Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Kiranga alikuwa anasali Kanisa Katoliki. Ilikuwaje akaanza kuamini hakuna Mungu?

Thibitisha kwamba anaonekana.
Wapi nimesema anaonekana..

Wewe ulianza kwa kusema kwanini watu wanaamini Mungu ambaye haonekani,, mm nikakuuliza unauhakika gani kwamba Mungu haonekani,, ww ukasema nithibitishe kwa kutuma picha,, nikakujibu Sina picha yake, kisha nikakuuliza Je, kama sina picha yake ndo ina maana ya kwamba Mungu haonekani ? , hujanijibu hili swali

Huoni kwamba ww ndo mwenye deni la kutuhakikishia kwamba Mungu haonekani na sio mm,,
 
Kwanini asiumbe ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea ?

Angeumba ulimwengu ambao hakuna mabaya yoyote,, bado kuna watu wangejitokeza kuhoji ( logically ) kwanini Mungu hajaruhusu mabaya kutokea ?

Kwahiyo kutoumba ulimwengu ambao hakuna mbaya ndo inathibitisha kuwa hakuna Mungu ?

Contradiction ipo wapi hapo ?

Huo ni ufinyu wako wa kufikiri, lakini sio contradiction

Lete hoja nyingine !!
Kwa hiyo mungu ana care sana sauti za watu wanazo hoji kiasi cha kumfanya afanye hayo wanayoyataka?

Mbona sisi hapa tumekua tukohoji kuhusu uwepo wake na hakuna chochote kilichofanya ajidhihirishe kua yupo kama kweli huyu mungu anajali watu wanao hoji?

Mara kadhaa hapa tumekua tukihoji kua mwacheni Mungu wenu ajitetee yeye mwenyewe kama kweli yupo. kwanini hakujitokeza kujitetea kama kweli ana jali watu wanaohoji?


Kwa hiyo mungu aliumba mabaya ili kukwepa lawama?

Alishindwa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayajadiliki kwa namna yeyote?

Kama mabaya ni sehemu ya mipango yake tutasemaje tuna mungu mwema kwa viumbe wake?

Kama mungu aliumba mabaya ili kukwepa lawama za watu endapo angeumba mazuri pekee yake, mbona bado watu wanalaumu kwa kuumba mabaya? Mbona lawama bado iko pale pale?

Kwanini huyo mungu aliumba mabaya kwa kudhani mazuri pekee yangefanya watu walaumu kwa kudai yawepo na mabaya ilihali bado watu wanalaumu kwa hayo mabaya aliyoyaumba?


Kama watu wakifanya mabaya ambayo yeye kayaweka kwa makusudi kwanini akasirike na kuwahidi kuwachoma moto wakati?

Kwa maana hiyo hata huko peponi tunakoambiwa hakuna mabaya, ni uongo tumedanganywa?
 
Safi kabisa,sasa tuambie huu ulimwengu na sisi binadamu imekuwaje tukawa hivi tulivyo,je tumejiumba wenyewe au tumetokea pasi na chochote ? Hili swali huwa unalikimbia.

Embu tupe uwezekano au tuonyeshe kwamba Mola si muhusika wa huu ulikwengu na utuonyeshe uwezekano wa uwepo wa kitu pasi na msanifu wake,mwenye kujua,mwenye maarifa na mfano wake.

Omyesha ukichaa wake uko wapi ?

Kadhalika mpaka visivyo onekana vinamtengenezaji wake. Roho,njaa,maumivu,majonzi na mfano wake vyote vinatoka kwa Allah.

Vipo visivyo onekana ila vinauashiria wake kwa vinavyo onekana kuonyesha uwepo wake. Akili huioni wewe ila mwenye akili unamuona na asiyekuwa na akili unamuona kadhalika. Yaani Allah haonekani Ulimwenguni ila kuna muda tutamuona kama vile tunavyo jua la utosi,lakini kwa kuwa kwa sasa haonekani ila kuna ishara zinaonyesha uwepo wake akili,mazingira,ufunuo na mfano wa hivi huonyesha uwepo wake.

Kwahiyo kufikiri kwa aina hiyo unavyofikiri wewe ufinyu wake ni kama umefungiwa ndani ya chumba kidogo chenye kidirisha kidogo,kisha ukatazama nje ukahitimisha juu ya kile ulichokiona ndiyo kitu kizima wakati uhalisia ni kitu kidogo sana kwenye kile kitu kizima.

Kadhalika visivyo onekana vinamtengenezaji wake na yeye ni Allah mtukufu na akasema yeye ndiyo mjuzi wa yale ya dhahiri na yale yaliyofichikana.

Quantum Physics ni nadharia tu ambazo hata wakubwa zako hawakuweza kuzithibitisha.

