Katika utawala wake, hayati Magufuli hakwenda New York kuhutubia UNGA, je tulirudi nyuma kiuchumi na kisiasa?

Katika utawala wake, hayati Magufuli hakwenda New York kuhutubia UNGA, je tulirudi nyuma kiuchumi na kisiasa?

waliovunja vibanda juzi usiku.
Ndio hao hao, kwenye vita wewe kama kiongozi lazima uwe na mtu/watu wa kubeba lawama! Nyerere alikuwa na Kawawa, Mkapa alikuwa na Sumaye, Kikwete alikosa huyo mtu, matokeo yake akanyanyasika sana hadi ikabidi aanze na kuwatumia matapeli wa kisiasa akina Mbowe na wenzake kufanikisha ishu zake, JPM alikuwa nao wengi; Makonda, Kabudi, Kangi n.k.! Mama ni mapema bado, but naona kama Mwigulu anaweza kuibeba hiyo role
 
Ila ww ni mpumbavu sana hata kifaa alichotumia kuingia hapa ni cha mzungu au kuna kiwanda cha simu hapa bongo?
[emoji23][emoji23][emoji23]Sasa kama utaendelea kuwaabudu namna hii utajitoa lini hapo ulipo ili nawe uwe na kifaa chako?

Mibavicha bure kabisa
 
Kama unammisi sana dikteta twende tukakufukie kwenye kaburi lake msituchoshe.

Zama za kishamba zimekwisha lazima mlikubali hili na hii nchi hatuwezi kurudia kosa kuwakabidhi washamba.
Dikteta alikuchapa akiwa hai na bado anakuchapa akiwa mfu!
 
tukijaribu kusimamia hoja na sio ushabiki..

Exposure na kwenda pamoja na dunia ni jambo zuri kuliko kujifungia ndani, sio ujanja kutohudhuria hivi vikao kama mkuu wa nchi, uwepo wa UN na mambo kama haya una maana ndio maana ukawepo huo utaratibu...Dunia imetoka mbali na kufika hapa na taasisi hizi zina mchango wake kuhakikisha dunia iko hapa.....

UN ilianzishwa kwa madhumuni maalumu hapa duniani baada ya miaka ya nyuma dunia kuwa shaghala bhaghala na watu kujifanyia mambo watakavyo kiasi cha vita na mauaji kuwa mengi...uwepo wa UN angalau umeleta amani na ustawi duniani...Vikao vya marais hufanyika kuwaweka pamoja marais na nchi zao kujadili ya duniani na kuwa na muafaka na mambo mbalimbali..

Mfano sasa marais wote duniani wasiwe wanahudhuria hivi vikao...maana yake UN itakufa...UN ikiwa haipo unafikiri maisha yatakuwaje duniani hapa?
 
Miaka mitano yote akiwa madarakani tuliwakilishwa na mawaziri wa nje. Na hakuna mtanzania aliyeona labda tumepungukiwa kiuchumi. Zaidi ya kuona maendeleo kwenye sekta za afya, miundo mbinu na ukusanyaji mapato.

Safari hii tumewakilishwa na mkuu wa nchi. Je, ndio kusema taasisi kubwa kama Imf, Wb na taasisi Tanzu za UN zitaisadia Tanzania na kupaaa kiuchumi? Je haya madhila ya kukosa ajira, kukosa madarasa, kukosa maji na uvunjifu wa haki za binadamu vitaisha?
Misukule ya dikteta mnatapatapa Sana, kwakuwa mungu wenu alikuwa haendi kwenye hiyo mikutano ya kimataifa,,mlitaka na Samia hasiende kuiwakilisha Nchi
 
Mayalla unataka kuniambia kuwa Magufuli hakuwa na exposure? Wasaidizi wake pia nao hawakuwa na Exposure? Nini maana ya kuwa na Balozi kama sio kutuexpose na mambo mbalimbali yanayoendelea huko ukizingatia uwepo wake wa muda mrefu katika mazingira hayo.

