Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

R.I.p kanali.............
Inavyosemekana dereva bajaji anaundugu na kigogo mkubwa tu hapa bongo.....so ngoma inaenda kua drooo........waswahili wanasema ukiyajuaaa ya mbele wenzako wanajua ya nyuma....
Na uyo kigogo kasema dogo asiguswe hata na kidole ataua mtu............
Yani una ndugu kigogo halafu waendesha bajaji?😂🤣only in bongo
 
Acha yamkute Bangi, Ushamba na kutaka Sifa za Kijinga kwa Wana ( Washikaji ) Kijiweni zimemuongoza vibaya.
Hawa boda na bajaj wabadilike kuna wengine jambo dogo tu wanalifanya linakuwa kubwa sijui ni uelewa mdogo. Na silaha wanazipenda sana wengine wanatumia kufanya uhalifu kwa mteja hasa nyakati za usiku.
 
Vijana wengi walishavurugwa (tulishavurugwa) kisaikolojia, wapo wengi ambao hawalipi kuchukua maamuzi magumu kama huyo mtuhumiwa, TUNAKOENDA NI TATIZO KUBWA SANA ZAIDI YA HILI. Kwani vijana hawana ajira, hawako vizuri kichwani, matatizo kibao kila upande, huyo ni mmoja ambaye kamezeshwa sumu na mfumo wa maisha ya sasa, na sio peke yake wapo wengi tu kama huyo,,,
 
Watamdedisha tu
Na ndugu nao hawatakubali watamalizana
Vijana wengi walishavurugwa (tulishavurugwa) kisaikolojia, wapo wengi ambao hawalipi kuchukua maamuzi magumu kama huyo mtuhumiwa, TUNAKOENDA NI TATIZO KUBWA SANA ZAIDI YA HILI. Kwani vijana hawana ajira, hawako vizuri kichwani, matatizo kibao kila upande, huyo ni mmoja ambaye kamezeshwa sumu na mfumo wa maisha ya sasa, na sio peke yake wapo wengi tu kama huyo,,,
 
Kanali upumbavu gani?ukileta ujinga Ahera madukani inakusubiri,yaan mtu anacheo cha tano jeshini anakua na akili za makuruti.


NapitaKamaRadi
Hawa wanajeshi huwa wana ubabe wa kifala sana kuna siku aling'ang'ania kumbeba binti pale mnarani kwenye bar ya fire ila tukamuokoa yule binti badala utongoze unaleta ubabe wa kifala eti mnanijua mimi ni nani
 
Inasemekana ( kwa aliyenipa Taarifa Kamili kuwa ) Dereva Bajaji jana Usiku katika Baa Moja maarufu iliyo kwa ndani ( Mafichoni kidogo ) mkabala na Petro Station ya PUMA Kawe alipishana Kauli na Mwanajeshi ( tena Mkubwa wa Cheo cha Kanali ) kuhusu Kuzibiana njia ya kupita.

Ambapo Afande Kanali alikuwa Kapaki Gari lake lililokuwa limezuia njia kwa mbele na Dogo ( Dereva Bajaji ) kuhoji kwanini Afande aliziba njia hali iliyomkwaza Afande ( wa Cheo cha Kanali Muro kama sijalikosea Jina lake ) ambapo Afande Kanali akatoka ndani ya Gari lake na Kumzaba Makofi Dereva Bajaji huyo.

Kisha nae ( Dereva Bajaji ) kwa Hasira akaamua kwenda kuchukua Bisibisi Bajajini Kwake na kuja Kumchoma nayo Afande Kanali upande wa Moyo hali iliyomfanya akimbizwe Lugalo Hospital kwa Matibabu na Umauti kumkuta huko huko Wodini.
Ubabe umezua umauti.
 
Sema washua wenye mamlaka huwaga wanajisahau sana , Kuna video nmeona mtandaoni Kuna dogo alikua anaendesha ist alichomekeana na land cruiser flan nyeus jamaa akaamza kumletea ubabe wa ki CIA dogo road kila akienda huku jamaa linamzibia njia dogo akaenda TikTok live akawa ana broadcast the whole shit maana alishahis hatari jamaa kufika makumbusho aka block njia akashuka kwa gar akaonekana na suti yake ya uzalendo nadhan alipigia wadau wakatoka mule chimbo lao la idara wakamuongoza dogo kuingia tunduni aku anaendelea kurusha mubashara tukio watu wa mabaka ya kenge wakashtukia kama mwamba anawarekodi ndo nkajua kabisa mwamba kaisha mule ndani kamera hapapatani kabisa na msala wa dogo sidhan ata familia yake kama inaweza kuusovu labda kwa vile sura za wahusika ziko online zinaweza kutumika kwenye mahakama za jadi kupata haki kama hakuachiwa lakin
Nchi za ulimwengu wa tatu zina mambo mengi sana ya ajabu ajabu
 
Vijana wengi walishavurugwa (tulishavurugwa) kisaikolojia, wapo wengi ambao hawalipi kuchukua maamuzi magumu kama huyo mtuhumiwa, TUNAKOENDA NI TATIZO KUBWA SANA ZAIDI YA HILI. Kwani vijana hawana ajira, hawako vizuri kichwani, matatizo kibao kila upande, huyo ni mmoja ambaye kamezeshwa sumu na mfumo wa maisha ya sasa, na sio peke yake wapo wengi tu kama huyo,,,
Kwahiyo ukimezeshwa sumu ndio uende kuua ?


Kila mtu mwenye ugumu wa maisha akisema awe violent nchi itakalika?


Hawa bodaboda Huwa wanajiona wajanja sana

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Ndugu zangu, Cheo ni kazini kwako. Na cheo chenyewe kitakutumikia endapo utajihesimu na kufata misingi na taratibu.

Thamani ya uhai, ni sawa kwa kila mmoja. Hakuna cha kanali wala cha dereva boda, thamani ya uhai wetu zinalingana.

Muheshimu kila mmoja na epuka ugomvi kwa gharama yeyote. Usianzishe ubabe wako kwa sababu ya nafasi yako. Tena sehemu yenyewe ni sehemu ya kulewa. Kila mtu akili zimeshamruka. Damu zinatembea kasi, pombe inakuwa kiongozi.

Mimi ni raia, ila kitu ambacho labda kitaniua siku moja ni kutokubali kuonewa. Sipo tayari kuonewa kwa gharama yeyote.

Iwe Generali au kuruta au raia mzibua vyoo, kila mmoja amheshimu mwenzake. Timing ni kitu kibaya sana. Na utajitutumua ukiwa hai tu. Ukishapigwa bisibisi ukafariki, huna tena cha kufanya. Na mateso atakayopokea muuaji wako hayana tena thamani kwako, haitarudisha uhai wako.

Eti umchape mtu makofi kwa sababu wewe ni mwanajeshi? Kuondoa tu gari na kumpisha mtu na mikosi yake apite ingepunguza nyota? Akili finyu.

Nachukia sana hii misemo kuwa kuna baadhi ya watu kwa sababu ni walinzi, wana uwezo wa kujiamulia kufanya chochote. Huu ni upumbavu.

Ukitaka kuheshimika, heshimu wenzako kwanza.
 
Back
Top Bottom