Juma Nature ndio best storyteller wa muda wote Bongo. Wasanii wachanga mnao-rap jifunzeni kwa Juma Nature

Juma Nature ndio best storyteller wa muda wote Bongo. Wasanii wachanga mnao-rap jifunzeni kwa Juma Nature

KILA ZAMA NA MFALME WAKE, SIKU HIZI WAMEUFANYA MZIKI RAHIS SANA

ETI WE MPELEKEE MOTO, UNAUA VIBE, SIJUI NIKAGONGEE NYAGI, SPONSOR NIACHIE MY WANGU, MARA PWAA PWAA PWA
 
[emoji523] Kwa sasa amna anaeweza kutoa kazi nchi ikashituka vipi kuhusu =Rapcha-Lissa

[emoji523] Kwa upande wangu MCs na storyteller bora kuwahi kutokea bongo ni Dizasta Vina

Lisa ngoma kali sana Rapcha kaonyesha uwezo wa juu pale.

Nimemjua Dizasta Vina last December jamaa anajua, ana uwezo mkubwa sana wa kuandika na ladha ya tofauti sana ambayo ni kama yake peke yake.

Bongo tumebarikiwa wasanii wakali sana hasa wa michano kila msanii ukimsikila ana ladha yake ya kipekee.
 
[emoji523] Kwa sasa amna anaeweza kutoa kazi nchi ikashituka vipi kuhusu =Rapcha-Lissa

[emoji523] Kwa upande wangu MCs na storyteller bora kuwahi kutokea bongo ni Dizasta Vina
Jamaa anasema eti dizasta ni msanii wa WhatsApp
 
DIZASTA VINA ANASIKILIZWA KWENYE WHATSAPP?
Mkuu nisaidie na mimi hapo
Sinaga muda wa kudownload nyimbo ila huwa nazisikia kwenye Tv/Radio na sehemu za starehe

Mfano tuchukulie wana Hip Hop wa zama hizi

Ngoma kama Wapolo, am leaving my life, Si wanataka kubang 😂😂, Maisha na Muziki, na nyimbo za Mcs kibao kama Young Lunya, msodoki nk nk zikitoka tu utazisikia radio na kwenye tv muda wote, ukipanda bajaji au dalala utazisikia, ukienda club ndio usiseme, ukiingia saluni au simu za vijana utazikuta, ukienda youtube unakuta viewers 1m+

Ukija sasa kwa hawa Mcs ambao wanasifiwa sana sana humu JF kama Akina Dizasta, Nikki Mbishi, Rapcha. nk nk nyimbo zao huwa zinapigwa wapi? Hazisikiki radioni au kwa uchache sana ukitoka, huzi sikii club, bajaji, saloon, wala kusikia labda Rapcha ana shows mikoani nk
Ukienda youtube unakuta viewers wachache sana
Cha ajabu ni kwamba wala nyimbo zao hazina matusi sana kama kabda za Lunya

Ukitembelea page zao sasa unakuta wana wafuasi wachache lakini wanavyo wanwagia sifa ni balaa
Na wengi wao kazi yao ni kupost kuponda akina Lunya na wengine wanaokimbiza mainstream
Na wengi wao wanauza nyimbo zao kwa Whatsap

Tatizo ni nini
Nahisi kunatatizo kwa hawa jamaa
Ndio maana wengi tunaona wanasikilizwa Whatsap

Kwa mtu kama mimi ambaye sina muda wa kudownload nyimbo nategemea Media zipige ndio niujue wimbo na kuupenda au la, hawa jamaa hawana nafasi kwangu
Trust me mkuu hivi ndivyo soko la muziki lilivyo........ kuusikia wimbo kwenye media kisha unakua mkubwa

Sisemi kama hawajui kuimba, hapana
Ila post hii wanachakujifunza, Enzi hizo Mcs walikua wasomi au walioishi mbele kama kundi la KWANZA UNITY, Nature alichofanya aka connect na uswazi wake watu wakamuelewa..... alikimbiza vibaya sana
Ni lazima ujue pia hadhira yako inataka nini badala ya kukomaa na culture ambayo hata wamarekani wenyewe imewashinda
 
Mkuu nisaidie na mimi hapo
Sinaga muda wa kudownload nyimbo ila huwa nazisikia kwenye Tv/Radio na sehemu za starehe

Mfano tuchukulie wana Hip Hop wa zama hizi

Ngoma kama Wapolo, am leaving my life, Si wanataka kubang 😂😂, Maisha na Muziki, na nyimbo za Mcs kibao kama Young Lunya, msodoki nk nk zikitoka tu utazisikia radio na kwenye tv muda wote, ukipanda bajaji au dalala utazisikia, ukienda club ndio usiseme, ukiingia saluni au simu za vijana utazikuta, ukienda youtube unakuta viewers 1m+

