Kikwete na Magufuli walishindwa kuingusha CHADEMA lakini Rais Samia ndani ya miaka minne ameshamaliza anachofanya ni kuinyonyoa manyoya

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Hakuna anayeamini!

Kikwete kwa Miaka kumi alishindwa kuizima CHADEMA na ilibaki kidogo Sana 2015 Akabidhi ofisi kwa upinzani.

Akaingia Magufuli, yeye ndiye akatumia zaidi mabavu na alishakiri hadharani anaenda kufuta upinzani kabla ya 2020 lakini alipata upinzani Mkali Sana kuwahi kutokea katika nchi hii.
Akashindwa!

Akaingia Samia, mwanamke ambaye kikawaida kulingana na jamii zetu mtu yeyote angeweza kumdharau.

Lakini Samia yeye nafikiri alisoma Mchezo wa Kikwete na Magufuli. Kikwete alitumia Njia peaceful kuikabili CHADEMA huku Magufuli akitumia Mabavu. Samia yeye style yake ni kudokoa huku kidogo huku kidogo yaani nguvu kidogo akili kidogo.

Uhakika uliopo ni kuwa CHADEMA imeshakatwa kichwa, Wachache wanajua ishaanguka. CCM wametulia kama sio wao, wananyonyoa manyoya tuu.

Yaani CHADEMA iliyoshindwa na wanaume Leo ndio hii Mwanamke kaipiga. Aiseeh!

Haya!
 
Mwanamke alimpiga chini Adamu aliyepokea maelekezo toka kwa Mungu sembuse hawa wanadamu wa kawaida.
Hata Ndelila alimshughulikia Samson mnadhiri wa Mungu.

Ila Lissu akiingia tutaanza upya hakuna shida...kinyume chake hata kutoa heshima ya mwisho hatutaruhusiwa
 
..kama Chadema imeangushwa kwa fedha basi mjue ni fedha za umma.

..kama Chadema imeangushwa kwa mabavu ya vyombo vya dola navyo ni mali ya umma.

..Samia kwa kutumia vibaya madaraka aliyopewa na umma ameiangusha Chadema.

..mimi nadhani hatupaswi kumsifia Raisi anayetumia vibaya madaraka yake.
 
Maadui wakubwa wa nchi hii ni ujinga maradhi na umasikini ingekuwa kawaondoa hao maadui watatu ingeleta tija zaidi kwa wat
Anz
Maadui wakubwa wa nchi hii ni watatu umasikini maradhi na ujinga nafikiri angepambana na hawa maadui watatu ingeleta tija zaidi kwa watanzania.
 
Unauhakika gani tupe facts bila kubwabwaja.
 
Na aliyetoa assist ni yule mwamba mwenyewe Freeman Mbowe yaani ametumika kukiua chama alichokijenga kwa wivu mkubwa.
 
Usichojua ni kwamba kuiua chadema isingekuwa hatua ya siku Moja hao wote walifanya part Yao huyu anamalizia na atakuja atakae weka jiwe la mwisho na chadema haitakuwepo tena
Kwa Sasa twende na Lissu kwanza
 
..tatizo kubwa zaidi ni Wasomi wa Kitanzania, waandishi mahiri kabisa, wanapoamini kwamba Maraisi wetu wanapaswa kusifiwa wanapotumia vyombo vya dola kuhujumu demokrasia na mifumo ya uchaguzi.

..Na tukienda mbali kidogo, tujaribu kuangalia nchi nyingine zilipoongozwa na viongozi wanawake kama India, wakati wa Indira Ghandi, au Uingereza, wakati wa Margareth Thatcher. Je, ni mambo gani kina mama hao walisifiwa nayo?

..Hivi kweli sifa ya kudhulumu haki ni jambo la kumsifia mwanamke wa Kitanzania, tena ambaye ni kiongozi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…