Kikwete alishindwa uongozi kama Rais na sasa ameshindwa tena kama Mstaafu

Kikwete alishindwa uongozi kama Rais na sasa ameshindwa tena kama Mstaafu

Wakati wa Utawala wake...

Huyu bwana ana Bahati mbaya sana. Haya ni Matokeo ya kuforce uongozi wakati hauna karama hizo, kuongoza watu siyo jambo jepesi inahitaji maono na busara hasa unapokuwa kwenye nafasi nyeti kama ya uraisi.

Enzi za utawala wake nchi ilikuwa ya hovyo tena hovyo kupitiliza kiufupi nchi aliiikabizi kwa mabwenyenye wachache. 2005 alipita wa kura nyingi sana 88%, lakini Awamu ya Pili pamoja na kuiba kura aliambulia kama sikosei ni 59% watu walikuwa wamechoka mithili ya harufu mbaya.

Huyu mwamba alipuyanga sana. Hakuna mtu alitaka hata kumsikia. Bila uongozi mbovu wa Kikwete Magufuli asingekuwa Raisi, Magufuli alikuja kunusuru nchi isiende kwa Wapinzani.


Kwa Nini kashindwa kama Mstaafu

Kwa utamaduni wa Kitanzania Raisi mstaafu ni Nguzo muhimu sana hasa pale taifa linapotaka kukosa mwelekeo, lakini pia anajukumu kuwaelekeza njia bora za kupita aliowaacha.

Nafikiri mnakumbuka ni namna gani Nyerere alivyokuwa macho hata baada ya kustaafu, alikuwa akisimama kusema jambo taarifa lazima litulie.

Vile vile Mkapa alikuwa akisimama kidete pale mambo yalivyokuwa yanaenda kombo hasa kipindi cha uchaguzi, sauti yake iliheshimika sana.

Leo hii tuna Kikwete sijui hata anafanya hini, suala lililoniuzi ni hili la Sukuma na Msoga gang kutokalipiwa hadharani tena kwa ukali; limeleta mgawanyiko makubwa sana. Mstaafu yupo anaongea kwa kujificha ficha, ovyo kabisa.

Kikwete anazidi kushindwa kwasababu hata ushauri anaotoa kwa Rais Samia unaonekana ni wa ovyo kwasababu unapingwa kila kona ndani na nje ya nchi. Mbaya zaidi hataki kutoka hadharani kuweka mambo sawa kama Mstaafu.

Kiufupi nafasi ya ustaafu haintendei haki, hii inatokana na kutokuaminika na watu wengi maana uongozi wake ulikuwa ni fedheha.

Namshauri Kikwete awe Mzalendo, kashazeeka atapendwa na wengi, aache kumpoteza Rais Samia na kuyumbisha Serikali.
 

Attachments

  • 032D27E6-54BF-4657-B927-EFB835801551.jpeg
    032D27E6-54BF-4657-B927-EFB835801551.jpeg
    116.8 KB · Views: 3
Nyinyi humu kila siku mnataka Kikwete asijihusishe na siasa ..astaafu..
Hadi mkampa jina "mstaafu aisetaka kustaafu"...
Halafu tena mnataka awe nguzo na kushauri?alazimishe ushauri wake usikilizwe hata kama wahusika hawataki??

Seriously mnatakaje???
Hivi Roma Mkatoliki alisema rimoti ya TV iko wapi vile?? [emoji12]
 
Wakati wa Utawala wake...

Huyu bwana ana Bahati mbaya sana. Haya ni Matokeo ya kuforce uongozi wakati hauna karama hizo, kuongoza watu siyo jambo jepesi inahitaji maono na busara hasa unapokuwa kwenye nafasi nyeti kama ya uraisi.

Enzi za utawala wake nchi ilikuwa ya hovyo tena hovyo kupitiliza kiufupi nchi aliiikabizi kwa mabwenyenye wachache. 2005 alipita wa kura nyingi sana 88%, lakini Awamu ya Pili pamoja na kuiba kura aliambulia kama sikosei ni 59% watu walikuwa wamechoka mithili ya harufu mbaya.

