JWTZ kuwatesa raia wanaovaa nguo za Jeshi ni ukatili

JWTZ kuwatesa raia wanaovaa nguo za Jeshi ni ukatili

IMG-20230830-WA0036.jpg
 
Hivi kwa huu unyama unaotendeka hapa chini hili linafaa liitwe jeshi la Wananchi wa Tanzania au jeshi la Maharamia dhidi ya wananchi wa Tanzania?

CDF haya ndio mafunzo mnaowapa vijana wenu dhidi yetu Watanzania wenzao?

Ni sheria gani ya nchi na hapo jeshini inaruhusu huu upuuzi unaofanywa na hawa makamanda dhidi ya huyu mtu ?

Hivi hawa askari wanatengeza chuki gani kati ya jeshi na wananchi?

Naomba hatua za kisheria zichukuliwe kwa hawa makamanda wote waliofanya huu upuuzi.

Wamewekwa busy wasichukue nchi kama kule Niger na Gabon leo
 
Sahihi sana mkuu, vita kuu ya pili ya dunia boats za raia zaidi ya 850 zilikwenda kuokoa askari wa Uingereza na allies ambao tayari walikuwa wamezungukwa,
Zaidi ya skari 336,000 waliokolewa, Operation Dynamo, inaitwa Miracle of Dunkirk, yalikuwa ni maajabu, jeshi la Hitler tayari lilikuwa karibu kuwamaliza askari hao na hawakuwa na mahala pakutokea, lakini kwa upendo wa wananchi waliamua kujitolea kwenda kuwakomboa askari hao, hata hivyo jeshi la Hitler lilijitahidi kuzuia uokozi huo lakini ndio hivyo kwa moyo waliokuwa nao wananchi wakashirikiana na jeshi hatimaye wakafanikisha operation hio ambayo haiwezi kusahaulika Miracle of Dunkirk.
Mfano mwingine tena, jeshi la Marekani wakati linafanya recruitment ya wanajeshi wa kupigana vita ya pili ya dunia kuna vijana wengi walikuwa na miaka 17 na 16 wako under age walidanganya umri wao, idadi yao ni kama 200,000.

Jeshi la Marekani muda wote hushawishi raia kwamba ni sehemu muhimu ya nchi, ni wajibu wa kila mwananchi kulinda nchi yake na jeshi ni kwa ajili yao. Watoto shule za Marekani wakitaka kutembelea kambi ya jeshi wanapokelewa na uongozi wanatembezwa kama kuonyeshwa silaha na kazi zake. Kuna career days wanajeshi wanaenda shule wanauliza nani anataka kuwa mwanajeshi na kufafanua branches za jeshi na kazi zake
1000w_q95.jpg


Hii ni Youth Army ya Urusi
1tLCl3iixXDH2XFrb4JVG5A.jpeg


Uko Israel na South Korea ndio usiseme maana almost kila mwenye afya aliwahi pitia jeshini. Kukutana na fundi seremala ambaye ni Sergeant ndani ya Israel ni kawaida, nchi ina watu wachache na maadui kila kona hivyo raia wote wanajua kupigana. Humtishii mtu na mabuti yako.

Nchi kama hizo zikivamiwa raia hujiona ni wanajeshi na wanajua cha kufanya sio kuanza kufundishana muda huo. Na sio kuanza kuogopa na kuona jeshi ni sehemu ya ukorofi, fujo, ugomvi na uonevu.
Tafsiri ya kuwa mwanajeshi kwa nchi nyingine maana yake discipline yako iko juu, utu wako uko juu, uelewa wako wa kisheria uko juu. Ukienda club ukajitambulisha mwanajeshi hakuna anayekuwa na wasiwasi kwamba utafanya fujo. Hakuna anayekutegemea utachukua sheria mkononi.

Njoo huku sasa mtu akikosa kazi ndio analazimisha kujiunga jeshi, uko akivaa buti anarudi kibanda umiza kulazimisha ugomvi. Sisi mwanajeshi kwa haraka haraka honestly tuna wasiwasi ni mlevi, mzinzi, hana financial discipline, mapenzi yanamtesa hajui kuchagua mke wa kuoa. Tafrani tu
 

Attachments

  • 1tLCl3iixXDH2XFrb4JVG5A.jpeg
    1tLCl3iixXDH2XFrb4JVG5A.jpeg
    99.3 KB · Views: 6
Mbona sioni mateso yoyote hapo, naona kama anawekewa alama kwenye ubongo wake kuziogopa kabisa nguo za jeshi, madhara ya hizi nguo ni mabaya kweli zinapokuja kuvaliwa na watu washenzi.
 
Mbona sioni mateso yoyote hapo, naona kama anawekewa alama kwenye ubongo wake kuziogopa kabisa nguo za jeshi, madhara ya hizi nguo ni mabaya kweli zinapokuja kuvaliwa na watu washenzi.
Watu washenzi kwani huzivaa wakati wa mchana ? Huwa wanazifaa wanapo enda fanya ushenzi wao
 
Kuvaa nguo za kufanana na zao ni kosa sawa hatukatai lakini Sheria gani inawapa mamlaka ya kupiga watu kisa wamevaa hizo nguo 🤔🤔 kwamba wao ni mahakama na mahakimu wanatoa hukumu 🤔🤔
 
Hivi kwa huu unyama unaotendeka hapa chini hili linafaa liitwe jeshi la Wananchi wa Tanzania au jeshi la Maharamia dhidi ya wananchi wa Tanzania?

CDF haya ndio mafunzo mnaowapa vijana wenu dhidi yetu Watanzania wenzao?

Ni sheria gani ya nchi na hapo jeshini inaruhusu huu upuuzi unaofanywa na hawa makamanda dhidi ya huyu mtu ?

Hivi hawa askari wanatengeza chuki gani kati ya jeshi na wananchi?

Naomba hatua za kisheria zichukuliwe kwa hawa makamanda wote waliofanya huu upuuzi.

Zamani nilikuwa mjinga sana nilikuwa ninawatetea sana wanajeshi kabla ya kugundua kuwa wengi wao ni watu wa hovyo sana.
 
Haikubaliki kuchukua sheria mkononi ila na raia pia wakumbuke hawaruhusiwi kuvaa nguo za jeshi.

Majeshi yetu yana udhaifu kwenye kufanya good judgement kwahiyo sio vizur kuwa provoke, unaweza kufa kirahisi sana
Mbona wanafunzi wanavaa suruali za kaki na kijani? Au yale sio mavazi ya majeshi yetu?
 
Sa hapo mateso yako wapi, we unajua wanachopitia mpaka wanavaa bakabaka, heshimu kazi ya watu afu hizo nguo usivae utaumia
 
Back
Top Bottom