Upepo wa Pesa
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 21,600
- 35,158
Wanakwepa tozoIla wahindi kubeba kweny mabegi mtu unakuta mtu ana million 200 chumbani kwake.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wanakwepa tozoIla wahindi kubeba kweny mabegi mtu unakuta mtu ana million 200 chumbani kwake.
Ungelianzisha kwa kuwarushia hata mawe.Daah, hata sielewi yani, nilihisi kama movie hivi wanaigiza sijui, hata sielewi yani
Hii wazungu kitaalamu wanaita, "going back to square A".Kuna bodaboda mbili zilipita speed kwenda uelekeo wa mtaa wa Lindi na Livingstone, kumbe bwana walikuwa wanamkimbiza mhindi aliyekuwa kwenye bodaboda nyingine ya mbele akiwa na begi mgongoni, inasemekena ni mauzo ya dukani, basi nikasikia puuu, kugeuka nikaona ile bodaboda ya mhindi ipo chini, na zile bodaboda zilizomgonga mmoja wao akashuka na kuanza kukata mikono ya begi kwa kisu, mhindi akang’ang’ani begi, maumivu ya kisu yalipozidi mhindi akaachia begi, jamaa akapanda kwenye pikipiki wakaamsha, halafu eti watu wanaangalia tu, mi nilitaka kwenda ila nikaona wale jamaa ili mibisu yao sio ya kitoto, wameanza kuondoka watu ndio wanajidai kuwakimbiza, wakatikomea kupitia pale kona ya Azam, livingstone pale.
Hadi sasa hali ni tete, polisi wawahi hapo kuchukua maelelezo.
========================
Halafu Nimekumbuka, hilo tukio limetokea mbele ya CCTV camera za duka la ‘New Tahery stores’ na ‘D&S Lab equipements’ mtaa wa Lindi, Polisi wakazitizame zile footage wanaweza kuwaona wale majambazi wakati wanakimbizana’ , wacheki footage time ya kuanzia muda nimepost hii thread kurudi nyuma, ni pembeni ya ile nguzo ndio walipomgalagaza mhindi, mbele ya duka la ‘New tahery stores’.
ukisema uzuie pikipiki kuingia kkoo unafeli kwakua wapo wamiliki wa biashara wana tumia pikipiki kama usafiri wapo watu wanajiingizia kipato cha msingi ni jamii kukataa uhalifu na kua na ushirikiano tatizo kkoo linakuja pale tukio linatokea huwez saidia kwakua ukiacha biashara yako bas ukirud hamna kituDawa ni pikipiki zisiruhusiwe ingia kkoo. Iwe marufuku kabisa kasoro za delivery, zenye delivery kit
haiondoi udhaif wa polisYaani raia mmeshindwa zuia uhalifu, halafu unauliza mahali polisi walipo!!
Unajua kuwa polisi mmoja anahudumia idadi ya watu wangapi?
Umenikumbusha riwaya ya kisa cha Chonya wa Chilonwa [emoji23] [emoji23] hongera sana mkuuDar utauawa mbele za watu hakuna atakayekusaidia.
Nilikuta ajali mbaya watu wamegongwa na gari na kurushwa mtaroni na wanavuja damu kama kuku aliyechinjwa na wakilia kuomba msaada lkn hakuna aliyesogea zaidi wanapiga picha tu na midume kibao imezunguka.
Ndipo nilipojitosa kuwatoa mtaroni na kuwafunga majeraha yao huku wengine wakishangaa tu hadi nilipowafokea sana ...akajitokeza jamaa mmoja akanisaidia kuwanyanyua.
Wakazi wa Dar ni wa ajabu sana
Yaani raia mmeshindwa zuia uhalifu, halafu unauliza mahali polisi walipo!!
Unajua kuwa polisi mmoja anahudumia idadi ya watu wangapi?
Ila mimi huwa nashindwa kuwaelewa watu wanaoporwa fedha karne hii ambapo kama ni mfanyabiashara kuna lipa namba kwa mitandao yote, mawakala wa benk zote wamejaa kila hatua mbili, hasa mijini, sasa ni kwa nini usubiri mpaka mauzo yafikie milioni 50??Pole sana kwa huyo aliyeibiwa....
Dar es Salaam ukishindwa kujitetea basi imekula kwako,,,, huu Mji hakuna anayejali...
Labda tu mambo ya umbea ndio wapo mstari wa mbele.
Hilo soko halina ulinzi?
Tumekuwa kama babu zetu wa zamani, maelfu wanapandishwa kwenye Meli na kuongozwa na mjinga mmoja aliyeshika gobole lenye risasi mbili wanashindwa kumnyanganya.Yan mtu anakisu tu mnatazama tu Kama mazezeta hao police wakiwapiga chuma hao wahuni Bado mnakuja kulalamika tu
Zanzibar wameweka Mayahudi.Hivi sababu ni udogo wa mji,!
Kwanini Zanzibar walifanikiwa kufunga cctv camera kwenye mitaa yote ya mjini!
Bongo imeshindikana nini?
Baba yako na Mama yako ni Watanzania?Hata katiba mpya wanamsubiri mbowe alete ,watanzania ni wajinga kama bata
wazaz kuwa watz km wengine hainifany nisiseme udhaifu wa raia wa hii nchi hii , naunga mkoj hoja kuwa watz hamna tofaut na wapuuz wengine kwny ulimwng huuBaba yako na Mama yako ni Watanzania?
Mungu akubariki sana mkuuNdipo nilipojitosa kuwatoa mtaroni na kuwafunga majeraha yao huku wengine wakishangaa tu hadi nilipowafokea sana ...akajitokeza jamaa mmoja akanisaidia kuwanyanyua.
Hakuna haja ya kuzuia pikipiki,ukisema uzuie pikipiki kuingia kkoo unafeli kwakua wapo wamiliki wa biashara wana tumia pikipiki kama usafiri wapo watu wanajiingizia kipato cha msingi ni jamii kukataa uhalifu na kua na ushirikiano tatizo kkoo linakuja pale tukio linatokea huwez saidia kwakua ukiacha biashara yako bas ukirud hamna kitu