Kamanda Mambosasa: Mwandishi Erick Kabendera anahojiwa uraia wake

Kamanda Mambosasa: Mwandishi Erick Kabendera anahojiwa uraia wake

Acha kujitoa akili, leo kwake kesho kwako hata kwa ndugu yako. Tutumie vichwa kufikiria kwa makini.
Kama angekua raia halali angetii wito tu. Ni either raia mkorofi au uraia wake una walakini au sio raia kabisa
 
Kuna wakati Hayati Mwalimu J.K.Nyerere alisema, "ukihoji sana uraia wa mtu katika Inchi ya Tanganyika/Tanzania hakuna atakaye kaa salama. Kila kabila hapa halina asili ya Tanganyika na hata jina Tanganyika halijulikana limetoka wapi."
Kitu cha maana kwa kila Mtanzania ni kuweka kumbu kumbu zake sawa ikiwa ikiwa ni pamoja na Kumbu kumbu muhimu kama vyeti halali vya kuzaliwa, wazazi walikozaliwa, shule ulizosoma n.k.
Hata kama hukuzaliwa Tanzania na kusomea Tanzania, kuna taratibu ya kufuata ili upate urai wa Tanzania.
Ndani ya Inchi yetu kuna Wahindi, Waarabu na hata Wazungu wana uraia wa Tanzania.
Kwa nini mtu anaanza kupelelezwa mambo yake na kukamatwa?
Jibu ni rahisi. Mtu kwa namna Fulani akianza kuchokonoa usalama wa Inchi kwa kufanya propaganda lazima Serikali imfuatilie nyendo zake na kumthibiti ili asije kuleta madhara kwa wengi.
Propaganda ni kumweleza mtu jambo nyeti kwa njia ya uovu au uongo ili kumtia hamasa na kumfanya achukue au atende jambo la uovu au jinai bila kufikiri kwa maslahi ya mfanya propaganda au kwa madhara ya mfanyiwa propaganda.
Kwa kifupi ukitenda kosa moja la jinai linasababisha wapelelezi kuongeza wigo wa kufuatilia nyendo zako zingine ambazo wanawasisi nazo.
Ukipekuliwa nyumbani kwako wakakukuta na bangi hawawezi kuicha tu kwa sababu lengo lao lilikuwa si kutafuta bangi.
Watanzania tunatakiwa kuwa watii na waaminifu kwa Serikali kama Nabii Yesu Kristo alivyokuwa mtii kwa mamlaka ya Ponsio Pilato hadi mauti, mauti ya Msalaba.
 
Walipomfuata Kabendera hawakujitambulisha.
Walimbeba mzobemzobe mbele ya mama yake mzazi ambaye pia ni Mgonjwa kwa mwaka wa tatu mfululizo sasa

Kwahiyo Mama yako akiwa Mgonjwa au Mahututi ndiyo kunazuia Polisi ( Mamlaka husika ) Kutekeleza wajibu wake wa Kisheria?
 
Huyo alikuwa na uhusiano na mtangazaji wa zamani wa Radio Rwanda marehemu Kabendera Shinani?
 
Kuna mmoja alikuwepo mtangazaji wa Rwanda aliitwa Kabendera Shinani. Nadhani hilo jina limemletea kizaazaa!
Hivi akiwepo mtu anaitwa Lazaro Mambosasa au john Magufuli kule Rwanda au Zambia au malawi itamaanisha kuwa hawa wenzetu si raia? au hiyo inaaply kwa sisi tusio na madaraka
 
Hii inadhihirisha kuwa watanzania ni vilaza,mtu akiwa anaandika habari za uchunguzi lazima wahoji uraia wake maana watanzania kazi yao ni kuandika habari za mara zari sijui Tanasha sijui Diamond. Hongera Eric wewe ni kipanga si mchezo kuandika nakala kwenye gazeti la The Economist.
Ni habari gani ya kiuchunguzi aliyoandika?
 