Huyu mwamba alipuyanga sana. Hakuna mtu alitaka hata kumsikia. Bila uongozi mbovu wa Kikwete Magufuli asingekuwa Raisi, Magufuli alikuja kunusuru nchi isiende kwa Wapinzani.


Kwa Nini kashindwa kama Mstaafu

Kwa utamaduni wa Kitanzania Raisi mstaafu ni Nguzo muhimu sana hasa pale taifa linapotaka kukosa mwelekeo, lakini pia anajukumu kuwaelekeza njia bora za kupita aliowaacha.

Nafikiri mnakumbuka ni namna gani Nyerere alivyokuwa macho hata baada ya kustaafu, alikuwa akisimama kusema jambo taarifa lazima litulie.

Vile vile Mkapa alikuwa akisimama kidete pale mambo yalivyokuwa yanaenda kombo hasa kipindi cha uchaguzi, sauti yake iliheshimika sana.

Leo hii tuna Kikwete sijui hata anafanya hini, suala lililoniuzi ni hili la Sukuma na Msoga gang kutokalipiwa hadharani tena kwa ukali; limeleta mgawanyiko makubwa sana. Mstaafu yupo anaongea kwa kujificha ficha, ovyo kabisa.

Kikwete anazidi kushindwa kwasababu hata ushauri anaotoa kwa Rais Samia unaonekana ni wa ovyo kwasababu unapingwa kila kona ndani na nje ya nchi. Mbaya zaidi hataki kutoka hadharani kuweka mambo sawa kama Mstaafu.

Kiufupi nafasi ya ustaafu haintendei haki, hii inatokana na kutokuaminika na watu wengi maana uongozi wake ulikuwa ni fedheha.

Namshauri Kikwete awe Mzalendo, kashazeeka atapendwa na wengi, aache kumpoteza Rais Samia na kuyumbisha Serikali.
Kikwete Ndio kiongozi pekee ambaye alikomaa Kidemokrasia na aliruhusu Wapinzani. Uliona kina Mbowe, Zitto, Slaa, Lissu na wengineo kipindi chake sababu hakua na Nongwa, Alipata kura chache sababu hakuiba uchaguzi.

Kikwete aliamini kwenye watu wenye Uwezo, Aliwarudisha Watanzania Vichwa kutoka nje waje kuiendeleza Nchi,

Uchumi ulikua toka $480 alioiacha Mkapa mpaka kufika $1000 na kuingia Uchumi wa kati, Hela Zilikua kede kede, wafanyakazi walikua wakipanda mishahara, Biashara zilishamiri, maisha Ya Mtanzania mmoja mmoja yalikua yanaimarika.
 
Uzi wako unahisia nyingi,Mzee Kikwete hana baya hakuwa na husda,chuki wala visasi.

mimi ninachojua utawala wa Kikwete alifungua sana nchi hasa kwenye kukaribisha wawekezaji ajira zilikua nyingi mzunguko wa pesa wa uhakika,watu waliuza na kununua biashara zilifanyika.

watu walikula bata wakasaza,siku za weekend majiji kama ya Dar,Mwanza na Arusha yalikua ya moto ni full hekaheka.

Kina nani waliokula bata na kwa gharama za nani? Tunataka uongozi thabiti nchi yetu isonge mbele.
Kinachoendelea sasa hivi ni nini?
 
Kikwete Ndio kiongozi pekee ambaye alikomaa Kidemokrasia na aliruhusu Wapinzani. Uliona kina Mbowe, Zitto, Slaa, Lissu na wengineo kipindi chake sababu hakua na Nongwa, Alipata kura chache sababu hakuiba uchaguzi.

Kikwete aliamini kwenye watu wenye Uwezo, Aliwarudisha Watanzania Vichwa kutoka nje waje kuiendeleza Nchi,

Uchumi ulikua toka $480 alioiacha Mkapa mpaka kufika $1000 na kuingia Uchumi wa kati, Hela Zilikua kede kede, wafanyakazi walikua wakipanda mishahara, Biashara zilishamiri, maisha Ya Mtanzania mmoja mmoja yalikua yanaimarika.