Hakuna kinacho vunja "cause" and "effect" wakati kuna msanifu na kuna malighafi na kuna kile kinachotarajiwa. Labda nikupe kazi utuonyeshe kwa namna gani (hili najua huwezi kuonyesha ila naonyesha ujinga wako ulipo mili) Quantum Physics ina vunja "cause" na "effect" katika uwepo wa kiti mathalani, kilichotengenezwa kwa malighafi ya mbao (Material cause), msanifu (first cause) na kiti(effect) chenyewe. Kwahiyo kwa vyovyote vile Quantum Physics haiwezi kubatilisha (disprove) Causality.

Hivi ushawahi kufundishwa somo la ukosoaji maana hapa hujagusa hata kile alichokiandika uliye "mquote" mwisho wake una dai kwamba umeonyesha ujinga wake ? Kwenye nini mantiki au falsafa au hiyo Quantum Physics ?
Kwani kila kilichopo lazima kiwe na chanzo?
 
Nadhani ata siku kama kweli Mungu yupo Mungu akimpa kiranga ajieleze kwanini akumuamini nadhani kiranga anaweza,
kumwambia sikukuamini kwakua sikukuona.
Kwahiyo mkuu Kiranga anadai kwamba yeye hamuamini Mungu ( Anadai kuwa Mungu hayupo ) kisa hajawahi kumuona ?

Je, ni sahihi mtu kuhitimisha kuwa hakuna kitu flani kisa tu hujawahi kukiona ?

Kwa Maan hiyo tunaweza kusema pia Kiranga haamini uwepo wa vitu kadhaa kwa sababu havionekani mfano, hewa (Air) , umeme, upendo, huruma, etc

Pia Kiranga haamini uwepo wa Wi-Fi ( Wireless Fidelity ) kitu ambacho kipo kwenye simu yake

Huoni kwamba kiranga ndo anajiletea contradiction yeye mwenyewe ?

Ebu tupevuke wakuu,, tusidanganywe na hayo mawazo mlosoma kwenye hvo vitabu vinavodai kwamba vinaleta logic kumbe vyenyewe ndo vinaleta contradiction !!
 
Naamka vipi wakati wewe unaye niamsha ndiyo umelala fofo.

Mfano wa fikra za utumwa ni upi ?
Fikra za utumwa ni wewe kuamini miungu ya waarabu ngano zao na mapokeo ya kale ya jamii hizo na kuzipractice katika maisha halishi ya Sasa
Kama sio ujuha na uwendawazimu ni nini Kama sio ugonjwa wa akili ingali wewe ni mtu mweusi Wala huna vinasaba vya jamii husika ya mashariki ya Kati?
Ndio maana nasema amka ewe mtu mweusi utoke katika fikra mfu za hizo jamii zao!

Kama hinielewi endelea kua mtumwa wao daima ila Mimi hunishawishi kama mtu mweusi wa huku nyumbanitu.
Kwa hiyo mungu ana care sana sauti za watu wanazo hoji kiasi cha kumfanya afanye hayo wanayotaka watu wake?

Mbona sisi hapa tumekua tukohoji kuhusu uwepo wake na hakuna chochote kilichofanya ajidhihirishe kua yupo kama kweli huyu mungu anajali watu wanao hoji?


Kwa hiyo mungu aliumba mabaya ili kukwepa lawama?

Alishindwa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayajadiliki kwa namna yeyote?

Kama mabaya ni sehemu ya mipango yake tutasemaje tuna mungu mwema kwa viumbe wake?

Kama mungu aliumba mabaya ili kukwepa lawama za watu endapo angeumba mazuri pekee yake, mbona bado watu wanalaumu kwa kuumba mabaya? Mbona lawama bado iko pale pale?

Kwanini huyo mungu aliumba mabaya kwa kudhani mazuri pekee yangefanya watu walaumu kwa kudai yawepo na mabaya ilihali bado watu wanalaumu kwa hayo mabaya aliyoyaumba?


Kama watu wakifanya mabaya ambayo yeye kayaweka kwa makusudi kwanini akasirike na kuwahidi kuwachoma moto wakati?

Kwa maana hiyo hata huko peponi tunakoambiwa hakuna mabaya, ni uongo tumedanganywa?
Hawatakuelewa hawa binadamu wenzetu wenye upofu wa fikra mkuu!
 
Unaweza kuthibitisha hii kauli yako ? Thibitisha kwanza kisha nikujibu madai yako uloweka chini yake !!
Hivi umesoma na kuelewa kilichoandikwa na target ya hiyo hoja ukajua inataka nini?

Nihakikishie kwanza hilo maana nimeanza kuwa na shaka na uelewa wako kupitia reply yako
 
Kutokuwa naimani katika nini ? Kama hali iko hivyo kwanini mnakana sasa ?
Katika mungu, dini, na habari nyingine zinazohusu supernatural power

Sasa unataka tukubali wakati hatuna imani?

