Kijana huyu kaniumiza sana ndugu wabaya sana

Kijana huyu kaniumiza sana ndugu wabaya sana

Yule mwamba sio afya ya akili wala nini ule ni mzigo kabisa. Afya gani ya akili tiba ni bangili ukiivua tu unatoroka!. Mtu anatembea umbali wa labda tuseme Tegeta hadi Mkuranga Mji kwa dakika chache tu. Tena yuko peku hana viatu na hatoki jasho hupo fit anawashangaa tu mliomfuata na kumrudisha shule.

Hii nimeishuhudia mwenyewe kipindi niko shule sasa huo ni ugonjwa gani wa akili?. Na jamaa alikuwa mtu mpole sana bwenini na ni kipanga kweli kweli.
Sasa mkuu wewe utasemaje mtu hana tatizo la akili kama huna taaluma husika? au unayo?

Na hayo mambo ya uchawi mbona waafrika tunayashikilia sana wakati hayaleti maendeleo?
 
Haya mambo yapo ila hospital zetu nazo saa ingine they do wrong diagnosis sasa ukija kuchanganya na roho za kutu za jamii yetu ndio hivo.
 
Sasa mkuu wewe utasemaje mtu hana tatizo la akili kama huna taaluma husika? au unayo?

Na hayo mambo ya uchawi mbona waafrika tunayashikilia sana wakati hayaleti maendeleo?
Wenzetu mambo ya Uchawi 'Halloween" wanatengeneza mabilioni.

Na kule U.K harry poter ndio usiseme mabilioni ya mabilioni ya £

Uchawi unaeleta maendeleo, inategeme fikra zako tu.

Maendeleo yapo.
 
Kuna wachawi wa rais hapo ikulu

Uchawi haupo. Ni imani za wajinga tu

Kiufupi, wajinga wakishindwa kuelewa kitu wanasingizia uchawi. Hakuna kitu kinafunua ujinga wa mtu kama imani yake juu ya habari za kichawi. Jinsi ilivyo kali ndivyo ujinga wake ulivyo mkali zaidi.
 
Tanzania matatizo ya afya ya akili yanaonekana ni uchawi.

Hakuna elimu ya afya ya akili.

Hakuna wataalam, na tiba toshelevu ya afya ya akili.

Kama unabisha muulize mtu yeyote magonjwa matatu tu ya akili uone...

Hii ni changamoto kubwa.

Tunaamini uchawi tu, hadithi za kutungwa ambazo hazina tija yeyote. Mwishoni mtu akishindwa kabisa kusaidika atatengwa kwa visingizio vya laana na mikosi.
We umezaliwa 2010 unajua nini zaidi ya definition ya chemistry!
 
Haya mambo nilikuwa siamini mpaka nilipozibwa pumzi na kukabwa roho na kunipa maradhi kwa kunilisha wakati nimelala wanafamilia wenye roho za kishetani. Ila nina ujumbe wao nawaambia kumamazen…u wachawi wakubwa.
 
Ni rahisi kusema haupo kwa kua halijakukuta, ila likikukuta utaelewa tu.
Siku ya mtihani wa taifa darasa la saba ,baada ya mtihani wa kwanza tulipata chai kama ilivyo ada ,kisha tukaingia pepa ya pili.Ikumbukwe pepa zilikua tatu siku hio,pepa ya pili tulipiga mpunga kama ratiba ilivyoapangwa.
Sasa baada ya kuingia pepa ya mwisho ,nikaanza patwa na maumivu makali mno mno ya tumbo nilijikaza mpka nikamaliza mtihani .Tumbo langu lilijigawa pande pili likitenganishwa na kitovu yaan juu na chini,Kufika nyumban kwan napo haikua mbali hali ilizidi kua mbaya zaidi.
Nilifikishwa hospital ya mkoa kwa kipindi hiko majibu yaliokuja ni kua utumbo ulikua umeenza kujifunga kwa sababu inaonesha sijala kwa muda mrefu (nimekaa na njaa muda mrefu).
Dawa nilizopewa hazikisaidia ila ikumbukwe tuliruhusiwa kurud home,jirani alinitib kwa dakika 5 kwa kunipa dawa nyeusi na aliponitizama akasema ni uswahili .Nachoka kuandika ila matukio yako matatu makubwa na moja limeniachia alama ya kudumu maishan ,nawachukia sana wachawi na sitokaa niwapende kamwe
 
Back
Top Bottom