Kati ya uMagufuli na Samia ni upi umejaa wahuni zaidi? Tuorodheshe matukio ya kihuni

Kati ya uMagufuli na Samia ni upi umejaa wahuni zaidi? Tuorodheshe matukio ya kihuni

Ukileta issue za 50/50 basi pia huyo Samia nae achukue 50 kwa uhuni wote wa awamu ambayo yeye ndio alikuwa makamu wa rais wa utawala wa Magufuli. We kubali tu aliyemkamata Mbowe na kumuwela ndani kwa tuhuma za ugaidi ni Samia na uzuri alishaeleza msimamo wake juu ya hiyo kesi ya Mbowe pale alipohojiwa na bbc.
Ok basi hilo tukubaki ni la Samia, japo mpika kesi ni Magufuli
 
Wafuasi wa Magufuli wanaituhumu serikali ya sasa kuwa ina wahuni, wakiongozwa na yule mtu wao aliyepelekwa Malawi na hashtag yake ya #KataaWahuni

Sasa nataka tuende kwa fact na records, mimi nataka waniambie ni uhuni gani umefanyika serikali ya Samia kushinda uhuni wa Serikali ya Magufuli

Kwa kuanzia tu, Kipindi cha Magufuli ndio mbunge alipigwa risasi katika viwanja vya Bunge na watu waliompiga kung'oa CCTV Camera zilizorekodi tukio

Kipindi cha Magufuli ndio watu walitekwa kwa wingi zaidi kama akina Kinguye, Ben Saanane, azory Gwanda, Mdude Chadema, Roma Mkatoliki, Mo Dewji, Abdul Nondo n.k

Kipindi cha Magufuli ndio mkuu wa mkoa huku akirekodiwa na Camera alivamia kituo cha Tv kuamrisha habari yake isomwe na wala hakuchukuliwa hatua yoyote

Kipindi cha Magufuli ndio tulisikia mkuu wa mkoa akipiga watu marufuku kuja kwenye 'mkoa wake'

Kipindi cha Magufuli ndio mtu kama Sabaya alitamba sana, na kuna matukio kibao kama ya ubakaji, uporaji, kubambikizia kesi n.k

Achilia mbali uhuni wa kuengua asilimia 90 ya wagombea wa upinzani kwenye uchaguzi Serikali za mitaa kwa kigezo kuwa hawajui kusoma wala kuandika

Achilia mbali kulazimisha na kuhonga wapinzani kujiuzulu ubunge na udiwani kisha kugombea tena jimbo hilo hilo ili Magufuli aonekane anapendwa

Ndio kipindi tumedanganywa miradi mikubwa tunajenga kwa fedha za ndani

Achilia mbali kauli za kihuni za Magufuli kama 'Baki na mavi yako nyumbani', 'Mnataka mpanuliwe wapi', na kusifia wake za watu hadharani

Huu ni uhuni mdogo sana kati ya uhuni mwingi aliokuwa akifanya Magufuli

Haya sasa niambieni matukio ya kihuni kwenye serikali ya Samia tulinganishe
Magu na genge lake sio tuu walikuwa wahuni bali matapeli
 
Upuuzitu umeandika hapa. Mkiambiwa vijana wa chadema ni malofa mnabisha. Hivi tundu lisu Anapigwa risasi Alafu mpata dereva wake anaenda kujificha nae hawataki atoe ushirikiano na polisi hivi mpaka hapo Mjajua tu kwamba tukio lile lilipangwa na chadema wenyewe?

Tumieni Akili Hata kidogo basi yakufikiria. Na sio ushabiki wakijinga mwenzenu Mwenyekiti kashalambishwa Asali nyie mnabaki kuropoka tu mitandaoni.
Kwa hiyo kwa nini Chadems hawajakamatwa? Chadema waling'oa hadi kamera za CCTV?
Halafu nchi hii ilikuwa na ulinzi hafifu sana hadi Chadema waingie viwanja vya Bunge wampige risasi mbunge bila kukamatwa, dhaifu sana... wangeweza hata kumuua Spika

Mnyeti , Makonda, Sabaya na walikuwa mabilionea kipindi cha Magufuli na nyie misukue mnaitwa wanyonge mnashangilia
 
Nilidhani ulitaka uambiwe uhuni wa awamu hii, kumbe haupo hapa kukubaliana na hilo na ndio maana unajaribu kutetea ili kupinga kwamba awamu hii hakuna uhuni.

