Tetesi: Kingunge kurejea CCM wiki hii?

Tetesi: Kingunge kurejea CCM wiki hii?

hata akirudi FICEM atasaidia nini? alikuwa huko tangu sijazaliwa nimezaliwa na sasa nazeeka akakimbilia cdm. tunashukuru amechangia kubusti cdm imepata wabunge wengi halmashauri nyingi. kwahiyo hata akiondoka hakuna shida tumeshmtumia ametunufaisha inatosha. arudi akamalizie uhai wake FICEM.
Na SACCOS imetuna na kujaa mihela

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Na SACCOS imetuna na kujaa mihela

Post sent using JamiiForums mobile app

Sio mihela tu... Halamashauri kubwa zote za ukawa.. Wabunge kutoka 45 mpaka kufikia takriban 130 haya ni mafanikio makubwa labda uwe zombi ushindwe kuelewa mafanikio haya.
 
Hahahahahahaaaa ni njaaa tu et mhenga yule anaongopa unataka mabadiliko kabla ccm haijaharibika kabla ya taa na tanu Leo unataka mabadiliko hahahahaaaaa

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Cha ajabu nini wakati kila mtanzania ana uhuru wa kwenda chama chochote anachopenda sera zake? Hata Lowassa anaweza kurudi CCM akitaka na Nape kwenda CHADEMA akiamua
 
kwani ccm wanachukua makapi wana nguruwe huko?! Maana waliohama kwenda chadema waliitwa makapi leo tena wanataka kuyachukua baada ya miaka 2 watayaita nini tena maana hata sifa ya kapi imekwisha labda wana taka kuchukua mbolea.
 
Kingunge hakuwahi kutoka ccm...hakujiunga na CDM ...yeye alikuja kuweka nguvu tu kwa lowassa ambaye aliamini kuwa kiongozi bora kuliko magufuli....
Hivyo anarejea wapi sasa ?


Makes lot of sense,
 
Naamini mzee hawezi fanya kitu ka hiyo[emoji23]

_Issac_
 
Kingunge hakuwahi kutoka ccm...hakujiunga na CDM ...yeye alikuja kuweka nguvu tu kwa lowassa ambaye aliamini kuwa kiongozi bora kuliko magufuli....
Hivyo anarejea wapi sasa ?
Tuseme anataka kurudi kwao ok fine ...hio itakuwa unafiki mkubwa wa ccm kumpokea...watakuwa watu wa ajabu sana kwani mtakumbuka hivi majuzi iliwafukuza wote walokua na msimamo wa kingunge hawa kina Sophia Simba na wenzake...hivyo hili litaonesha kuwa hawana msimamo.
Wakirudi hawatakuwa na msimamo huo tena, tutakuwa wamoja

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
 
Kwani Lowasa au Dr Slaa na yule Sumaye waliwahi kurudisha kadi za CCM?!!
Katika katiba yenu ya ccm inazuia mtu kuwa mwanachama wa chama kingine then akaendelea kuwa mwanachama wa ccm, hivyo Dr Slaa, Lowassa na Sumaye automatically siyo wanaccm tena mara tu baada ya kuchukua kadi za Chadema hadi hapo watakapofuata utaratibu mwingine wa kurudi ccm kama mwanachama mpya, kuhusu Mzee Kingunge yeye hajawahi kuhamia chama chochote kile zaidi tu ya kumuunga mkono Lowassa.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Abaki huko huko azungushe mikono na kuwasaidia chadomo kudeki lami
 
Back
Top Bottom