Kamanda Mambosasa anasema:

Erick Kabandera alikamatwa nyumbani kwake baada ya kukataa wito halali wa Jeshi la Polisi

Awali aliandikiwa barua ya wito ajili ya mahojiano lakini alikaidi kutii wito halali wa Polisi

Jeshi la Polisi likimwita mtu kwa hiari akikaidi, sisi tunamwezesha atii

Baada ya kukamatwa tumesikia watu mbalimbali wakidai ametekwa. Niseme hajatekwa lakini kwa jeuri akawa amekaidi kutii wito.

Aliitwa kuhusiana na Utata wa Uraia wake. Kwa kushirikiana na Uhamiaji, tunafuatilia uhakika wa uraia wake pale atakapotoa vielelezo mbalimbali kuthibitisha uraia wake. Sasa tunaye, taratibu nyingine za kiupelelezi zinaendelea.

Hajatekwa, amekamatwa na tunaye Central Police.

Upelelezi unaendelea, tukikamilisha upelelezi matokeo ya upelelezi ni kupelekwa mahakamani

Kwakuwa alikaidi wito, hatukuwa na namna zaidi ya kumkamata na kumshikilia

=====

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUKAMATWA KWA ASKARI BANDIA ALIYEVALIA CHEO CHA MKAGUZI MSAIDIZI WA POLISI.

Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es Salaam linamshikilia DAUDI RAMADHANI IDDY (23) mkazi wa Tabata Segerea kwa kujifanya ofisa wa Polisi, akiwa amevaa sare za Jeshi la Polisi na cheo cha mkaguzi msaidizi wa Polisi( Assistant Inspector).

Mnamo tarehe 19.07.2019 Jeshi la Polisi lilipata tarifa toka kwa askari wa Jeshi la kujenga taifa (JKT) makao makuu Mlalakuwa, kuwa kuna kijana mmoja amevaa sare za Jeshi la Polisi wana mashaka naye.

Makachero wa Jeshi la Polisi walifika makao makuu ya JKT Kumkamata na kufanya naye mahojiano,mtuhumiwa alikiri kujifanya yeye ni afisa wa Polisi na kufanya utapeli.

Pia alikiri kupitia mafunzo Jkt huko Mafinga mwaka 2006 na kujitolea kwa mujibu wa sheria katika kambi hiyo.

Mtuhumiwa alifanyiwa upekuzi na kupatikana na vifaa vifuatavyo;
1.sare moja ya Polisi aina ya kaki

2. vyeo vya(Cpl, Sgt na cheo cha mkaguzi msaidizi

3 pea moja inaya kombati Jungle green.

4.pingu moja.

5.kofia moja ya askari wa usalama barabarani.

6.radio ya upepo moja aina ya motorola.

7 mikanda miwili ya Jkt.

8.mkanda mmoja wa bendera wa Jeshi la Polisi, buti na viatu vya kawaida.

Upelelezi wa kina unaendelea na mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili.

KUKAMATWA KWA MWANDISHI WA HABARI.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia ERICK KABENDERA, (39) mkazi wa Mbweni, Mwandishi wa habari, kwa mahojiano.

Mnamo tarehe 29/07/2019 mtuhumiwa alikamatwa nyumbani kwake na Jeshi la Polisi baada ya kukataa wito wa Jeshi la Polisi.

Aidha mwandishi huyo awali aliandikiwa barua ya wito kufika Polisi kwa ajili ya mahojiano lakini alikaidi wito huo.

Ndugu waandishi wa habari niseme utii wa sheria bila shuruti ni muhimu sana kuzingatiwa kwani ukishindwa kutii sheria inakuwa shuruti. Baada ya kukamatwa mwandishi huyo tumesikia taarifa mbalimbali zikisambaa kuwa mwandishi huyo ametekwa, niseme kuwa mwandishi huyo hajatekwa ila tumemkamata kwa mahojiano. Aidha mtuhumiwa huyo kuna mashaka makubwa kuhusiana na uraia wake tutakapobaini mara moja tutamkabidhi kwenye idaya ya uhamiaji ili kushughulika naye na ndiyo maana alikuwa akikaidi wito wa polisi na kujihami kuwa ametekwa.

LAZARO B. MAMBOSASA – SACP KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
30.07.2019
hii ni ile mutoto ya marehemu kabendela Shinani? aliyejinyongea ziwani au
 
Back
Top Bottom