Joyce Ndalichako na Kiingereza kibovu tena

Joyce Ndalichako na Kiingereza kibovu tena

Joyce Ndalichako anapenda kuongea Kiingereza lakini Kiingereza hakimpendi. Hebu aliyemuelewa hapa atuambie alikuwa anataka kusema nini?

Hii ni mara ya 2 ndani ya siku 60 kwa Waziri kuongea Kiingereza chenye uvunjifu wa sarufi na tafsiri ya neno kwa neno toka Kiswahili kuja Kiingereza. Ya kwanza ni pale alipokuwa anamtishia Mkandaarasi wa kichina kuwa nitakusweka ndani (You will stay inside)

USHAURI:
Namshauri Mh Waziri awe anaongea kwa Kiswahili tu au awe anasoma hotuba alizoandikiwa na wataalamu. Kinyume chake anadhalilisha PhD yake na Vyuo vilivyompa hizo shahada.

Zaidi soma: Hivi hiki ndicho Kiingereza cha Profesa Ndalichako?
View attachment 1355606

PhD na lugha wapi na wapi. Umekwama wapi. Mkuu. Watu tuliandika PHD kwa kijerumani lakini Sio kwamba tunakimaster. Ni scientific work so one needs Hilfe Anapokuwa amemalizana na Maprofessor wanaomsaidia. Anapewa mtaalamu wa lugha na Fach the anarekebisha.

Wazo lako la kuandika ndo Point. Kwa kuwa Ni muhimu kwa kiongozi kufikisha ujumbe kama anavyokusudia. Na Lugha Ni Tool muhimu ya kufanya hivyo
 
PhD holder na kingereza kama chake ni aibu kwa taifa, kuna wanaodai kuwa hiyo PhD yake niya kuunga na gundi(japo si neno zuri), na moja ya ushahidi wa hilo ni kingereza chake. Nitajie mtu mwingine mwenye PhD kama yake anayeongea broken hivyo.(Nb mtoe jiwe mana yake pia ni fake)
Sijapanic dogo na katika jibu la msingi ungekuwa na akili ya kusoma vitu between the line ungekuwa umeshaelewa. kiingereza ni somo miongoni mwa masomo mengi. Performance ya kwenye Science si lazima kujua English grammar. Na wewe ni kwa sababu tu uelewa wako ni mwembamba ndiyo maana unapata shida na hivi vitu. Naendelea kukusisitiza hata hiyo PhD yake haina uhusiano wowote ule na English grammer.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, kuna uhusiano mkubwa sana wa elimu na ufasaha wa lugha. Hata ukienda US, UK, Canada etc. watu ambao hawajasoma hawaongei lugha kwa ufasaha kama waliosoma. Nia utawajua kirahi tu. Same Tanzania, pamoja na kwamba Kiswahili ni lugha yetu bado pia tunajifunza Kiswahili mashuleni. Kuna watu wengi tu (asilimia kubwa) wamejifunzia kuongea Kiswahili mashuleni. Watu wengi (hata humu) kwa kufuatilia maandishi ya wengi utaona ni jinsi gani tunapishana kwa ufasaha wa Kiswahili.

Tatizo kubwa la Ndalichako siyo tu kwamba ameongea broken English bali ameshindwa kufikisha ujumbe kwa walengwa.Zaidi ya Watanzania sidhani kama wengine wamemuelewa alikuwa anataka kusema nini.....!!

Mkuu tatizo lako unachanganya baina ya kuongea na kuandika maneno ya kisomi kwenye nyanja fulani na kuongea lugha fulani kwa ufasaha,ishu ya mtu kuweza kuzungumza lugha fulani kwa ufasaha zaidi ,sometimes ni ya kimazingira zaidi na wala sio uwezo wake kielimu!!
 
Hii nayo ni habari?

Jamani tuache ujinga basi maana nyie wenyewe mfumo wetu wa elimu mnaujua.

Mtu mwingine mpaka anapata PhD neo analoweza kulitamka kwa ufasaha ni 'is'.
Ongezea 'so as' na 'apart from that',utafikiri anaandika essay za form three B.
 
