Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kutokea ni contradiction.

Kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea na hakuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezi kutokea?
Kwanini asiumbe ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea ?

Angeumba ulimwengu ambao hakuna mabaya yoyote,, bado kuna watu wangejitokeza kuhoji ( logically ) kwanini Mungu hajaruhusu mabaya kutokea ?

Kwahiyo kutoumba ulimwengu ambao hakuna mbaya ndo inathibitisha kuwa hakuna Mungu ?

Contradiction ipo wapi hapo ?

Huo ni ufinyu wako wa kufikiri, lakini sio contradiction

Lete hoja nyingine !!
 
mimi hua nashangaa sana kuona kiranga anabishana na officiaboy + jurjani.

Like how can you argue with someone who is mentally unstable to grasp the concept you are trying to say?.

kiranga kauliza "thibitisha mungu yupo" ila wanajibu kua "thibitisha hayupo", utadhani kisichopo kipo kuthibitishika hakipo.

mi nadhani muache kubeat around the bush, mthibitishieni huenda akawa mfuasi wenu, people are won over na sio kumdictate kwa vitisho vya adhabu za moto na kaburi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiranga amekuwa limited kwenye space na time amesahau Mungu yupo beyond space, time, and matter

mtu aliyetengeneza kompyuta software na code hayupo kwenye kompyuta yupo nje ya huo mfumo



 
Kwanini asiumbe ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea ?

Angeumba ulimwengu ambao hakuna mabaya yoyote,, bado kuna watu wangejitokeza kuhoji ( logically ) kwanini Mungu hajaruhusu mabaya kutokea ?

Kwahiyo kutoumba ulimwengu ambao hakuna mbaya ndo inathibitisha kuwa hakuna Mungu ?

Contradiction ipo wapi hapo ?

Huo ni ufinyu wako wa kufikiri, lakini sio contradiction

Lete hoja nyingine !!
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani hakuna contradiction.

Kwa sababu.

Mabaya kutowezekana si contradiction kwa Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote.

Mabaya kuwezekana ndiyo contradiction.

Umeelewa hilo somo?
 
Mi nadhani Kiranga sio kwamba ahamini uwepo wa Mungu ila yeye tu anataka uthibitisho wa kuwa Mungu yupo na umu wote tumeshindwa mthibitishia naisi apa ni Mungu mwenyewe anapaswa kujionesha kwa kiranga ili amuamini.

nadhani ata siku kama kweli Mungu yupo Mungu akimpa kiranga ajieleze kwanini akumuamini nadhani kiranga anaweza,
kumwambia sikukuamini kwakua sikukuona.

Nadhani swala la kiranga ni Mungu tu mwenyewe aingilie kati kama kweli yupo.

Sent from my TECNO K8 using JamiiForums mobile app
 
Najua na nimefanya makusudi. Kwanini iwezekane kila mtoto akizaliwa awe ni muislam ila baadaye abadilishwe na dunia? Kama ukristo ulikuwapo kabla ya uislam na Yesu alikuja kuwakomboa wanadamu wote,kwanini na Muhamad asiwe miongoni mwao. Sijui kama utaelewa mantiki ya niandikayo.
[emoji16][emoji16] nimependa sana kwa namna ulivyompa huo ufafanuzi sijui kama atakuelewa?
 
Fikra za utumwa ni wewe kuamini miungu ya waarabu ngano zao na mapokeo ya kale ya jamii hizo na kuzipractice katika maisha halishi ya Sasa
Kama ni habari za kweli vipi hatupaswi kuziamini na kuzifanyia kazi ?

Habari gani ya kuhusu Uafrika wako ni sahihi na umeihakiki ?

Hii maana ya utumwa naipata wapi ?

Fikra gani hizo za waarabu zinakinzana na uhalisia wa leo ?
Kama sio ujuha na uwendawazimu ni nini Kama sio ugonjwa wa akili ingali wewe ni mtu mweusi Wala huna
Shida yako huja hoja na hutetei unachokiamini,unaishia kulalama jaribu kujenga hoja.

Hivi tofauti yangu na muarabu au mzungu au muhindi ni nini ? Hivi unayapima mambo kwa kutumia nini ?
Ndio maana nasema amka ewe mtu mweusi utoke katika fikra mfu za hizo jamii zao!
Sasa unaniamsha vipi wakati wewe umelala usingizi wa PONO,amka kwanza wewe kisha tujadiliane jambo hili kwa uadilifu na uwazi bila jazba za kipuuzi.
Kama hinielewi endelea kua mtumwa wao daima ila Mimi hunishawishi kama mtu mweusi wa huku nyumbanitu!
Lengo siyo kukushawishi na sipo hapa kwa ajili hiyo,nipo hapa kwa ajili ya kufikisha na wenye haki na wa kweli muwajue na ukweli wenyewe muujue.

