Julius Nyerere alikuwa mtu sahihi kupewa nchi kwa mazingira ya kipindi kile

Julius Nyerere alikuwa mtu sahihi kupewa nchi kwa mazingira ya kipindi kile

Ndo changamoto yake ana-amini ana hatimiliki ya ukweli wengine ni uongo
Chan...
Hapana sina hatimiliki ya historia hii ila mimi ni sehemu ya historia hii.

Nimeitafiti na kuandika kitabu ambacho kimesahihisha historia ambayo ilidhaniwa ndiyo historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Vipi Chuo Cha CCM Kivukoni itaandika historia ya TANU Abdul Sykes asitajwe?

Baba yake ni mmoja wa waasisi waliosisi African Association na mmoja wa waliojenga ofisi ya chama hicho.

Abdul Sykes ndiye aliyempokea Julius Nyerere na akaishi na yeye alipoacha kazi ya ualimu.

Kadi yake ya TANU ni No. 3, No. 2 ni ya Ally Sykes na No. 1 ya Julius Kambarage Nyerere, Territorial President wa TANU.

Kadi ya Julius Nyerere aliyeiandika ni Ally Sykes.

Usajili wa chama cha TANU wamefanya hawa watu watatu.
Kadi 1000 za kwanza za TANU kanunua Ally Sykes kutoka mfukoni kwake.

Inakuwaje wazalendo hawa hawatajwi katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Mnao ukweli kushinda huu?
Mnalo jibu?

Mlango bado uko wazi na mnayo haki ya kuandika ikiwa mnaona historia niliyoandika mimi si ya kweli.

Miaka 25 imepita hakuna aliyeweza kufanya hili.
Kitabu kinakwenda chapisho la nne.

1707077540717.png

1707077926044.jpeg

1707077370454.jpeg

Ally Sykes na Julius Nyerere, 1958​
 
Nyerere aliwekwa au kupachikwa na waingereza kwenye siasa ili kupunguza makali na kuchelewesha harakati za kudai uhuru na pia kuhakikisha maslahi yao na wamisionari yasiathirike ndani ya Tanganyika huru.
Ndio maana baada ya uhuru walikuja haraka kumuokoa pale jeshi lilipoasi.
Wakati huo huo waingereza walikataa kumsaidia mfalme wa Zanzibar wakati wa mapinduzi sababu walikua nao ni washiriki wa siri kwenye mapinduzi.
Pia Nyerere alikua na ukaribu na waingereza hasa gavana wa mwisho wa Uingereza nchini Richard Turnbull. Nyerere hakuwahi kupata misukosuko ya kisiasa kama kufungwa au matatizo mengine sababu waingereza walikua wamemuweka pale.

Waingereza walipatwa na wahka kuona wengi wa wanaharakati wa uhuru ni waislamu japo wao hawakua na lolote la kidini zaidi ya kudai uhuru kwa niaba ya wayanganyika wote. Ndio maana walimkaribisha Nyerere kwa mikono miwili.

Nyerere alikuja kugeuka na kuingiza siasa za ujamaa pamoja na kujihusisha na harakati za ukombozi wa nchi zilizo kua bado kupata uhuru kwa ushawishi wa viongozi wengine katika Afrika ndio uhusiano na waingereza ukaanza kuchachuka.

Na ni uhakika na ukweli wengi wa wakiristo walikua na msimamo wa wamisionari katika suala la Uhuru. Wamisionari na wakoloni waingereza walikua lao moja kuendeleza utawala wa kikoloni. Hakuna nukuu katika historia kuwa kanisa lilitoa tamko la kusapoti tanganyika ipatiwe uhuru.
 
Tanzania wameshapita marais waislamu watatu inamaan hawajakiona unachoongea na kukifanyia kazi ulishawah jiulizaga hili swali
Chan...
Mimi sikuandika kitabu hiki kwa ajili ya maraisi.

Nimeandika kitabu hiki kusahihisha historia iliyokuwapo ambayo haikuwa sawa.

1707078194892.png

Nikimtunuku nakala mbili za kitabu cha Abdul Sykes Mzee Ally Hassan Mwinyi Ukumbi wa Korea, 2014​
 
Chan...
Mimi sikuandika kitabu hiki kwa ajili ya maraisi.