Safari ya siku tatu ndio ikuexpose kwenye mambo chungu nzima yanayoweza kulifaa taifa lako, like seriously! Raisi Kikwete alishinda ulaya na Amerika lakini bado hatukuwa hata robo ya hizo nchi kiuchumi, kielimu, kisiasa n.k.

Unataka kuniambia kweli kwamba Magufuli hakuwa na exposure ya dunia na yanayoendelea! Acha hizo mkuu, mama kaamua kudance na dunia, period.
Nitafurahi kama tunaweza ku discuss, bila kumbeza marehemu, exposure ni personal, sio transferable useme kwa vile Balozi Dr. Mahiga amekaa Marekani na kuzunguka dunia 20 years, hivyo baada ya kuteuliwa na JPM, anaihamishia hiyo exposure yake kwa JPM. Exposure ni kama dose, ili upate exposure, ni lazima wewe ndio uwe exposed na sio kuwakilishwa.

Mtu ujifungie chumbani kwako for 5 years huku ukituma watu wakuwakilishe, what do you expect?.
P
 
Angeenda kuongea nini wakati mtu mwenyewe ni kilaza alichoweza yeye kufokafoka hovyo na kutisha wengine kwa kujiona ni mwamba,yule mtu hakustahili kabisa kuwa kiongozi mkuu.
 
Nitafurahi kama tunaweza ku discuss, bila kumbeza marehemu, exposure ni personal, sio transferable useme kwa vile Balozi Dr. Mahiga amekaa Marekani na kuzunguka dunia 20 years, hivyo baada ya kuteuliwa na JPM, anaihamishia hiyo exposure yake kwa JPM. Exposure ni kama dose, ili upate exposure, ni lazima wewe ndio uwe exposed na sio kuwakilishwa.

Mtu ujifungie chumbani kwako for 5 years huku ukituma watu wakuwakilishe, what do you expect?.
P
Asante kwa majibu na pia nakubaliana na tahadhari uliyoitoa.

Kwa ufahamu wangu ni kuwa raisi ni taasisi iliyosheheni uwakilishi wa mamlaka ya raisi sehemu mbalimbali ndani ya nchi na nje ya mipaka yake kwa mujibu ya sheria na katiba ya nchi husika. Uwakilishi huo lazima uzingantie taaluma au uelewa wa mambo fulani kwa undani zaidi ili kuweza kusaidia raisi kufanya maamuzi yaliyo sahihi kutokana na ukweli kuwa raisi hana uelewa wa profession zote hata angekuwa nani.

Kwa mustakabali huo, raisi kwa utashi wake pekee hawezi kuongoza nchi na ukategemea mambo yaende inavyopaswa, tuchukulie mfano, raisi aliyesomea taaluma ya sanaa akajipeleka yeye kama yeye kichwa kichwa kupata ushauri au kufunga makubaliano yahusuyo taaluma ya sayansi bila kutegemea technical expertise kutoka kwa Msaidizi wake atakuwa akijidanganya na kulipeleka taifa shimoni.

Realistically, President is just nation’s political icon who has to resonate with his colleagues about all national aspects prior to its adherence, meaning that, the exposure of his associates is akin and very crucial than what you might be thinking.

Miaka minne ya Trump bila kuja Africa haikumzuia yeye kuwa exposed na yale yanayoendelea huku, zaidi zaidi aliipunguzia serikali/ wanachi mzigo wa gharama za kusafirisha presidential delegation, Kupanga ni kuchagua, na raisi wetu aliyepita kwa hili alilipanga vizuri sana. Ninachokiona hapa ni hali ya kutaka kushindana kuhudhuria vikao vya maraisi na first world countries ambazo kwa namna moja ama nyingine they have managed to do so using our own resources, this is according to colonialism without forgetting to mention the ongoing neocolonialism.
 
Miaka mitano yote akiwa madarakani tuliwakilishwa na mawaziri wa nje. Na hakuna mtanzania aliyeona labda tumepungukiwa kiuchumi. Zaidi ya kuona maendeleo kwenye sekta za afya, miundo mbinu na ukusanyaji
Miaka mitano yote akiwa madarakani tuliwakilishwa na mawaziri wa nje. Na hakuna mtanzania aliyeona labda tumepungukiwa kiuchumi. Zaidi ya kuona maendeleo kwenye sekta za afya, miundo mbinu na ukusanyaji mapato.