Kama unadhani nilivyomuelewa mimi sio sahihi na cha ajabu ndio tumemuelewa hivyo, je yeye mwenyewe Samia mbona hajarekebisha kwa kutoa ufafanuzi wa kauli yake ya kula kwa urefu wa kamba? We wewe dalili gani ya kuthibitisha kwamba ulivyomuelewa wewe ndio sahihi katika awamu hii ya watoto wa mjini?

Magufuli alijaribu kuweka nidhamu kwa kiwango alichoweza hata kama ilikuwa ni nidhamu za hofu ila zilisaidia kwa kiasi chake, sasa niambie Samia yeye toka aseme ni nidhamu za uoga yeye kafanya nini kujenga nidhamu ya za hiari?
Uhuni upi umetaja? Kupindisha maana ya meneno ndio uhuni?
Kwani kula kwa urefu wa kamba kuna maana gani kama tukichukulia kama nahau?
Nipe mifano halisi ya uhuni kama ya Bashite kuvamia Clouds na Bunduki
 
Wafuasi wa Magufuli wanaituhumu serikali ya sasa kuwa ina wahuni, wakiongozwa na yule mtu wao aliyepelekwa Malawi na hashtag yake ya #KataaWahuni

Sasa nataka tuende kwa fact na records, mimi nataka waniambie ni uhuni gani umefanyika serikali ya Samia kushinda uhuni wa Serikali ya Magufuli

Kwa kuanzia tu, Kipindi cha Magufuli ndio mbunge alipigwa risasi katika viwanja vya Bunge na watu waliompiga kung'oa CCTV Camera zilizorekodi tukio

Kipindi cha Magufuli ndio watu walitekwa kwa wingi zaidi kama akina Kinguye, Ben Saanane, azory Gwanda, Mdude Chadema, Roma Mkatoliki, Mo Dewji, Abdul Nondo n.k

Kipindi cha Magufuli ndio mkuu wa mkoa huku akirekodiwa na Camera alivamia kituo cha Tv kuamrisha habari yake isomwe na wala hakuchukuliwa hatua yoyote

Kipindi cha Magufuli ndio tulisikia mkuu wa mkoa akipiga watu marufuku kuja kwenye 'mkoa wake'

Kipindi cha Magufuli ndio mtu kama Sabaya alitamba sana, na kuna matukio kibao kama ya ubakaji, uporaji, kubambikizia kesi n.k

Achilia mbali uhuni wa kuengua asilimia 90 ya wagombea wa upinzani kwenye uchaguzi Serikali za mitaa kwa kigezo kuwa hawajui kusoma wala kuandika

Achilia mbali kulazimisha na kuhonga wapinzani kujiuzulu ubunge na udiwani kisha kugombea tena jimbo hilo hilo ili Magufuli aonekane anapendwa

Ndio kipindi tumedanganywa miradi mikubwa tunajenga kwa fedha za ndani

Achilia mbali kauli za kihuni za Magufuli kama 'Baki na mavi yako nyumbani', 'Mnataka mpanuliwe wapi', na kusifia wake za watu hadharani

Huu ni uhuni mdogo sana kati ya uhuni mwingi aliokuwa akifanya Magufuli

Haya sasa niambieni matukio ya kihuni kwenye serikali ya Samia tulinganishe
Polepole, ni kati ya wahuni waliokuwa wanasimamia manunuzi ya watu.

Polepole ni kati ya wahuni waliokuwa vigeugeu, waliosema katiba ni muhimu, lakini walivyokuwa ndani ya Serikali ya kihuni, wakasema kuwa watanzania hawahitaji katiba, bali wanataka maji, chakula na barabara.

Na sahizi, mhuni kama Polepole atageuka na kusema kuwa katiba ni hitaji la wananchi.

Hakukuwahi kutokea Serikali ya kihuni, Serikali ya kilaghai na udhalimu, kama awamu ya 5.

Tugange yajayo, tupate katiba mpya ya kuzuia kabisa wahuni kama Polepole, na Serikali ya kihuni kama awamu ya 5, kuja kupata nafasi ya kupngoza nchi kihuni.
 
Kinachoitwa uwekezaji ni kukaribisha wezi kuiba rasilimali zetu.

