Kama kipato chako ni chini ya milioni Tano kwa mwezi wewe ni Maskini

Kama kipato chako ni chini ya milioni Tano kwa mwezi wewe ni Maskini

Kwa hiyo bwana Robert haya ni maoni yako na mtazamo wako tu si uhalisi? Kwamba mtu anaepata 5m kwa mtazamo wako ni nasikini ila si uhalisia?

Umaskini na utajiri ni dhana aliyonayo mtu.
Ni mtazamo tuu.
Wapo Watu wanajiona matajiri na hawajawahi kushika pesa hata shilingi mia moja.

Umaskini wa Ulaya na umaskini wa Afrika ni tofauti.
Umaskini wa mjini na maskini wa kijijini ni tofauti.
Tukija kwenye uhalisia (mantiki), kwenye mantiki jambo likiwa kweli sehemu A lazima liwe kweli sehemu B.

Ni maoni na mtazamo tuu. Ndio maana humu kila mmoja anakuja na vile ajuavyo.
Ila wapo wale wafuatao upepo yaani waliokariri maoni na mitazamo ya wengine hasa wasomi waliozoea kukaririshwa na kupuuzia maoni na mitazamo yao
 
Hata hizo Data au takwimu ni mitazamo ya Watu.

Ni sawa na aliyesema maskini ni yule anayeishi chini ya dola moja. Huo ni mtazamo wake. Na sio Fact. Kwa sababu zipo jamii zimaishi vizuri pasipo kutumia pesa hata shilingi moja.

Milo mitatu usifikiri ni hiyo iliyojaa wanga. Hapa tunazungumzia balanced diets, kisha gari kali ambayo mafuta hayasumbui, watoto wanasoma shule nzuri, mavazi ya kisasi, jumba zuri.
Haya embu niambie hiyo milioni tano inatosha nini hapo.

Ndio maana kwa nchi yetu mtu anayelipwa milioni tano hata TRA akifika kwake kuna maisha wakiona anayo lazima waseme ni mwizi.

Kwa sababu milioni tano ni maskini aliyechangamka.
Mkuu,
Haya ni maoni na mtazamo wako, hauna mchanganuo wowote, huwezi kumshawishi mtu kuamini unachoongelea. Ili umshawishi mtu kuwa anayepata 5m kwa mwezi ni masikini, lazima uje na vigezo, takwimu zikiambatana na idadi ya watu, eneo husika nk. Sasa wewe ukisema anayepata 5m ni masikini, huku ukisema hata mlo kamili hawezi kumudu, huna uhalisia, huna vigezo wala huna takwimu za kukusaidia na kutushawishi.

Mfano, ukisema mwenye 5m kwa mwezi hawezi kumudu hata mlo kamili, kwako milo kamili mitatu kwa siku ni milo gani, isije kuwa watu unaongelea frequencies tofauti za maisha, huenda unamaanisha kula milo mitatu Serena hotel, wakati sisi tunaongelea kuipa familia yako milo kamili mitatu.

Funguka.
 
Kwema Wakuu!

Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.

1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.

2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.

Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.

3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.

Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.

Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.

Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.

Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.

Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).

Ijumaa Kareem


Wewe ni mtu wa hovyo sana
 
Mkuu,
Haya ni maoni na mtazamo wako, hauna mchanganuo wowote, huwezi kumshawishi mtu kuamini unachoongelea. Ili umshawishi mtu kuwa anayepata 5m kwa mwezi ni masikini, lazima uje na vigezo, takwimu zikiambatana na idadi ya watu, eneo husika nk. Sasa wewe ukisema anayepata 5m ni masikini, huku ukisema hata mlo kamili hawezi kumudu, huna uhalisia, huna vigezo wala huna takwimu za kukusaidia na kutushawishi.

Mfano, ukisema mwenye 5m kwa mwezi hawezi kumudu hata mlo kamili, kwako milo kamili mitatu kwa siku ni milo gani, isije kuwa watu unaongelea frequencies tofauti za maisha, huenda unamaanisha kula milo mitatu Serena hotel, wakati sisi tunaongelea kuipa familia yako milo kamili mitatu.

Funguka.

Mlo kamili inafahamika, ujumlisha na mahitaji mengine muhimu kwa kiwango cha juu.
 
Andika ili hata asiyefahamu ajue mlo kamili ni nini na kwa siku familia ya kawaida ya watu watano inaweza kutumia shilingi ngapi kupata mlo kamili.
Mlo kamili ni moja ya mfano wa mahitaji ya mtu anayotakiwa kuwa nayo.
Mtu mwenye kipato cha milioni tano hana uwezo wa kula mlo kamili alafu muda huohuo asomeshe shule za kitajiri, awe na nyumba ya kifahari, alafu hapohapo aendeshe gari kali, alafu hapohapo, yeye na familia wavae nguo Standard,

Sasa wewe umekalia hapohapo kwenye mlo utadhani ndio hitaji Pekee
 
Kipato cha Dola 2000 Kwa mwezi..naona unastandard nzuri YA maisha japo WW Sio tajiri Ila upo kwenye good standard of life
 
Mlo kamili ni moja ya mfano wa mahitaji ya mtu anayotakiwa kuwa nayo.
Mtu mwenye kipato cha milioni tano hana uwezo wa kula mlo kamili alafu muda huohuo asomeshe shule za kitajiri, awe na nyumba ya kifahari, alafu hapohapo aendeshe gari kali, alafu hapohapo, yeye na familia wavae nguo Standard,

Sasa wewe umekalia hapohapo kwenye mlo utadhani ndio hitaji Pekee
I rest my case!
 
Duh hapa tunapeana presha na kupata mental illness!
Ila sawa mkuu...
Tutaishi hivyo hivyo....
 
Umaskini ni nini mkuu? Unapimwaje au unapimwa katika scale gani?
Mkuu wewe kama ukiwa huna mali za kuachia watoto wako na wajukuu wako siku ukiondoka hapa duniani wewe ni masikini. Achana na upumbafu wa kusema urithi wa mtoto ni elimu, achia watoto na wajukuu mali watayoiendeleza.
 
Kwema Wakuu!

Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.

1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.

2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.

Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.

3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.

Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.

Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.

Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.

Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.

Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).

Ijumaa Kareem
...Wewe uko Kundi Gani, Mkuu Mtibeti ?? [emoji848][emoji848]
 
Masikini ni mtu ambae hawezi kupata mahitaji ya msingi kama chakula,mavazi na malazi..

Kampeni iliopo duniani kwa sasa ni kupunguza masikini ila haimaanishi kuongeza matajiri kwa sababu kua tajiri sio hitaji la msingi la binadamu

Kama unasehemu ya kulala +unakula na kunywa+unapata mahitaji ya msingi Tambua kua unaendelea vizuri sana!! Hakuna kiwango cha fedha ambacho kinaweza kukutosheleza lakini hata wataalamu wamefanya tafiti kadhaa na kuthibitisha kua kama unaweza kutumia $5 kwa siku kwa nchi za kusini mwa Africa basi unaendelea vizuri..

Watz wengi wanakipato cha chini ya milioni1 kwa mwezi (sio nzuri na sio mbaya pia),Wenye kipato cha juu ya milioni 1>>> wengi bado wanaishi kwa kujibana sana..

Na hata ile 1% wanastress zao huko Masaki na Oysterbay
 
Back
Top Bottom