Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
- Thread starter
-
- #441
Kwa hiyo bwana Robert haya ni maoni yako na mtazamo wako tu si uhalisi? Kwamba mtu anaepata 5m kwa mtazamo wako ni nasikini ila si uhalisia?
Mkuu,Hata hizo Data au takwimu ni mitazamo ya Watu.
Ni sawa na aliyesema maskini ni yule anayeishi chini ya dola moja. Huo ni mtazamo wake. Na sio Fact. Kwa sababu zipo jamii zimaishi vizuri pasipo kutumia pesa hata shilingi moja.
Milo mitatu usifikiri ni hiyo iliyojaa wanga. Hapa tunazungumzia balanced diets, kisha gari kali ambayo mafuta hayasumbui, watoto wanasoma shule nzuri, mavazi ya kisasi, jumba zuri.
Haya embu niambie hiyo milioni tano inatosha nini hapo.
Ndio maana kwa nchi yetu mtu anayelipwa milioni tano hata TRA akifika kwake kuna maisha wakiona anayo lazima waseme ni mwizi.
Kwa sababu milioni tano ni maskini aliyechangamka.
Kwema Wakuu!
Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.
1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.
2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.
Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.
3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.
Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.
Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.
Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.
Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.
Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).
Ijumaa Kareem
Mkuu,
Haya ni maoni na mtazamo wako, hauna mchanganuo wowote, huwezi kumshawishi mtu kuamini unachoongelea. Ili umshawishi mtu kuwa anayepata 5m kwa mwezi ni masikini, lazima uje na vigezo, takwimu zikiambatana na idadi ya watu, eneo husika nk. Sasa wewe ukisema anayepata 5m ni masikini, huku ukisema hata mlo kamili hawezi kumudu, huna uhalisia, huna vigezo wala huna takwimu za kukusaidia na kutushawishi.
Mfano, ukisema mwenye 5m kwa mwezi hawezi kumudu hata mlo kamili, kwako milo kamili mitatu kwa siku ni milo gani, isije kuwa watu unaongelea frequencies tofauti za maisha, huenda unamaanisha kula milo mitatu Serena hotel, wakati sisi tunaongelea kuipa familia yako milo kamili mitatu.
Funguka.
Andika ili hata asiyefahamu ajue mlo kamili ni nini na kwa siku familia ya kawaida ya watu watano inaweza kutumia shilingi ngapi kupata mlo kamili.Mlo kamili inafahamika, ujumlisha na mahitaji mengine muhimu kwa kiwango cha juu.
Mlo kamili ni moja ya mfano wa mahitaji ya mtu anayotakiwa kuwa nayo.Andika ili hata asiyefahamu ajue mlo kamili ni nini na kwa siku familia ya kawaida ya watu watano inaweza kutumia shilingi ngapi kupata mlo kamili.
mm ni last born mkuuWe jamaa unapenda kujiliza sana
I rest my case!Mlo kamili ni moja ya mfano wa mahitaji ya mtu anayotakiwa kuwa nayo.
Mtu mwenye kipato cha milioni tano hana uwezo wa kula mlo kamili alafu muda huohuo asomeshe shule za kitajiri, awe na nyumba ya kifahari, alafu hapohapo aendeshe gari kali, alafu hapohapo, yeye na familia wavae nguo Standard,
Sasa wewe umekalia hapohapo kwenye mlo utadhani ndio hitaji Pekee
I rest my case!
Daaaaaah,Kwa hiyo unataka kusema kuwa mwanachi ana uchumi wake binafsi eti.Mzunguko wa biashara hujui ikoje au🤔.Wananchi vipato vyao viliathirikaje ?
Mkuu wewe kama ukiwa huna mali za kuachia watoto wako na wajukuu wako siku ukiondoka hapa duniani wewe ni masikini. Achana na upumbafu wa kusema urithi wa mtoto ni elimu, achia watoto na wajukuu mali watayoiendeleza.Umaskini ni nini mkuu? Unapimwaje au unapimwa katika scale gani?
masikini cv anaitoa wapi mkuu. hebu kuwa na hurumaKama wewe ni maskini njoo bandarini na CV yako, natafuta makuli.
Hahaha rich gang mentality. I approveKama huwezi kutengeneza atleast 1B kwa mwaka wewe ni maskini. Sina mengi zaidi.
Basi ngoja nilete waarabumasikini cv anaitoa wapi mkuu. hebu kuwa na huruma
unatafuta masikini yupi kati ya hayo ma group
...Wewe uko Kundi Gani, Mkuu Mtibeti ?? [emoji848][emoji848]Kwema Wakuu!
Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.
1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.
2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.
Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.
3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.
Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.
Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.
Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.
Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.
Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).
Ijumaa Kareem