Ukisema Mbowe hajui kingereza mimi sishangai kwa sababu ya level ya elimu yake, lakini msomi wa PhD kuongea broken ki kituko cha dunia.Kumbuka hatuzungumzii utendaji wake

Sent using Jamii Forums mobile app
Na yule pale hakuwekwa kwa sababu ni anajua au hajui kiingereza. Wewe level yako ya uelewa ni ndogo sana hivyo hata dhana nzima ya PhD hunayo. Ungekuwa unajua japo kidogo vitu hivi vya kitaaluma usingezumza huu upupu. Unapoandika thesis hasa kwa level hizo Master or PhD ziko ambazo supervisors wala hawahitaji Kiingereza chako bali presentation ya mawazo na findings zako. Ndiyo maana kabla ya difference hapo ndo unashauriwa sasa kupeleka thesis yako kwa mtaalum wa lugha kuifanyia edition kwa maana ya upangaji wa grammar nk. Kama kiingereza ni kigezo kwa levels hizo basi na lugha nayo ingekuwa inasahihishwa. Lkn pia kuna Master na PhD zinasomwa kwa lugha tofauti tofauti japokuwa wewe umekariri kiingereza tu. Kuna watu wanaenda soma Ujeruman, Portugal, China nk ambao hujifunza lugha za nchi hizo na kisha kusoma levels hizo. kwa wewe mwenye uelewa mdogo utahoji tu kwa nn hajui kiingereza vizuri wakati ana PhD. Kiingereza ni lugha tu kama kimakonde na ukitaka kujua hilo vuka hapo malawi utakuta dogo yupo porini anachunga kamaliza primary lkn anapiga kiingereza kwa mjinga kama wewe ukimuona utasema huyu nchini kwetu anafaa kuwa Rais wa nchi.
 
Umedai kuwa English ni lugha ya tatu (sijui ni ya tano) lakini ukweli ni kuwa English ndio official business and legal language kwa Tanzania. Sasa iweje PhD holder aliesoma elimu yake yote kwa Kiingereza, kafanya kazi katika mazingira Kiingereza kinapotumika ashindwe kuongea passable English? Unaona ni jambo la kawaida kabisa hilo?
Kwanza kabisa hapana mahali niliposema English ni lugha ya Tatu wala ya Tano....

Nimesema kuwa ni lugha ya kiofisi(Official language)hapa naomba tuelewane kuwa lugha kuwa official haimaanishi kuwa inazungumzwa maofisini na katika Shughuli za serikali...

Mfano kwenye sheria kila kifungu kipo kwa English na makabrasha yote ya sheria yapo kwa lugha hiyo ila kila process inayohusisha mazungumzo hutumia kiswahili...
Naomba tuangalie bungeni lugha inayopatikana kwenye maandishi huwa English ila majadiliano huwa kwa kiswahili.

Kwenye vikao vya kisheria na kiserikali English hutumika kwenye maandishi ila majadiliano hufanyika kwa Kiswahili..

Sehemu Pekee Ambayo English hutumika kwenye maongezi ni pale tu ofisa anapokutana na Foreigners ama katika shughuli za kidiplomasia zinazohusisha nchi na nchi..Kwa kuzingatia haya matumizi ya English yanakuwa tena si kama lugha ya pili bali lugha ya wataalam..

Tukija shuleni hasa shule zetu za serikali na hata baadhi ya binafsi Masomo yote isipokuwa kiswahili hufundishwa kwa kutumia kiswahili na huandikwa kwa English, Kwa mazingira haya ni ngumu mwanafunzi kuwa mjuvi wa lugha hii ya English kwa ufasaha ni vile inahitaji jitihada binafsi kuweza kuimudu.

Bado tunaathiriwa na Lugha zetu za asili ambazo kimsingi hata wasomi wengi wa nchi yetu wanayo changamoto hii kwani huanza kuzungumza mfano Kisukuma halafu huja Kujifunza Kiswahili na baadaye English mashuleni..Sasa ukiangalia hapo kila lugha ina namna ya kuzungumza ambapo huaribu huzungumzaji wa English nzuri yenye kupendeza kuisikia na kueleweka..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani kiswahili kenya ni lugha ya lazima kufundishia kama kingereza Tanzania ?

