Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Hii siyo kweli hakuna akili inayo kubali kwamba kila ambacho kipo basi kitumike,hilo halipo. Ndiyo maana mola wetu akatuweka wazi juu ya yote yenye manufaa na yote yenye hasara na akaweka mlango wa kutubia kwa yale tunayo kosea.

Lazima tuyaeupuke sababu yeye amelazimisha tuyaepuke na ametupa bishara ya adhabu.
Kwa maana hiyo mabaya yaliumbwa kwa lengo lipi?

Mungu alikurupuka?
 
Hapo tumeelewana mkuu,, tuko pamoja..


Hii logic sio sahihi,, Ngoje nikupe huu mfano mdogo...


Mungu ni muweza wa wote na ndo maana haitotokea atengeneze kitu ambacho hawezi kukimudu,,

Kwa hio unampangia vya kufanya muumba wakoo, ivi hupati mashakaa kwamba inaonekana humjui muumba wako kwani unamjua kutoka kwa maandishi ya watu wengine ambao ndio aliamua kujionyesha kwao. Kwa nini hakutufungulia nasi tumjue kama hao wengine,. Ivi unanipata kweli
 
nayosemaa,
Ivi unajua sifa mojawapo ya mjinga.... Mjinga huwa anaamini sana yale aliyojifunza na inakuwa ngumu kwake kubadilika kutokana na maarifa mapya yanayokinzana na ujuzi wake wq awali.
Hii si maana ya mjinga,mjinga ni yule asiyejua jambo fulani.

Maana uliyo itoa ni maana ya mpumbavu. Yaani yule anaye jiona anajua na hajui na hajijui kama yeye hajui.

Rekehisha kiti chako kwanza kisha ukipambe.
Socrates alisemwa na oracle hio kale ya ugiriki kama mtu aliye na busara kuliko wote. Jee unajua sentensi inayojumuisha mafunzo yake yote inasemaje...
Inasema hivi " ninachojua kwa uhakika ni kwamba sijui kitu"
Alikuwa sahihi katika hili na kweli alikuwa hajui. Kujua kama wewe hujui ni hatua na wewe ni mwerevu,tena kusema hujui kwa kile ambacho hukijui ni nusu ya elimu.
Na je unajua ugonjwa wa akili upo vipi sifa za wenye ugonjwa wa akili unazifahamu? Nafahamu chache kama kusikia sauti kichwani, kuona vitu ambavyo havipo, na kuwa na mashaka kama kuna kitu kinakwangalia matendo yako na kina kalamu kinaorodhesha, tena mpaka hata chooni bado tu kinakufatilia nyendo hata mawazo kinahesabia,
Kuna namna kadhaa za kutoa maana ya jambo,hapa nagusia namna ya kuarifisha tamko kwa mfano. Nasema mimi,Wakana mungu ni wagonjwa wa akili,sasa ukitaka kumjua mgonjwa wa akili katika aina za ugonjwa wa akili basi watazame wakana mungu.

Sifa nazijua,kuna ugonjwa wa akili na kuna wasi wasi.
Kuhusu proof ngoja nikupe somo kidogo tuu
Jambo linakuwa linathibitishwa pale zaidi ya ushahidi moja unapotolewa
Mfano
Geogre washington ameacha shahidi nyingi sana kuna barua alizoandika, kuna kaburi, kuna story za watu waliokutana,kuna evidence ya vita aliyopigana,
Huu siyo ushahidi wa kuonyesha yeye alikuwepo,tukienda katika misingi ya uhakiki wa habari. Sifa ya masimulizi yawe ya kweli lazima kuwe na mpokezi wa habari hiyo tena awe amemuona au huyo amepewa habari na yule aliyemuona. Kuhusu machapisho hichi si kigezo mpaka ubainike ukweli juu ya wale wali mdiriki tena wawe na sifa ya ukweli.

Story za watu walio kutana naye zimesimuliwa na nani na tunazipata wapi ?

Unao ushahidi kuonyesha ya kuwa hizo barua ameandika yeye ?
Na pia unaongea watu kukimbia maswali huna lolote watalamu wa psychology wanajua tuu hio ni self defence yaani unapakazia wengine madhaifu ambayo unayo
Kwanza suala la wao kukimbia maswali labda wewe umeamua kupoteza muda kwa kuandika uongo.

