Tetesi: Kikao cha dharura cha wakuu wa vyuo vyote vikuu nchini kinaendela mjini Dodoma , kuna tatizo kubwa

Tetesi: Kikao cha dharura cha wakuu wa vyuo vyote vikuu nchini kinaendela mjini Dodoma , kuna tatizo kubwa

Niulize swali hivi Elimu Msingi inayoishia darasa la 6 Mtaala wake umeanza kutekelezwa???

Kama ndio ina maana mwaka huu kuna mitihani miwili ya wahitimu yaani wanaomaliza mfumo wa 7 Msingi na hawa wa miaka 6.??????

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ZEIN inter university challenge iliishia wapi? maana pale ndio nilikuwa ninapima ubora wa vyuo vyetu vya bongo dgidi ya vyuo vya Nigeria, Kenya na Uganda maana kila swali likiulizwa mmbongo utasikia PASS, PASS ,PASS
 
Mnaongelea kuwepo kwa rushwa ya ngono tu kama vile hamuelewi jinsi tuhela twa mikopo ya wanafunzi tunavyoishia kwa wahadhiri mafisadi ili watoe maksi za upendeleo kwa wavulana na wasichana!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo sio chuo tatizo laanzia shule za msingi....

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu una akili sana.Na chimbuko la msingi ni maslahi duni kabisa anayopewa mwalimu wa msingi na sekondari.Hawa watu wamesahaulika,dharaulika,kila mtu anaenda kuwafokea na kuwatishia.Nimeongea na walimu wengi sana aisee wapo kwenye mgomo baridi.Yani they don't care kuhusu kufundisha vile inavyotakiwa kabisa.Halafu baraza la mitihani linaogopa kufelisha wanafaulisha then haooo chuo.Waendelee kula maisha ila kizazi cha hovyo kinajengwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni Kweli kabisa. Elimu ya Tanzania imeporomoka kwa hatua za makusudi hadi kufika hapa ilipo. Mwalimu Nyerere aliporomisha elimu iliyoachwa na mkoloni kwa kuanzisha UPE. Kwenye UPE sifa za kuwa mwalimu wa shule ya msingi ikawa kujua kusoma na kuandika na mafunzo ya muda mfupi. Wakapita akita Mungai na Uharibifu wao Elimu ya Sekondari. Akaja Lowasa na Kulazimisha kila Kata iwe na Shule ya Sekondari. Jambo Jema nila maandalizi. Shule zipo hazina walimu bora wala vyumba vya maabara na stadi za maisha. Elimu ya Sekondari imeongeza idadi ya wahitimu na si ubora. Ugonjwa wa idadi ukahamia vyuo vikuu. Kikwete akajenga chuo kikuu kibwa zaidi Tanzania kule Dodoma. Wenyewe wanakiita UDOM. Uwiano wa wanafunzi kwa mhadhiri mmoja hapo UDOM 200. Yani mwanafunzi anasoma miaka mitatu hajui hata sura ya mhadhiri mmoja. Wahadhiri hawa hawalipwi vizuri hivyo hawana muda wala motisha wa kusahisha kwa umakini mitihani, wala mafunzo kwa vitendo. Unatarajia Nini?

Kuanzia Elimu ya Msingi, ambapo ndipo mizizi ilipo ya Elimu, walimu wanaochaguliwa ni wale waliofeli, ili wasilipwe vizuri, na hivyo hawafanyi kazi ya ualimu, bali kushinda shuleni na watoto wetu. TUNACHEKELEA. Sekondari zetu zina walimu sawa na wanafunzi wao. SIYO MAKOSA YA WALIMU. Walipata Elimu Duni, nao wanfundisha hivyo kwa uduni wao. Wengi huchoka na kuanza KUPENDANA.

Hawa wote ambao wamekosa elimu ya msingi na sekondari iliyobora, ndio wanaingia vyuo vya juu Tanzania. Hawana misingi, hawana ubora, hawana lugha. Wanakutana na mhadhiri ambaye nayo ni zao la mfumo huohuo ulioharibika 1978. Duara hili la uduni wa elimu Tanzania haliwezi kuzalisha Wahitimu Bora kuweza kutenda na kushindana katika soko la Afrika Mashariki na Afrika kwa Ujumla. Usipokuwa kwa wachache waliondolewa hapa nchini tangu elimu ya msingi. Ukiingia Twitter utawajua.