Ukija sasa kwa hawa Mcs ambao wanasifiwa sana sana humu JF kama Akina Dizasta, Nikki Mbishi, Rapcha. nk nk nyimbo zao huwa zinapigwa wapi? Hazisikiki radioni au kwa uchache sana ukitoka, huzi sikii club, bajaji, saloon, wala kusikia labda Rapcha ana shows mikoani nk
Ukienda youtube unakuta viewers wachache sana
Cha ajabu ni kwamba wala nyimbo zao hazina matusi sana kama kabda za Lunya

Ukitembelea page zao sasa unakuta wana wafuasi wachache lakini wanavyo wanwagia sifa ni balaa
Na wengi wao kazi yao ni kupost kuponda akina Lunya na wengine wanaokimbiza mainstream
Na wengi wao wanauza nyimbo zao kwa Whatsap

Tatizo ni nini
Nahisi kunatatizo kwa hawa jamaa
Ndio maana wengi tunaona wanasikilizwa Whatsap

Kwa mtu kama mimi ambaye sina muda wa kudownload nyimbo nategemea Media zipige ndio niujue wimbo na kuupenda au la, hawa jamaa hawana nafasi kwangu
Trust me mkuu hivi ndivyo soko la muziki lilivyo........ kuusikia wimbo kwenye media kisha unakua mkubwa

Sisemi kama hawajui kuimba, hapana
Ila post hii wanachakujifunza, Enzi hizo Mcs walikua wasomi au walioishi mbele kama kundi la KWANZA UNITY, Nature alichofanya aka connect na uswazi wake watu wakamuelewa..... alikimbiza vibaya sana
Ni lazima ujue pia hadhira yako inataka nini badala ya kukomaa na culture ambayo hata wamarekani wenyewe imewashinda
Well uko sahihi audience na content anayotoa ni vitu viwili tofauti. Tamaduni Muzik, Kikosi Kazi, Ghetto Ambassador, Dizasta Vina and the likes wanaimba "ngumu sana" yaani zile nyimbo ambazo unatumia akili sana kung'amua lyrics na verse zake., kitu ambacho kwa wabongo walaji (fans) hawataki kuumiza kichwa... Wanataka ile kitu inachezeka kidogo na inasound

Na kwa upande wa media baadhi ndio wanasupport hizi kazi zao na tena unakuta wanaziplay kidogo sana tofauti na hizi nyimbo simple tu na hata kule mjini youtube viewers ni wachache mno sana kwa hiyo ndio sometimes wanaganga njaa kwa whatsapp na email hivyohivyo kibishi

Halafu EMcees wengine wameona ni bora waswitch style kutoka hardcore kwenda laini kwa sababu ya soko ndio linatoka hivyo, ukiimba ngumu utaishia kusikiliza huko ghetto na huko vilingeni kwenu lakini kuja kutoboa sahau! Ni wachache sana wanaoweza kutoa hit ambayo itatikisa Tz nzima kila mahali inachezwa
 
Huyo dizasta akaandike kitabu hii ni sanaa huwezi kufanya delivery kama unatusomea kitabu.

Skills hana wala mistari ya maana.

Wewe utakuwa wale masela wanajiita watunza misingi [emoji23][emoji23]
Eti "... Skills hana wala mistari ya maana... "
Labda kama unaongea kinyumenyume.
 
Eti "... Skills hana wala mistari ya maana... "
Labda kama unaongea kinyumenyume.
Yule ni mwandishi wa vitabu talent yake ipo uko, huu ni muziki uwezi kutuletea manyimbo yana part 1 mpaka part 8 ukimsikiliza kama unaperuzi kurasa 😂😂😂😂

Sikiliza maisha ya boarding ya JMo au Mikasi ya Ngwea ukafundishe watunza misingi ni nini storytelling.
 
Kwenye muziki wa hiphop bongo hakujawahi kutokea msanii mwenye nguvu kama Juma Nature.

Juma Nature aliingia kwenye muziki akaukuta umejaa umarekani mwingi na akaubadilisha mchezo kabisa. Silaha yake kubwa ilikuwa ni storytelling.

Ipo wazi Juma Nature ndio bingwa wa storytelling kibongobongo. Alianza na story ya kigheto ghetto mpaka simulizi za ex wake Sinta. Na alivutia kwa sababu alitumia ucheshi na lugha za uswazi.

Kwa sasa muziki wa bongo unafanya vizuri kwenye waimbaji ila upande wa rap ni kama umekufa. Kwa sasa hawezi simama rapa akachana nchi ikastuka.

Shida kubwa marapa wa sasa wamewekeza kwenye mistari konde yani ufundi wa kugeuza geuza mashairi na wengine wameingia kwenye trap wanajikuta kina Dababy au Migos hakuna localisation.