Sisi tunataka uthibitisho, unao hapo?
 
Kama mabaya ni sehemu ya mipango yake tutasemaje
Kwani unapofanya mabaya huwa unalazimishwa au kwa hiyari yako ? Sasa inakuwaje unauliza swali ambalo ukifikiria vizuri jibu unalipata hapo hapo.

Mola ametupa mtihani ambao una majibu,na ndiyo maana kuna toba ukikosea unatubia,yaani unasahihisha kosa,lakini muda huo huo ambao wewe unafanya uovu kuna wenzako wanafanya mema.

Mabaya siyo kwamba uyafanye bali uyaepuke na umeshaambiwa kabisa kwamba ukifanya uovu unalipwa kadha na ukifanya wema unalipwa kadha. Sasa kwanini usifanye mema ulipwe pepo na uwezo wa kufanya mema unao,sasa hii ndiyo maana halisi ya "Free Will" yaani uhuru ulio kamilika.
 
Bila shaka isipokuwa Mola yeye ndiyo hana chanzo na hakitanguliwa na kutokuwepo,yeye yupo.
Well, kumbe sio muhimu kua na chanzo ili kitu kiwepo

Back to your question

Niulize tena kuhusu chanzo cha ulimwengu now nitakujibu
 
Hivi umesoma na kuelewa kilichoandikwa na target ya hiyo hoja ukajua inataka nini?

Nihakikishie kwanza hilo maana nimeanza kuwa na shaka na uelewa wako kupitia reply yako
Nimesoma na nimeelewa hoja yako,, kwangu mimi hio hoja yako sio sahihi ( madai ya uongo ),, hio ni kwangu mimi...
Sasa nimekutaka uthibitishe hio hoja yako kwanza ili nione ukweli wake, wewe uliskia wapi au umeona wapi,,

If you assert a claim without valid proof, then it is considered as void !!
 
Katika mungu, dini, na habari nyingine zinazohusu supernatural power

Sasa unataka tukubali wakati hatuna imani?

Sisi tunataka uthibitisho, unao hapo?
Safi kabisa,ni wakati gani mtu anatakiwa akanushe jambo ? Akiwa hajui au akiwa na ujuzi wa jambo hilo ?

Naomba unielezee kutokuwa na imani katika Mungu kukoje,navyo jua mimi ni kuwa ni katika ukanushaji na kukataa juu ya uwepo wa mungu,sasq swali ilikuwaje mkafikia huku je ushahidi wa kutokuwepo mungu mnao ? Usilete hoja za dhana,mara ooh labda mara kadha,hizi habari hatutaki na usilete mambo ya logic sababu logic ni dhaifu mno.

Huna imani vipi,wakati imani yako ni kutokuwepo kwa mungu. Atheism nayo ni imani,ndiyo maana hata maana yako uliyo itoa iko dhidi ya uhalisia.

Atheism ni kuto amini juu ya uwepo wa Mola. Maana kutokuwa na imani juu ya kitu fulani ni kukikanusha. Muwe mnajifunza hata lugha na maneno yake katika maana.

Uthubitisho siyo tu kwamba ninao,bali upo na muda wowote na utoa.

Lakini suala la ithibati katika adabu za mjadala,yule anaye kanusha ndiyo huwa ana haki zaidi ya kuthibitisha juu ya kile anacho kikanusha sababu yeye hudhaniwa ya kuwa ana ujuzi mkubwa juu ya jambo hilo. Lakini hili huwa mnalikimbia na kuthbitisha ya kuwa hamna ujuzi ila tu sababu mko huru kusema au kuandika mnacho kitaka basi mnaandika tu.
 
Kwani unapofanya mabaya huwa unalazimishwa au kwa hiyari yako ? Sasa inakuwaje unauliza swali ambalo ukifikiria vizuri jibu unalipata hapo hapo.

Mola ametupa mtihani ambao una majibu,na ndiyo maana kuna toba ukikosea unatubia,yaani unasahihisha kosa,lakini muda huo huo ambao wewe unafanya uovu kuna wenzako wanafanya mema.

Mabaya siyo kwamba uyafanye bali uyaepuke na umeshaambiwa kabisa kwamba ukifanya uovu unalipwa kadha na ukifanya wema unalipwa kadha. Sasa kwanini usifanye mema ulipwe pepo na uwezo wa kufanya mema unao,sasa hii ndiyo maana halisi ya "Free Will" yaani uhuru ulio kamilika.
Kwanini niwe na kazi ya kuepuka mabaya wakati mungu aliyaumba kwa ajili yangu?