Wanafunzi wenye vipaji na ambao wanafika vyuo vya juu wana hali mbaya ya maisha. Hawana fedha za Kujikimu na Jamii haijali. Wanalala na njaa, kuwa wachafu, na kusinzia mbele ya wahadhiri.

MAPUNGUFU HAYA HAYAWEZI KUMALIZWA KWA KIKAO CHA DHARURA. INAHITAJIKA MIKAKATI YA KUONDOKANA NA DUARA LA ELIMU DUNI. MIMI NA WEWE TUNATAKIWA KUCHUKUA HATUA. HAWA WENYE MIAKA HAMSINI NA ZAIDI MADARAKANI WAMEKWAMA.
Janga limeanzia mbali sana hili. "My wangu".

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanapoteza muda na pesa za walipa kodi. Tatizo ni kwamba wizara inataka kukusanya kutoka isipotawanya.. bhaasi. Wizara inasimamiwa na profesa lakini ana mtizamo kama wa mbuni, kufunika kichwa kwenye mchanga.
Tatizo ni kwamba serikali inakwepa jukumu muhimu kuwekeza kwenye vyuo vikuu, haijengi miundombinu, haiajiri wanataaluma, waliopo ni wazee na hawalipwi inavyostahili. Wanafunzi ni wengi kupindukia uwezo wa vyuo katika kila namna. Mwanataaluma anafundusha wanafunzi 500+, atoe assignments 2, seminars 2, labwork 3, theory test 2, final exam 1, asimamie yeye, asahihishe yeye, atoe matokeo yeye, na ahakikishe kila mwanafunzi aliye na tatizo analitatua kikamilifu.. Huo ni uongo na haiwezekani kamwe.

Tatizo wasomi wamekuwa wanafiki mno, hayo hawayasemi, wanaishia kuchakachua elimu. Ndo maana si ajabu kukutana na mhitimu asiyewezaandika barua ya kuomba kazi

Uhuni mtupu. Tatizo wanalijuwa, hakuna mchawi mwingine tofauti na serikali
 
Kuna tetesi kuwa kikao cha dharura kimeitishwa mjini Dodoma kinachowakutranisha wakuu wote wa vyuo vikuu nchini.

Hatua ya kuitia kikao hicho imetokana na hali mbaya ya wahitimu wa vyuo vikuu nchini ambapo mara wanapoajiriwa katika sehemu mbalimbali wanashindwa kufanya kazi ambazo zingine ni rahisi kabisa.

Wahitimu wengine wanashindwa kuandika barua za maombi ya kazi, kushindwa kufanya majaribio mbalimbali na hata pia kushindwa kuandika taarifa kwa kwa lugha ya Kiswahili na pia kwa lugha ya kiingereza.

Waziri wa elimu profesa Naalichako ameamua kuitisha kikao hicho kujadili kuona wapi kuna tatizo.

Pia kikao hicho kinatarajiwa kujadili hali ya utoaji wa rishwa ya ngono kwa wanafunzi wa kike vyuoni ambapo huadiwa alama za juu ili kufaulu mitihani yao ya mwaka wa mwisho kwa masharti ya kushiriki vitenndo vya ngono na wahadhiri wao.

Ni muhimu taarifa kama hizi zikawekwa kwenye umma ili kuuelimisha kuhusiana na hali halisi ya kudorora kwa kwa kasi ya juu kwa utaji wa elimu ya juu nchini na kuachia wanafunzi khasa wa kike kutegema kutoa miili yao ili kupata alama nzyri.
Hao wanaojadili na wanaojadiliwa wote sawa sawia.sasa ndalichako ukimsikiliza pumba zake anatofauti gani na yericko nyerere.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uendeshaji wa elimu hapa Tanzania wapewe kanisa Katoliki waiendeshe angalau kwa miaka 10 ili waweke msingi thabiti halafu ndio serikali ikabidhiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
Waking kibao mbona wanapitia shulebzao kuanzia chekechea Hadi vyuo vyao vikuu vilivyoko nchini.