MCs wadogo jifunzeni kwa Juma Nature aliingia kwenye game na silaha yake kubwa ilikuwa kuelezea story haswa za uswazi. Aliisimamisha mitaa akawa jina la mchezo.

Jifunzeni storytelling... hakuna mwanadamu anayeweza kuukwepa mtego wa story kila binadamu anapenda kusikia visa mbalimbali.

FA alitupa kisa cha aliyekufa kwa ngoma... Profesa akatuletea mwanasiasa muongo muongo kwenye ndio mzee... Ngwea akatupa story za ghetto lake.... J Mo akatupa mawili matatu kuhusu mabalaa ya mvua na jua...Nature ndio aliua kabisa akatusimulia Mzee wa Busara, Drama za Sinta. Mtoto Iddi nk

Hii ndio siri pekee nataka niwape vijana wadogo mnaoingia kwenye muziki wa hiphop kama mnataka kutengeneza pesa...Hakikisha unachokiandika hata yule beki tatu anaeosha vyombo nyumbani anaweza kuvutiwa na kukiimba.

Maisha ya binadamu ni hadithi.

Lakini msiandike story kama mtu anasoma kitabu cha Shigongo. Andaeni content zenye ubunifu wa kimuziki. Hii ndio siri ya Juma Nature kuubadili mchezo na akaibeba Temeke mabegani, Storytelling.

Akitokea storyteller wa rap kuna pesa yake nyingi sana ya kubadilisha maisha yako na family yako.
Kasikilize kiberiti nyimbo ya fid q, hiyo juzi.. Au tafuta nyimbo yake yeyote... Sikiliza.. Ndio utajua hip hop ni nini....
 
Kasikilize kiberiti nyimbo ya fid q, hiyo juzi.. Au tafuta nyimbo yake yeyote... Sikiliza.. Ndio utajua hip hop ni nini....
Hakuna kitu unaweza nifundisha wewe kuhusu hiphop, hapa bongo hiphop imepokelewa sebuleni kwetu.
 
Kwa ujumla wapo wasanii wa Hip Hop waliofanya vizuri sana lakini hadi leo hii hakuna mwana Hip Hop yeyote aliefanikiwa kuwashika washabiki wa muziki kama Juma Nature aka Kibla aka Kiroboto.......... HAKUNA

Hapa hatuzungumzii ubora wa mashairi au nguzo za Hip Hop......... hapa tunaongele Mc aliyekuwa anapendwa sana na kujizolea mashabiki lukuki

Katika historia ya muziki wa Tanzani ni kawaida sana kusikia mwana bongo fleva kama Ali kibakuli, Domo, Marioo, Nandy, Konde nk wakipiga show popote pale Tz na kujaza uwanja lakini sio kwa mwana Hip Hop, ila hii haikuwa hivyo kwa Kiroboto enzi za uhai wake kisanii

Kiroboto alikua ni gumzo tena enzi hizo hakuna social media ilikua ni magazeti ya udaku tu
Watu walimfuatilia Kibla kama unavyoona nyakati hizi anavyofatiliwa Domo
Habari za Kibla na Sinta ilikua ni zaidi ya Domo na Zari, kila alichofanya au kuimba Kibla ilikua ni habari kubwa

Alijaza shows zote mikoani Kibla kama Kibla na sio lundo la wasanii kama Fiesta
Uzinduzi wa Ugali pale Diamond Jubilee itabaki kuwa historia isiofutika

Yalikuwepo na yalikuja majina makubwa sana kwenye Hip Hop Tz, 2proud, Ay Fa, Prof Jay, Fid Q, Afande Sele,Gk, Ngwea, Ulamaa,Insp Haroon, Joh Makini, nk nk lakini hakuna hata mmoja aliyefanikiwa kuwashika washabiki kama Juma Nature
Sasa hivi kuna wasanii wazuri wa Hip Hop lakini wanaelezeke vizuri sana kwenye kuwachambua ubora wao LAKINI sio kwenye kuwashika mashabiki
Kibla ndio wasanii wa kwanza kwanza kuanza kuteuliwa kwenye tuzo za channel or Mtv kama sijajosea

Nakumbuka tulienda uzunduzi wa albamu ya Ugali pale Jubilee na washkaji tukaishia kukaa nje ya ukumbi hadi show ikaisha
Nyomi lililokuwa pale ni hatari halafu sasa watoto wa uswazi tu full uhuni yani

Nature na Mr Nice enzi za uhai wa sanaa zao itabaki kuwa historia
Na tena angalau Mr Nice tunaona wakina Diamond wanavunja rekodi zake lakini kwa upande wa Hip Hop Kiroboto hakuna mwana Hip Hop amevunja rekodi zake
 
Back
Top Bottom