Julius Nyerere alikuwa mtu sahihi kupewa nchi kwa mazingira ya kipindi kile

Maajabu kuna mapimbi waliolishwa chuki za kisiasa na ubaguzi wa kidini wanamchukia nyerere haswa.

Hawajui bila huyo jamaa huenda hii nchi isingekalika kwa changamoto za ubaguzi wa ukanda&ukabila, bila kusahau udini,

Wapuuzi wachache wanaoamini maendeleo ya kuletewa na wazungu ndio hawa hawa wanalalamika kwanini nyerere hakuwa upande wa Mabepari na wanyonyaji, wanalalamika mpaka leo maajabu baada ya nchi kufuata huo mfumo mbona bado hayo maendeleo hakuna?

Wote wanaomlalamikia nyerere ni wale wale ambao babu zao walishiriki kuwauza ndugu zetu utumwani, pia baadhi yao ndio hawa hawa waliokuwa waoga wa kupambania uhuru badala yake wakawa wakijificha vichakani huko wakazaliana na kuleta matoto mambumbumbu yanayolalamika kila jambo, kila kitu yanaamini kitaletwa kwa kuwa chini ya mzungu.

Hawa watu ni hatari kwa Taifa hili.
 
Kuna darkside ya TANU ambayo hata wewe huwezi kuyataja sababu waliokuadisia hawakukuambia lakin haya niliyoandika kwenye uzi ni ukweli mtupu

Swala la power struggle lilikuwepo
Moja ya Power struggle iliyosababisha wapasuke ilikuwa Bibi Titi na baadhi walitaka Tanzania ijiunge na Muslim Association iliyokuwa chini ya Gamal Abdel Nasser Egypt

Nyerere alipinga hii kitu kwa nguvu na akaanzisha BAKWATA, ndio ilichochea mpasuko wake na kina Bibi Titi
 
Kuna darkside ya TANU ambayo hata wewe huwezi kuyataja sababu waliokuadisia hawakukuambia lakin haya niliyoandika kwenye uzi ni ukweli mtupu

Swala la power struggle lilikuwepo
Chan...
Hatuwezi kuvutana katika nani anasema kweli.

Kuhadithiwa ni sehemu muhimu sana kama " secondary source'' katika utafiti wowote halikadhalika kusoma nyaraka kama, "primary source,' vyote vinakubalika katika Research Methodology.

Mimi nimemuandika Nyerere ndani ya kitabu cha Abdul Sykes chenye kurasa 416 na Maktaba yangu ni kati ya maktaba tatu Bora zenye taarifa za Nyerere.

Nimesoma Nyaraka za Sykes zenye taarifa za kila mtu aliyehusika katika harakati za African Association kuanzia 1929 hadi TANU 1954.

Nawajua kwa majina wote hao.

Nimeshirikishwa katika uandishi wa kitabu cha maisha ya Julius Nyerere kilichoandikwa na Prof. Issa Shivji na jopo lake.

Hakuna ukweli katika hayo uliyoandika.
Kama kulikuwa na power struggle taja majina ya wahusika.



Ofisi ya African Association siku ya ufunguzi wake 1933
(Picha kwa hisani ya Maktaba ya Picha ya Sykes)
 
Pearce,
Hapana hapajakuwa na Muslim Association chini ya Gamal Abdul Nasser.

Wala hapajakuwa na kutaka Waislam kujiunga na taasisi yoyote nje ya Tanganyika.

Wala hapajakuwa na power struggle.
Kuna paper nimeandika, "Islam and Politics in Tanzania," (1989).

Waislam wa Afrika ya Mashariki walikuwa na umoja wao East African Muslim Welfare Society (EAMWS).

EAMWS ilipigwa marufuku na serikali na kuundwa BAKWATA kwa kuwa ilikuwa inajenga Chuo Kikuu.

Hili halikutakiwa.

Hii itakusaidia kuelewa mengi.
 

Huu ni uongo ulio wazi,mnafanya hivi kwa maslahi ya nani hasa?je ninyi ni watanzania ama mamruki?
 

Uongo mwingine huu hapa,histria ya mchongo kutoka kwa islamic propagandist
 
WAzee wake Mohammed Said walikuwa bize kupigania uhuru wa daresalamu sio Tanganyika.
Mangungo...
Ungeacha kejeli na kuuliza yale usiyojua ungenipa mimi fursa ya kukueleza historia hii kama ilivyokuwa.

Faida ya elimu ni pale inapowanufaisha wale wale wasiyokuwanayo.