Safari hii tumewakilishwa na mkuu wa nchi. Je, ndio kusema taasisi kubwa kama Imf, Wb na taasisi Tanzu za UN zitaisadia Tanzania na kupaaa kiuchumi? Je haya madhila ya kukosa ajira, kukosa madarasa, kukosa maji na uvunjifu wa haki za binadamu vitaisha?

mapato.

Safari hii tumewakilishwa na mkuu wa nchi. Je, ndio kusema taasisi kubwa kama Imf, Wb na taasisi Tanzu za UN zitaisadia Tanzania na kupaaa kiuchumi? Je haya madhila ya kukosa ajira, kukosa madarasa, kukosa maji na uvunjifu wa haki za binadamu vitaisha?
Nchi huongozwa kwa Principles na si matakwa au utashi wa mtu mmoja! Magufuli hakuwa na exposure yoyote na pia hakuwa mjuzi wa lugha yoyote zaidi ya kisukuma, hivyo kufanya mapungufu yake binafsi kuwa msingi wa kuendesha Taifa ilikuwa ni ujinga na unafiki tu!
Wito kwa akina Mwigulu wanaoonekana kuupenda sana Urais,hawana budi kujenga communication skills kwani hatutakubali tena kuwa na Rais very poor on communication skills kama alivyokuwa Magufuli.
 
Exposure ya mawaziri isingeweza kumsaidia Rais Magufuli kwa namna yoyote ile. Magufuli hakuwa mtu wa kuamini katika mawazo ya watu wengine. Aliamini katika anachokitaka yeye tu.

Kumpa exposure Magufuli kupitia mawaziri ni jambo ambalo lisingewezekana kabisa. Na uthibitisho wa hilo, angalia alivyoongoza nchi such primitively huku akijisifu na kuwajaza ujinga mwingi watu wasio na uelewa.
 
Angeenda kuongea nini wakati mtu mwenyewe ni kilaza alichoweza yeye kufokafoka hovyo na kutisha wengine kwa kujiona ni mwamba,yule mtu hakustahili kabisa kuwa kiongozi mkuu.

hahaaa,na alijua kuwafilimba.
 
Ni juha tu anayeweza kufikiri kwamba akijifungia tu Nyumbani kwake bila kutembelea majirani na marafiki Wenye maendelo kuliko yeye kubadilishana nae Mawazo kutamletea maendelo.

Huko kukosa exposure ndio kumepelekea uwanja wa kimataifa kujengwa porini usipotumika, kununua ndege cash money Kama tajiri wa madawa kulevya.
Na hayo ni Yale tunayoyajua tu, yapo mengi ya Siri ambayo amepigwa kimya kimya Kwa Ushamba tu
 
Sidhani kama kwenda UN ni kupiga hatua. Au kuwa na hyo exposure unayoisema. Si mara ya kwanza Tanzania kuhudhuria hivyo vikao. Toka Nyerere, Mwinyi, Mkapa, na Kikwete. Tena Kikwete aliizunguka dunia nzima.

Magufuli kwenda UN hakuwahi hata siku moja. Lakini aliifanya Tanzania kuwa ya kisasa. Katika utawala wake Tanzania ilisikika kila mahala. Watu waliiongelea Tanzania kwa mafanikio ya kiuchumi. Nilishawahi kusema humu. Nchi fulani Ulaya walikuwa wakijadili Magufuli alivyo weza kuwa na miradi mikubwa ya kiuchumi.

Reli ya SGR,kufufua reli ya Moshi Arusha hadi Dar. Kujenga Bwawa la Nyerere, kufungua masoko ya madini, na kiwanda cha uchenjuaji. Kuhamishia Makao Dodoma, kufufua shirika la ndege ATCL, kuyawezesha mashirika ya Posta na Simu. kujenga hospitali na vituo vya afya muhimbili sasa ni moja ya hospitali zinazoaminika. Kujenga madaraja na barabara za kisasa. Ni mengi kutaja huyu mnae msema hakuwa na exposure, lakini kafanya haya yote ndani ya miaka 5.

