Kilimo cha Kisasa cha Mahindi: Mbegu bora, Mbolea bora na magonjwa

Kilimo cha Kisasa cha Mahindi: Mbegu bora, Mbolea bora na magonjwa

Huo ni ugonjwa wa mahindi na jamii yake unaoitwa head smut unaosababishwa na fangasi aina ya Sphacelotheca reiliana.Wadudu hawa huweza kuenezwa kwa masalia ya shambani,vifaa vya kulimia na mara chache upepo.
NB:Ni vema sana kutofautisha na common smut unaoenezwa na ustrago maydis.
Asante sana mkuu kwa ufafanuzi huo! Hii ndo HF bhanaa!
 
Ingekuwa kwenye zao la SERENA , LULU au MTAMA ningesema 'CHIKWILILI''......................!!!
 
Alitaka kujua kama huo ni ugonjwa ama sio Hakuhitaji msaada Wa tiba
 
Huo ni ugonjwa wa mahindi na jamii yake unaoitwa head smut unaosababishwa na fangasi aina ya Sphacelotheca reiliana.Wadudu hawa huweza kuenezwa kwa masalia ya shambani,vifaa vya kulimia na mara chache upepo.
NB:Ni vema sana kutofautisha na common smut unaoenezwa na ustrago maydis.
Uko sawa kabisa mkuu.

Angoe na kutia kiberiti
 
USHAURI WA KILIMO/MIFUGO

Yamenikuta...Mahindi yanaharibika shambani
Ugonjwa huo unaitwa "Common Smut" na unasababishwa na fungus aitwaye Ustilago maydis .
Huyu fungus anaishi kwenye udongo na anaweza kukaa kwenye udongo kwa miaka mingi.
Huwa anaingia kwenye mmea wa mahindi kupitia vidonda na mbegu zake hukua na kuwa mmea kamili. Huyu fungus hula sehemu za chembe za uhai (cells) za mmea na kuziua. Anashambulia sehemu yoyote ya mmea ikiwa ni shina, majani, masuke, na gunzi. Hutengeneza vinundu fulani ambavyo ukivipasua vinatoa unga mweusi. Unga huo punje zake ndio mbegu za Ustilago maydis.
Ugonjwa huu huenea kwa kusambazwa mbegu zake na upepo,maji,wanyama,nk.
KUDHIBITI COMMON SMUT
Ugonjwa huu wa common smut hauna dawa kwa hiyo njia ya kuudhibiti usitokee au usishambulie kwa kiwango kikubwa ni kama ifutavyo:
1.Tumia mbolea yenye uwiano mzuri wa nitrogen na phosphorus. Udongo wenye nitrogen nyingi hufanya mimea kuwa laini na kukua haraka. Mimea hii hushambuliwa kwa urahisi na ugonjwa huu. Lakini phosphorus ya kutosha huzuia mashambulizi kwa kuwa hufanya mmea kuwa imara na.mgumu. Epuka kutumia samadi nyingi.
2. Epuka kujeruhi mimea. Mimea yenye vidonda hushambuliwa kwa urahisi zaidi.
3.Dhibiti wadudu waharibifu. Wadudu hutoboa mmea na kuujeruhi kwa hiyo hufanya mmea ushambuliwe kwa urahisi.
4. Hali ya ukame hufanya mashambulizi kuongezeka kwa hiyo kama inawezekana epuka kipindi cha ukame kulima mahindi kama hutaweza kumwagilia maji.
5. Acha kupanda mahindi kwenye eneo lenye historia ya kutokeza ugonjwa huu mara kwa mara. Panda mazao mengine
6.Kulima kwa kugeuza udongo ili ule wa juu ufukiwe chini sana kunaweza kupunguza tatizo kwa huwa.huyu fungus huishi kwenye udongo wa juu.
7.Muhimu zaidi: Tumia mbegu zenye kustahimili ugonjwa hasa hybrids.
Ugonjwa wa comon smut hauna dawa ukishaingia shambani lakini hasara unayosababisha haizidi 5%. Ukizingatia njia hizo za kuzuia unaweza ukautokomeza shambani mwako.
 
kiukweli huo sio ugonjwa bali nikilimo kisicho zingatia ubora wa mbegu,, kwa muonekano hapo ni mbegu isio bora
 
sio ugonjwa, huo bali hutokea kitu hicho ktk mbegu zisizo na ubora ,kwa lugha nyepesi yaani nimtu kachota mahindi ndani kwake nakwenda kupanda shambani ,, matokeo ndo hayo mahindi huzaa makire
 
Habarini za adhuhuri wakuu,, Mkulima anapanda mahindi na yanaota na kukua vizuri, cha kushangaza badala ya kutoa mbelewele inatokea kitu cheusi kama mkaa! Na hapo usitegemee kupata tena mhindi hata kidogo! Nisaidieni wanaJF najua hapa ni kila kitu napaamini sana, Asanteni!
6356e9d355f1def2a3920508bc7e5364.jpg

Ni wapi huku mkuu mahindi yameshakua hivi?
 
