Kariakoo inakuwaje duka Moja la simu Kuna wauzaji zaidi ya 20

Tz kuna upuuzi na ushamba sana ktk biashara... Ndio maana wafanyabiashara WaTz wanafirisika au wanafirisiwa na banks... Mtu ana biashara yake ya kawaida tu ila bidhaa anawaachia madalali wauze...
Ukitaka usipigwe bei fanya kwanza window shopping au peruzi ktk mitandao kujua bidhaa husika inauzwa bei gani ili ukienda dukani usiibiwe
 
Unaenda dukani mmiliki ana kaa pembeni anamuachia winga
Matokeo yake kila mtu anaye kuja anauziwa bei yake
 
Sehemu ambayo vitu vinakua inflated kwa asimilia 1000% ni karume aisee.......ukitaka kitu nenda masoko mengine kama Tandika,Ilala,Tandale etc ila sio KARUME,..........kitu kinauzwa pale mwanza lango elfu 40 karume kinauzwa laki na 20 na hakuuzii chini ya hapo,.......kasumba imeatawala wafanyabiashara kua karume Kuna pesa
 
Watu hawajui.. Facebook ndo mtandao wa kujua bei halisi
 
hao wauzaji wa LANGO wao wanachukua wapi mzgo?
 
ni kweli kabsa facebook n sehem ya kujuwa bei halisi ya bidhaa.

huwa nashangaa humu jamiiforum kuna watu wanasemaga eti watumiaji wa Facebook ni washamba. hua najisemea ihiiiiiii😳😳
Facebook kibaishara ndo mtandao unaolipa zaidi kuliko jf. Sijajua Instagram mana naona ukifanya kibiashar kule unatakiwa uwe advanced kidogo. Ila Facebook ina watu makini sana yani very serious na maisha halisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…