Yaani kwa mapito yako yanaonyesha wazi kabisa hata nikikupa miaka kumi ujenge hoja hutaweza zaidi ya kung'ang'ania Uafrika halafu mkibaguliwa mnalialia,Uafrika,uarabu,uzungu na usio kuwa huo ni vitimbalilusho tu ili watu tupate kufahamiana ila hakuna mbora zaidi ya mwingine ila yule mwenye kutenda ya kumpendeza Allah basi. Sasa imani gani wa kiafrika una mafundisho yaliyo nyooka na yaliyodhbitiwa zaidi ya harakati na ujinga.

Ukiwa na hoja na ukiona haja ya kujadili hili,nistue mimi nipo.

Shukrani.
 
Kwanza kabisa, kitu kuwa na mtengenezaji wake si lazima mtengenezaji wake awe Mungu.
Safi kabisa,sasa tuambie huu ulimwengu na sisi binadamu imekuwaje tukawa hivi tulivyo,je tumejiumba wenyewe au tumetokea pasi na chochote ? Hili swali huwa unalikimbia.

Embu tupe uwezekano au tuonyeshe kwamba Mola si muhusika wa huu ulikwengu na utuonyeshe uwezekano wa uwepo wa kitu pasi na msanifu wake,mwenye kujua,mwenye maarifa na mfano wake.
Pili, dhana nzima ya kusema Mungu asiyeonekana yupo, kwa sababu kika kinachoonekana kina mtengenezajinwake ni kichaa cha aina fulani.
Omyesha ukichaa wake uko wapi ?

Kadhalika mpaka visivyo onekana vinamtengenezaji wake. Roho,njaa,maumivu,majonzi na mfano wake vyote vinatoka kwa Allah.
Yani ni bora ungesema habari ya vitu vinavyoonekana kuhalalisha uwepo wa Mungu anayeonekana.
Vipo visivyo onekana ila vinauashiria wake kwa vinavyo onekana kuonyesha uwepo wake. Akili huioni wewe ila mwenye akili unamuona na asiyekuwa na akili unamuona kadhalika. Yaani Allah haonekani Ulimwenguni ila kuna muda tutamuona kama vile tunavyo jua la utosi,lakini kwa kuwa kwa sasa haonekani ila kuna ishara zinaonyesha uwepo wake akili,mazingira,ufunuo na mfano wa hivi huonyesha uwepo wake.

Kwahiyo kufikiri kwa aina hiyo unavyofikiri wewe ufinyu wake ni kama umefungiwa ndani ya chumba kidogo chenye kidirisha kidogo,kisha ukatazama nje ukahitimisha juu ya kile ulichokiona ndiyo kitu kizima wakati uhalisia ni kitu kidogo sana kwenye kile kitu kizima.
Zaidi, kudai kila kitu kinachoonekana kinq mtengenezaji wake, hujaongelea visivyoonekana.
Kadhalika visivyo onekana vinamtengenezaji wake na yeye ni Allah mtukufu na akasema yeye ndiyo mjuzi wa yale ya dhahiri na yale yaliyofichikana.
Na unaonesha hujasoma Quantum Physics ambayo inavunja cause and effect.
Quantum Physics ni nadharia tu ambazo hata wakubwa zako hawakuweza kuzithibitisha.

Hakuna kinacho vunja "cause" and "effect" wakati kuna msanifu na kuna malighafi na kuna kile kinachotarajiwa. Labda nikupe kazi utuonyeshe kwa namna gani (hili najua huwezi kuonyesha ila naonyesha ujinga wako ulipo mili) Quantum Physics ina vunja "cause" na "effect" katika uwepo wa kiti mathalani, kilichotengenezwa kwa malighafi ya mbao (Material cause), msanifu (first cause) na kiti(effect) chenyewe. Kwahiyo kwa vyovyote vile Quantum Physics haiwezi kubatilisha (disprove) Causality.
Umeonesha ujinga wako.
Hivi ushawahi kufundishwa somo la ukosoaji maana hapa hujagusa hata kile alichokiandika uliye "mquote" mwisho wake una dai kwamba umeonyesha ujinga wake ? Kwenye nini mantiki au falsafa au hiyo Quantum Physics ?
 
Hizi ni za kumpa officialboy , zinaweza kumsaidia.Mimi nishazitoa sana hapa.

Za kutoka Quran na Biblia, hata wiki hii nimeziweka hapa.
Umezitoa halafu huwezi kuzitetea unakimbia kimbia mwisho unakuja kuleta tarjama ya Qur'aan ya Yusuf Ali kwa ujinga wako una dai kuwa ndiyo Tafsiri ya Qur'aan,kisha ukaweka kitabu cha historia sasa sijui kinajibu nini katika Tafsiri ya Qur'aan kwa dhati ya aya,kadhalika huenda hata vile vitabu ulivyo weka sura yake ya nje hukuvisoma,sidhani kama ungevisoma ungeleta hizo unazo dai kuwa ni Cotradictions.

