Kila Mtanzania asali, huenda kukawa na mtikisiko

Nina hisia tu kwamba death squad ya mitaa ya Upanga/au Carrier corps inaweza kufanya jambo kwa mtu anayewanyima raha sana kwa sasa. Yule ambaye hatikisiki. Wahusika muongezeeni ulinzi wa uhakika.

Taharuki zisizo na kichwa wala miguu za nini? Anyway hata akiongezewa ulinzi watu wakiamua kumuondoa wanamuondoa tu
 
Umesema tulishatabiri jee ulitabiri na nani wakati mtabiri mkuu Sheikh Yahya alishafariki siku nyingi au umetabiri na yule mbunge machachari wa...acha vitisho havilipi
 
Shida ni kwamba sio rahisi kuombea kitu usichokijua. Ungetoa ufafanuzi ili tujue nini cha kuombea otherwise itakuwa kama dinj zinazotufanyia sisi waumini muda mwingine.
 
Huu ni upuuzi. Vatican wamefunga makanisa. Saudi Arabia wamefunga misikiti. Nyie wanafiki ambao mchana mnaimba jina la Mungu usiku mna tunguri ndo mwajifanya wacha Mungu? Acheni dhihaka hizi.
We ya huku yanakuhusu nini mkuu?
 
Mayahudi nao walikua wanajichanganya na mambo ya Dunia kwa kupindisha sheria na kujiona wao wana hekalu la kukutania lakini walilenga fedha na biashara ndani ya hekalu.
Walijua Mungu anakaa ndani ya hekalu lililojengwa na binadamu.
Yesu akawaambia kuwa siku zinakuja ambapo watu watamuabudu Mungu katika Roho na kweli na sio kule Yerusalem wala kwenye mlima .Matokeo yake hata Hekalu lao lilivunjwa kwa sababu ya unafiki wao wa kumkataa Masihi na Mfalme wa Haki Yesu Kristo.

Leo tunaweza kufungua milango ya misikiti na Makanisa lakini bado inatupasa kufanya toba ya kweli na kutenda haki kwa wote.
Kuna siasa za dhulma duniani na hasa miaka hii ya kuanzia 2015 kuendelea mpaka sasa Dunia imekua na viongozi wababe sana waliojiona kuwa Miungu watu. Matokeo yake wote wameufyata mbele ya kirusi cha Corona kisichoonekana kwa macho. Tanzania pia tulikuwa na baadhi ya viongozi wasiojali maumivu ya wengine. Leo nao wameanza kutubu na kujishusha kama binadam.

Ni kweli tunahitaji sana kuomba Mungu na kutubu kweli mana kwa miaka ya hivi karibuni haki ilikua inayumbishwa sana na watawala. Maisha ya watu yalikosa thamani kabisa. Kuna watu walikua wanahamasisha mauaji mpaka Bungeni na kwenye mitandao kwa sababu tu ya tofauti za kisiasa.
Hao watu kwa kweli ni lazima watubu kweli vinginevyo yanayotokea duniani ni stahili ya kizazi hiki kinachoshabikia uovu na viongozi katili wasiojali uhai wa mtu mmoja mmoja.
Hongera sana kwa wale walioona dhambi waliyoifanya kwa Taifa na kuamua kutubu na kujinyenyekeza kwa Mungu.
Waendelee na utakatifu huo huo mpaka October kwenye Uchaguzi wasimamie Uchaguzi huru na wa haki ili tupate viongozi wachaMungu na waadilifu. Huwezi kusema unamuomba Mungu akutendee haki wakati wewe hutendi haki.
Huwezi kumwomba Mungu asimamie maandiko yake wakati wewe hausimamii vyema sheria zinazoongoza eneo lako. Kila mtu atende haki na kumwona mwenzake ni bora kama yeye binafsi. Tusibaguane kisiasa wala Kikabila ndipo tutakapoona umuhimu wa kuacha milango ya nyumba za ibada wazi. Vinginevyo ni kumdhahaki Mungu. Na janga hill la Corona ni LA Dunia nzima ikiwa na maana kuwa ni pigo kama yale ya Wamisri enzi za Farao.
Watawala wa Dunia wamekua waovu sana. Walafi,wazinzi, washirikina, wabinafsi, wenye tamaa, watesaji, wapenda majivuno, wanaopenda kuogopwa na kutukuzwa kuliko Mungu unabidi wajishushe kwa kulazimishwa na kiumbe kidogo kabisa kinachoitwa Corona.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo kila kiongozi anayekuka ugali na mlenda mzalendo, VP kuhusu mm nayekula ugali WA muhogo na mboga dada kisamvu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnaendelea kumuomba mungu aliyeletewa na hawa mnaowaita mabeberu? au mmesahau tulikua tunasali chini ya miti kabla hawajaja kuomba mvua inyeshe?
Binadamu wengi ni stupid inashangaza sana, maombi kila siku watu wanaombea taifa, siku tatu watu walikaa wanaomba daily wengine makanisani wengine majumbani, huyo mungu hasikii tu anataka wote muanze kulia ndiyo ashuke? haha atakua ana tabia kama za magu za kujionaona yupo juu mumnyenyekee sana ndiyo ajionyeshe? acheni ujinga
 
Ukisoma tu comments za huu Uzi unajua tu Kuna tatizo mahala kwenye hii nchi
 
Sawa
Je watu hawafi kwa COVID19?
Na umejuaje kama ni hilo?
Je jumuia za Kimataifa zipo pamoja nasi?
Je huoni kama tunakaribia kupoteza pambano dhidi ya Kenya ambaye ndio alikuwa mshindani wetu katika Gateway?
 
Ushabiki wenu wa kipumbavu ndiyo utakaoangamiza taifa hili. Maana huo ushabiki unawafanya kuwajengea chuki wengine. Ndiyo sababu kila kitu nyie mmna base kwa chadema tu. Au mnalipwa hizo buku saba zinasomwa humu? Chuki kumbuka huambatana na visasi, leo mtatamba, ipo siku hamtajidai hivi. Either haohao unaowachukia au haohao ndugu zako ndiyo watakao kushughulikia.
Usidanganyike na mambo ya mihemuko mtandaoni Mkuu

Nchi ipo shwari

Hao Chadema wakishashiba lazima waingie mtandaoni kupiga umbeya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ni mpumbavu masaa 24 unawaza mambo ya CCM na chadema

Haya ni Madhara ya kutokuwa na kazi za kufanya na ya kimaskini

Mtu smart kichwani hawezi masaa 24 yupo mtandaoni kujadili ccm na chadema

Tafuta pesa mkuu, Muda unapoteza utaumbuka uzeeni

Hao ccm na Chadema hasa viongozi wa juu ni matajiri wa kutupwa wewe ngumbaru fanya kazi

Usidanganyike na mambo ya mihemuko mtandaoni Mkuu

Nchi ipo shwari

Hao Chadema wakishashiba lazima waingie mtandaoni kupiga umbeya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…