefu gani ndani ya maji ili asiguze sakafu ya tank kwa mshindo mkubwa. Aliidharau Gravitional force (g). Alipotumbukia wanashangaa hatoki nje mwenyewe wakawahi kumtoa kavunjika viungo.
 
Back
Top Bottom