Unaandika kama vile umeshiba ghahawa....unamdanganya nani? 😂😂😂😂😂
 
Kina nani waliokula bata na kwa gharama za nani? Tunataka uongozi thabiti nchi yetu isonge mbele.
Kinachoendelea sasa hivi ni nini?
Walikula bata waliofanya kazi,biashara na wakulima waliolima mazao yao.

Kiongozi thabit utampata wapi kweye nchi ya watu wasiojitambua,wajinga wenye upumbavu?

Kinachoendelea sasa ni watu wajinga na wapumbavu wanaoendekeza kulalamika mpaka kwenye vitu wasivyovijua.
 
Leo hii tuna Kikwete sijui hata anafanya hini, suala lililoniuzi ni hili la Sukuma na Msoga gang kutokalipiwa hadharani tena kwa ukali; limeleta mgawanyiko makubwa sana. Mstaafu yupo anaongea kwa kujificha ficha, ovyo kabisa.

Kikwete anazidi kushindwa kwasababu hata ushauri anaotoa kwa Rais Samia unaonekana ni wa ovyo kwasababu unapingwa kila kona ndani na nje ya nchi. Mbaya zaidi hataki kutoka hadharani kuweka mambo sawa kama Mstaafu
Huyo ni mission town tu mtoto wa mjini hana jipya zaidi ya ubishoo
 
Kufungua nchi, kwani nani aliifunga? Tusiongelee uongozi kama vile tunafanya kitchen party
Mkuu mimi nimezaliwa miaka ya 80, miaka ya 90 hata kukuta TV kwenye Majumba ya watu ilikua ni Anasa, ila wakati wa mkwere sio tu karibia kila Nyumba unakuta TV na vitu vyengine vya Anasa bali ni vya Bei ghali zaidi. Zamani TV ziliuzwa bei rahisi ila siku hizi watu wengi wananunua TV za Malaki.

Kipindi chake biashara ilishamiri Tukaanza kuona kukua kwa loose Cargo wa Tanzania wenyewe wakawa wanaenda Dubai na China kuleta mizigo Makabila yanayojielewa Yakaanza kukua kiuchumi.

TBC ambayo ilikua ikipatikana Dar na miji mikubwa Ikasambazwa Tanzania Nzima, sababu ya Tido Mhando, Tido alikuwa poached toka BBC akaletwa Nyumbani, TBC ikaanza kuonesha ligi ya Uingereza na vipindi kama Ze comedy, wakati huu TV ya Taifa Ikawa Inaangalizika.

Muulize Mhenga yoyote Zamani ilikua kumaliza La saba ni big deal, ukifaulu ukipangiwa sekondari Boarding kijiji kizima lazima wajue, Kikwete Akajaza Mashule Ya kata kibao na Vyuo vikaongezeka maradufu mpaka kufikia Stage degree imekua kama la 7

Mitandao ya Simu ikaletwa kwa Kasi, Internet ikaanza kupatikana kwa kila mwananchi, vifurushi vikashuka bei, akawaleta hadi Halotel ambao walisambaza internet hadi vijijini,

Kutokana na charisma yake jamaa alifanikiwa kuwashawishi watu wengi kuja kuwekeza Tanzania kama Dangote,
images (15).jpeg


Kifupi jamaa alifungua nchi sana.
 
Mkuu mimi nimezaliwa miaka ya 80, miaka ya 90 hata kukuta TV kwenye Majumba ya watu ilikua ni Anasa, ila wakati wa mkwere sio tu karibia kila Nyumba unakuta TV na vitu vyengine vya Anasa bali ni vya Bei ghali zaidi. Zamani TV ziliuzwa bei rahisi ila siku hizi watu wengi wananunua TV za Malaki.

Kipindi chake biashara ilishamiri Tukaanza kuona kukua kwa loose Cargo wa Tanzania wenyewe wakawa wanaenda Dubai na China kuleta mizigo Makabila yanayojielewa Yakaanza kukua kiuchumi.

