Kama sio tajiri na huna asset, kusomesha watoto shule za gharama ni ujinga unaongeza umaskini kwenye ukoo

Kama sio tajiri na huna asset, kusomesha watoto shule za gharama ni ujinga unaongeza umaskini kwenye ukoo

Bu

Huo upumbavu binafsi nilishakiri humu sitakaa nifanye [emoji16][emoji16][emoji16]! Hio hela bora umwekezee mtoto tu akija kukua mtu mzima apate pa kushika. Ni fedhea sana kulipa mamilioni kisha mtoto aje kuzunguka na kibahasha kama mwendawazimu [emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mie huwa nabaki kushangaaaah "hiiiiiiiii"
 
Mimi sijasoma huko Academy lakini siwezi kushindwa kujieleza mbele ya mtu yeyote.

Tunahadaika kirahisi sana.. watoto wengi wa Academy wanajua kiingereza kidogo na kiswahili kidogo.. huo ndio ubaya..

Mawazo yao mengi yanaathiriwa. Na mazingira ambayo ni ya kiswahili.. anajifunza nadharia kwa kizungu.. halafu aje awe mbunifu wa kuzitumia nadharia hizo kwa kiswahili kuvumbua haiwezekani.

Watoto walipaswa wasome kila somo kwa kiswahili.. mwalimu angekuwa na uwezo wa kuwa extra na kuaccomodate knowledge mpya kirahisi.. na elimu ingekuwa relevant. na wapate waalimu wa kingereza ikibidi kutoka Uingereza wawafundishe lugha ya kiingereza.

Nadharia content yake haibadilishwi na lugha. Ukifunza hesabu kwa kichina, kiarabu au kiingereza inabakia kubwa hesabu tuu... Mpe mtoto ujasiri wa kujifunza katika lugha ambayo anauhuru nayo.. hizo nyingine ni lugha tu za kuwasilisha anachokijua.
Hakika
 
Ni ishu kama utaonekana una umuhimu mahali uende ukasaidie ulipwe pesa! Ila kwa trend inavyoenda 30yrs ahead hii elimu ya kibongo haitakuwa na maana yeyote.
AAA ya PCM A level . katika 10, 8 watatoboa
 
Unatumia nguvu nyingi sana ktk kumsomesha mtoto, mwisho mtoto anamaliza Shule hana kazi na wewe mzazi huna kitu. Hata akipata kazi fedha anaanza kukurudishia kwa kukulea.

Ila ukianza kuwekeza, hata kama atapata Elimu ya kawaida. Mzazi akipata hela mtoto lazima atapata hela.
Hii ndio inaitwa Critical thinking! Walioachana na shule mapema watakuwa mbali sana katika umri ambao watoto wako ndio wanamaliza na mavyeti wanayo ya degree ila kazi hamna! Mzazi umetumia mamillion kibao kusomesha mtu ambaye inabidi uendelee kumlea. Wakati wenzie wana maisha wanaoa 😂😂😂
 
Kujiamini unamjengea mtoto wewe mwenyewe.

Kujifunza kutafuta maarifa ni zao la malezi hasa nyumbani.. mtoto anatakiwa ajifunze kupata kwa kutafuta.. sio kupewa..

Wengi majobless wanaopaka Poda sinza wamesoma Medium kwa wengi ni swala jipya.. maana ndio tunashtuka.. ila hazina jipya lolote.. niamini.

Tumesomesha sana huko private na kumalizia Bablo na bado anafika UD anakuta vipanga wamesoma shule ya msingi yombo, sekondari gongo la Mboto, highschool Benjamini na wanamyoosha na in two or three years kingereza nao wanakijua na wanajua kuona fursa na kuzitumia.

Wanamuuzia mwanao T-shirt za kuprint, wanamleta visheti ambavyo yeye hajui hata kupika, wanaleta ubuyu.. yeye anatoka umtafutie na kazi...
Pita kwa mangi pata 1 kubwa baridi, nakuja kulipa wallah.
 
90% ya wasomi wanafanikiwa?? Ebu tupe definition ya kufanikiwa kwanza!! Maana hao wasomi wa kutegemea mshahara na kununua gari na kujenga kwa mkopo,mshahara ukitoka tarehe 28 baada ya siku 10 ushakata ndio mafanikio hayo?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Oya mkuu FRESHMAN uko pande zipi kesho nikutoe offer moja matata?

Huu ni moja ya uzi bora kabisa wa mwaka huu.

Mimi natumia formula moja: Ni lazima, sio ombi yaani ni lazima wanangu wote level ya primary wasomee shule za kawaida.

Primary ndio level nzuri zaidi ya kujua IQ ya mtoto. Sasa kama umempeleka hizi shule ambazo mwanafunzi wa 1 anakuwa na A na wa mwisho pia ana A kasoro wanazidiana maksi tuu, hapo huwezi kujua uwezo binafsi wa mwanao.

Mtoto akisoma primary za kawaida na akawa hakosi kuwepo kwenye top ten ama five ama three ama akawa anaongoza kabisa basi jua hapo una jembe na unachotakiwa na kumboost kidogo tuu na atafanya maajabu mpaka utashangaa. Sasa huyu hata akienda secondary za kawaida atafanya vzr tuu lkn usiache kumpa guidance.