Kuna vyuo vyao vikuu Vingine vimefungwa na serikali kwa kukosa ubora
 
Tatizo siasa tumeipa kipaumbele sn.
Ajira zenyewe kujuana Elimu imekua bure. Tunatarjia nn?
 
Kuna tetesi kuwa kikao cha dharura kimeitishwa mjini Dodoma kinachowakutranisha wakuu wote wa vyuo vikuu nchini.

Hatua ya kuitia kikao hicho imetokana na hali mbaya ya wahitimu wa vyuo vikuu nchini ambapo mara wanapoajiriwa katika sehemu mbalimbali wanashindwa kufanya kazi ambazo zingine ni rahisi kabisa.

Wahitimu wengine wanashindwa kuandika barua za maombi ya kazi, kushindwa kufanya majaribio mbalimbali na hata pia kushindwa kuandika taarifa kwa kwa lugha ya Kiswahili na pia kwa lugha ya kiingereza.

Waziri wa elimu profesa Naalichako ameamua kuitisha kikao hicho kujadili kuona wapi kuna tatizo.

Pia kikao hicho kinatarajiwa kujadili hali ya utoaji wa rishwa ya ngono kwa wanafunzi wa kike vyuoni ambapo huadiwa alama za juu ili kufaulu mitihani yao ya mwaka wa mwisho kwa masharti ya kushiriki vitenndo vya ngono na wahadhiri wao.

Ni muhimu taarifa kama hizi zikawekwa kwenye umma ili kuuelimisha kuhusiana na hali halisi ya kudorora kwa kwa kasi ya juu kwa utaji wa elimu ya juu nchini na kuachia wanafunzi khasa wa kike kutegema kutoa miili yao ili kupata alama nzyri.
Kikao cha namna hii kimechelewa sana. Hicho kikao kitatenda jambo jema sana kama kitaamua iundwe tume yenye watalaam na wafanye utafiti wa kuna na kuja na suluhisho la matatizo. Hiyo tume ikusanye maoni kutoka kwa wadau wengi na itoe mapendekezo ya ni nini kifanyike. Juzi nilikuwa nafanyakzai fulani na dada mmoja aliyemaliza Masters Degree Chuo Kikuu Mlimani, du.... aisee Mungu ndiye anajua. Mambo basic ya four six hajui yaani kichwani ni mweupee...
 
Watu waliohitimu vyuo miaka ya nyuma asilimia kubwa ni wapumbavu mno, wanajikuta wapo smart, hapo asilimia kubwa wameunga elimu na vyeti Feki kibao
 
Kikao cha namna hii kimechelewa sana. Hicho kikao kitatenda jambo jema sana kama kitaamua iundwe tume yenye watalaam na wafanye utafiti wa kuna na kuja na suluhisho la matatizo. Hiyo tume ikusanye maoni kutoka kwa wadau wengi na itoe mapendekezo ya ni nini kifanyike. Juzi nilikuwa nafanyakzai fulani na dada mmoja aliyemaliza Masters Degree Chuo Kikuu Mlimani, du.... aisee Mungu ndiye anajua. Mambo basic ya four six hajui yaani kichwani ni mweupee...
Umejuaje Kama ni mweupe ?
 
Joyce alikuwa mhadhiri UDSM. Anajua kabisa tatizo la rushwa ya ngono UDSM.
Katika hao wakuu wa vyuo aliowaita, wapo miongoni mwao waliotoa marks ili wapate ngono kwa wanafunzi. Hilo pia analijua fika. Wapo wanaotumia wahadhiri wengine kuwatafutia dogodogo wa kutafuna.Wakifeli marks zinabadilishwa kwa nguvu ya wakubwa.
Wasipoteze hela za umma kufanya vikao wakati tatizo na wahusika wanajulikana.
👊👊👊
 
Back
Top Bottom