Kimaandiko, baada ya Mungu, wazazi wanafuata, Kisha mume/mke

Kimaandiko, baada ya Mungu, wazazi wanafuata, Kisha mume/mke

Yesu akusema ila makanisa yenu na nyinyi wakristo ndiyo mlio tunga uongo wa kujikweza kwa kujitukuza mbele ya watoto wenu kwa kujitambulisha kuwa nyinyi ni miungu wa pili ...huko ndiyo kujikweza ...yesu alikataza hata kuitwa bwana na mwalimu akisema msiitwe bwana wala mwalimu kwa kuwa bwana wenu ni mmoja na mwalimu wenu ni mmoja ...tena akasema aliye mkuu kati yenu ni yule aliye mtumishi chini ya wote.
Mzazi ni muungu wa pili baada ya Mungu sababu amepewa nafasi hiyo na Mungu.

Kumuheshimu mzazi ambaye tayari amejishusha Kwa kuwatumikia watoto na kuwalea, isitafsirike kuwa huko ni kuwakweza ,hapana.
 
Salaam, shalom!!

Tukifuata maelekezo ya Mungu, mfumo wa utawala uko wazi kabisa kwamba,

Ndani ya NDOA, kimamlaka, mume na mke ni kitu kimoja, pale juu wenye mamlaka ni wazazi wa kimwili na kiroho.

Mlio ndani ya NDOA, mnaowapa wake zenu nafasi ya kwanza baada ya Mungu, mnakosea sana ikiwa wazazi wenu Bado wako hai.

Hawa watumishi wa siku hizi wanapotosha sana, mmoja akasema, katika gari yake, aliye na nafasi ya kukaa KITI Cha mbele ni mke wake pekee, kama hayupo KITI hicho kitabaki wazi akimaanisha Upendo Kwa mkewe na nafasi anayompa.

Tufuate mfumo alioweka Mungu Ili tuwe salama.

NB: Mamlaka ya wazazi ni nje ya chumba Chumba Cha wanandoa, ni ya kiushauri na kiheshima tu kama miungu wetu duniani baada ya Mungu.

Karibuni 🙏
“Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.

— Mwanzo 2:24 (Biblia Takatifu)
 
Sijasema hilo mkuu hata kumtukana mpita njia haiwezekane sembuse baba mzazi mkuu acha bagi tafadhari.
Kumbe leo mnaanza kukana kuwa nyinyi sio mnaosema BORA UNITUKANIE BABA YANGU KULIKO MAMA YANGU MZAZI ...kumbe wanao sema hivyo ni wavuta bangi ? Mbona atujawahi kukusikia mkiwakosoa hao wanao sema hayo maneno maana vi vijana wengi sana utawasikia wanaongea kuwa bora kumtukana baba mzazi kuliko mama tena awakuishia hapo kwa upumbavu bali wakavuka na mipaka na kusema laana kubwa ni ile itokayo kwa mama kuliko baba ! Hata hapo kwenye laana pana upotofu mkubwa watu amjiulizi kwanini ...yakobo na esau walikuwa wanagombania baraka kutoka kwa baba yao Isaka na si mama yao mzazi je kwanini mama yao naye alishiriki kutafuta baraka za isaka kwa mtoto aliye mpenda zaidi kwanini asingesema kuwa kama isaka atampa baraka esau basi mimi mama yao nitampa baraka yakobo?..tumieni akili
 
Salaam, shalom!!

Tukifuata maelekezo ya Mungu, mfumo wa utawala uko wazi kabisa kwamba,

Ndani ya NDOA, kimamlaka, mume na mke ni kitu kimoja, pale juu wenye mamlaka ni wazazi wa kimwili na kiroho.

Mlio ndani ya NDOA, mnaowapa wake zenu nafasi ya kwanza baada ya Mungu, mnakosea sana ikiwa wazazi wenu Bado wako hai.

Hawa watumishi wa siku hizi wanapotosha sana, mmoja akasema, katika gari yake, aliye na nafasi ya kukaa KITI Cha mbele ni mke wake pekee, kama hayupo KITI hicho kitabaki wazi akimaanisha Upendo Kwa mkewe na nafasi anayompa.

Tufuate mfumo alioweka Mungu Ili tuwe salama.

