Pre GE2025 Kinana: Rais Samia wanayemsema ndio ameleta uhuru uliopo nchini sasa hivi, akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?

Pre GE2025 Kinana: Rais Samia wanayemsema ndio ameleta uhuru uliopo nchini sasa hivi, akisema kuanzia leo hakuna maandamano itakuwa nini?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Makamu Mwenyekiti wa CCM anazungumza na waandishi wa habari na wanaCCM katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Dodoma. Kikwete anategemewa kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo kujibu shutuma mbalimbali zilizoibuliwa na upinzania ambazo CCM wameziita ni za kibaguzi dhidi ya Muungano.


Kinana
CHADEMA wametutuhumu CCM, Serikari na Rais kwa mambo ya uongo. Hatukatai kukosolewa na kusahihishwa, lakini hatukubali kuzuliwa wala kushtumiwa kwa mambo ambayo hayapo au ni ya kutunga. Kubwa walilofanya kwenye mizunguko yao ni kujenga chuki na mfarakano miongoni mwa Watanzania.

Kinana ajibu haya maswali:
1. Kwa nini leseni ya Tanzania haitumiki Zanzibar
2. Kwa nini Mtanganyika hawezi kununua ardhi Zanzibar
3. Kwa nini Mtanganyika hawezi kuwa DC Zanzibar
4. Kwa nini Wazanzibar wengi wameajiriwa Wizara ya Afya huku Tanganyika wakati afya siyo suala la Muungano
5. Kwa nini Mtanganyika hawezi kupiga kura Zanzibar
6. Kwa nini Wazanzibar wanakuwa viongozi kwenye masuala yasiyo ya Muungano Tanzania


NB: Wazanzibar wanabinya nafasi za Waislam wa bara kuwa Rais Tanzania maana mara nyingi Rais akitakiwa kuwa Muislam anatokea Zanzibar na akiwa Mkristu anatokea Bara. Hii siyo sawa maana Waislam wa Bara wanakuwa wanabaniwa nafasi ya kuwa Rais. Kati ya Marais watatu Waislam wa Tanzania wawili wametoka Zanzibar. Na JK alikuwa rais kwa sababu Zanzibar ilinyimwa zamu yake la sivyo hatungeweza kuwa na Muislam wa bara RAIS hadi leo
 
Kumbe hakunaga namna Rais wa Nchi ataweza kujiweka kando na Uteuzi wa viongozi wakuu wa Tume Huru ya Uchaguzi

Hata Kenya na Africa Kusini ambako makamu Mwenyekiti wa Chadema mh Tundu Lisu anaona Tume Huru ya Uchaguzi ni Bora Bado Mwenyekiti anachaguliwa na Rais

Nasubiri majibu ya Tundu Antipas Lisu kwa makamu Mwenyekiti wa CCM komredi Kinana

Nawatakieni Dominica Njema
 
Makamu Mwenyekiti wa CCM anazungumza na waandishi wa habari na wanaCCM katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Dodoma. Kikwete anategemewa kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo kujibu shutuma mbalimbali zilizoibuliwa na upinzania ambazo CCM wameziita ni za kibaguzi dhidi ya Muungano.


Abdulrahman Kinana

CHADEMA wametutuhumu CCM, Serikari na Rais kwa mambo ya uongo. Hatukatai kukosolewa na kusahihishwa, lakini hatukubali kuzuliwa wala kushtumiwa kwa mambo ambayo hayapo au ni ya kutunga. Kubwa walilofanya kwenye mizunguko yao ni kujenga chuki na mfarakano miongoni mwa Watanzania.

Hoja zao na ufafanuzi wa Chama cha Mapinduzi
1. Katiba
Wanasema wanataka Katiba Mpya na kutushawishi katiba mpya ni muhimu - Mwaka jana 2023 tumekubali hoja ya katiba mpya, na wanatanzania wanaitaka katiba mpya, tunachobishania ni lini, wao wanataka ipatikane leo. Rais Samia wakati anandoa zuio la mikutano ya hadhara alikubali pia kuhusu suala la katiba. Haya mambo yanahitaji muda na tafakuri, lakini wenzetu wanasema hapana, katiba inahitajika sana.

Katiba yetu imepokea mabadiliko mara 14, na ukitazama madailiko hayo mara nyingi yalilenga siasa, madaraka na uchaguzi, hata msukumo wa sasa wa CHADEMA lengo lake ni uchaguzi. Serikali imetunga sheria tatu za uchaguzi ambazo zimepita bungeni na Rais kutia saini, sheria ambazo zilitolewa maoni na wadau mbalimbali ikiwemo mpaka bungeni kwa siku nne, ambapo hoja za msingi zilikubaliwa lakini CHADEMA hawakuridhika, bado wasema Rais asihusishwe kwenye uchaguzi wa viongozi wa Tume, sijaona nchi ambayo Rais hahusishwi kwenye maamuzi mfano China, India, Kenya, Afrika Kusini kote Rais anakuwa na maamuzi fulani juu ya Tume.

CHADEMA walitaka suala la Katiba liwe la CHADEMA na CCM kama chama kikuu cha upinzani na chama tawala, hili haliwezi kufanyika, sababu katiba sio suala la vyama hivi viwili pekee.

Kwa sheria hii nawahakikishia Tume hii itakuwa Huru na kufanya kazi kwa uadilifu, Mweyekiti, Makamu na watendaji watakula kiapo kufanya hiyo kazi, labda kama tunataka malaika kufanya hizo kazi, lakini kazi hizi lazima zifanywe na binadamu.

Sheria ya Uchaguzi
Muungano
Kuligawa taifa katika majimbo

Unawateua unawaapisha wakutii wewe kisha unasema wako huru! Ni ujinga.
 
Makala na Nchimbiwazee wa "kutatua kero kisayansi" wako wapi ...

Tulitegemea wao ndio wamjibu Lissu.
Hawawezi propaganda hao.

Huoni mzee wa propaganda anavyojaribu kuspin. Eti katiba mpya inahitaji muda... Wakati mchakato ulishaanza miaka 10 iliyopita. Naona Warioba watakufa bila kuona matunda ya kazi yake.
 
Nyangumi wa siasa za Tanzania amepiga chafya katikati ya bahari ya siasa Tanzania, wimbi lake si dogo, na usiombe ukutwe na "kimbunga" cha chafya hiyo, Toleka Kibinda.

Kama ni gari, limekaa switch on, oil ipande, tayari kwa safari ya uchaguzi 2024/2025, hapa CCM huwa wanakuwa na umoja kama ruba na ngozi, au siafu
 
Tutaona kama waandishi hao watathubutu kumuuliza kuhusu ile katiba iliyoandaliwa na Jaji Warioba, thubutu.
 
Kinana katoa Siri Chadema mlitaka vyama vingine visihusishwe kwenye kikosi Kazi Cha Katiba mpya
Hivi kwa akili tu ya kawaida unaweza kuamini hilo. Wote tunajua basics za katiba mpya. Uzuri tulishaona mchakato wake before.

Kinana ni spin master wa CCM aliyebakia kwa sasa. Anachokifanya ni propaganda tu.

Hivi kajibu na maswali ya Muungano...!?
 
Masikini Comrade amebaki peke yake kama kisiwa kisicho na wavuvi, CCM ni hivi sasa ni sawa na kasha tupu baada ya Mangula kuchoka na kukabidhi mitambo kwa Nape! Ukimuangalia Kinana unamuona kuwa hana mtu anayeweza kuongea naye lugha moja wakaelewana ndani ya chama.
Uzushi hausaidii
 
Back
Top Bottom