Kisha sasa wanao ambao watakuwa wazito ndio uelekeze nguvu kubwa kwao. Sio watoto wote wanakuwa wanahitaji nguvu kuuubwa sana, hivyo ni jukumu la mzazi kufanya sorting ya kujua huyu anakaa hapa na huyu anakaa pale.
 
Nimekupenda bure, umeolewa wewe?

Maana wanawake ndio wanazipenda hizi shule za mamilioni vibaya mno ili wauze sura kwa marafiki zao
Ktk maisha yangu nilishasema na hata watu wanajua, watoto wangu watasoma government school, haijalishi sijui nna pesa kiasi gan hat km cha kuweza kuhimili private..

Nyumbani kwetu wazazi wangu wana uwezo mkubwa tyuuh kifedha wa kuweza kutusomesha kwenye shule za magari ya njano, ila walitupitisha ktk shule za kidumu na mifagio huku wakiweka asset za baadae kwetu na wakitiliaa mkazo ktk kupata elimu yetu,

Kwa wakati ule tuliona wazazi ni bakhili na wabinafsi kwa kutuweka shule ambazo hazifanani na uwezo wala status zao km wazazi wa watoto husika, ila leo hii tunajivunia mno tena sana. Na tunashukuru zaidi kwani wazazi walikua wanatengeneza kitu muhimu na bora kwetu.

Now nipo chuo 2nd yr, na faculty yangu n 4yrs, na nasoma kwa pesa zangu, maana sikuomba na wala kuhitaji mkopo, asset ninazomiliki binafsi, kwangu tosha kabisa ku survive maisha yangu yote, na hapa nilipo wala sitegemei ajira hapo baadae labda itokee tyuuh. Ila sio mie kuzunguka na bahasha za kakhi mtaani. Hilo halitakuwepo na halipo.

Nawashukuru sana wazazi kwa msingi huu waliouweka ambao leo tunafaidi matunda yake.
 
Mimi namtazamo mwingine japo sitofauti sana na wewe mimi naona ni vyema kipindi hichi wazazi wenye kipato cha kawaida wakawa na malengo ya kuja kuwekeza zaidi kwa watoto wao kwenye elimu ya juu huku chini hakuna haja sana sababu watoto wanaishia kujua lugha tu
Lugha ndio kilakitu mkuu, sikulazimishi lakinin.

Waswahili walisema Samaki mkunje angali mbichi, na shombo lake,
Hapo kwenye Shombo nimechomekea kidogo😛

Madhara ya kuwasomesha watoto awali 'Msondongoma praimari' ni makubwa kuliko faida.

Toto linalemazwa kwa kukaririshwa, linapita kimungumungu hadi Juu,
Matokeo yake na 'Lidigrii' lake lakini hovyo kabisa.
Mahala pa 'Lake' linasema na kuandika 'Rake' bila soni.

Aibu gani hii.
 
True.. mtu analipa milioni 3 ama nne kwa mwaka ili mwanae ajue kiingereza tu... huku sylabus anayofundishwa mwanae wa tusiime ni ile ile ambayo wa elimu bure anafundishwa. Tofauti ni lugha tu.

Tatizo la elimu yetu ni sylabus.. jaribu kuwaza hiyo milion 3 kila mwaka mnunulie kiwanja ndani ya miaka 7 atakuwa na asset kiasi gani huyo mtoto.

Mtoto atakuwa na uhakika wa kupata elimu ya juu ama basic need hata kama mzazi umefariki...
Kwahiyo Kiwanja ni bora kuliko Elimu?

Dunia inishushe kituo cha pili jamani.
 
Ktk maisha yangu nilishasema na hata watu wanajua, watoto wangu watasoma government school, haijalishi sijui nna pesa kiasi gan hat km cha kuweza kuhimili private..

Nyumbani kwetu wazazi wangu wana uwezo mkubwa tyuuh kifedha wa kuweza kutusomesha kwenye shule za magari ya njano, ila walitupitisha ktk shule za kidumu na mifagio huku wakiweka asset za baadae kwetu na wakitiliaa mkazo ktk kupata elimu yetu,

Kwa wakati ule tuliona wazazi ni bakhili na wabinafsi kwa kutuweka shule ambazo hazifanani na uwezo wala status zao km wazazi wa watoto husika, ila leo hii tunajivunia mno tena sana. Na tunashukuru zaidi kwani wazazi walikua wanatengeneza kitu muhimu na bora kwetu.

Now nipo chuo 2nd yr, na faculty yangu n 4yrs, na nasoma kwa pesa zangu, maana sikuomba na wala kuhitaji mkopo, asset ninazomiliki binafsi, kwangu tosha kabisa ku survive maisha yangu yote, na hapa nilipo wala sitegemei ajira hapo baadae labda itokee tyuuh. Ila sio mie kuzunguka na bahasha za kakhi mtaani. Hilo halitakuwepo na halipo.

Nawashukuru sana wazazi kwa msingi huu waliouweka ambao leo tunafaidi matunda yake.

Naomba basi nikuoe.. hela sina za kuonekana tajiri ila njaa sitakulaza
 
Back
Top Bottom