Kaya 644 Magomeni kota zagomea kusaini mkataba kununua nyumba

Kaya 644 Magomeni kota zagomea kusaini mkataba kununua nyumba

Wajengewe kwa mkataba upi?

Hivi kama serikali ilivunja nyumba za watu bila malipo,

Hili la wapangaji hewa litawashinda?

Hao walikuwa wapangaji sio wenye maeneo wala ardhi haikuwa Yao,
Hawakuwahi kulipa Kodi ya ardhi wala jengo hapo Kota.
Sasa wanachodai nn?

Wakati mwingiine upole ukizidi Sana unakuwa ni tatizo.

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
Si ndo demokrasia na uhuru uliopitiliza. Kila mtu anadhani anauwezo wa kuamka asubuhi na kulia shida zake na zikatatuliwa.
Hili swala sijui lilianzia wapi
 
Wao ni wapangaji tu,
Tena walilipwa na pesa z kwenda kupanga nyumba miaka 3.

Tatizo ni kwamba wamevamia wajanja wa mjini na kuwaweka watu pandikizi humo ili baadae wamiliki hizo Kota.

Mimi nilishafuatwa na jamaa kwamba Kuna mtu anaandikisha wakazi wa Kota ,
Na anahitaji 1 million aniweke kwenye group la wakazi.

Wamedanganyana kwamba watapewa bure,,
sasa Kuna watu humo wanaugulia maumivu ya 1 million za kuhonga.

Lengo Lao ni kuzipata kwa rahisi ili na wao waziuze kwa wahindi kama ilivyokuwa kwa NHC Upanga,kkoo,Posta,Fire,keko,nk..

Serikali isimamie kwenye bei hiyo,,isipunguwe hata thumni.

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
Hakika,Serikali isimamie hvyo hvyooo
 
ila ninachowaonea huruma, watakaokaa mle, wajue kuna service charge (umeme, maji, majitaka,usafi). ama la, yatakuwa magofu kama ya nyumba za polisi muda si mrefu.
 
Kwahiyo unataka kusema hakuna aliyeunganishiwa umeme kwa 27K
Hata mimi nilifungiwa kwa 27k, lakini hii bei ya magu haiakisi bei halisi ya kuwekewa umeme. Bei tu ya ule waya wa kutoa umeme kwenye nguzo ya tanesco kuuleta kwenye nyumba yako ni 10k kwa mita. Bado mita na vitu vingine
 
Wengi wanaoishi hizo nyumba ni watumishi wa umma, wanalipa kodi wanapojisikia PIA kodi ni ndogo sana, watumishi wa umma wanapenda dezo sana, na wengi walioingia hapo ni kwa vimemo.

sasa wao wanataka wauziwe kwa bei wanazozitaka wao (inaonekana kabisa), serikali inaela ujinga, eti wanaenda kumwambia Raisi,

watu weusi tuna shida mahali, KABISA
Hahaha.. Mbeleko imeanza kutatuka.
 
Nyumba za makazi zikijengwa Chanika hizo biashara kwenye hayo maeneo zitafanywa na wanyama au wadudu?
Kwanza fahamu maana ya CBD, yaani central business district, yaani unasafiri kuja eneo la biashara kufanya kazi na kurudi maeneo ya mbali ya makazi ambayo ni nafuu kimakazi!! Huna kazi yenye kueleweka unang'ang'ania kukaa CBD kimakazi!??? Hapana!! Hata ulaya haipo
 
Ni uhuni uko hapo magomen. Kuna mana tuko mtaa mmoja ameachiwa nyumba na mumewe.

Ameifungia chini tena ipo vizuri. Kaenda kupiga kambi kule magomeni ili ionekane hana nyumba. Na ana mtoto mmoja tu. Tena ni mvuta bangi. Aliyekataa hata kusoma.

Yaani watanzania ni mara nyingi tunalaumu viongozi lakina hata sisi tunu ya uzalendo hatuna. Na anajidai ameokoka. Kwanini asiache wenye uhitaji kweli wakakaa humo? Mungu atusanehe hakii.
 