Watanzania baadhi ni wanafiki, wamezoea kujipendekeza ili wapate vyeo au njia za kujipatia pesa. Magufuli aliziba mianya yote, waliotegemea vyeo hawakupata. Wakaanza kujenga chuki zisizo na maana. Ndo maana hadi leo wanachukia hadi marehemu, wanafurahi mtu kufa utadhani wao wataishi milele.

Mama Samia apewe muda msimpe sifa zisizo stahili. Make hadi sasa ni ngumu kujua tunaelekea wapi. Nini hasa vision ya kiongozi wetu. Anaeogopa kutatua kero za wananchi hadharani. Kutwa nzima ni safari. Kikwete alisafiri lkn hatukuwahi kuona exposure hiyo ikiletwa Tanzania. Nilishawahi kwenda nchi fulani, katika mji wao mmoja ni mji wa kawaida tu. Nikafika hotel moja, nikaambiwa Rais Kikwete alipenda kufikia pale kalala mara kadhaa. Nikajiuliza Rais wa nchi anazurura hadi kuwa mteja wa hotel.

Msiyo mpenda Magufuli mtazidi umia na kuangaika. Yeye amepumzika. Alifanya yake kwa Tanzania. Swala kujiuliza wewe hapo umeifanyia nini Tanzania? Je japo unaishi haki gani unaitenda kwa wananchi wengine na kwa nchi yako?

Mauaji na utekaji umekuwepo Tanzania vipindi vyote. Wakati wa Kikwete tulijionea wasio julikana wakimteka Ulimboka, waandishi wa habari wakiteswa na kuuwawa. Mwanasiasa Mkongwe wa NCCR Dr. Mvungi alilalamika anafatiliwa baadae alivamiwa na kukatwa mapanga hatimaye alipoteza maisha.

Leo tunajifanya mabaya yote ni ya Magufuli. Tuache uzandiki. Magufuli aliirejesha heshima ya Tanzania.
Hakuna nchi duniani iliendelea kwa Demokrasia never. Marekani yenyewe wanawake wameanza kupiga kura miaka ya 60 japo walipata uhuru wao toka karne ya 18. Nchi nyingi za Ulaya zimeongozwa kimabavu ndo maana zilifanikiwa.

Leo mnadanganyika na Demokrasia na Human Right.
China inademokrasia gani? Na human rights zipi? Nchi za arabuni, Dubai, Saudia na nyinginezo wapi demokrasia na human right, mbona zimeendelea kuliko sisi tunao thamini wazungu.

Rwanda leo inasonga mbele wapi Demokrasia na human rights? Ethiopia inakuwa kwa kasi haijawahi kuwa na demokrasia wala human rights zenu. Libya ilikuwa bila demokrasia. Walipotaka Demokrasia wamejikuta kubaya.

Nasema hatuhitaji kuiga kila tuletewacho na mzungu. Tuwe na demokrasia yetu model tofauti na wazungu. Tunatofauti kubwa za kitabia na mazingira na wao hatuhitaji kuiga kila kitu. Kama ni human right Marekani imeua watu wangapi huko mashariki ya kati? Ni watu wangapi uuwawa marekani kila siku?

Imeua viongozi wangapi kwa uongo wa demokrasia.
Watanzania tubadilike hasa wachache tusiyoitakia mema nchi yetu kisa chuki binafsi. Umieni tu Magufuli atabaki kuwa kiongozi wa aina yake. Alie paisha jina la Tanzania. Nikizunguka ulimwenguni uwa naulizwa nchi ya Nyerere, kingine Magufuli alikuwa kiongozi mleta maendeleo, utasikia vizuri havidumu. Hao ndo wanao ongelewa sana.
Nawapenda Haiti, walikuwa hawampendi Rais wao, waliandamana kumpinga hakuleta maendeleo, ila alipouwawa Haiti waliumia, walihudhunika. Walisema japo walimpinga lakini hakustaili kuuwawa.

