Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Mara nyingi nimekuwa nikiwaza huyu member hapa JF atakuwa alikutana na incident iliyomfanya akamchukia Mungu.

Hapa anaeleza namna alivyokuwa anasali na Nyerere pale St Peters




My take, huyu anahitaji kuombewa ili amrudie muumba wake.
Mshana Jr
Jamaa hata yale maajabu ya musa kuwekwa museum pale misri yanamfanya asiamini kama kuna Mungu....
 
Chanzo ni muhimu,na hapo hakuna mwanya unao onyesha kuokuwa na umuhimu wa chanzo.

Sababu tunapo mzungumzia Mola ambaye ni "Necessary Being" yaani uwepo hauna kinyume sababu yeye ni ndiyo mwanzo,ukiuliza kumbe hakuna umuhimu inabidi utuonyeshe wewe kwamba huko kutokuwa na umuhimu kunawezekana vipi kisha utuambie imekuwaje ulimwengu uko hivi ulivyo.

Sasa nikuulize vipi wakati hili ndiyo swali ambalo mnashindwa kulijibu kila siku.
Nilikia nashindwa kujibu kwasababu nilikua nadhani chanzo ni muhimu ili kitu kiwepo, ila now umenifunza kua chanzo si muhimu

Nadhani hata wewe huna haja ya kuuliza tena hilo swali kwasababu majibu unayajua kua hakuna chanzo
 
Jamaa hata yale maajabu ya musa kuwekwa museum pale misri yanamfanya asiamini kama kuna Mungu....
Musa gani?

Unajuaje ni musa wa vitabuni na sio kibopa tu wamtaani?
 
Kila kilichopo kwenye space, time and matter lazima kiwe na chanzo,,

Nimsaidie kukuuliza hilo swali unalotaka akuulize ?
Hujalielewa swali

Swali limeuliza "kila kilichopo ni lazima kiwe na chanzo"

Majibu ya swali hapo ni mawili tu (ndio/hapana)
 
Kwanini niwe na kazi ya kuepuka mabaya wakati mungu aliyaumba kwa ajili yangu?
Sababu amekupa uwezo wa kuyaepuka na hiyo si kazi tena.
Ingekua mabaya yanatakiwa kuepukwa basi Mungu huyu angetuepushia kwa kutoyaruhusu kuwepo.
Una akili ndogo sana,mabaya yana athari hasi ndiyo maana lazima yaepukwe. Kitu kinacho dhuru wewe kiakili au kimaana au kihisia,hicho ni kibaya kwako vipi huwa unakiepuka au unazembea ? Unauliza maswali ya kitoto sana.

Unakubali kama kuna mbaya bilashaka,kama unakubali vipi tena usema "...ingekuwa..." nilishakwambia ya kuwa usiwe unajenga hoja kwa dhana lazima ukosee kama unavyokosea hapa.
Kwa fact ya kidini tu swala hilo haliingii akilini, kitendo cha yeye kuyaruhusu ili yawepo maana yake yatumike (kama isingekua kutumika asingeyaumba) halafu wewe ukawa unayaepuka. huoni kwamba ni dhambi unafanya kufru kwa kumkosoa mungu kua kazi yake ya kuumba mabaya ina makosa??
Hii siyo kweli hakuna akili inayo kubali kwamba kila ambacho kipo basi kitumike,hilo halipo. Ndiyo maana mola wetu akatuweka wazi juu ya yote yenye manufaa na yote yenye hasara na akaweka mlango wa kutubia kwa yale tunayo kosea.

Lazima tuyaeupuke sababu yeye amelazimisha tuyaepuke na ametupa bishara ya adhabu.
 
navyo jua mimi ni kuwa ni katika ukanushaji na kukataa juu ya uwepo wa mungu,sasq swali ilikuwaje mkafikia huku je ushahidi wa kutokuwepo mungu mnao ? Usilete hoja za dhana,mara ooh labda mara kadha,hizi habari hatutaki na usilete mambo ya logic sababu logic ni dhaifu mno.
Ushahidi gani ambao ulitarajia sisi tungekuwepo nao ambao ungekushawishi wewe kua tumeweza kuthibitisha Mungu hayupo?

Wewe unaamini katika Mungu Allah

Unaweza kuthibitisha miungu mingine inayoabudiwa na dini zingine zilizo kinyume na Mungu wako kua haipo?

Ukiweza hilo nitatumia njia hizo hizo ulizotumia wewe kukuthibitishia Mungu wako hayupo
 
Hilo swali ni la uongo,, ni swali la kizushi..
Swali lako lazima liwe na mipaka,,

Hivi unaujua ulimwengu.?

