Kila mtu ana jambo lake ambalo anajua akilisema watu hawatamuamini

Kila mtu ana jambo lake ambalo anajua akilisema watu hawatamuamini

Kuna mdada alikua secretary ofisini kwetu, aliacha kazi na kuja kunisaidia kulea mtoto nyumbani kwangu. Ilikua ghafla tu, mimba yangu ilivyokua kubwa alisema hataki niteseke, nikafikiri utani ila niliishia kuishi naye vyema kwa miaka mitatu Alimpenda mtoto wangu sana, mtoto alivyoanza kindergaten akaomba kurudi kwao Tabora. Hiyo ilikua almost 17 years ago, baada ya muda tulipotezana akawa hapatikani tena kwenye simu yake. Huwa namkumbuka sana na mpaka leo sijajua kwa nini alifanya yale maamuzi.
Ana mbingu yake aisee😍
 
Kuna mtoto siku Moja uwanjan alikuwa anacheza na wenzake sasa wakampiga akawa akiwakimbiza hawapati akageuka paka wale watoto wakakimbia kutoa taarifa na Mimi nilishuhudia live bila bando ila Kuna M2 ukimwambia anakwambia movie hasa vitoto vya mjini
Hehehe
 
Kuna mdada alikua secretary ofisini kwetu, aliacha kazi na kuja kunisaidia kulea mtoto nyumbani kwangu. Ilikua ghafla tu, mimba yangu ilivyokua kubwa alisema hataki niteseke, nikafikiri utani ila niliishia kuishi naye vyema kwa miaka mitatu Alimpenda mtoto wangu sana, mtoto alivyoanza kindergaten akaomba kurudi kwao Tabora. Hiyo ilikua almost 17 years ago, baada ya muda tulipotezana akawa hapatikani tena kwenye simu yake. Huwa namkumbuka sana na mpaka leo sijajua kwa nini alifanya yale maamuzi.
Jesus Christ .... Aiseeee!

Nimeushangaaa huu upendo


Ni upendo wa ajabu sana ... Itakuwa na wewe una roho nzuri sio wale wadada wenye visiraniii
 
Nina maumivu kutokana na my previous relationship ambayo ilikuwa rasmi kuharibika ilikuwa mwaka juzi!

Lakini hayo maumivu ninayo mpaka Leo! Kiasi kwamba siwezi kutongoza, na hata nikiona mdada mzuri mwenye kunivutia!

Nakosa hata nguvu ya kutongoza ... Jambo la ajabu ni kuwa nawezaje kuwa katika maumivu since mwaka juzi update?

Hii miaka mitatu since mwaka juzi! Maombi yangu ya kumuomba Mungu aniue ni mengi kuliko maombi ya shukurani
 
Nina maumivu kutokana na my previous relationship ambayo ilikuwa rasmi kuharibika ilikuwa mwaka juzi!

Lakini hayo maumivu ninayo mpaka Leo! Kiasi kwamba siwezi kutongoza, na hata nikiona mdada mzuri mwenye kunivutia!

Nakosa hata nguvu ya kutongoza ... Jambo la ajabu ni kuwa nawezaje kuwa katika maumivu since mwaka juzi update?

Hii miaka mitatu since mwaka juzi! Maombi yangu ya kumuomba Mungu aniue ni mengi kuliko maombi ya shukurani
Duuh kiongozi hili jambo zito, pole sana una watu huwa unaongea nao kuhusu hili?
Usiombe Mungu akuue, bado tunakuhitaji.
 
Nina maumivu kutokana na my previous relationship ambayo ilikuwa rasmi kuharibika ilikuwa mwaka juzi!

Lakini hayo maumivu ninayo mpaka Leo! Kiasi kwamba siwezi kutongoza, na hata nikiona mdada mzuri mwenye kunivutia!

Nakosa hata nguvu ya kutongoza ... Jambo la ajabu ni kuwa nawezaje kuwa katika maumivu since mwaka juzi update?

Hii miaka mitatu since mwaka juzi! Maombi yangu ya kumuomba Mungu aniue ni mengi kuliko maombi ya shukurani
Pole ndugu
 
Duuh kiongozi hili jambo zito, pole sana una watu huwa unaongea nao kuhusu hili?
Usiombe Mungu akuue, bado tunakuhitaji.
Hapana Sina watu wa kuongea na kuhusu hili jambo! ... Ajabu ni kuwa watu wangu wengi wa karibu wananiamini Mimi mtu imara sana.

Wananitegemea kwa ushauri, malusuhishi na maelekezo ya mambo mengi sana ya kiroho! .. kama muda huu nimetoka kuongea na simu karibia 45, na jamaa angu!

Akinipa mrejesho wa semina aliyofanya na mwitikio mkubwa aliopata na kunipa shukurani kwa tips, token na maombi ninayoomba nae kwani yanampa Matokeo!