Pili,suala la wao kukimbia maswali hilo silisemi mimi bali wengi katika wanao jadiliana nao huwa wanasema watu hawa wanakimbia maswali,lakini siyo kwamba wanakimbia kwa kupenda,sababu hawana elimu na hawana cha kutoa,asiyenacho atatoa nini ? Sasa huwezi bishana na ukweli zaidi ya kuumia na kupoteza muda.

Kama una hoja jenga hoja na ujibu maswali yanayo ulizwa humu.
Nikuulize swali je ni kitabu gani cha mkusanyiko wa waandishi ambao hao waandishi sio wao walioandika hicho kitabu?
The History of Andalusia.
 
Hii logic sio sahihi,, Ngoje nikupe huu mfano mdogo...

Yaani umwambie computer scientist atengeneze application ya simu ambayo hata yeye atashindwa kuimudu,, huoni kwamba hayo madai hayana mantiki (logic),, inawezekana vp akatengeneza codes ambazo yeye atashindwa kuzichambua ? Hii hoja sio sahihi
Ehee hii sentensi inaonyesha jinsi gani ulivyo makini kutambua yaliyo ya uwongo.

Sasa hushtuki kuona sentensi zenye logic za uwongo zikihusishwa moja kwa moja na muumba

Na kwanini utoe mfano wa computer scientist ambayo wote tunakubali yupo kulinganisha na kiumbe wa kufikirika, kwani umekosa mifano yote ya kufikirika na kukimbilia mfano halisi, au hujui mfano wa kufikirika nikupatie... Kwenye avenger tony (iron man) pamoja na bruce (hulk) walitengeneza programu JARVIS ambayo ikawazidi akili, unasemaje juu ya hili
 
Nakubaliana nawewe maana ukienda nchi kama Saudi arabia wanawake wanajistili sana ila unakuta kesi za ubakaji ni nyingi ila kuna nchi bado watu wana achia matiti wazi mpaka leo lakini akuna baya linalo tendeka dhambi na dhani ipo akilini mwetu tu.
Mkuu, naomba nipingane na wewe kidogo. Dhambi inaitwa dhambi si kwa sababu Saudia Arabia kwao si dhambi halafu nchi zingine ni dhambi, BALI KWA SABABU MUNGU Kasema ni dhambi. Kwahiyo kama Mungu amesema kwa mfano usizini, basi hiyo ni dhambi hata kama Mwanasayansi mwenye PhD 20 anasema tendo hilo sijui linapunguza stress na blah blah kibao, na akaleta ushahidi wake na reaserches zake.

Mfano mzuri ni suala la Homosexuality yaani mapenzi ya jinsia moja. Hili ni suala ambalo lipo wazi kwamba ni dhambi na ni machukizo machoni pa BWANA, Full stop. Ila angalia sasa Mataifa ya Magharibi yanasema otherwise kwamba sio dhambi, ni haki ya binadamu nk nk.

Shetani anatumia trick ile ile aliyotumia kwa Eva, kwamba Mungu amesema msile eti mtakufa?? Anatembea mule mule kwenye ulichosema Mungu kisha ana-twist maelekezo ya Mungu na kuweka yake. No wonder why the Bible named Him The Great Deceiver.
 
Si kweli.

Kwahiyo unataka kutuambia kutokujua na kukataa uwepo wa mungu hivi viko sawa ns ndiyo "Atheism" hii ?

Sasa kama hata kutofautisha kati ya kutokujua na kukana unashindwa inakuwaje una mkana Mungu ?
Hahaha a million dollar question. Eti watoto ni atheists duh
 
Jurjani

Nashindwa kuthibitisha kama una kimbia swali au unatapatapa

Nii hili swala la mgonjwa wa akili hebu niambie hawa watu kwenye hii mifano kama ni wazima. Moja... Anataka kumchinja mtoto wake kwa sababu kuna sauti kasikia kichwani mwake ikimwambia atende hivyo. Mbili... Anasema aliona mti unawaka moto bila kuungua. Tatu... Watu wanaamini kuna mtu hapo kale kidogo alitembea juu ya maji.