Mimi nakuhusia kama unataka kukosoa dini hasa ya Uislamu unatakiwa usome sana tena sana.
 
Najua na nimefanya makusudi. Kwanini iwezekane kila mtoto akizaliwa awe ni muislam ila baadaye abadilishwe na dunia? Kama ukristo ulikuwapo kabla ya uislam na Yesu alikuja kuwakomboa wanadamu wote,kwanini na Muhamad asiwe miongoni mwao. Sijui kama utaelewa mantiki ya niandikayo.
Ukristo lini uliwahi kuwepo kabla ya Uislamu labda kabla ya Uislamu huu aliokuja nao Mtume wetu ila kwa Uislamu wa ujumla hakuna mtume ambaye hakuwa Muislamu,welaketofautiana sheria tu ila imani yao wote ni moja.

Ukiambiwa ya kila mwanadamu anazaliwa katika umbile la UISLAMU haimaanishi Uislamu huu bali ule Uislamu wa ujumla wa kupokea na kukubali juu ya uwepo wa Mola na dunia imeumbwa na Mola na Mola ndiye anae paswa kuabudiwa peke yake hii kwa istilahi huitwa "Fitrah("original disposition", "natural constitution", or "innate nature".). Kwahiyo watakao mbadilisha kuwa mmajuzi,myahudi au mkristo ni wazazi wake.
 
Hata shetani ana uwezo mkubwa sana ilo si tatizo . hata wana sayansi wana uwezo mkubwa sana na Akili nyingi. kuwa na Akili na uwezo mkubwa sana sio sababu ya kutoamini Mungu. Mungu na uwezo wa Mtu ni vitu viwili tofauti kabisa. Mungu ni Mungu alinganishwe na kitu chochote. Mwamini Mungu siku ya Mwisho ukimkuta hujapata hasara , pia ukimkosa hauna hasara pia. Amini usiamini Mungu yupo. yeye ni Alfa na omega. wa kwanza na wa Mwisho.
 
Kuna watu hawafahamu contradiction

Contradiction ni pale sentensi mbili au zaidi zinapokinzana maana zikiwa zina lengo la kueleza jambo moja.

Mfano. Juma ni mbabe sana anapiga watu mtaa mzima, juma alipigwa na jirani yake hamisi.
Katika mfano wetu tutaona ukinzani uliopo juma kama ni mbabe mtaa mzima iweje apigwe na hamisi.

Nadhani tumeelewa somo

Sasa nagusia juu ys muumba na sifa zake tuone kama zinakinzana

Mungu anaweza yote.
Katika hii sentensi inaleta tasfiri ambazo zinakinzana, kama anaweza yote ina maana anaweza tengeneza jambo kubwa ambalo hata yeye hataliweza na hivyo kuondoa maana ya kuweza vyote.

Mungu anajua yote
Hii sentensi ina maana huwezi kufanya jambo ambalo halijui, yeye anajua hata kabla hujafanya ( mfano yesu alijua yuda atamsaliti) sasa kama alijua kuwa akituumba tuta feli test yake ya loyalt kwa kula tunda kwa nini ATUADHIBU wakati alijua nature yetu ni dhaifu, na kwa nini atuumbe dhaifu wakati anaweza vyote.

Mungu ni mkuu wa haki.
Yeye ndio mwenye haki ya kweli hapana mahala pengine unaweza pata haki ya kweli zaidi ya kwake. Ata mwendazake alivyoondoka watu wanahusisha na utendaji mkuu wa muumba katika kutenda haki pasipo kuangalia una cheo gani. Sasa ukinzani unakuja kwamba ni haki ya aina gani mtu mwenye kosa la kudanganya na mwenye kosa la kuuwa kuadhibiwa adhabu ya aina moja kuchomwa moto milele. Na ni adhabu ya aina gani isiyo na mwisho (hata mahakama zetu zina hekima juu ya hili maana kuna kuhuku mwaka, miezi)

Sisi wanadamu ni viumbe ambao tunafikirina hilo ndio jambo la msingi linatutofautisha na viumbe wengine sasa kama hatutumii akili zetu kufikiri basi ni kosa kubwa sana mbele ya ulimwengu,
 
Mkuu, umeongea kitu muhimu sana.

Watu wengi matendo yao hayaoneshi kwamba wanaamini Mungu, na ironically, mara nyingine sisi tusioamini Mungu ndio tunaotenda matendo yanayoendana na imani za kuamini Mungu.

Nitakupa mfano mmoja mdogo tu.