Ingekua mabaya yanatakiwa kuepukwa basi Mungu huyu angetuepushia kwa kutoyaruhusu kuwepo.

Kwa fact ya kidini tu swala hilo haliingii akilini, kitendo cha yeye kuyaruhusu ili yawepo maana yake yatumike (kama isingekua kutumika asingeyaumba) halafu wewe ukawa unayaepuka. huoni kwamba ni dhambi unafanya kufru kwa kumkosoa mungu kua kazi yake ya kuumba mabaya ina makosa??
 
Nimesoma na nimeelewa hoja yako,, kwangu mimi hio hoja yako sio sahihi ( madai ya uongo ),, hio ni kwangu mimi...
Sasa nimekutaka uthibitishe hio hoja yako kwanza ili nione ukweli wake, wewe uliskia wapi au umeona wapi,,

If you assert a claim without valid proof, then it is considered as void !!
Ebu nifafanulie umeelewaje hoja yangu?
 
Well, kumbe sio muhimu kua na chanzo ili kitu kiwepo

Back to your question

Niulize tena kuhusu chanzo cha ulimwengu now nitakujibu
Yaani hawa watu wanavituko sana wanakwambia ulimwengu na vitu vyote viliumbwa na Mungu,yaani yeye ndio chanzo kwa kuviumba
Hapo hapo ukiuliza chanzo Cha huyo Mungu wanakwambia Hana mwanzo Wala mwisho
Yaani wanakua na logic zenye contradictions kibao
 
Well, kumbe sio muhimu kua na chanzo ili kitu kiwepo
Chanzo ni muhimu,na hapo hakuna mwanya unao onyesha kuokuwa na umuhimu wa chanzo.

Sababu tunapo mzungumzia Mola ambaye ni "Necessary Being" yaani uwepo hauna kinyume sababu yeye ni ndiyo mwanzo,ukiuliza kumbe hakuna umuhimu inabidi utuonyeshe wewe kwamba huko kutokuwa na umuhimu kunawezekana vipi kisha utuambie imekuwaje ulimwengu uko hivi ulivyo.
Niulize tena kuhusu chanzo cha ulimwengu now nitakujibu
Sasa nikuulize vipi wakati hili ndiyo swali ambalo mnashindwa kulijibu kila siku.
 
Safi kabisa,ni wakati gani mtu anatakiwa akanushe jambo ? Akiwa hajui au akiwa na ujuzi wa jambo hilo ?

Naomba unielezee kutokuwa na imani katika Mungu kukoje,navyo jua mimi ni kuwa ni katika ukanushaji na kukataa juu ya uwepo wa mungu,sasq swali ilikuwaje mkafikia huku je ushahidi wa kutokuwepo mungu mnao ? Usilete hoja za dhana,mara ooh labda mara kadha,hizi habari hatutaki na usilete mambo ya logic sababu logic ni dhaifu mno.

Huna imani vipi,wakati imani yako ni kutokuwepo kwa mungu. Atheism nayo ni imani,ndiyo maana hata maana yako uliyo itoa iko dhidi ya uhalisia.

Atheism ni kuto amini juu ya uwepo wa Mola. Maana kutokuwa na imani juu ya kitu fulani ni kukikanusha. Muwe mnajifunza hata lugha na maneno yake katika maana.

Uthubitisho siyo tu kwamba ninao,bali upo na muda wowote na utoa.

Lakini suala la ithibati katika adabu za mjadala,yule anaye kanusha ndiyo huwa ana haki zaidi ya kuthibitisha juu ya kile anacho kikanusha sababu yeye hudhaniwa ya kuwa ana ujuzi mkubwa juu ya jambo hilo. Lakini hili huwa mnalikimbia na kuthbitisha ya kuwa hamna ujuzi ila tu sababu mko huru kusema au kuandika mnacho kitaka basi mnaandika tu.
Kukanusha jambo ni common sense tu ndo inayohitajika

Unauthibitisho kua sndanguja yupo? Vipi unapinga kua hayupo?

Kwasababu niko naye kichwani mwangu anasema kua alimuumba huyo mola na kua sio mola ndo chanzo cha vyote.

Kwasababu huwezi kuthibitisha hayupo haitamaanisha hayupo.

Kwakuthibitisha kua sndakuja yupo nitamuachia sentensi ya mwisho aandike yeye

"TUMA 5,000,000 KWA SCARS HARAKA IWEZEKANAVYO MIMI NI MUUMBA WAKO"
 
Kwani wewe unadhani nimeelewaje ?

Ingekuwa kuna kupeana tuzo za kukimbia maswali,, aisee wewe ningekupa PhD
So hata ku brief ulichoelewa nacho huwezi?

Nitakua na hakika gani na kauli yako uliyosema mwanzo kua umeelewa?
 
Back
Top Bottom