Wewe huna elimu ya historia hii na kama huna ni busara kwako kuuliza ili ufahamishwe ili ujitoe kwenye ujinga.

Ukisoma Tanganyika Intelligence Summary taarifa za kikachero kutoka Special Branch utaona mtandao wa TAA na viongozi wake uliokuwa majimboni.

Pili ukisoma Nyaraka za Sykes utaona barua ambazo zilikuwa zikichapwa kwa siri nyumbani kwa Ally Sykes na kusambazwa Central Line na wanaharakati wa TAA.

Historia hii yote imo katika kitabu cha Abdul Sykes.
Huo ujinga uliokuwanao katika historia ya uhuru ni wa kujitakia.

 
Shida ni kwamba unajipa hati miliki ya ukweli.Kwamba unachokitoa wewe ni ulweli ila cha wengine ni uongo.Kuna tafiti na kumbukumbi za kihistoria nyingi zinapingana na unachokieleza.Historia ya Uhuru wa Tanganyika inaongelea watanganyika kutafuta uhuru kwa umoja wao bila kujali dini zao waliangalia maslahi ya nchi yao.Usitugawe!
 
Nan...
Sithubutu kujipa hatimiliki ya ukweli wa historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nikifanya hivyo nitakuwa mjinga.

Mimi nilichokuzidini ni kuwa nimetafiti historia hii na nimeandika kitabu.

Lakini kubwa sana nimejaaliwa kuzisoma Nyaraka za Sykes na nimesoma mswada wa kitabu cha maisha yake alioandika kabla ya kufa kwake mwaka wa 1949.

Hakuna tafiti za historia ya uhuru wa Tanganyika kama unavyodai na zingekuwapo kungekuwa na vitabu vyake.

Ikiwa labda kwa bahati mbaya mimi sijaona na wewe umeona weka hapa hizo rejea.

Mimi nilikuwa sipungui Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam East Africana.

Hapo ndiyo kuna kila kitu.

Hapo kuna historia ya African Association Seminar Paper ya Aisha "Daisy" Sykes: "The Life of Kleist Sykes, " (1968).

Tazama maajabu haya.
Mimi sijamgawa yeyote.

Ilipokuja kuandikwa historia ya TANU na Chuo Cha CCM Kivukoni (1981) watafiti walikataa kupokea historia ya Sykes katika uasisi wa African Association 1929, uongozi wa TAA 1954 na kuundwa kwa TANU 1954.

Bahati nzuri mimi hawa waliofanya haya ni baba na babu zangu.

Najua historia zao.

Haikuwa shida kutambua kuwa hawa wamefutwa katika historia kwa kuwa waliokuwa madarakani baada ya uhuru walikuwa na hofu ya kuona Waislam ndiyo walioongoza mapambano ya kudai uhuru.

Ukinilaumu mimi ati nawagawa watu itabidi uwalaumu Chuo Cha CCM Kivukoni kwa kuandika historia ya uongo.

Leo kupitia utafiti na kitabu nilichoandika mnaisoma upya historia ya uhuru.
 
Sisi kupitia mabandiko yako tunaona mambo kadhaa nitayataja.
1.Tunaona unavyojitahidi kuzivua harakati za wazee wako Utanganyika na kuzivika Uislamu.(Hapa tunataka kujua kama wazee wako walipigania uhuru kama watanganyika au waislam.
2.Tunaona jitihada zako za kuwatenganisha wakristu na struggle za uhuru(Hapa ninachojua wakristu walipigania uhuru kama watanganyika hawakuwa na ambitions za kuusimika ukristu wao)
3.Tunaiona chuki yako na wenzio kwa wakristu.
4.Tunafanya assesment ya mikakati yenu ya kupambana na wasio wa imani yako.
5.Tunaiona kiu yenu ya kulisilimisha taifa
6.Tunajipanga kimkakati katika nyanja zote.
WE ARE WATCHING!
 
Nan...
Mbona unaleta vitisho ndugu yangu?
Yote uliyoandika mie siko huko.

Nilichokitaka nimefanikiwa na ilikuwa kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika na kuonyesha mchango wa Waislam.
 
Nyerere alirithi kiti cha uenyekiti wa TANU wenye ombwe la uongozi
 
Ndo mfano wa changamoto TANU ilikua nayo
 
Walikua wanapigania uhuru wa waislamu au watanganyika
Kwenye haya maelezo yako ndo jibu la power struggle niliyokua naiongelea
 
Ndo changamoto yake ana-amini ana hatimiliki ya ukweli wengine ni uongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…