Hawa watu wanaubinadamu. Siyo baadhi ya watanzania, ambao kufa wanadhani ni kwa watu fulani tu, wanashangilia. Nami nasema mfanyao hivyo nanyi mtakufa na hamjajiuliza mtakufa vifo vya namna gani.
Narudia kusema Mch. Mtikila Nyerere alipo kufa alisheherekea. Leo yupo wapi? Je, kifo chake kilikuwaje? Japo tunapingana lkn tujifunze kuwa na utu. Pia tusidhani Mzungu ni kila kitu. Tunawaabudu sana. Na mzungu ukimshobokea anakusanifu. Wanapenda msimamo wa mtu.
Kuna mengine umesema yaliyo sahihi lakini kuna mengine, umesema kwa mahaba.

Hivi kwako wewe 12,000km+ na 2,000km +; nani amefanya kazi kubwa zaidi? Awamu ya Kikwete, zaidi ya 12,000km za barabara za lami zilijengwa. Barabara ndefu za kilometa nyingi. Wakati wa Magufuli zimejengwa chini ya 3,000km, nyingi ni barabara za mitaa mijini. Nani alifanikiwa zaidi?

Wakati wa Kikwete, per capita kwa miaka 10 ilipanda kwa $380, wakati wa Magufuli kwa miaka 5, ilipanda kwa $80. Nani alifanya vizuri zaidi?

Wakati wa Kikwete utalii ulikuwa unakua kwa 15%, wakati wa Magufuli 3.6%. Nani alifanya vizuri zaidi?

Ukuaji wa jumla wa uchumi wakati wa Kikwete ulikuwa 7%, wakati wa Magufuli ulishuka mpaka 1.9%, kisha ukapanda mpaka 4.5%, ndiyo ikawa mwisho.

Wakati wa Kikwete, ujenzi wa chuo Kikuu Dodoma. Wakati wa Magufuli hakuna.

Wakati wa Kikwete, ujenzi wa hospitali kubwa na za kisasa Mloganzila, taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Hospitali ya Benjamin Mkapa. Wakati wa Magufuli ujenzi wa vituo vya afya na hospitali, thamani yake yote haikufikia thamani ya Mloganzila pekee.

Magufuli alifaa kuwa msimamizi. Kwenye ujenzi wa barabara wakati wa Kikwete alisimamia vizuri, lakini kwenye uongozi mkuu wa nchi alipwaya sana. Hii naongelea kwa ujumla, siyo kwa kumlinganisha na Samia au Kikwete.

Ili tutoke mahali tulipo, tunahitaji kiongpzi mwenye uwezo mkubwa zaidi kuliko Magufuli, kuliko Kikwete, kuliko Samia, na kuliko Mwinyi. Tulihitaji kiongozi mwenye uwezo, angalao wa kiwango cha Mkapa. Watu wengi hawajui, lakini mambo aliyoyafanya Mkapa, ukimwacha Nyerere, hakuna Rais mwingine aliyeweza kuyafikia. Hata mafanikio madogo yaliyopo sasa, msingi wake ulijengwa na Mkapa.
 
[emoji23][emoji23][emoji23]Sasa kama utaendelea kuwaabudu namna hii utajitoa lini hapo ulipo ili nawe uwe na kifaa chako?

Mibavicha bure kabisa
Ni kweli nchi inahitaji kujenga uwezo wa ndani. Lakini utajengaje ukijitenga na waliokutangulia?

Tujifunze toka China. Wachina siku za nyuma walijitenga na nchi za Magharibi. Matokeo yake ikawa hohe hahe.

Baadaye wakagundua makosa yao. Wakafungua milango kwa makampuni ya mataifa ya Amerika na Ulaya. Makamouni ya Ulaya na America yakawekeza heavily in China, na yanaendelea kuwekeza. Mpaka leo China ndiyo nchi inayovutia wawekezaji wengi toka Ulaya, America na Asia kuliko nchi yoyote.

Matokeo yake, uchumi wa China ukapaa maradufu, maendeleo ya tekinolojia yakaongezeka sana. Leo hii, angalao katika makampuni makubwa 10 nchini Chima, moja, kampuni ya Huawei, ni kampuni ya China. Mengine yote ya kigeni, lakini wanapiga hatua. Ukijitenga hufiki popote. Unakuwa nao, huku unajenga uwezo wako wa ndani.
 