TBC ambayo ilikua ikipatikana Dar na miji mikubwa Ikasambazwa Tanzania Nzima, sababu ya Tido Mhando, Tido alikuwa poached toka BBC akaletwa Nyumbani, TBC ikaanza kuonesha ligi ya Uingereza na vipindi kama Ze comedy, wakati huu TV ya Taifa Ikawa Inaangalizika.

Muulize Mhenga yoyote Zamani ilikua kumaliza La saba ni big deal, ukifaulu ukipangiwa sekondari Boarding kijiji kizima lazima wajue, Kikwete Akajaza Mashule Ya kata kibao na Vyuo vikaongezeka maradufu mpaka kufikia Stage degree imekua kama la 7

Mitandao ya Simu ikaletwa kwa Kasi, Internet ikaanza kupatikana kwa kila mwananchi, vifurushi vikashuka bei, akawaleta hadi Halotel ambao walisambaza internet hadi vijijini,

Kutokana na charisma yake jamaa alifanikiwa kuwashawishi watu wengi kuja kuwekeza Tanzania kama Dangote, View attachment 2661248

Kifupi jamaa alifungua nchi sana.
Nadhani hujui unachooandika. Mabadiliko ya Technology. Hayasubiri mtu. Hakuna Mtu anaweza kuyazuia

Kusema eti kaleta mtandao wa simu ni uongo. Sema alitawala kipindi amabcho mapinduzi ya Technology ya simu yalikuwa yamepamba moto.

Miaka ya 90 wapi walikuwa wanatumia simu ambako Sisi TZ hatukuwa nazo?

Huyo Tido mhando Muullize kilichompata Hadi Leo Yuko Azam na siyo TBC. Ile serikali ilikuwa imejaa ulaghai mwingi sana...

Kuhusu shule Aliendeleza alipoishia Mkapa pamoja na UDOM. Ndo maana siku Ile ikulu ya Chamwino inazinduliwa alianza kusema vitu ambavyo Hata hatuvielewi

Cha Pekee anachoweza kujisifu Kikwete ni Ujenzi wa miundo Mbinu ya Barabara hapoo Hata akijipiga kifua alifanya kazi
 
Wakati wa Utawala wake...

Huyu bwana ana Bahati mbaya sana. Haya ni Matokeo ya kuforce uongozi wakati hauna karama hizo, kuongoza watu siyo jambo jepesi inahitaji maono na busara hasa unapokuwa kwenye nafasi nyeti kama ya uraisi.

Enzi za utawala wake nchi ilikuwa ya hovyo tena hovyo kupitiliza kiufupi nchi aliiikabizi kwa mabwenyenye wachache. 2005 alipita wa kura nyingi sana 88%, lakini Awamu ya Pili pamoja na kuiba kura aliambulia kama sikosei ni 59% watu walikuwa wamechoka mithili ya harufu mbaya.

Huyu mwamba alipuyanga sana. Hakuna mtu alitaka hata kumsikia. Bila uongozi mbovu wa Kikwete Magufuli asingekuwa Raisi, Magufuli alikuja kunusuru nchi isiende kwa Wapinzani.


Kwa Nini kashindwa kama Mstaafu

Kwa utamaduni wa Kitanzania Raisi mstaafu ni Nguzo muhimu sana hasa pale taifa linapotaka kukosa mwelekeo, lakini pia anajukumu kuwaelekeza njia bora za kupita aliowaacha.

Nafikiri mnakumbuka ni namna gani Nyerere alivyokuwa macho hata baada ya kustaafu, alikuwa akisimama kusema jambo taarifa lazima litulie.

Vile vile Mkapa alikuwa akisimama kidete pale mambo yalivyokuwa yanaenda kombo hasa kipindi cha uchaguzi, sauti yake iliheshimika sana.