Nilikuwa katika kundi moja, mtu mmoja akawa analalamika anaumwa katika hilo kundi.

Wale watu wa kwenye hilo kundi wote wanajinasibu na imani ya Mungu.Kila mmoja akawa anasema "tutakuweka kwenye maombi", na "Mungu atakusaidia".

Mimi siamini katika maombi wala Mungu kumsaidia mtu mwenye matatizo, kwa sababu siamini Mungu yupo. Nakwenda kwa falsafa za kwamba, matatizo ya mtu yatamalizwa na mtu, maombi ni kujiliwaza tu na Mungu hayupo.

Nikaguswa sana na kilio cha yule mtu, ni dada wote tunamjua, hana uwezo, na pale kwenye kikundi kuna watu wana uwezo wa kumsaidia wanajibalaguza kumuombea kwa Mungu.

Mimi nikatembeza muamala chapchap yule dada asaidiwe, nikamtumia rafiki yetu mwingine alikuwa Dar alikuwa na wasaa wa kuweza ku organize mgonjwa apelekwe hospitali.

Kuna rafiki yetu mwingine daktari aka arrange hospitali yule dada apokewe.

Ndani ya muda mfupi ule muamala wangu ukawa umeshawezesha yule mgonjwa akatiwe bima, aanze matibabu.

Huku wengine waliojikita kumuombea mgonjwa kwa Mungu wakawa kama wameona aibu, ukatembea mchango kusaidia mgonjwa.

To make a long story short, wale watu wanaoamini Mungu waliofundishwa usamaria mwema na kusaidia watu wenye matatizo wote walikuwa wanaangaliana wakati mwenzao, rafiki yao waliyemjua kwa miaka mingi anakaribia kufa. Na ninaposema anakaribia kufa si utani.Yule rafiki yetu daktari alikuja kutuambia kwamba pale tungechelewa kidogo tu habari ingekuwa tofauti sana.

Nikatokea gubegube tu hata siamini Mungu yupo, lakini kwa sababu siamini Mungu yupo hilo ndilo limenipa wajibu mimi kufanya kazi ya kusaidia mwenyewe bila kumsukumizia mzigo huo Mungu, kwa sababu najua Mungu hayupo. Nikaanzisha msaada chapchap.

Sasa hapo utaona wasioamini Mungu wanafanya usamaria mwema kirahisi kama vile wanaamini Mungu, wanaoamini Mungu wameendekeza ubinafsi.

Hii dunia kama watu wangekuwa kweli wanaamini Mungu yupo kama wanavyodai, maovu mengi sana yangetoweka.

Watu wanaiba mpaka misikitini. Waziri Mkuu katudanganya msikitini kwamba rais mzima anapiga kazi.

Halafu utaambiwa huyo naye anaamini Mungu.

Ni kweli anaamini Mungu?

Bora hata mimi nimesema siamini Mungu na sijadanganya msikitini kama yeye!
Mkuu

Huoni kwamba wadau 'walipomuweka dada yetu kwenye maombi' ndo sasa Mungu akakugusa wewe kutembeza muhamala?

Ama ulitegemea Mungu ashuke kutoka mbinguni aonekane waziwazi akimsaidia dada yetu?
 
Si kweli.

Kwahiyo unataka kutuambia kutokujua na kukataa uwepo wa mungu hivi viko sawa ns ndiyo "Atheism" hii ?

Sasa kama hata kutofautisha kati ya kutokujua na kukana unashindwa inakuwaje una mkana Mungu ?
Atheism ni lack of beliefs
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani hakuna contradiction.

Kwa sababu.

Mabaya kutowezekana si contradiction kwa Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote.

Mabaya kuwezekana ndiyo contradiction.

Umeelewa hilo somo?
Hivi unaelewa maana ya contradiction ?

Inatakiwa uoneshe matukio mawili yanayokinzana,, yaani utuoneshe matukio mawili au zaid ya Mungu ambayo hayawezi kutokea mda mmoja kwa pamoja...

Sasa kuwa mjuzi wa yote na uwezo wote kunahusiana nini na yeye kuamua kuumba ulimwengu wake ambao ameruhusu hayo mabaya yatokee ??

Ina maana akiwa mwenye uwezo wa yote ni lazima azuie mabaya ?

What if mabaya angeyazuia, ina maana kwako ww Mungu asingekuwa na contradiction, sawaa

Je utaongelea vp wale ambao wangekuja kuhoji ya kwamba kwanini Mungu asiruhusu mabaya kutokea, kwa point yako na wao wangesema Mungu ana contradiction,,

Sasa huoni kwamba ww ndo unajiletea contradiction mkuu na sio Mungu

Mfano ulotoa haina logic kabisa,, jitafakari zaid !!
 
Back
Top Bottom