Nimeandika kitabu hiki kusahihisha historia iliyokuwapo ambayo haikuwa sawa.

View attachment 2894474
Nikimtunuku nakala mbili za kitabu cha Abdul Sykes Mzee Ally Hassan Mwinyi Ukumbi wa Korea, 2014​
Asa wasipoipitisha isomwe mashuleni yaani ingie kwenye mtaala itakua na maana gani
 
Uandishi sio mzuri mjitahidi
Kabla ya Julius Nyerere hajawa kiongozi wa TANU na hali ya siasa za Tanzania zilikua kama ifuatayo;-

Changamoto kubwa ya TAA na baadae TANU ilikuwa ni power struggle kila mtu alikua anataka awe kiongozi na hakuna mtu aliyeweza kuunganisha wanachama ambao walikua makundi makundi. Hii ilipelekea TANU kuwa na wakati mgumu sana sababu kama hamna maelewano kabla hata ya uhuru mkija kupewa nchi itakuaje

Hakuna kiongozi wa TANU aliyekua na maono mapana ya kuunganisha nchi kwani wengi wao walidhani wanadai uhuru wa Dar es Salaam, walikua na ufahamu na nchi nzima ili hawakuwapa uzito maeneo mengine ya nchi.

Changamoto lingine ni swala la udini, viongozi wa TANU walitaka nchi kuwa ya kislamu na kuongozwa kislamu kitu ambacho mkoloni alikikataa sababu walitaka mtu atakaye leta usawa kwa dini zote kumbuka kabla ya uhuru waislamu walikua asilimia 35 na wakristo 30 na ndio mara ya mwisho Tanganyika kufanya sensa kujumuisha kipengele cha dini.
Na concern kubwa sana ya mkoloni ni swala la udini sababu kuna kosa alilifanya India na Pakistani hakutaka tena lijirudie Tanzania swala la usawa kwa dini zote alilichukulia kwa uzito mkubwa sana

Mkoloni aliwapa masharti kabla hawajarudi tena ku-discuss juu ya uhuru wawe wamesha-sort out juu ya swala la uongozi kwa sharti la awe mkristo, amesoma na mwanachama hai wa TANU kwa hiyo bila kupenda ikabidi wamchague Julius Nyerere

Nyerere kuwa kiongozi wa TANU ni uamuzi wa kutokupenda kwa wapigania uhuru na ndio the only best choice ambayo ilikuwepo kunauwezekano wako ambao walikua wazuri zaidi kwa kigezo cha elimu na uongozi zaidi ya Julius Nyerere ila wengi wao walikua ni wachungaji na mapadre kwa hiyo ingewawia vigumu kuunganisha nchi

Kwa hiyo Nyerere na mapungufu yake alikua ni mtu sahihi kupewa nchi kwa mazingira ya kipindi kile
X + 35 + 35 = 100
X + 65 = 100
X = 100 - 65
X = 35%

Je, hawa asilimia 35 walikuwa kundi gani? Hawana dini (wapagani)?!
 
Asa wasipoipitisha isomwe mashuleni yaani ingie kwenye mtaala itakua na maana gani
Chanee,
Sidhani kama kitabu hiki kitapewa ithbati ya kusomwa shule.

Kuna mwanafunzi wa Ph D alikuja kwangu kunihoji alikuwa anaandika Thesis yake.

Katika mazungumzo yetu akaniambia kuwa Supervisor wake amemwambia kitabu cha Abdul Sykes kisiwe katika rejea zake.

Ikiwa Chuo Kikuu kitabu hiki wanakikwepa na hapo ndipo penye uwanja wa kushindanisha mawazo itakuwaje katika shule za msingi na sekondari?

Kulikuwa na mradi wa Oxford university Press, Nairobi kusomesha Kiingereza shule za msingi na wakati huo huo wanaposomesha Kiingereza vitabu vitakavyotumika viwe ni vitabu vinavyosomesha historia.

