Uchaguzi 2020 Kamati ya Maadili ya Uchaguzi yamsimamisha James Mbatia kufanya kampeni kwa siku 7

Uchaguzi 2020 Kamati ya Maadili ya Uchaguzi yamsimamisha James Mbatia kufanya kampeni kwa siku 7

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Kamati ya Maadili imemkuta Mgombea wa Jimbo la Vunjo kupitia NCCR Mageuzi, James Mbatia na hatia katika tuhuma ya uvunjivu wa Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020.

Hivyo Kamati hiyo imemsimamisha James Mbatia kufanya kampeni kwa muda wa siku 7 kuanzia tarehe 17 Oktoba 2020 hadi tarehe 23 Oktoba 2020 kwa mujibu wa Kanuni ya 5.11 (d) ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020.

Hiyo ni baada ya Kamati ya Maadili Jimbo la Vunjo iliyokaa Oktoba 16, 2020 kupitia tuhuma ya uvunjivu wa Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020 dhidi Mbatia ya kujihusisha na kutumia kipeperushi cha kampeni ambacho hakijaidhinishwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Vunjo.

332D03CF-7792-4DAA-833B-4F5E2211AD43.jpeg
 
... heri wewe uliyefunuliwa jicho la "rohoni" kuyaona hayo. Bonge la igizo ili haki ionekane inatendeka kwa wote.
Mie pia nanusa kuwa kuna adhabu ya siku 7 inayohusu kina fulani wa upinzani hasa ili wasi conclude kampeni zao vizuri. Sheria ya uchaguzi Tanzania ni mbaya na ya ovyo kuliko sheria zote duniani.

Eti mgombea aweza kuenguliwa kwa kuandika Chama cha Demokrasia na Maendeleo badala ya CHADEMA na mwingine akaenguliwa kwa kuandika Chadema vadala ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Tume ni hiyohiyo yenye vigezo tofauti vya hukumu. Kijisababu kinatafutwa tu ili mtu anayeonekana tishio akwamishwe. Mbatia ni nani? Amefanya kampeni wapi na wapi wakati wa kampeni hii ya uraisi?

Nangojea kuona mizengwe mingi inayohusu mawakala wa wagombea. Hawataapishwa, majina yao hayatawakilishwa vituoni, watakatazwa kuingia vituoni na mizengwe mingine mingi.

Tume ni ya makada wa Ccm, wasimamizi wa kila jimbo ni makada wa Ccm na tutarajie tu migogoro kwa kuwa wanajua hamna njia nyingine ya kushinda ila kwa kuiba tu!
 
Mie pia nanusa kuwa kuna adhabu ya siku 7 inayohusu kina fulani wa upinzani hasa ili wasi conclude kampeni zao vizuri. Sheria ya uchaguzi Tanzania ni mbaya na ya ovyo kuliko sheria zote duniani. Eti mgombea aweza kuenguliwa kwa kuandika Chama cha Demokrasia na Maendeleo badala ya CHADEMA na mwingine akaenguliwa kwa kuandika Chadema vadala ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Tume ni hiyohiyo yenye vigezo tofauti vya hukumu. Kijisababu kinatafutwa tu ili mtu anayeonekana tishio akwamishwe. Mbatia ni nani? Amefanya kampeni wapi na wapi wakati wa kampeni hii ya uraisi?
Nangojea kuona mizengwe mingi inayohusu mawakala wa wagombea. Hawataapishwa, majina yao hayatawakilishwa vituoni, watakatazwa kuingia vituoni na mizengwe mingine mingi. Tume ni ya makada wa Ccm, wasimamizi wa kila jimbo ni makada wa Ccm na tutarajie tu migogoro kwa kuwa wanajua hamna njia nyingine ya kushinda ila kwa kuiba tu!
Mbatia anagombea Ubunge Vunjo na sio urais mkuu

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Kamati ya Maadili imemkuta Mgombea wa Jimbo la Vunjo kupitia NCCR Mageuzi, James Mbatia na hatia katika tuhuma ya uvunjivu wa Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020

Hivyo Kamati hiyo imemsimamisha James Mbatia kufanya kampeni kwa muda wa siku 7 kuanzia tarehe 17 Oktoba 2020 hadi tarehe 23 Oktoba 2020 kwa mujibu wa Kanuni ya 5.11 (d) ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020

Hiyo ni baada ya Kamati ya Maadili Jimbo la Vunjo iliyokaa Oktoba 16, 2020 kupitia tuhuma ya uvunjivu wa Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020 dhidi Mbatia ya kujihusisha na kutumia kipeperushi cha kampeni ambacho hakijaidhinishwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Vunjo

Anayewindwa ni Mbowe , huyu kafungiwa ili ku balance mambo , kama unabisha subiri .
 
Back
Top Bottom