Kabisa,,

magomeni kota walikuwa wanakaa bure miaka Zaidi ya 30,
Walipoambiwa wahame wakasema hawana pa kwenda,,
Serikali ikawalipa pesa za Kodi.,
Kuna watu nawajuwa walishajenga maeneo Yao sehemu nyingine muda mrefu na pale waliweka watu kama walinzi kulinda Kota zao walizokuwa wanaishi..

Na wanapata stahiki zote kama wapangaji wa Kota wakati kiuhalisia hawaishi hapo ,,

Serikali ichukuwe hatua kwenye Kota zote wanazoishi wapangaji wake.
%100 wanaishi bure bila malipo yeyote,

Mwisho wa siku kwenye kuhama linakuwa tatizo Kama Kota magomeni.

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
Basi NHC ina ugonjwa wa kufisha. Kwanini wanatizama hayo yakijiri.?
 
Kwani wakati wanajengewa maghorofa walikubalianaje?

Hapa kuna changamoto hsikutolewa elimu kwa kina.

Bei huenda ikawa sawa, hivi Magomeni kupata eneo pekee(kumhamisha mtu) yake ni kiasi gani?
 
Kwani wakati wanajengewa maghorofa walikubalianaje?

Hapa kuna changamoto hsikutolewa elimu kwa kina.

Bei huenda ikawa sawa, hivi Magomeni kupata eneo pekee(kumhamisha mtu) yake ni kiasi gani?
Walipewa Kodi miaka 3 wakapange kwengine,
Wakaambiwa watarudi wakae bure miaka 3.

Kwa hili nawalaumu serikali.

Inakuwaje mpangaji wa eneo la serikali wageuzwe kama wamiliki wa eneo?
Hao wakazi wa magomeni kota ni wapangaji tu.
walipaswa wapewe notice ya kuondoka ,,
Kama watashindwa kulipa gharama husika.

A tenant will always be a tenant.

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
 
Basi NHC ina ugonjwa wa kufisha. Kwanini wanatizama hayo yakijiri.?
NHC wanakuwa hajuwi kama watu wanauziana umiliki wa upangaji.

Mfano Mimi nina rafiki yangu alikuwa mpangaji pale ghorofa za keko NHC.
Ilikuwa ni chumba na siting room,Jiko choo,store,

Jamaa kipindi kile 2005 alikuwa akilipa 50000 tu.
Akaja akatokea mtu akampisha kwa 7 millions cash.
Yeye akahamia kwenye nyumba yake aliyojenga.
Kinachofanyika ni mpangaji wa zamani kwenda NHC na kubadilisha umiliki wa upangaji kwa mpangaji mpya.

Mpangaji ataendelea kulipa pesa Ile Ile kila mwezi,
Hakuna mambo ya pesa ya udalali wala Kodi ya mwaka mzima ..

Kwahyo hizo NHC flats za Posta,kkoo,Upanga zote zilikuwa zinamilikiwa na watu weusi baadae wakawauzia wahindi na waarabu.,

Hao wapangaji wa magomeni kota wasilete janja janja ,,
Kama hawana cash wakanunuwe kisemvule na chamazi.
Watapata nyumba kwa pesa hizo 12 millions na sio magomeni.

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
 
Watafutiwe Viwanja chalinze, wajengewe chumba sebule wapewe!, ili kupisha wenye uwezo wazinunue kwa bei stahili 75-80ml.
 
Watafutiwe Viwanja chalinze, wajengewe chumba sebule wapewe!, ili kupisha wenye uwezo wazinunue kwa bei stahili 75-80ml.
Wasijengewe nyumba waliovunjiwa nyumba zao ,
Tena walikuwa wamiliki halali wa maeneo yao,
Wajengewe watu ambao ni wapangaji..


Kamai litaiwezekana hilo basi Africa kweli ni
shit hole

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
 
Duniani hakuna kitu cha bure, hao wananchi walipaswa kulielewa hilo tangu awali...