Karibu sana
 
officialboy

Si umesema kwamba Mungu hawezi tengeneza jambo likamshinda.

Sasa nakuuliza umejuaje ? Huoni kuwa unamwekea mipaka , kwa sentensi hio huoni kwamba inaonyesha hawezi vyote, na kama ukikimbilia logic huoni kuwa kama mtu tu anaweza pata mawazo ambayo muumba wake hawezi kufanya huoni kuwa ushategua logic
 
Jurjani

Nashindwa kuthibitisha kama una kimbia swali au unatapatapa

Nii hili swala la mgonjwa wa akili hebu niambie hawa watu kwenye hii mifano kama ni wazima. Moja... Anataka kumchinja mtoto wake kwa sababu kuna sauti kasikia kichwani mwake ikimwambia atende hivyo. Mbili..


. Anasema aliona mti unawaka moto bila kuungua. Tatu... Watu wanaamini kuna mtu hapo kale kidogo alitembea juu ya maji.

Karibu sana
Naona unapoteza kumbukumbu,hapo awali ulitaja sifa unazo ona wewe ya kuwa ni za mgonjwa wa akili,mimi nikakupa sifa anuai ya mgonjwa wa akili. Sasa unaposema nakimbia swali wakati nilikwambia hayo si sifa anuai ya mgonjwa wa akilo mpaka itakapo thibitishwa sababu hayo yanaingia katika mawenge,wasi wasi na kuchezewa na shetani. Sasa huenda nilicho kiandika ni kipya kwako au hukukielewa,ila kuhusu jibu nilikujibu vizuri sana.

1. Sauti hizo hazimaanishi kuwa huyo ni mgonjwa wa akili sababu hata mtu mzima na afya yake ya akili hali hizi huwa zinawatokea watu. Ndiyo maana ukimuuliza anakujibu na anakuwa na kumbukumbu kabisa.

2. Nukta ya pili ya kuona mti,vipi iwe ishara ya mtu kuwa hana akili ? Au mgonjwa wa akili ? Nitakuuliza aliona ndotoni au na je hali hiyo ni yenye kujirudia rudia au ?

3. Huu mfano ni mfu na unaonyesha huna maarifa juu ya haya mambo. Huu tunauita ni muujiza na wenyewe huzingatiwa kwa mizani ya aina mbili. Mzani wa karama kwa wale waja wema ambao ni wacha mungu walikuwa wanafanya sana mambo yasiyo kuwa ya kawaida,ila wapo marafiki wa shetani nao hufanya mambo ya ajabu ila kwa kuificha haki na kudhihirisha upotevu.

Mimi nakuuliza swali sasa,kwanini umetoa mifano ya uongo ?
 
mimi hua nashangaa sana kuona kiranga anabishana na officiaboy + jurjani.

Like how can you argue with someone who is mentally unstable to grasp the concept you are trying to say?.

kiranga kauliza "thibitisha mungu yupo" ila wanajibu kua "thibitisha hayupo", utadhani kisichopo kipo kuthibitishika hakipo.

mi nadhani muache kubeat around the bush, mthibitishieni huenda akawa mfuasi wenu, people are won over na sio kumdictate kwa vitisho vya
Mimi nafikiri makosa ni kujadili kitu bila kujua maana yake ni nini.

In this thread neither Kiranga nor the proponents has attempted to define God.

Lakini pia hakuna aliyeeleza uthibitisho maana yake ni nini.

Sasa kama hayo mawili hayajafanyika, dhana yote inakosa mantiki; hivyo ni mabishano tu yasio na maana.
 
Naona unapoteza kumbukumbu,hapo awali ulitaja sifa unazo ona wewe ya kuwa ni za mgonjwa wa akili,mimi nikakupa sifa anuai ya mgonjwa wa akili. Sasa unaposema nakimbia swali wakati nilikwambia hayo si sifa anuai ya mgonjwa wa akilo mpaka itakapo thibitishwa sababu hayo yanaingia katika mawenge,wasi wasi na kuchezewa na shetani. Sasa huenda nilicho kiandika ni kipya kwako au hukukielewa,ila kuhusu jibu nilikujibu vizuri sana.