Hakuna unyama uliofanyika kama kuwaondoa wamasai kwa kutumia majeshi yetu kwenye ardhi yao na kumpa mwekezaji.

Ni jambo la aibu mno kusitisha mradi wa Bwawa la Nyerere na kuanzisha mwingine wa Gesi.

Wizi na ubadhirifu wa fedha za miradi na huduma mbovu ni jambo la kawaida kabisa kwa sasa.

Kuruhusu wafanyabiashara kupandisha bei wanavyojisikia ni kitendo cha kuwaumiza wananchi ambacho serikali imekibariki.

Kwa ufupi ni kwamba awamu hii imejaa uovu mwingi kuwahi kutokea katika historia ya Taifa letu.
Wamasai mbona wanahama wenyewe kwenda handeni? Kama muwekezaji atatuongezea pato tuache tung'ang'anie wamasai?

Huduma mbovu na ubadhirifu vilitokea sana kipindi cha Magufuli kuliko kipindi chochote, na ushahidi ni taarifa ya CAG

Kupanda bei ni dunia nzima, nenda hapo Kenya kilo moja ya unga inauzwa 2000

Bwawa la Nyerere halijasitishwa kama una ushahidi uweke hapa
 
Kama hoja yao ingekuwa ni serikali ileile wala nisingeanzisha huu uzi kuwahoji, hoja ya kuwa utawala uliopita ulikuwa perfect na huu qa sasa umejaa wahuni ndio nataka tujadili
Huyu unayesema siyo muhuni ndiyo alikuwa Makamu, hata kutoa comparison ni kosa kubwa. She was enabler!
 
Nafasi za bahati, yoyote hawezi jiamini, ilikua bahati KWa mwendazake vilevile imekua bahati tu KWa aliemfuatia, ya mwenzake yalisikitisha Sana na ya Sasa yanasikitisha Sana, hakuna jipya
Ila ile awamu ya 5, awamu ya Jiwe, ilikuwa awamu ya uongozi wa kibaradhuli.

Uongozi unaoua wanaokosoa, ni uongozi wa kishetani, ambao hauwezi kupata nafasi ya kuoshwa kwa namna yoyote ile.

Marehemu Magufuli ataendelea kukumbukwa kwa vizazi vingi kama mtawala baradhuli, muuaji, mtesaji na ambaye hakukubali kukosolewa kutokana na uuaji, utekaji na utesaji watu. Makosa mengine yote, kama uwongo na kuharibu uchumi, kuvunja haki za uhuru wa watu, udikteta, kutapanya pesa ya umma, uporaji wa pesa za watu na kuwabambikia watu kesi, ataweza kusamehewa lakini ushetani ule wa kuua na kuteka watu, kamwe hautasahaulika. Alijipa mamlaka ya kuondoa uhai wa watu, kama vile yeye ndiye anayeugawa, hakujua kabisa, shetani alimpumbaza, hata asijue kuwa hata yeye hawezi kukikwepa kifo.

Watawala na sisi sote tulio hai leo, tuogope kutenda maovu, tuogope na tusisogelee wala kuwaza kuwaua wanadamu wenzetu. Uhai wa mtu ni mali ya Mungu, ndiye aliyetupatia, na ndiye mwenye uwezo wa kuundoa.
 
Hii siyo hoja, ni haja kubwa!

Mleta mada, hii mada yako inasaidia nini maisha ya watanzania?

Jinga kabisa
Mleta mada, ana hoja kubwa kwa watu wenye akili.

Utawala wa kihuni wa awamu ya 5, utafanyiwa rejea kwa miaka mingi kama mfano mbaya wa utawala ambao nchi iliwahi kutumbukia.

Ulikuwa utawala wa kishetani, kwa kioimo chochote kile, kwa mtu aliye na akili timamu.
 
Wamasai mbona wanahama wenyewe kwenda handeni? Kama muwekezaji atatuongezea pato tuache tung'ang'anie wamasai?

Huduma mbovu na ubadhirifu vilitokea sana kipindi cha Magufuli kuliko kipindi chochote, na ushahidi ni taarifa ya CAG

Kupanda bei ni dunia nzima, nenda hapo Kenya kilo moja ya unga inauzwa 2000

Bwawa la Nyerere halijasitishwa kama una ushahidi uweke hapa
Jonny,
Matukio gani mapya ambayo hayakuwepo kabla ya Magufuli? Wewe hujaona hata kidogo hicho kiini macho cha CAG? CCM ni CCM, walikaa na kujua wampakazie vipi JPM. Wewe unaamini zile ndege hazikununuliwa? Lile bwawa la umeme ni baya kwa nchi? SGR ? Hujaona EPA, IPTL, Singasinga, Simba Trust etc etc etc huwa mnasahau mapema sana.
CAG aliandika ile Kwa maelekezo, uwe unachanganya na zako
 
Nilidhani ulitaka uambiwe uhuni wa awamu hii, kumbe haupo hapa kukubaliana na hilo na ndio maana unajaribu kutetea ili kupinga kwamba awamu hii hakuna uhuni.

Kama unadhani nilivyomuelewa mimi sio sahihi na cha ajabu ndio tumemuelewa hivyo, je yeye mwenyewe Samia mbona hajarekebisha kwa kutoa ufafanuzi wa kauli yake ya kula kwa urefu wa kamba? We wewe dalili gani ya kuthibitisha kwamba ulivyomuelewa wewe ndio sahihi katika awamu hii ya watoto wa mjini?

Magufuli alijaribu kuweka nidhamu kwa kiwango alichoweza hata kama ilikuwa ni nidhamu za hofu ila zilisaidia kwa kiasi chake, sasa niambie Samia yeye toka aseme ni nidhamu za uoga yeye kafanya nini kujenga nidhamu ya za hiari?
Mleta mada, naamini anataka hoja halisia, mambo yanayoenekana wazi. Kupigwa risasi Tundu Lisu, utalinganisha na kauli ya kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake? Kuwasweka ndani watu aluowaita wahujumu uchumi kumbe nia yake ni kuwapora pesa zao ili apate utajiri yeye binafsi, utalinganisha na mfumko wa bei ambao ni matokea ya mambo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi?

Hatukawahi kuwa serikali ya kihuni, kishetani, na yenye ubaradhuli wa kiwango kisichoelezeka, kama ile ya marehemu Magufuli. Mambo aliyokuwa akifanya ni mambo ya kishetani kabisa: kuua watu, kuteka, kuwabambikia watu kesi za uhujumu uchumi, kwapumbaza watu wenye akili ndogo waobe kuwa nchi inapaa ilihali ilikuwa ikiporomoka kila kukicha.
 
Kinachoitwa uwekezaji ni kukaribisha wezi kuiba rasilimali zetu.

Hakuna unyama uliofanyika kama kuwaondoa wamasai kwa kutumia majeshi yetu kwenye ardhi yao na kumpa mwekezaji.

Ni jambo la aibu mno kusitisha mradi wa Bwawa la Nyerere na kuanzisha mwingine wa Gesi.

Wizi na ubadhirifu wa fedha za miradi na huduma mbovu ni jambo la kawaida kabisa kwa sasa.

Kuruhusu wafanyabiashara kupandisha bei wanavyojisikia ni kitendo cha kuwaumiza wananchi ambacho serikali imekibariki.

Kwa ufupi ni kwamba awamu hii imejaa uovu mwingi kuwahi kutokea katika historia ya Taifa letu.
Awamu zote, kuna makosa Serikali hufanya lakini yale ya awamu ya 5 hayakuwa makosa bali ni ushetani. Shetani aliishi ikulu, akafanya kazi ya kuliangamiza Taifa, akawapata mashetani wadogo wa kusaidia kuangiza Taifa, wale wa kumwimbia sifa kwa nia ya kuwapumbaza waliokuwa na uelewa duni.
 
Upuuzitu umeandika hapa. Mkiambiwa vijana wa chadema ni malofa mnabisha. Hivi tundu lisu Anapigwa risasi Alafu mpata dereva wake anaenda kujificha nae hawataki atoe ushirikiano na polisi hivi mpaka hapo Mjajua tu kwamba tukio lile lilipangwa na chadema wenyewe?

Tumieni Akili Hata kidogo basi yakufikiria. Na sio ushabiki wakijinga mwenzenu Mwenyekiti kashalambishwa Asali nyie mnabaki kuropoka tu mitandaoni.
Aheri ungetulia, uache wenye akili wajadili hoja.
 