Kitachofanyika labda ni kupunguziwa makato kwa mwezi lakini sio kukaa bure wakati serikali iliweka mpunga wake hapo...
 
View attachment 2508191

Dar es Salaam. Wakazi 644 wa Magomeni Kota wamegomea kusaini mkataba wa kuanza kununua nyumba hizo, kwa madai kwamba bei waliyoletewa sio rafiki na haiendani na hali ya uchumi wao.

Aidha wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aingilie kati kwa kuwa bei ya Serikali iliyowasilishwa ni kati ya Sh48 milioni na Sh56 milioni ni kiwango kikubwa wanachochukulia kama mtego wa kutaka kuwafukuza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa juzi na serikali kupitia kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambaye ni msimamizi wa mradi huo, mkataba huo unaanza kutumika kuanzia Februari 8 mwaka huu hivyo Kaya hizo zinapaswa kusaini kwa bei waliyoletewa.

Mwanasheria wa wakazi hao, Twaha Taslima akisoma barua iliyoandikwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Daud Kandoro, kwenda kwa wakazi hao, jana siku ambayo walifanya kikao mkoani Dar es Salaam, alisema bei iliyowasilishwa na serikali awali ilikuwa ndogo.

“Bei ambayo ilipendekezwa na Serikali awali ilikuwa ni Sh12 milioni hadi Sh17 milioni, iliyotolewa Juni mwaka jana, haikukidhi thamani ya eneo, haikujumuisha faida wala huduma za maeneo yanayozunguka makazi hayo ambayo ni jumuishi,” amesema.

Taslima amesema, "Njia mojawapo ya kuchukua ni kuiomba Serikali au kwenda mahakamani. Bei ya chumba na sebule kwa Sh48. 5 milioni na vyumba viwili na sebule Sh56.8 milioni inaweza isiwe rafiki na mnunuzu asimudu," alisema Taslima.

Mwenyekiti wa Wakazi wa Magoneni Koti, George Abel, amesema kwamba bei zilizokokotolewa siyo rafiki kwa wakazi hao, licha ya Serikali kuongezewa mkataba wa kulipa na kuishi kutoka miaka 10 hadi 15.

Amesema kuwa bei hiyo inatakiwa kila mkazi alipie Sh300,000 kwa mwezi hivyo kwa mwaka ni Sh3.6 milioni akisema kiasi hicho ni kikubwa ikizingatiwa baadhi ya wakazi tayari ni wazee na wastaafu.

"Tumepokea barua hii ikiwa zimebaki siku tatu tu kwamba tusaini mkataba wa manunuzi, tukutane tujadiliane kabla ya tarehe 8, Februari, mwaka huu, hizi bei si rafiki haziendani na hali za wakazi walio wengi," amesema Abel.

Mmoja wa wakazi wa nyumba hizo, Salama Goronga (65), amesema barua hiyo iliyosomwa kwao, ikionyesha bei hiyo imewahuzunisha kwa kuwa haiendani na hali zao kimaisha.

"Mimi nina wajukuu, na iliposomwa barua machozi tu yameanza kunitoka hiyo pesa nitatoa wapi, nitaondoka hapa niende wapi," amesema Salama.

Mkazi mwingine, Mwajuma Hamisi (82), amesema ana watoto wawili wa walioolewa ndio wanaomtunza kwa kumnunulia chakula na mahitaji mengine, hivyo itawawia vigumu leo hii waanze kumtafutia kodi mara atakapoondoka kwenye makazi hayo kutokana na kushindwa kulipia.

"TBA wanaotaka hizo nyumba, leo bei hii, kesho hii, tutalipaje mimi mzee, wanitoe hapa si aibu kwangu, mamilioni hayo nitayatoa wapi," amesema Mwajuma.

Alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi kutoka idara ya miliki TBA, Said Mndeme amesema “Masuala hayo aulizwe mkuu wa taasisi ndiye anayejua,” amesema.

Mwananchi

12m? Kweli hamna shukrani
 
Back
Top Bottom