Kabla hujanunua Azam TV pitia hapa; Usije kujuta

Kabla hujanunua Azam TV pitia hapa; Usije kujuta

mkuu Fanya utafiti wa kina kabla ya kununua usije nunua Azam kwa mategemeo makubwa ukaambulia patupu! Jaribu kuangalia Zuku maana wana afadhali! ila jiridhishe kwanza

kabla ya kununua zuku akae akijua kua mwisho wa mwezi ukifika wanakomba channel zote hakuna cha locals wala loko
 
Mvua ikinyesha kidogo chanel zote zinakata hazionyeshi
 
Hivi haiwezekani kuangalia TV yoyote duniani through internet?. Natamani sana hii kitu, sema internet yenyewe TZ bado sio stable.
 
Azam wamelewa sifa

chanel e wameondoa tu bila kujali wateja wake

za kihindi ndo wamejaza kuliko za aina zingine
ajabu unazipata hata kama huzilipii..

mpira hata chan tu au cecafa hakuna
kuna ndondo cup tu na vodacom...

azam washajifanya 'wamefanikiwa'
Kwa kuiondoa ETV Africa kunanifanya nirudi kwenye Startimes ambako nitawaona kina Roman Reign na Dean Ambrose na WWE yao,

Kwa heri Azam TV
 
Mimi nina mawazo tofauti kidogo, sijaona king'amuzi ambacho kinakurudishia thamani ya pesa yako kama cha azam, kwanza kiko unlocked na uwezo wa kufungua FTA channels japo si zile zenye BISS kEYS etc, na kama ukichoka huduma za azam unabadilisha tu uelekeo wa dish na kunasa zingine, kina kidhi thamani ya pesa zako
 
Ni matumaini yangu kuwa wengi ni buheri wa afya na manaendelea vema na majukumu ya kila siku!

Ukweli kuwa wengi wetu tuna mategemeo makubwa kutoka Azam tv tofauti na ukweli ulivyo...

Lengo la Uzi huu si kuharibu biashara ya Azam Bali kueleza uma ukweli halisi wa mambo!

So nitaelezea mambo muhimu ya kuyafahamu kabla ya kununua Azam TV.

1. Bei ya decoder hubadilika wakat wowote bila taarifa! mwezi wa 1,2016 nimenunua 140,000 hadi sasa tar 7 Marc imefika 170,000.

2. Channel ya kawaida tuu kama BBC, Fox, CNN, AL-Jazeera, France 24, mpaka ulipe 20,000 kwa mwezi.

3. Sinema zetu utapata bongo movie za 2005 kushuka chini Mara nyingine movie hurudiwa kwa week Mara 3, No latest movie ujue hivyo!

4. Organization ya channel iko hovyo! Unaweza kulipwa kifurushi cha 12,000 lakini kupata channel moja hadi nyingine ni shughuli! Channel za kihindi tu ndo ziko pamoja!

5. Tegemea kupata channel kibao za kiarabu na nyingine zisizoeleweka ni lugha gani!

6. Wapenzi wa channel "e" mujue kuwa haipo Azam TV!

7. Ukienda kununua watakuambia vipeperushi vya list za channel na bei ya vifurushi vimeisha maana wanajua ukiangalia channel zao na bei utaghairi kununua" maana haviendani!

Thanks..
Azam TV wanaboa sana,hata presenters wao wanaboa sana, sidhani kama wote ni professionals
 
Mi nimefunga geto na nalipia Azam Sport Hd ili niwe namuona Mess tu maana ndie anayenifanya niangalie kila game anayocheza Barca ila lasi yeye HD wasingeniona…

Mipira imenifanya nitumoe Azam tv nikiangalia LIGA BBVA na VPL kwa Yanga yangu basi nabirudika sana lakini hawako fair kwenye bei kwa maana ile elfu 15 ya Azam Sport HD haina maana kutuwekea chanel ya Azam sport Hd na zile za Manchester Unt, Liverpool na Real Madrid tu pale ilitakiwa Ukilipia kile chanel zote za.michezo zifunguliwe kama Kombat Sport, Fox zote na etc yaani kulipia 15 elfu kwa Azam Sport Hd sawa umenunua Chanel moja tu maana zile nyingie na Man u, Liverpool na Madrid hazina maana huwa hazionyeshi ata mipira live
 
sasa mbona mnatuchanganya. anyway ni angalizo zuri
 
Mi nimefunga geto na nalipia Azam Sport Hd ili niwe namuona Mess tu maana ndie anayenifanya niangalie kila game anayocheza Barca ila lasi yeye HD wasingeniona…

Mipira imenifanya nitumoe Azam tv nikiangalia LIGA BBVA na VPL kwa Yanga yangu basi nabirudika sana lakini hawako fair kwenye bei kwa maana ile elfu 15 ya Azam Sport HD haina maana kutuwekea chanel ya Azam sport Hd na zile za Manchester Unt, Liverpool na Real Madrid tu pale ilitakiwa Ukilipia kile chanel zote za.michezo zifunguliwe kama Kombat Sport, Fox zote na etc yaani kulipia 15 elfu kwa Azam Sport Hd sawa umenunua Chanel moja tu maana zile nyingie na Man u, Liverpool na Madrid hazina maana huwa hazionyeshi ata mipira live

kweli mkuu zile channel za Man U ,Liverpool na Madrid hazina maana! ni kutangaza timu zao tuu!!!!hakuna mech ya live labda za watoto
 
Kwa kuiondoa ETV Africa kunanifanya nirudi kwenye Startimes ambako nitawaona kina Roman Reign na Dean Ambrose na WWE yao,

Kwa heri Azam TV

tupo pamoja
 
Mkuu kunasiku nilibeba pesa kabisa kununua, asee baada ya kufika kwa muuzaji, wakara akanipigia hesabu ikafika 230000, na hicho ni kifurushi cha 12000, asee nlirudi na kuendelea na king'amzi changu cha startimes, maana nliona ni uhalooo mtupu, bei zao zinabadilika kama kinyonga, tena ukienda umevaa tai hata laki3, wanakugonga,

Kibaya zaidi hao wauzaji, asee wanampozi balaa, nlimkuta dada mmoja pale kimara mwisho kama unaenda sokon duh, ni shidaaaa, ila walekebishe bei na vifurushi, kisha hao wauzaji wafundishwe kuongea na wateja..

Halafu bei ya kufunga hlo dishi et 30000, jaman huu ndo ujasiliamali,? Halafu nikamwambia basi niuzie nnafundi wangu, akaniambia kikiharibika hawatahusika, mpaka leo sitaki kuwasikia azam, mpra ntaangalia ukumbini, newz itv na startive
Kuhusu wauzaji, Tanzania tuna shida sana eneo la custommer care
 
kwa hela unayolipa unastahili kupata chaneli hizo, elfu 15! unataka kuona epl, la liga, vpl da wewe umezidi bana! kwa hela hiyo labda ufunge cable. Watu hawana shukurani badala ya kuwashukuru azam mnawashutumu, njooni huku dstv kwenye ubora mnaoutaka.
 
Back
Top Bottom