Kikwete mbona Magufuli alipofariki dunia hukumuelezea kirefu kama kwa Membe?

Kikwete mbona Magufuli alipofariki dunia hukumuelezea kirefu kama kwa Membe?

Katika Mkeka wako nimetafakari mara mbili mbili hasa pale Ulipoandika nanukuu...."Mimi (Wewe) na Marehemu Membe kwa nyakati tofauti mlipitia Changamoto (Misukosuko) ya Kimaisha ila mkapeana moyo".... mwisho wa Kukunukuu.

Binafsi kama GENTAMYCINE imenibidi nianze kutafuta kama kuna Mkeka wako wowote ule uliuandika pale Rais wa Awamu ya Tano Dk. John Pombe Joseph Magufuli alipofariki dunia tarehe 17 Machi, 2021 ila sijaupata hadi hivi sasa.

Hata hivyo Pole sana Kaka Mtu JMK.
Acha kuingilia maisha ya watu, jifunze kutofautisha mtu binafsi na cheo. Kikwete na Membe huenda walijuana tangu utotoni, huyu mtu wako wamekutana uzeeni sasa unataka adimulie kuwa yeye Kikwete na Magufuli waliwinda njiwa pori pamoja! Haiwezekani.

Ninakushauri tiatia maji haraka ili nawe uje ielezewe kwa kirefu, japo utata utatokea kama wewe ni Mkurya kweli au Mjaluo. Acha kutamani vya wenzako.
 
Mimi sipo hapa kumtetea yeyote sijawahi kufanya ujinga huo, Makamba ni upuuzi tu kama wapuuzi wengine, ila kumbuka Makamba ni msomi mzuri wa Biblia na anaijuwa vizuri na hayo yamo ndani ya Biblia.

Na wewe kama unaamini Magufuli alikuwa mzuri basi hawezi kufa ataendelea kuishi.
Kuna wakati unajibu kwa munkari kama mkeo kakunyima uchi...tulia tulia Matola jibu bila mihemuko
 
Acha porojo, mimi sio team Magufuli, kilichonisikitisha ni huyo mzee Makamba kukosa haya, kujikomba kwa Samia kuwa wazuri hawafi akimaanisha Magufuli kafa kwasababu alikuwa ni mbaya.

Huo ni unafiki kujikomba kwa mkuu mpya kwa ajili ya asali ya mwanae
Hakuna nafsi ambayo haitaonja mauti, kujadili hili ni kunipotezea muda na sina muda huo.

Alamsiki.
 
Hakumuelewa kama nyinyi ambavyo hamjamuelewa.

angeishia kwenye statement ya kuwa "watu wazuri hawafi", ingemaanisha ulichokisema. Lakini alienda mbele na kusema "ndio maana JK yuko hapa anadunda na kuwataja watu kadhaa walio hai"

Nilifikiri wewe upo vizuri upstairs, kumbe na wewe ni hamna kitu. statement rahisi hivi unashindwa kui analyze, ama unafikiri mimi ni mmoja wa maboya unaobishana nao huku kila uchwao?
 
angeishia kwenye statement ya kuwa "watu wazuri hawafi", ingemaanisha ulichokisema. Lakini alienda mbele na kusema "ndio maana JK yuko hapa anadunda na kuwataja watu kadhaa walio hai"

Nilifikiri wewe upo vizuri upstairs, kumbe na wewe ni hamna kitu. statement rahisi hivi unashindwa kui analyze, ama unafikiri mimi ni mmoja wa maboya unaobishana nao huku kila uchwao?
Haijalishi yupo hai au kafariki, mtu mzuri hafi
 
Acha kuingilia maisha ya watu, jifunze kutofautisha mtu binafsi na cheo. Kikwete na Membe huenda walijuans tangu utotoni, hiyu mtu wako wamekutana uzeeni sasa unataka adimulie kuwa yeye Kikwete na Magufuli waliwinda njiwa pori pamoja! Haiwezekani.
Ninakushairi tiatia maji hsraka ili nawe uje ielezewe kwa kirefu japo utata utatokea kama wewe ni mkurya kweli au mjaluo, acha kutamani vya wenzako.
Kama ulipata kusoma vijarida vya Sani zamani kulikuwa na maborn town na Bush stars.

Hicho ndicho kinachotusumbuwa sasa hivi hapa JF, Kikwete na Membe na Lowasa ni Watoto wa mjini, haingewezekana hata kidogo hata kama wangesoma pamoja watu hawa kuwa na urafiki na mtu mshamba kama Magufuli.

Kwahiyo hapa Kikwete amempoteza Collogue wake ambao hata sisi binafsi tunao watu hao ambao ni bora kuliko hata ndugu zako wa damu.

Kinachoendelea hapa ni kujifyatuwa akili tu kwa Watoto wa marehemu na kujizima data.
 
It is very simple, mwendazake kabla ya mwendazake 'recently' hakuwa kitengo.
 
Back
Top Bottom