Kabla ya kuja watu weupe waafrika tuliamini uwepo wa Mungu ila hatukuamini uwepo wa shetani

Kama unamuamini Mungu wa kweli, sasa kabuli la babu yako nila nini?? unaenda kutafuta nn??
mtu aliyekufa anaweza kukusaidia kitu..? wakati yupo huko na yeye anasubr hukumu yake.


NAONA UNAFANYA OPOTOSHAJI TU
Unapomuomba Yesu na Bikira Maria wakusamehe dhambi zako je unatofauti gani na hao wanaowaomba wapendwa wao??

Tenaa wewe unawaomba watu wasiokua na nasaba ya ukoo wako
 
Vipi ambao walikufa bila kuijua iyo kweli Mungu anawajibika nao vipi mkuu? Atawaacha wale bata mbinguni kwa sababu hawakuwa na taarifa au atawatupa motoni maana hawakumfata?
 
Unapomuomba Yesu na Bikira la Maria wakusamehe dhambi zako je unatofauti gani na hao wanaowamba wapendwa wao??

Tenaa wewe unawaomba watu wasiokua na nasaba ya ukoo wako
Futa hiyo Maria kwanza ndio twende sawa.
 
Mungu (nguvu kuu) kila jamii ilikuwa na namna yake yakumfikia mungu (nguvu kuu) katika dunia nzima, kwetu afrika tulikuwa na njia zetu za kumfikia mungu na kutusaidia

Mizimu ni watu wema au mababu zetu waliokufa lakini katika uhai wao walikuwa watu wema walikuwa machifu,waaguzi,walinzi wa ukoo,watabiri n.k hawa watu roho zao hubaki katika ulimwengu kusaidia jamii zao husaidia kwakuwa wapo karibu sana na nguvu kuu( mungu) ndomana wakiombwa na kukumbukwa na jamii zao husaidia bila shaka lolote

Lakini pia kuna mizimu mibaya mababu zetu waliokuwa wachawi,wasaliti,walozi nao pia roho zao hua zinabaki duniani kuendeleza mambo yao waliowaachia mikoba huwaomba wawasaidie kazi zao za uchawi na ulozi na huwasaidia pia

Note: kila jamiii ina namna yake yakumfikia mungu (nguvu kuu) maamuzi ni yako kufata jamii yako ili umfikie mungu au kufata jamii nyingine wazungu,waarabu,wachina,waizraeli n.k ili umfkkie mungu(nguvu kuu)


_mzoma
 
Amini nakwambia SIKU UTAKaYOKUFA HUKO UENDAKO UTAKUTANA NA WATU ULIO WAACHA DUNIANI, Utajua Mungu alioo uliza adam uko wapi ilikuwa na maana ipi.
PILI nikumbe mm halafu ukaabudu miungu mingine huyo utaratibu hata kwa mdudu mwenye hekima ndogo kama ya nyuki HAKUBALI.Christ mwenyewe alipimwa imani na ni pure God blood sasa Ibrahim ni Nani!?

Huo uzao wa kwanxa kasome vizur(Angel of Death,Among of the First order angels of God) ulivo mnafik huuliz kifo cha mtoto wa farau
 
Bikra maria bado yupo hai au sio???

Halafu anakuwaje bikra wakati alikwisha zaa???
Kuhusu Kuabudu bikira maria ilo mbona liko wazi ni Ni ufedhuli unao fanywa na makanisa ya kiroma wabudu sanamu.
pili aliitwa bikira keasababu alibeba mimba bira kumjua mwanaume
 
Yan umetulia kabisa una andika mizimu ni watu wema kwel??! Mizimu si watu tena ni nafsi za wafu uwe mwema uwe mbaya. Na haiwez kusaidia chochote
 
Waliwezaje kuwasaidia mababu zetu..? Wazungu wameshakuloga
Wazungu wameshimamisha SANAMU ya mbuzi, sasa huoni mm na hao ni tofati.
Nikwambie jambo rafiki, ambayo kwa sasa hata mitaani kwenu utayaona. Familia zote zenye asili uganga wa kienyeji au uchawi ndo hua zina sumbuliwa na pepo walio weka magano na marehemu kipindi akiwa hai na Mtu agano lake lilipo ndo mauti yake ilipo,na kizazi cha kwake hadi za nne ni mali ya mkuu wa pepo na muhusi juu,
Sasa kinacho tokea pepo wanachukua sura na sauti ya mareheru kukutaka ww ufanye au uendeleze alicho kuwa anafanya marehem sasa utasema Huu ni mzimu wa marehemu.?Hahafu zamani jamii nzima itafuata kila kitu chief atacho taka usidhani mababu wote walikuwa wanapenda kwa hiyo ukitaja mababu walikuwa hivi usijumuishe wote,Amini na kwambia tungepata story za miiko na sheria za kafara za kila kabila na chief na miungu yao nakwambi kwa free will ww unge kimbia, Kazome kwenye Miti mikubwa na mapango kuna nn waulize waganga na wachawi wanajua, kuwa makin
 
Vipi ambao walikufa bila kuijua iyo kweli Mungu anawajibika nao vipi mkuu? Atawaacha wale bata mbinguni kwa sababu hawakuwa na taarifa au atawatupa motoni maana hawakumfata?
Ni jukumu la kwanza na la juu kabisa la kila kiumbe mwenye akili kujifunza
kutoka katika Maandiko ukweli ni nini, na kisha kutembea katika nuru na
watie moyo wengine wafuate mfano wake. Tunapaswa kujifunza siku baada ya siku
Biblia kwa bidii, ikipima kila wazo na kulinganisha andiko pamoja na maandiko. Kwa msaada wa Mungu tunapaswa kuunda maoni yetu
sisi wenyewe kama ambavyo tunapaswa kujibu wenyewe mbele za Mungu. - E .G White ( The Great Controversy)

Kitafute hiki kitabu, kitakusaidia sana katika maswali mengi yanayohusu imani yako na Mungu.
 
Kuhusu Kuabudu bikira maria ilo mbona liko wazi ni Ni ufedhuli unao fanywa na makanisa ya kiroma wabudu sanamu.
pili aliitwa bikira keasababu alibeba mimba bira kumjua mwanaume
Na wewe unaamini alibeba mimba bila kuto*bw*??
 
Mzimu ni marehemu, ambapo Kiafrika kiasili tuliamini kuwa wafu wapo karibu na Mungu hivyo tulikuwa tunaomba mizimu utusaidie maana wao wapo karibu na Mungu. Ni sawa na Wakatoliki wanavyoamini katika saints.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…