Ya mwendazake ilijaa wahuni, majambazi, wabakaji na mashetani!
Mama ana nia nzuri sana lakini amezungukwa na wahuni na walafi walikubuhu!
 
Ila ile awamu ya 5, awamu ya Jiwe, ilikuwa awamu ya uongozi wa kibaradhuli.

Uongozi unaoua wanaokosoa, ni uongozi wa kishetani, ambao hauwezi kupata nafasi ya kuoshwa kwa namna yoyote ile.

Marehemu Magufuli ataendelea kukumbukwa kwa vizazi vingi kama mtawala baradhuli, muuaji, mtesaji na ambaye hakukubali kukosolewa kutokana na uuaji, utekaji na utesaji watu. Makosa mengine yote, kama uwongo na kuharibu uchumi, kuvunja haki za uhuru wa watu, udikteta, kutapanya pesa ya umma, uporaji wa pesa za watu na kuwabambikia watu kesi, ataweza kusamehewa lakini ushetani ule wa kuua na kuteka watu, kamwe hautasahaulika. Alijipa mamlaka ya kuondoa uhai wa watu, kama vile yeye ndiye anayeugawa, hakujua kabisa, shetani alimpumbaza, hata asijue kuwa hata yeye hawezi kukikwepa kifo.

Watawala na sisi sote tulio hai leo, tuogope kutenda maovu, tuogope na tusisogelee wala kuwaza kuwaua wanadamu wenzetu. Uhai wa mtu ni mali ya Mungu, ndiye aliyetupatia, na ndiye mwenye uwezo wa kuundoa.
Hasaa! Na kulinda uhai wa raia ndiyo jukumu la kwanza la Rais na siyo kuhatarisha. Hata wanyama wa aina moja wanateteana Watanzania tumepumbazwa tunashabikia kuondoa uhai wa binadamu, wenzetu, kuteswa, wenzetu kuwekwa mahabusu/ jela kwa mambo ya kisiasa. Ukitazama tabia ya nyati wa porini utaona jinsi anavyo yakataa mambo hayo kwa nguvu zake zote akifanyiwa nyati mwingine! Maendeleo ni ya nini kama hayaji kunufaisha ujumla wetu wa sasa na vizazi vijavyo!!

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
 
Ok basi hilo tukubaki ni la Samia, japo mpika kesi ni Magufuli
Mbona unakuwa mzito kukubali tu moja kwa moja uhuni wa Samia hadi umuhusishe na Magufuli? Hili limeisha kuwa ni uhuni wa Samia.
 
Hasaa! Na kulinda uhai wa raia ndiyo jukumu la kwanza la Rais na siyo kuhatarisha. Hata wanyama wa aina moja wanateteana Watanzania tumepumbazwa tunashabikia kuondoa uhai wa binadamu, wenzetu, kuteswa, wenzetu kuwekwa mahabusu/ jela kwa mambo ya kisiasa. Ukitazama tabia ya nyati wa porini utaona jinsi anavyo yakataa mambo hayo kwa nguvu zake zote akifanyiwa nyati mwingine! Maendeleo ni ya nini kama hayaji kunufaisha ujumla wetu wa sasa na vizazi vijavyo!!

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
Hakika umenena vema. Awamu ya 5 ilizidiwa ustaarabu hata na maisha ya wanyama. Fisi pamoja na tabia zake za ajabu, lakini hatafuni watoto wake, ila hapa tulikuwa na Rais anasikia faraja kuondoa uhai wa wale aliorakiwa kuwalinda.
 
Uhuni upi umetaja? Kupindisha
maana ya meneno ndio uhuni?
Kwani kula kwa urefu wa
kamba kuna maana gani kama
tukichukulia kama nahau?
Nipe mifano halisi ya uhuni
kama ya Bashite kuvamia
Clouds na Bunduki
Samia anasema kabisa wajipimie wasivimbiwe, maelezo ya Samia yapo wazi kwamba sawa wanaiba inajulikana ila wasipitilize hadi kuathiri miradi na hadi mfano alitoa. Kwahiyo mkuu ni wewe ndio unajaribu kutaka kupindisha alichokikusudia Samia.

Na ndio maana hawezi kuja kutolea ufafanuzi hiyo kauli, ni uhuni ambao unataka kuukataa.
 
Back
Top Bottom