Pre GE2025 Kauli ya Lema, Mbunge wa zamani wa Arusha juu ya Makonda inafikirisha sana

Pre GE2025 Kauli ya Lema, Mbunge wa zamani wa Arusha juu ya Makonda inafikirisha sana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapa Samia alinajisi nchi. Mtu mwenye kutilia mashaka kama huyu hakupaswa kabisa. Suala la drug dealers na Gwajima tu linatosha
 
Makonda anawatesa sana machadema!

Mlisemaga akitoka madarakani mtamshughulikia, ila kakaa bila cheo muda wote na leo kapewa cheo bado anawachachafya huku mmeufyata.
Sasa bora huyu je Dkt Magufuli ambaye ni mifupa na bado inawatesa. Sasa wamemgeukia Dkt Samia hahaha. Hawa ni chama mfu linaongozwa na wasiokuwa na akili
 
Hivi Lemma amemaliza kulipa madeni yake? Karibu benki zote zinamdai wakati akiwa ughaibuni, na nyumba zake Dar na Arusha ilikuwa zipigwe mnada.

Pia alimponza kaka yake aliyekuwa akimiliki Villa Park Mwanza mpaka akafungiwa. Aliigeuza Villa Park ofisi ya Chadema ya Mkoa, wakati Villa Park alikuwa kapanga katika eneo la CCM.
Kwa hiyo kwa maelezo haya tayari Makonda kawa msafi?
 
Mbunge wa zamani wa Arusha juu ya Makonda inafikirisha sana na kuogofya.

Nafikiri mh Lema anajiamini sana kupitiliza kwenye taifa linalo on ongozwa na ccm.

Naomba tumsikilize kwa makini alafu tujadili.

View attachment 2886672
Uwezo wa Lema mdogo sana....Yaani wao wanapfanya jogging na kuyaita maandamano wanakua wamesahau kua hamna hivyo alivyo vitaja.
Wakati wanasema Lowassa ni fisadi alafu mwisho wa cku wakampa nafasi ya kugombea Urais
 
Lema ni mtu mjinga na wa ovyo tu. Mtu mnamuona nyie mbaya kwa kua amedhuru maslahi yenu binafsi ya kifisadi. Mnamzushia uongo wa mauaji na ukatili bila ushahidi wowote. Mahakama zipo mbona hawaendi kumshitaki ili afungwe. Kipi wanaogopa. Mama kawapa fursa kumshitaki sabaya kwa kua na yeye na wao ni kitu hikohiko lakini mbele ya haki wameangukia pua. Na kwa makonda wakishitaki ni hayohayo tu maana ni uzushi tu dhidi ya mtu anayetetea maslahi ya umma na kutetea wanyonge.
Ebu twambie sababu haswaa iliyo wafanya USA kumpiga marufuku Makonda kukanyaga USA
 
Shukrani saaana mkuuu lemma kwa kusimama kidete kumsemea Ben saa 8. Huwa namshangaa mbowe kukaa kimya huku familia ya Ben saa 8 iko njia panda pia serikali,jeshi la polisi wanaona ni sifa kuvunja sheria.huku wakitutaka sisi kutii sheria bila shuruti.
Kwanza ilipaswa kuandamana juu ya mauaji ya Ben.
 
Makonda anawatesa sana machadema!

Mlisemaga akitoka madarakani mtamshughulikia, ila kakaa bila cheo muda wote na leo kapewa cheo bado anawachachafya huku mmeufyata.
na zaidi sana wanaweweseka mno hawa ndrugo zango waTanzania wa upinthani 🐒
 
Alitakiwa aseme makonda alimwambia nini kuhusu Ben sanane kama yeye Lema anaogopa kusema alichoambiwa na makonda, je huyo makonda aliemfanyia ubaya au pengine kumuua Ben sanane akiulizwa kuhusu hilo ataweza kusema? Yaani muuaji aseme ameua?
Ilitakiwa afichue uovu wa makonda na siyo kumfichia siri kushindwa kufichua siri na kutoa ushahidi ni kushiriki uhalifu.

..waandishi wa habari wamuulize Makonda kuhusu tuhuma za utekaji na mauaji dhidi yake.

..tuhuma kama hizo zingekuwa zinasema kuhusu kiongozi wa Chadema waandishi wangemuandama kwa maswali kila wanapopata nafasi.

..waandishi wa habari hapa Tanzania wanaogopa kuwauliza viongozi wa Ccm maswali magumu.
 
Back
Top Bottom