Leo hii tuna Kikwete sijui hata anafanya hini, suala lililoniuzi ni hili la Sukuma na Msoga gang kutokalipiwa hadharani tena kwa ukali; limeleta mgawanyiko makubwa sana. Mstaafu yupo anaongea kwa kujificha ficha, ovyo kabisa.

Kikwete anazidi kushindwa kwasababu hata ushauri anaotoa kwa Rais Samia unaonekana ni wa ovyo kwasababu unapingwa kila kona ndani na nje ya nchi. Mbaya zaidi hataki kutoka hadharani kuweka mambo sawa kama Mstaafu.

Kiufupi nafasi ya ustaafu haintendei haki, hii inatokana na kutokuaminika na watu wengi maana uongozi wake ulikuwa ni fedheha.

Namshauri Kikwete awe Mzalendo, kashazeeka atapendwa na wengi, aache kumpoteza Rais Samia na kuyumbisha Serikali.
Burning... ! Hivi ukishastaafu bado unakuwa unaongoza nini! Aisee tuache chuki binafsi. Mwache Mzee Apumzike kabisa
 
Nadhani hujui unachooandika. Mabadiliko ya Technology. Hayasubiri mtu. Hakuna Mtu anaweza kuyazuia

Kusema eti kaleta mtandao wa simu ni uongo. Sema alitawala kipindi amabcho mapinduzi ya Technology ya simu yalikuwa yamepamba moto.
Wakati wenzetu wanamiliki TV sisi tulikua hatumiliki, ila Kikwete Alipokuza uchumi wa mtu mmoja mmoja sio tu watu wanamiliki TV bali TV za bei ghali. Kawaida kukuta mtu Ana TV inch 32 ama zaidi.

Mambo ya Foleni yaliongezeka sana kipindi cha Kikwete watu wengi walijiweza kununua Usafiri Binafsi.
Miaka ya 90 wapi walikuwa wanatumia simu ambako Sisi TZ hatukuwa nazo?

Halotel wameletwa na Kikwete mwenyewe,

Viettel started investing in the country in 2011 and planned $736 million in investment after the then president Jakaya Kikwete made a state visit to Vietnam. The goal of the government was to encourage rural mobile connectivity in the country where and the government saw fit to increase competition by allowing Viettel to operate in the country.[4]

Nimetoa Wikipedia, na hapo cha kuangalia ni vijijini, Kuna Nchi zimeendelea kibao hawana Mitandao ya Simu vijijini, Halotel walivyokuja internet ikapatikana karibia 95% ya Nchi.
Huyo Tido mhando Muullize kilichompata Hadi Leo Yuko Azam na siyo TBC. Ile serikali ilikuwa imejaa ulaghai mwingi sana...

Kuhusu shule Aliendeleza alipoishia Mkapa pamoja na UDOM. Ndo maana siku Ile ikulu ya Chamwino inazinduliwa alianza kusema vitu ambavyo Hata hatuvielewi
Haijalishi kama project ilianzia kwa Mkapa ama La, kwa Kikwete kuendeleza Hio project imeonesha ukomavu wake, baada ya Shule za Kata Magu alitakiwa kudeal na walimu kuendeleza Hio project ila yeye akasusa kabisa kuajiri na kuharibu mipango yote Ya waliomtangulia.

Hii ni tweet ya HESLB mwaka 2015


Toka wanafunzi 40000 ku graduate mpaka 200,000 sio mchezo.
Cha Pekee anachoweza kujisifu Kikwete ni Ujenzi wa miundo Mbinu ya Barabara hapoo Hata akijipiga kifua alifanya kazi
 
Walikula bata waliofanya kazi,biashara na wakulima waliolima mazao yao.

Kiongozi thabit utampata wapi kweye nchi ya watu wasiojitambua,wajinga wenye upumbavu?

Kinachoendelea sasa ni watu wajinga na wapumbavu wanaoendekeza kulalamika mpaka kwenye vitu wasivyovijua.

Hakuna hatari kubwa kama hao unaowaita wajinga na wapumbavu wakiamua kupindua meza. Huwa wanafanya maajabu yasiyotegemewa.
 
Back
Top Bottom