Na wengine wengi! Ila hakuna mtu anayejua Hali ninayopitia ... Wanaaminigi Mimi mtu imara sana! Pengine ni kwa Sababu ya neema ya Mungu aliyonipa kwa kupenda kucheka na kutabasamu muda wote!

Sina Cha kupoteza! Siwezi kujiua ila ikimpendeza Mungu ni vema tu nikafa!

Kila kitu kwangu kime stack! Jamii forum ndo inanipaga faraja na kucheka!

Hawa jamaa wamekuwa kama ndugu kwangu humu ndani wananijali sana na wananipa moyo wa kusonga mbele Intelligent businessman Bolotoba Edo kissy na wengine nimewasahau!
 
Nikiwaambia watu mimi mwenyekit wa Jumuiya wanacheka mpaka wanakaa chini😂😂🙌
Sikujui wala sijakuona ila Mimi mwenyewe nimesoma hapa nimecheka Sanaa!

Yaani wewe ni mwenyekiti wa Jumuiya? Jumuiya hii hii ya kuomba na kusali nyumba kwa nyumba? Au Jumuiya ingine mkuu?
 
Hapana Sina watu wa kuongea na kuhusu hili jambo! ... Ajabu ni kuwa watu wangu wengi wa karibu wananiamini Mimi mtu imara sana.

Wananitegemea kwa ushauri, malusuhishi na maelekezo ya mambo mengi sana ya kiroho! .. kama muda huu nimetoka kuongea na simu karibia 45, na jamaa angu!

Akinipa mrejesho wa semina aliyofanya na mwitikio mkubwa aliopata na kunipa shukurani kwa tips, token na maombi ninayoomba nae kwani yanampa Matokeo!

Na wengine wengi! Ila hakuna mtu anayejua Hali ninayopitia ... Wanaaminigi Mimi mtu imara sana! Pengine ni kwa Sababu ya neema ya Mungu aliyonipa kwa kupenda kucheka na kutabasamu muda wote!

Sina Cha kupoteza! Siwezi kujiua ila ikimpendeza Mungu ni vema tu nikafa!

Kila kitu kwangu kime stack! Jamii forum ndo inanipaga faraja na kucheka!

Hawa jamaa wamekuwa kama ndugu kwangu humu ndani wananijali sana na wananipa moyo wa kusonga mbele Intelligent businessman Bolotoba Edo kissy na wengine nimewasahau!

Sina Cha kupoteza! Siwezi kujiua ila ikimpendeza Mungu ni vema tu nikafa!
Ndugu huwezi kufa kabla yangu😂 kiufupi tufe tuende wapi tuzidi kupeana moyo na maombi mambo yetu yakae sawa.
 
Sikujui wala sijakuona ila Mimi mwenyewe nimesoma hapa nimecheka Sanaa!

Yaani wewe ni mwenyekiti wa Jumuiya? Jumuiya hii hii ya kuomba na kusali nyumba kwa nyumba? Au Jumuiya ingine mkuu?
Dah haya bwana
Mimi ni mwenyekit wa jumuiya ya kusali kila jumamosi Kkkt.
Ila nikiwaambiaga watu nipo busy na mambo ya jumuiya wanacheka.


Aaargh nitaanza kuwa serious
 
Sina Cha kupoteza! Siwezi kujiua ila ikimpendeza Mungu ni vema tu nikafa!

Kila kitu kwangu kime stack! Jamii forum ndo inanipaga faraja na kucheka!

Hawa jamaa wamekuwa kama ndugu kwangu humu ndani wananijali sana na wananipa moyo wa kusonga mbele Intelligent businessman Bolotoba Edo kissy na wengine nimewasahau!
Mkuu hebu achana na wazo la kufariki, una jua wewe ni mkubwa Sana kwangu!.

2015 nili kuwa kinda Sana, Kama ni mishe bado najaribu ku sort out kwa ajili yako!.

Hali ngumu hupita, ila wagumu tuna dumu.
 
Sawa ndugu😂
Unajua nimeanza kupoteza kumbukumbu Edo!

Leo nilinunua maji ya Lita Moja na nusu! Nikanywa ... Kuna ishu nikawa nafanya!

Baadae naenda kuangalia maji kwenye friji sioni! Nikasema labda nimeyasahau kijiweni!

Nimerudi kijiweni hakuna maji! Nikamwambia mwenye duka! Nina kiu Sina hela naomba maji ntakulipa nikipata hela!

Jamaa angu akatokea nikawa namwambia nimepoteza maji ... Akacheka sanaaa!

Akasema tulikuwa wote! Ulikunywa maji yote na kopo Lile pale ulilitupa!.

😂 .. oyaa ogopa sana depression sio kitu kizuri
 
Back
Top Bottom