NB: Mamlaka ya wazazi ni nje ya chumba Chumba Cha wanandoa, ni ya kiushauri na kiheshima tu kama miungu wetu duniani baada ya Mungu.

Karibuni 🙏

Mwalimu, kuwa mwili mmoja ni jambo kubwa zaidi. "nyama katika nyama zangu; mifupa katika mifupa yangu"
 
Mzazi ni muungu wa pili baada ya Mungu sababu amepewa nafasi hiyo na Mungu.

Kumuheshimu mzazi ambaye tayari amejishusha Kwa kuwatumikia watoto na kuwalea, isitafsirike kuwa huko ni kuwakweza ,hapana.
Tumia akili yesu kasema aliye mkuu ni yule aliye mdogo na mtumishi chini ya wote ...je mitume awakuwa na wazazi je mitume na wazazi wao ni yupi.mkuu mbele za mungu ...mfano mtume musa na wazazi wake ni yupi mkuu je yesu na wazazi wake ni yupi mkuu ? Je Mariamu ni mungu wa yesu ?
 
Mwalimu, kuwa mwili mmoja ni jambo kubwa zaidi. "nyama katika nyama zangu; mifupa katika mifupa yangu"
Sasa aliye mwili mmoja nawe, iweje umpe nafasi ya kwanza zaidi hata ya wazazi🤔
 
NiLikuwa nasoma nilipofika hapa nikaacha
N
dani ya NDOA, kimamlaka, mume na mke ni kitu kimoja, pale juu wenye mamlaka ni wazazi wa kimwili na kiroho.

wazazi wa kiroho ni uongo hao unaowaita wazazi kiroho ni walezi na ni washauri tu.
 
  • Kicheko
Reactions: M45
Mzazi ni muungu wa pili baada ya Mungu sababu amepewa nafasi hiyo na Mungu.

Kumuheshimu mzazi ambaye tayari amejishusha Kwa kuwatumikia watoto na kuwalea, isitafsirike kuwa huko ni kuwakweza ,hapana.

hapa inategemea na mzazi mwenyewe alivyojiweka, Je anamfuata Kristo? maana Yesu anasema, apendaye baba au mama kuliko mimi hanistahili!

tunaposoma kuhusu kuwaheshimu baba na mama tujue mpaka uliko ili tusije mkosea Mungu.

“Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

— Mathayo 10:37 (Biblia Takatifu)
 
NiLikuwa nasoma nilipofika hapa nikaacha
N
dani ya NDOA, kimamlaka, mume na mke ni kitu kimoja, pale juu wenye mamlaka ni wazazi wa kimwili na kiroho.

wazazi wa kiroho ni uongo hao unaowaita wazazi kiroho ni walezi na ni washauri tu.
Kwahiyo ukaona kuliko kuwaheshimu wazazi wa kimwili na kiroho kimamlaka ni Bora mamlaka hayo umpe mkeo🤔
 
hapa inategemea na mzazi mwenyewe alivyojiweka, Je anamfuata Kristo? maana Yesu anasema, apendaye baba au mama kuliko mimi hanifai!

tunaposoma kuhusu kuwaheshimu baba na mama tujue mpaka uliko ili tusije mkosea Mungu.
Mzazi awezi kuwa Mungu wa pili wala wa tatu ...mungu ni mmoja tu amri ya kwanza kabisa kati ya amri kumi imesema wazi na yesu mwenyewe aliulizwa swali.kuwa ni ipi amri iliyo kuu na ya kwanza ...kasomeni alicho jibu jesu wenu mwenyewe kuhusu mungu kuwa ni mmoja ....wakristo wa makanisani ni wapumbavu sana mnapotosha waziwazi mafundiyo ya biblia yenu wenyewe...mariamu awezi kuwa ni mungu kwa yesu
 
hapa inategemea na mzazi mwenyewe alivyojiweka, Je anamfuata Kristo? maana Yesu anasema, apendaye baba au mama kuliko mimi hanifai!

tunaposoma kuhusu kuwaheshimu baba na mama tujue mpaka uliko ili tusije mkosea Mungu.

“Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

— Mathayo 10:37 (Biblia Takatifu)
Apendaye baba na mama kuliko Mimi hanistahili,

Hiyo haimaanishi kuwapa Heshima.

Mfano watumishi wa Mungu ni wazazi kiroho sasa kuwapenda na kuwashimu ni vyema.
 
Back
Top Bottom