Waandishi wa Kenya na Uganda kati yao waliandika vitabu 15 lakini hapakuwa na mwandishi hata mmoja kutoka Tanzania kwa hiyo hapakuwa na kitabu cha historia kutoka Tanzania.

Oxford wakanitafuta na wakaniomba niandike kitabu ili Tanzania nayo iwemo katika mradi huo.

Mimi nilikuwa sijawahi kuandika kitabu cha watoto wadogo shule ya msingi.

Oxford wakaniambia kuwa watanielekeza namna ya kuandika vitabu kwa ajili ya watoto wadogo.

Oxford wakaniletea vitabu vingi vya watoto niangalie.
Nikawapatia mswada.

Kitabu hiki kilichapwa na Oxford wakaja kukizindua Kilimanjaro Kempski na walialika media zote pamoja na maofisa wakubwa wa Wizara ya Elimu.

Nilipewa muda wa kukiwasilisha kitabu changu katika hadhira ile.
Kitabu hiki kikapigwa vita kisipewe ithbati ya kusomeshwa shule za Tanzania.

Wakati haya yanatokea Oxford walikuwa wana mswada wangu mwingine wanajitayarisha kuuchapa.

Mswada huu haukuchapwa na kwa masikitiko wakaniambia kuwa liko tatizo kwa hiyo sitakuwamo katika mradi wa kuandika vitabu vya watoto kwa upande wa Tanzania.

Kitabu hiki kinasomwa kote katika shule za msingi nje ya Tanzania na sasa kipo katika toleo la pili.

Halikadhalika niliombwa na mchapaji mmoja wa Kenya kuandika historia ya Kura Tatu mwaka 1958 kuadhimisha miaka 40 ya Uamuzi wa Busara wa Tabora wakiamini kuwa kitabu hiki kitakuwa sehemu muhimu ya historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kitabu hiki nacho kikapigwa vita.
Hiki ni kisa kirefu.

1707081179955.png

First Edition
1707081027647.png

Second Edition
1707081337676.png

Mohamed Seif Khatib katika Uzinduzi wa Kitabu, ''The Torch on Kilimanjaro''
Kilimanjaro Kempinski Hotel kulia kwake ni Sheikh Abdillah Nassir
1707081627553.png
 
Chanee,
Sidhani kama kitabu hiki kitapewa ithbati ya kusomwa shule.

Kuna mwanafunzi wa Ph D alikuja kwangu kunihoji alikuwa anaandika Thesis yake.

Katika mazungumzo yetu akaniambia kuwa Supervisor wake amemwambia kitabu cha Abdul Sykes kisiwe katika rejea zake.

Ikiwa Chuo Kikuu kitabu hiki wanakikwepa na hapo ndipo penye uwanja wa kushindanisha mawazo itakuwaje katika shule za msingi na sekondari?

Kulikuwa na mradi wa Oxford university Press, Nairobi kusomesha Kiingereza shule za msingi na wakati huo huo wanaposomesha Kiingereza vitabu vitakavyotumika viwe ni vitabu vinavyosomesha historia.

Waandishi wa Kenya na Uganda kati yao waliandika vitabu 15 lakini hapakuwa na mwandishi hata mmoja kutoka Tanzania kwa hiyo hapakuwa na kitabu cha historia kutoka Tanzania.

Oxford wakanitafuta na wakaniomba niandike kitabu ili Tanzania nayo iwemo katika mradi huo.

Mimi nilikuwa sijawahi kuandika kitabu cha watoto wadogo shule ya msingi.

Oxford wakaniambia kuwa watanielekeza namna ya kuandika vitabu kwa ajili ya watoto wadogo.

Oxford wakaniletea vitabu vingi vya watoto niangalie.
Nikawapatia mswada.

Kitabu hiki kilichapwa na Oxford wakaja kukizindua Kilimanjaro Kempski na walialika media zote pamoja na maofisa wakubwa wa Wizara ya Elimu.

Nilipewa muda wa kukiwasilisha kitabu changu katika hadhira ile.
Kitabu hiki kikapigwa vita kisipewe ithbati ya kusomeshwa shule za Tanzania.

Wakati haya yanatokea Oxford walikuwa wana mswada wangu mwingine wanajitayarisha kuuchapa.

