Kinana: Rais wa Tanzania aliyekula kiapo hawezi kufanya jambo ambalo halina maslahi na nchi yake

Kinana: Rais wa Tanzania aliyekula kiapo hawezi kufanya jambo ambalo halina maslahi na nchi yake

Huyu nae anaongea nini bwana..?
Mkapa wakati anakula hela za EPA kwenye re election campaign zake hakuwa ameapa kuilinda na kuitetea nchi..?
Wao wakae kimya tu wakati wanakula, that's the better thing wanaweza kufanya at the moment. Nchi yenyewe ni kama haina kiongozi tu saivi.
 
wtf…
Kinana asitufanye Sisi hamnazo
By the way hatukumchagua huyo
 
Baada ya Uvumi mkubwa wa kumhusisha Kinana na Kupinga uwekezaji wa Bandari Kwa DP World, hatimaye afunguka.

Akihutubia mkutano wa hadhara Mkoani Mara Kinana amesema Watanzania wasiwe na Wasiwasi Kwa sababu Rais Samia ameapa kulinda na kuhifadhi Katiba ya Nchi hivyo hawezi kuwauza Kwa kufanya jambo ambalo Halima maslahi Kwa Nchi.

My Take
Hakuna wa kurudisha Wala kukwamisha uwekezaji bandarini


=======
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)-Bara, Abdulrahman Kinana amewataka Watanzania kutokuwa na wasiwasi juu ya mkataba wa ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na ya Dubai kwani Rais Samia Suluhu Hassan, ameapa kuilinda na kuitetea Katiba kwa maslahi yao.

Kinana amesema hayo leo Jumatano, Julai 26, 2023 wakati akihutibia mkutano wa hadhara, Musoma Mjini, Mkoa wa Mara akiwa kwenye mwendelezo wa ziara zake katika mikoa ya Dodoma, Manyara, Mara, Simiyu na Tabora.

“Kuna mjadala mkuuuuubwa na mpana wa bandari, mjadala huu umefika wakati unawachanganya Watanzania. Wamuamini nani. Nataka niwahakikishie, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyekula kiapo hawezi kufanya jambo ambalo halina maslahi na nchi yake.

“Kama Rais tangu achukue nchi (Machi 19, 2021), amefanya yote haya, kwa nini auze nchi, ili iweje? lakini mkisikiliza mjadala, wote wanaotetea, wanaoupinga, wanaoukosoa hakuna anayesema tusifanye uwekezaji, hata mmoja, wote wanakubali kuna haja ya kuwekeza ili kuongeza ufanisi na kuongeza mapato,” amesema Kinana

Kinana amesema, Serikali imesema ipatokea kila ushauri na CCM imeitaka Serikali isikilize ushauri, maoni na hoja zinazotolewa. Haya yote yatafanyiwa kazi. Haiwezekani rais akapuuza yote haya na mmemuona Rais tangu mjadala umeanza, amekaa kimya, anapigwa vita.

“Kamanda mzuri wa vita si yule vita inapokuwa hivi anabadili mbinu na mikakati, kamanda mzuri ni yule anayetulia. Nahodha mzuri wa chambo si yule anayeyumbishwa bali anatulia na kuona anakabiliana nayo viti,” amesema Kinana.

Watanzania wasiwe na wasiwasi wakatai IGA imeshasainiwa na kupitishwa bungeni, na kujinasua hapo ni mamilioni ya US dollars katika arbitration case kubwa?

What is Kinana talking about? Who is he fooling?
 
Kinana amesema, Serikali imesema ipatokea kila ushauri na CCM imeitaka Serikali isikilize ushauri, maoni na hoja zinazotolewa. Haya yote yatafanyiwa kazi
Hapa naona sawa, hiki ndiyo tunachotaka sasa, hapa hatuna neno tunasubiri.

Ila siyo zile ngonjera zingine za wapambe wengine, kwamba kila kitu kiko sawa mia kwa mia.
 
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdurhaman Kinana, amezungumzia mjadala wa uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam huku akiweka wazi kuwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoingoza haiwezi kuuza bandari hiyo na kuhoji Rais auze bandari kwa maslahi yapi.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Mkendo Musoma Mjini Kinana alianza kwa kueleza kuwa liko jambo la bandari linazungumzwa na mjadala mkubwa, unaendelea kuwa mrefu, mjadala mpana.

“Nataka niwahakikishie msiamini kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyekula kiapo eti atafanya jambo ambalo halina maslahi na nchi. Haiwezi kutokea, Rais ambaye tangu amechukua usukani amefanya mambo mengi mazuri, kwa nini aende kuuza bandari, sababu ni ipi?

“Ili apate nini, ili iweje na ukisikiliza huu mjadala usikilizeni kwa makini na mmeshausikiliza, wote tunaoutetea, wanaopinga pamoja na wanaokosoa hakuna anayesema kwamba kusiwe na uwekezaji hata mmoja kwani wote wanakubali kwamba kuna haja ya kuwekeza na lengo ni moja tu kuongeza ufanisi na kuongeza mapato.
WhatsApp Image 2023-07-26 at 21.17.34.jpeg
 
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdurhaman Kinana, amezungumzia mjadala wa uwekezaji katika Bandari ya Dar es Salaam huku akiweka wazi kuwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoingoza haiwezi kuuza bandari hiyo na kuhoji Rais auze bandari kwa maslahi yapi.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Mkendo Musoma Mjini Kinana alianza kwa kueleza kuwa liko jambo la bandari linazungumzwa na mjadala mkubwa, unaendelea kuwa mrefu, mjadala mpana.

“Nataka niwahakikishie msiamini kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyekula kiapo eti atafanya jambo ambalo halina maslahi na nchi. Haiwezi kutokea, Rais ambaye tangu amechukua usukani amefanya mambo mengi mazuri, kwa nini aende kuuza bandari, sababu ni ipi?

“Ili apate nini, ili iweje na ukisikiliza huu mjadala usikilizeni kwa makini na mmeshausikiliza, wote tunaoutetea, wanaopinga pamoja na wanaokosoa hakuna anayesema kwamba kusiwe na uwekezaji hata mmoja kwani wote wanakubali kwamba kuna haja ya kuwekeza na lengo ni moja tu kuongeza ufanisi na kuongeza mapato.
View attachment 2700029
Wanasiasa ni shida Sana kwahiyo Prof. wa Sheria ISSA Shivji ni Muongo
 
Back
Top Bottom