Wakulima wa mahindi mbolea gani ni nzuri kwa kilimo Icho ...cha mahindi.
 
kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbali mbali ya nchi ni bora kupeana ushauri jinsi ya kuchagua mbegu maana wakulima wengi ndipo wanapofeli.
AINA
Mbegu za mahindi
zimegawanyika katika makundi
matatu kulingana na siku za
kukomaa (maturity period).
Makundi hayo ni kama
yafuatayo;
1 . Mbegu zinazokomaa
mapema (Early maturity)
-Mbegu hizi hukomaa mapema
sana kuanzia Siku 80 hadi
siku 100.
2 . Mbegu zinazokomaa muda
wa kati (Medium maturity)
-Mbegu hizi hukomaa muda
wa kati kuanzia siku 115 hadi
siku 140.
3 . Mbegu zinazochelewa
kukomaa (Late or Full season
maturity)
-Mbegu hizi huchelewa
kukomaa kuanzia siku 150 na
kuendelea.
Nchini Tanzania aina
mbalimbali za mbegu chotara
za mahindi zimekua
zikitumiwa na wakulima
waliowengi. Zifuatazo ni aina
za mbegu chotara za Mahindi
zinazozalishwa nchini
Tanzania.
1 . Uyole Hybrid ( UH 6603 na
UH 615)
2 . TMV ( TMV1, TMV2 na
nyinginezo)
3 . SITUKA
4 . Meru
Vile vile mbegu za mahindi
chotara za nchi jirani zimekua
zikitumiwa na wakulima wa
Tanzania. Mbegu hizo ni kama
zifuatazo;
1 . SEEDCO
2 . PANNAR
3 . Na nyinginezo nyingi.
NAMNA YA KUZITAMBUA
MBEGU ORIJINO NA FEKI
Sekta ya kilimo hususani
upande wa pembejeo za
kilimo, umevamiwa sana watu
wasio waaminifu kwa maana
kwamba wanazalisha na
kusambaza pembejeo feki.
Makampuni ya mbegu nao
wanajitahidi kwa kadri
wanavyoweza kuandaa mbegu
zao katika hali ya usasa zaidi
ili kuzitofautisha na mbegu
feki.
Zifuatazo ni njia za
kuzitambua mbegu feki au
orijino;
1 . Mbegu orijino lazima iwe
imethibitishwa na taasisi
husika inayohakiki ubora wa
mbegu . kwa mfano nchini
Tanzania kuna taasisi ya
kiserikali inayohakiki ubora wa
mbegu inayoitwa TOSCI
(Tanzania Official Seed
Certification Institute). Mbegu
yoyote orijino lazima iwe na
kibandiko cha TOSCI. kama
haina itakuwa ni feki.
Vilevile kuna baadhi ya mbegu
mfano Pannar huwa zinakua
na kibandiko cha rangi ya bluu
kichoonyesha uthibitisho wa
ubora wa mbegu hiyo kutoka
kwenye taasisi ya nchi husika
kama Zambia au Afrika kusini,
kama haina kibandiko hicho
itakua ni feki.
2 . Kifungashio cha mbegu
orijino lazima kiwe na tarehe
ya mbegu ilipotengenezwa ,
kwa sababu kitaalamu mbegu
lazima itumike ndani ya miezi
sita tangu kufungashwa
kiwandani. Baada ya miezi sita
kupita inatakiwa mbegu hiyo
irudishwe kiwandani kwa ajili
ya kufanyiwa majaribio kama
bado ina ubora wa kuota au
haupo.
ANGALIZO
Ili kujihakikishia ununuzi
mzuri wa mbegu kwenye
maduka ya pembejeo ni vema
kudai risiti, Risiti hii lazima
ionyeshe jina la mwenye duka,
aina ya mbegu uliyonunua.
Umuhimu wa risiti ni
kukusaidia kipindi ambapo
utakuta mbegu uliyonunua
isipoota vizuri au ikiwa feki.
Pia ni muhimu kutunza baadhi
ya vifungashio vilivyotumika ili
vikusaidie siku za usoni
patakapotokea changamoto
yoyote itakayohitaji kuhakiki
ubora wa mbegu uliyonunua.

0716238374, 0683361843
 
Mkuu palizi ya pili sasa unaongelea mbegu?
 
Back
Top Bottom