Mswada huu haukuchapwa na kwa masikitiko wakaniambia kuwa liko tatizo kwa hiyo sitakuwamo katika mradi wa kuandika vitabu vya watoto kwa upande wa Tanzania.

Kitabu hiki kinasomwa kote katika shule za msingi nje ya Tanzania na sasa kipo katika toleo la pili.

Halikadhalika niliombwa na mchapaji mmoja wa Kenya kuandika historia ya Kura Tatu mwaka 1958 kuadhimisha miaka 40 ya Uamuzi wa Busara wa Tabora wakiamini kuwa kitabu hiki kitakuwa sehemu muhimu ya historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kitabu hiki nacho kikapigwa vita.
Hiki ni kisa kirefu.

View attachment 2894513
First Edition
View attachment 2894511
Second Edition
View attachment 2894514
Mohamed Seif Khatib katika Uzinduzi wa Kitabu, ''The Torch on Kilimanjaro''
Kilimanjaro Kempinski Hotel kulia kwake ni Sheikh Abdillah Nassir
View attachment 2894525
We unadhani sababu ni nini na kwanini nyerere alimcancel abdul sykes kwenye historia japokua alimpokea kama unavyosema
 
We unadhani sababu ni nini na kwanini nyerere alimcancel abdul sykes kwenye historia japokua alimpokea kama unavyosema
Chan...
Swali hili lilimtaabisha sana Prof. Haroub Othman.

''Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa, katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa.

Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh Abdallah Chaurembo.

Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima.

Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes).

Swali hili hata mimi linanitaabisha hadi leo.


1707111095812.png

Dossa Aziz akitunikiwa medali na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere​
 
Chan...
Swali hili lilimtaabisha sana Prof. Haroub Othman.

''Tarehe 27 Aprili, 1985 Julius Kambarage Nyerere, sasa akijulikana kama Baba wa Taifa, katika sherehe kubwa katika viwanja vya Ikulu, alitoa jumla ya medali 3979 kwa Watanzania waliochangia katika maendeleo ya taifa.

Kati ya wale ambao walipewa medali hizo alikuwa Sheikh Abdallah Chaurembo.

Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima.

Baada ya siku chache kupita, Nyerere kama mtu aliyegutuka alimualika Dossa Aziz Ikulu.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes).

Swali hili hata mimi linanitaabisha hadi leo.


View attachment 2894722
Dossa Aziz akitunikiwa medali na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere​
Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima.

Hili ndo swali ambalo wewe ungekuja na majibu yake watu wangekuelewa tofauti na hapo ni kama unarusha jiwe gizani
 
Nyerere nikiongozi mpumbavu tuh kwa asilimia kubwa, mroho wa madaraka hakuwa na mipango mizur ya wapi kuipeleka nchi yake, wakamjengea jina na cheo kisha wakaanza kumuabudu kama ilivyo sasa, sijaona impact yyte kiuchumi kwa nyerere kuzid kumuenzi nikuzid kusifia upumbavu wake
 
Wazalendo waliotajwa ndani ya kitabu hiki ambao walipigania uhuru wa Tanganyika, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa katika orodha ile ya heshima.

Hili ndo swali ambalo wewe ungekuja na majibu yake watu wangekuelewa tofauti na hapo ni kama unarusha jiwe gizani
Chan...
Nije na jibu kwani mimi ndiye niliyewafuta katika historia?

Mimi baada ya kuona hayo majibu yangu kwa historia hiyo iliyokuwa na upungufu mkubwa ni kitabu nilichoandika nikawataja wale waliofutwa.

Leo tuko hapa tunaijadili historia hii.
 
Chan...
Nije na jibu kwani mimi ndiye niliyewafuta katika historia?

Mimi baada ya kuona hayo majibu yangu kwa historia hiyo iliyokuwa na upungufu mkubwa ni kitabu nilichoandika nikawataja wale waliofutwa.

Leo tuko hapa tunaijadili historia hii.
Tuondoe mambo ya walikua dini gani swali ni kwanini hawakutajwa na walipigania uhuru
 
Back
Top Bottom