1. Sauti hizo hazimaanishi kuwa huyo ni mgonjwa wa akili sababu hata mtu mzima na afya yake ya akili hali hizi huwa zinawatokea watu. Ndiyo maana ukimuuliza anakujibu na anakuwa na kumbukumbu kabisa.

2. Nukta ya pili ya kuona mti,vipi iwe ishara ya mtu kuwa hana akili ? Au mgonjwa wa akili ? Nitakuuliza aliona ndotoni au na je hali hiyo ni yenye kujirudia rudia au ?

3. Huu mfano ni mfu na unaonyesha huna maarifa juu ya haya mambo. Huu tunauita ni muujiza na wenyewe huzingatiwa kwa mizani ya aina mbili. Mzani wa karama kwa wale waja wema ambao ni wacha mungu walikuwa wanafanya sana mambo yasiyo kuwa ya kawaida,ila wapo marafiki wa shetani nao hufanya mambo ya ajabu ila kwa kuificha haki na kudhihirisha upotevu.

Mimi nakuuliza swali sasa,kwanini umetoa mifano ya uongo ?

Tulia usome kwa umakini mbona waongea mambo ambayo sijakuuliza.

Jibu no 1. Kama unamfahamu huyo mtu ambaye anasikia sauti kichwani au kama ni wewe hilo sio ishara njema ndugu ni mojawapo ya viashiria ya kuwa unapoteza, wahi hospitali kabla hujaanza kujibizana na hizo sauti

Jibu no 2. Sijakwambia kwamba ueleze mtu akiona mti unawaka moto bali nilitaka unieleze utamchukuliaje mtu anayekuambia kwamba kulikuwa na moto unawaka na hauunguzi. Sijui kama unanisoma

No 3. Bado unafanya mchezo wa kufafanua , mi nakuuliza swali we unaanza kufafanua ivyo ndo ulivyofundishwa huko shuleni. Nadhani nimedhihisha kwamba wewe ndio mkimbiaji maswali.

Hakuna haja ya kukimbia maswali papana nayo. Pia katika paragraph ya kwanza nashangaa upo confident kabisa ukisema mtu kachezewa na shetani yaani unaona ni point kabisa ya kuweka. Mbona una mawazo ya kizamani sana dunia ishapita zama za kumsingizia shetani. Mbona mambo yanaelezeka vizuri tu kutoka kwa matabibu wetu, kwa hilo inaonekana ni mtu usiyetaka kuwajibika yaani ukikamatwa ndo wale utasikia shetani kanipitia.
 
Hiyo nimekuonyesha ya kuwa hilo nawezana tunarudi kwenye asili,sababu ukivunja msingi ndiyo umeangusha jengo.

Lakini ulitakiwa uainishe ya kuwa unazungumzia ng'ombe au ?Ng'ombe yupo ila naongelea ubatili wa ng'ombe kufanywa mungu.
ulitakiwa uthibitishe hiyo miungu haipo ili tujue kweli inawezekana

Wewe umeonesha kukubali kua miungu hiyo ipo ila umekanusha hiyo miungu sio ya kweli kitu ambacho hukutakiwa kufanya

Thibitisha hiyo miungu haipo
 
Kukanusha jambo usilo lijua ni ujuha,yaani upunguwani.

Sasa usiseme tu ni akili ya kawaida katika upuuzi. Yaani mtu jambo hulijui unalikanusha mwisho unasema ni akili ya kawaida ? Hili si sawa.
kuna kitu kinaitwa "burden of proof"

Vile vile uwongo hauhitaji maarifa makubwa kuugundua wala sio tija kuwa na jibu sahihi ili uweze kujua kitu fulani ni uwongo
 
Kukanusha jambo usilo lijua ni ujuha,yaani upunguwani.

Sasa usiseme tu ni akili ya kawaida katika upuuzi. Yaani mtu jambo hulijui unalikanusha mwisho unasema ni akili ya kawaida ? Hili si sawa.

Huyu simjui. Ni nani huyu ?
unataka kumjuaje, wakati jina nimekuwekea pamoja na uhusika wake unaomtambulisha yeye ni nani?
 
Back
Top Bottom