Sent using Jamii Forums mobile app
sina hakika kama ni ya lazma au laaa ila ni lugha rasmi na ya taifa unaweza itumia popote kwenye shughuli za serikali so ni kama kuna umuhimu mtu kama senatpr Gidion Moi kuifaham kiufasaha ila haifahamu kwa ufasaha huo na hajadhuru utendaji wake same applies to Mama Ndari
 
Joyce Ndalichako anapenda kuongea Kiingereza lakini Kiingereza hakimpendi. Hebu aliyemuelewa hapa atuambie alikuwa anataka kusema nini?

Hii ni mara ya 2 ndani ya siku 60 kwa Waziri kuongea Kiingereza chenye uvunjifu wa sarufi na tafsiri ya neno kwa neno toka Kiswahili kuja Kiingereza. Ya kwanza ni pale alipokuwa anamtishia Mkandaarasi wa kichina kuwa nitakusweka ndani (You will stay inside)

USHAURI:
Namshauri Mh Waziri awe anaongea kwa Kiswahili tu au awe anasoma hotuba alizoandikiwa na wataalamu. Kinyume chake anadhalilisha PhD yake na Vyuo vilivyompa hizo shahada.

Zaidi soma: Hivi hiki ndicho Kiingereza cha Profesa Ndalichako?
View attachment 1355606
Basics free basic primary education ands the they decision was made make sure that all all tanzanian children of Tanzanian give aaaaah
Yaani hivyo😏😏😏😏😏
 
Mkuu tatizo lako unachanganya baina ya kuongea na kuandika maneno ya kisomi kwenye nyanja fulani na kuongea lugha fulani kwa ufasaha,ishu ya mtu kuweza kuzungumza lugha fulani kwa ufasaha zaidi ,sometimes ni ya kimazingira zaidi na wala sio uwezo wake kielimu!!
Mkuu, nazungumzia vyote. Mfano linganisha Kingereza cha Rooney na Tony Blair.
 
Hivi Kuongea English ndio Ishara ya usomi!???

Watanzania English sio lugha yetu ya kwanza wala ya pili,mara nyingi tunaitumia tuwasilianapo na wageni na pia katika shughuli za kiofisi!!

English sio lugha yetu mama hivyo huwezi ukaiongea kama ambavyo inaongelewa America na Uingereza...Halafu tambua yeyote anayejifunza English ukubwani lazima akumbane na changamoto kwenye kuongea...

Kwa Mfano ili uwe mjuvi wa English lazima uwe mzuri kwenye" Pronunciation " hapa hubeba asilimia 60 kwenye uongeaji wa lugha hii..

"Stress" Mikazo ya maneno hapa napo ndipo shida hutokea kwa watu ambao English sio lugha mama na hapa hubeba asilimia zisizopungua 40.

Intonation,Rythm...kila lugha ina mfumo wake na mpangilio wake wengi kiswahili kimetuathiri sana na hzi lugha zetu za makabila...

Ni ngumu kuongea English yenye kupendeza masikio ya watu tusiongee kwa mihemko aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivyo vyote tunavielewa, kinachogomba hapa ni grammar. Kwenye grammar hakuna kisingizio kwa sababu makosa yake yanaweza usieleweke kabisa.
 
Ni vizuri wawe wanaongea Kiswahili ili wakalimani nao mkono uende kinywani
 
Akapractise huko na mabeberu ili hizo tafsiri za kutoka kwenye Kiswahili kwenda kwenye Kiingereza zipotee.
Amekaa darasani miaka zaidi ya 10, kama ameshindwa kujiboresha hata tukimpeleka kwenye sitting room ya malkia Elizabeth ll atatoka bure tu
 
Hivi wanaopata Ph.D kwa somo specialization lwa somo la kiswahili hua wanasoma kiswahili kwa kiingereza? Ha ha ha ha

Harafu siyo wote wamesoma kwa kiingereza kama mnavyodhania, wengine wamameliza form form four wakaenda urusi hadi kuwa ma prof kwa kutumia lugha ya kirusi ama kichina ama kijuremani nk.
 
Back
Top Bottom