Kama kipato chako ni chini ya milioni Tano kwa mwezi wewe ni Maskini

Kama kipato chako ni chini ya milioni Tano kwa mwezi wewe ni Maskini

Hakuna utajiri mkubwa kama kua na afya njema na kuwa ni mtu mwenye kushukuru, haya maisha ya show off unaweza ingaza hata zaidi ya milioni 10 na ukawa ni mtu wa stress tu.
Ndugu zangu mara moja moja mkipata nafasi muwe mnatembelea mahospitalini kuwajulia hali wagonjwa msisubiri mpaka nyinyi wenyewe muugue ndio muende hospital.
Kuna rafiki yangu alitaka kujiua kisa duka lake limeungua, alijifungia ndani wiki nzima hataki hata chakula, baada kupata hizo habari nikaenda kwake nikaforce twende tukatembee apunguze stress, alinikatalia katakata baada ya kumlazimisha sana ndio akakubali, ilikua ni jumapili nilinunua vizawadi kidogo halafu moja kwa moja nikampeleka Ocean Road kwenda kuwajulia hali wagonjwa wa Cancer.
Baada ya kurudi tu home kitu cha kwanza jamaa aliomba ugali, baada ya kula na kushiba akipiga goti kumshukuru Mungu kwa neema kubwa ya afya aliyonayo.
 
Hakuna utajiri mkubwa kama kua na afya njema na kuwa ni mtu mwenye kushukuru, haya maisha ya show off unaweza ingaza hata zaidi ya milioni 10 na ukawa ni mtu wa stress tu.
Ndugu zangu mara moja moja mkipata nafasi muwe mnatembelea mahospitalini kuwajulia hali wagonjwa msisubiri mpaka nyinyi wenyewe muugue ndio muende hospital.
Kuna rafiki yangu alitaka kujiua kisa duka lake limeungua, alijifungia ndani wiki nzima hataki hata chakula, baada kupata hizo habari nikaenda kwake nikaforce twende tukatembee apunguze stress, alinikatalia katakata baada ya kumlazimisha sana ndio akakubali, ilikua ni jumapili nilinunua vizawadi kidogo halafu moja kwa moja nikampeleka Ocean Road kwenda kuwajulia hali wagonjwa wa Cancer.
Baada ya kurudi tu home kitu cha kwanza jamaa aliomba ugali, baada ya kula na kushiba akipiga goti kumshukuru Mungu kwa neema kubwa ya afya aliyonayo.

Afya kila mtu anaweza kuwa nayo.
Lakini utajiri ni zawadi ya wateule wachache
 
Kwema Wakuu!

Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.

1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.

2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.

Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.

3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.

Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.

Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.

Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.

Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.

Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).

Ijumaa Kareem
Hivi viwango ni vya Ulaya au Africa?
 
Umaskini au utajiri ni vile unavoyaona mambo kwa mtazamo wako binafsi!!

Vipimo vingi vya umaskin sio halisi ni vya kutengeneza kutokana na malezi na makuzi ya mtu au elimu feki ambayo haisadifu uhalisia!!

fedha sio chakula Wala afya SEMA Kuna watu wachache sana walizifanya hizI karatasi zionekane za maana kumbe ni ujinga mtupu!!

kwangu mimi simuoni mtu tajiri Sana eti kisa ana makaratasi meeengi kwenye nyumba iitwayo Benki!!


Umaskini was kumiliki fedha au kuthaminisha kitu kwa fedha ni WA kutengeneza na elites fulani na kutuaminisha eti hizo karatasi ndio thamani ya status ya mtu kwenye jamii!!
 
Kwema Wakuu!

Kuna aina tatu za Maskini.
1. Maskini wa kutupwa (Fukara)
2. Maskini wa kawaida
3. Maskini aliyechangamka.

1. Maskini Fukara
Maskini Fukara hili kundi ni wale Watu ambào kula yao ni mshikeshike, hawana pakuishi, yaani hawa ndio huitwa hohehahe. Hawa kwa asilimia kubwa wamekata tamaa ya maisha. Na ukikutana nao moja kwa moja umaskini ndio utambulisho wao.

2. Maskini wa Kawaida.
Hili ni kundi ambalo wengi tupo hapa.
Hawa wanapata kiasi mahitaji yao ya msingi lakini sio Quality. Yaani atakula ndio chakula lakini sio mlo kamili.
Yaani yeye kila siku maugali na maharage sio shida. Kuvaa nguo za mtumba ni jambo la kawaida. Mpya ni mara mojamoja.

Makazi yao ni vibanda fulani ambavyo vinawastiri na baridi, jua na mvua. Ingawaje wao wenyewe huita nyumba lakini kimsingi sio nyumba.

3. Maskini waliochangamka.
Kundi hili ni lile la wenye vipato ambavyo ni kati ya milioni moja mpaka tano.
Kwa Tanzania kundi hili nalo hujiona limetoboa lakini kimsingi ni kundi maskini tuu kwani vipato vyao haviwezi kukidhi mahitaji ya msingi kwa kiwango kikubwa.

Mfano mtu mwenye kipato cha milioni moja mpaka tano hana uwezo wa kula milo mitatu kamili mwaka mzima pasipo kupasua matairi. Hapohapo hana uwezo wa kuishi kwenye makazi mazuri na kuvaa nguo Standard. Ni lazima kimoja atashindwa. Hapohapo awe anabima nzuri ya afya. Gari nzuri ambayo mafuta kwake sio tatizo, huku anasomesha watoto shule nzuri. Utagundua hicho kipato ni kidogo mno.

Kundi hili linanafasi ya kupambana na kuingia kundi la matajiri daraja la chini ambao kipato chao ni milioni 10 mpaka milioni mia moja.
Ishu inakuja pale ambapo Watanzania wengi tukishapata tumilioni mbili kwa mwezi ndio tunaona tumeshatoboa na tunaanza kubweteka ilhali kimsingi bado tupo tabaka la juu la maskini.

Unapoambiwa nchi yako ni maskini elewa kuwa robo tatu ya wananchi vipato vyao kwa mwezi havitoboi milioni tano.

Ukisikia mtu anakuita Maskini na unajiona una maisha mazuri. Sijui gari, nyumba na unapesa za kubadilisha mboga alafu muda huohuo kipato chako halifiki milioni tano jua anahaki ya kukuita hivyo.

Ingawaje umaskini kwa upande mwingine ni mtazamo. Mtu anaweza kuwa Maskini wa kipato lakini akawa anajiona tajiri(mental illness) alafu yupo mwenye kipato cha milioni 100 alafu anajiona maskini(hana shukrani).

Ijumaa Kareem
Sure
 
Back
Top Bottom