Je, binadamu anaweza kuGrasp vitu ambavyo vipo beyond ulimwengu ?

Nimsaidie kukuuliza lile swali ?
Kuweka mipaka ni kukubali kupachika uwongo kwa makusudi

Njia ya uwongo haiwezi kukufikisha kwenye jibu la ukweli

Namimi siko tayari niruhusu uwongo, niko tayari kusema sijui kuliko kupindua pindua kanuni ili mradi nipate jibu ambalo litakalonipa faraja

Kila kilichopo ni lazima kiwe na chanzo?
 
.

Huna imani vipi,wakati imani yako ni kutokuwepo kwa mungu. Atheism nayo ni imani,ndiyo maana hata maana yako uliyo itoa iko dhidi ya uhalisia.

Atheism ni kuto amini juu ya uwepo wa Mola. Maana kutokuwa na imani juu ya kitu fulani ni kukikanusha. Muwe mnajifunza hata lugha na maneno yake katika maana.
Kutokuwepo kwa imani, sio kuwepo kwa imani

Ukishasema "haipo" maana yake "haipo" kauli yako ya pili kua "ipo" itakua na contradiction
 
Kwanini usitumie njia zako ww kuthibitisha kuwa Mungu wake hayupo,, Kwanini utegemee jinsi atakavyopinga usahihi wa Miungu wa dini zengine ?

Ina maana hoja zako ww haziwezi kusimama kivyake ?
Kipi kilichokufanya uhisi sijafanya hivyo?

Umesoma kwa kuelewa hiyo hoja nzima au umeidandia tu?
 
Kukanusha jambo ni common sense tu ndo inayohitajika
Kukanusha jambo usilo lijua ni ujuha,yaani upunguwani.

Sasa usiseme tu ni akili ya kawaida katika upuuzi. Yaani mtu jambo hulijui unalikanusha mwisho unasema ni akili ya kawaida ? Hili si sawa.
Unauthibitisho kua sndanguja yupo? Vipi unapinga kua hayupo?
Huyu simjui. Ni nani huyu ?
nasema kua alimuumba huyo mola na kua sio mola ndo chanzo cha vyote.
Kwamba haya umesema wewe,basi ni jukumu lako kututhibitishia ya kuwa yeye amefanya hayo. Hayo aliyo yasema tunayapata wapi ?

Nasubiri ithibati.
Kwasababu huwezi kuthibitisha hayupo haitamaanisha hayupo.
Maana yake hapa ukishindwa kuthbitisha unathibitisha ya kuwa wewe huna elimu juu ya hilo unalo kanusha,na usahihi ulitakiwa ukae kimya mpaka siku utakapo weza kuthibitisha hilo. Hamfundishwi adabu za kielimu.

Sasa kipi kilicho kupa ujasiri udai ya kuwa Mola hayupo,na huku unashindwa kuthibitisha. Tumekubali kwamba huwezi kuthibitisha basi tuambie kipi kimekupelekea ukanushe na je kwa mizani ipi imekupelekea wewe ukahitimisha ya kuwa Mola hayupo.
"TUMA 5,000,000 KWA SCARS HARAKA IWEZEKANAVYO MIMI NI MUUMBA WAKO"
Nimecheka sana,ndiyo maana huwa tunawaambia akili hamna.

Mola gani anatoa amri ya kutumiwa hela,huyu Mola dhaifu sana.
 
Nilikia nashindwa kujibu kwasababu nilikua nadhani chanzo ni muhimu ili kitu kiwepo, ila now umenifunza kua chanzo si muhimu

Nadhani hata wewe huna haja ya kuuliza tena hilo swali kwasababu majibu unayajua kua hakuna chanzo
Soma nilicho kiandika kisha ukielewe na ujibu swali nililo kuuliza.
 
Kumbe hujui huwa vinakuwa wapi, sasa unaulizaje swali ingawa hujui vitu vinakuwa wapi ?

Narudia tena,, swali lako ni la uongo na la kizushi,, halina usahihi !!
Nikisipojua wapi vinapokua hiyo itafanya huko vilikokua visiwepo?

Mimi nazungumzia kila chenye sifa ya "kuwepo" no matter where it is. Hoja yangu haizungumzii eneo au makazi ya hivyo vitu vilipo bali kokote kule as long as vipo basi vitakua vimeguswa na hoja yangu

Kila kilichopo ni lazima kiwe na chanzo?
 
Back
Top Bottom