Kuna mengine umesema yaliyo sahihi lakini kuna mengine, umesema kwa mahaba.

Hivi kwako wewe 12,000km+ na 2,000km +; nani amefanya kazi kubwa zaidi? Awamu ya Kikwete, zaidi ya 12,000km za barabara za lami zilijengwa. Barabara ndefu za kilometa nyingi. Wakati wa Magufuli zimejengwa chini ya 3,000km, nyingi ni barabara za mitaa mijini. Nani alifanikiwa zaidi?

Wakati wa Kikwete, per capita kwa miaka 10 ilipanda kwa $380, wakati wa Magufuli kwa miaka 5, ilipanda kwa $80. Nani alifanya vizuri zaidi?

Wakati wa Kikwete utalii ulikuwa unakua kwa 15%, wakati wa Magufuli 3.6%. Nani alifanya vizuri zaidi?

Ukuaji wa jumla wa uchumi wakati wa Kikwete ulikuwa 7%, wakati wa Magufuli ulishuka mpaka 1.9%, kisha ukapanda mpaka 4.5%, ndiyo ikawa mwisho.

Wakati wa Kikwete, ujenzi wa chuo Kikuu Dodoma. Wakati wa Magufuli hakuna.

Wakati wa Kikwete, ujenzi wa hospitali kubwa na za kisasa Mloganzila, taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Hospitali ya Benjamin Mkapa. Wakati wa Magufuli ujenzi wa vituo vya afya na hospitali, thamani yake yote haikufikia thamani ya Mloganzila pekee.

Magufuli alifaa kuwa msimamizi. Kwenye ujenzi wa barabara wakati wa Kikwete alisimamia vizuri, lakini kwenye uongozi mkuu wa nchi alipwaya sana. Hii naongelea kwa ujumla, siyo kwa kumlinganisha na Samia au Kikwete.

Ili tutoke mahali tulipo, tunahitaji kiongpzi mwenye uwezo mkubwa zaidi kuliko Magufuli, kuliko Kikwete, kuliko Samia, na kuliko Mwinyi. Tulihitaji kiongozi mwenye uwezo, angalao wa kiwango cha Mkapa. Watu wengi hawajui, lakini mambo aliyoyafanya Mkapa, ukimwacha Nyerere, hakuna Rais mwingine aliyeweza kuyafikia. Hata mafanikio madogo yaliyopo sasa, msingi wake ulijengwa na Mkapa.
Upo vizuri.
 
Hatukurudi nyuma! Tuliingia uchumi wa kati ambapo hatukuwa. Watanzania tunaona na tunamkumbuka kwa mazuri
Anayefikiria kuwa Magufuli ndiye alituingiza kwenye uchumi wa kati, ni mjinga hasa, asiye na uelewa wowote.

Mkapa alipandisha per capita yetu kwa $400, Kikwete alipandisha per capita yetu kwa $380, na Magufuli alipandisha kwa $80. Nani alikuwa the weakest performer?

Projections za Mkapa, ilikuwa kwa vile Mwinyi alipandisha per capita $50, yeye kwa $400, anayefuata (Kikwete) akipandisha angalao kwa $800, na Rais anayefuata (Magufuli) angepandisha hata kwa $800 hiyo hiyo, Tanzania tungekuwa kwenye uchumi wa kati wakati wa awamu ya 5; tukiwa na per capita ya $2,400. Lakini mpaka leo tupo kwenye $1,100. Hatujafikia hata 50% ya matarajio ya Mkapa. Lakini wajinga wanashamgilia.

Ukweli ni kwamba, mpaka leo, Tanzania bado ni maskini sana, na mwanga haupo. Nchi kama Botswana ina per capita $18,110. Namibia $4,175, Madagasca $17,320 Ukiacha Madagascar iliyopata uhuru mwaka 1960, haya mengine ni mataifa yaliyopata uhuru baadaye sana baada ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom