Kiranga na jamaa zake wanaweza wasionekane kwenye thread mbalimbali lakini uzi wowote unaomsifia Mungu huwakosi

Kiranga na jamaa zake wanaweza wasionekane kwenye thread mbalimbali lakini uzi wowote unaomsifia Mungu huwakosi

Wewe Kama Imani Yako inategemea watu wengine ushafeli Imani si lazima ifuatwe na kila mtu ni neema ya Mungu watu kuwa katika Imani, usitishike na kelele maana miruzi mingi hupoteza mbwa
 
JF ni public forum, kila mtu ana uhuru wa kuchangia mada anayoitaka.

Na kila mtu ana mada zake pendwa, wengine mada za michezo hawakosi, wengine mada za siasa hawakosi. Na sisi hizi ndizo mada zetu, tatizo lako nini?

Usiulize kwa nini Kiranga anachangia sana mada hizi. Huu ni uhuru wangu. Jibu hoja.

Ukiuliza sana swali hilo utakuwa kama unafanya censorship hawa wakina Kiranga wasiandike.

Mimi hata sianzishi mada mkuu. Mada wanaanzisha wengine. Nyingine wala sizioni watu wananiita nichangie, wanapenda kujua mawazo yangu.

Tatizo lako nini?

Hupendi kuona mawazo tofauti na yako?

Kubali tu kuwa kuna watu tofauti na wewe.

Mbona sisi tumezungukwa na watu wanaoamini Mungu na kila siku tunalazimishwa kusikia habari za Mungu, ambazo tunaona ni uongo tu, na bado tunadunda tu?

Acha kufanya censorship.

Waachie watu waandike wanavyotaka.

Wewe pia unaruhusiwa kuandika unavyotaka hatujawahi kukuzuia kuanzisha au kupost mada zako.
Wewe jomba una busara ile laana.
 
Kwenye nyuzi zangu alijitokeza tokeza, "nikampasua kwa moto na nyundo ivunjayo miamba vipande vipande huyo shetani aliye nyuma yake." Amechukia sana mpaka ameamua kuniweka kwenye ignore list 🙂. Namuombea Mungu amhurumie na kumuokoa. Tumsamehe tu bure, hajui alitendalo. Hata sisi kabla Yesu hajatuokoa, tulikuwa kama yeye.

Na wewe tumia nyundo hii:
Yeremia 23:29 BHN
Neno langu ni kama moto; ni kama nyundo ipasuayo miamba vipandevipande.
Kuna wengi wamejificha kwenye kichaka cha kumwamini Mungu lakini umbea wao, ufiraji wao, umalaya wao........

Ogopa sana wale wasiochelewa kanisani wana balaa.
 
Lakini kwanini Mungu akuzwe kuliko uwezo wake?

Ni mwenye huruma lakini hatujawahi kuona akihurumia walemavu waliotapakaa dunia nzima, Amewapa ulemavu na pia wengi wao amewapa ufukara means huyo Mungu hana huruma.

Je, Ni wagonjwa wangapi wamefariki kwa kukosa pesa?

Je, Ni watoto wangapi wasiokuwa na hatia wamefariki katika vita?

Orodha ni ndefu na huenda huyo Mungu anakuzwa kuliko uwezo wake. Au anasikia ila uwezo wake ni mdogo.
 
Kwanza kabisa hakuna binadamu. Unless one of your ancestors aliitwa Adam.

Neno "binadamu" lina mzizi wa ki etimolojia wa "bin Adam", kusema kwamba watu wote ni uzao wa Adam.

Huyo Adam hakuna ushahidi kwamba alikuwapo. Wasomi wa Biblia ya kiyahudi (Old Testament) wanasema huyo Adam hakuwapo, hiyo ni hadithi yabkuelezea mabadiliko ya jamii ya Kiyahudi tu.

Kasome kitabu cha Dr. James Kugel aliyefundisha masomo ya Biblia mpaka Harvard kinaitwa "How To Read The Bible : A Guide To Scripture Then And Now". Professor Kugel kaandika vizuri sana kuhusu habari hii.

Sasa, unless baba yako au ancestor wako mmoja anaitwa Adam, na wewe ni bin Adam kwa maana ya kwamba ni mtoto wa huyo baba/ babu anayeitwa Adam, jina "binadamu" ni misnomer.

Pili, kwa kujibu swali la "watu walitoka wapi", naweza kuwa sina jibu kamili la watu walitoka wapi lakini nikajua kuwa hawakuumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote.

Swali la watu walitoka wapi ni kubwa, ni gumu, linahitaji maelezo mengi, maelezo ya kitaalamu, utaalamu ambao pengine sina, na hata ule ambao ninao mwingi una controversy, na mimi sipendi kujadili masuala argumentative ambayo siwezi kuyatatua kwa truth table.

Hapa kuna ujinga mwingi, kuna wajinga wengi, watu hawajui evolution tu ni nini, na mimi sina haja wala appetite ya kutoka kwenye reli ya mada yangu ya msingi.

Mada yangu ya msingi ni hii.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Swali la watu walitoka wapi si langu. Kwa sababu sijawahi kudai kuwa najua watu walitoka wapi. Hili ni swali la kila mtu.

Swali langu ni hili.

"Unasema Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo, unahakikishaje Mungu huyo si chanzo cha maisha ya watu?".

Swali hili ndilo langu. Kwa sababu linauliza kuhusu Mungu ambaye mimi nimesema hayupo.

Kama unaniuliza swali hilo, niko tayari kukujibu.

Lakini swali la mtu kaanza vipi naweza kukutafutia vitabu vya wanazuoni tusome wote tuelezane hapa aya kwa aya. Sitaki kukupa jibu kwa sababu hata mimi mwenyewe najaribu kujifunza zaidi kuhusu swali hili.

Lakini, kabla ya kujua jibu sahihi najua jibu si Mungu.

Umenielewa?
Umesema huna ufahamu kuhusu origin ya watu na viumbe wengine na bado unabisha kuhusu uwepo wa Mungu, kwa nini usiseme kwamba huna ufahamu pia kuhusu uwepo wa Mungu badala ya kuhitimisha kwamba Mungu hayupo? wee jamaa chenga sana.
 
Umesema huna ufahamu kuhusu origin ya watu na viumbe wengine na bado unabisha kuhusu uwepo wa Mungu, kwa nini usiseme kwamba huna ufahamu pia kuhusu uwepo wa Mungu badala ya kuhitimisha kwamba Mungu hayupo? wee jamaa chenga sana.
Unaniuliza uelewe au unanisimanga?

Naweza kusema Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo kwa sababu ya contradiction iliyopo katika Epicurean paradox.

Unaelewa Epicurean Paradox ni nini?

Kwani nikiulizwa hivi.

What is the square root of 4?

Nikaajua kuwa the square root of 4 must be less than 4.

Siwezi kujua kuwa 10 haiwezi kuwa square root of 4 kabla hata sijajua square root of 4 ni nini, kwa sababu 10 ni kubwa kuliko 4 na hivyo haiwezi kuwa square root ya 4?

Kwani siwezi kujua jibu hili si sahihi, wakati natafuta jibu sahihi, bila kujua jibu sahihi?

Mbona unafanya logical non sequitur fallacy?

Unaelewa ninachoandika au unaona kizunguzungu?
 
Unaniuliza uelewe au unanisimanga?

Naweza kusema Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote hayupo kwa sababu ya conyradiction ikiyopo katika Epicurean paradox.

Unaelewa Epicurean Paradox ni nini?

Kwani nikiulizwa hivi.

What is the square root of 4?

Nikaajua kuwa the square root of 4 must be less than 4.

Siwezi kujua kuwa 10 haiwezi kuwa square root of 4 kabla hata sijajua square root of 4 ni nini, kwa sababu 10 ni kubwa kuliko 4 na hivyo haiwezi kuwa square root ya 4?

Kwani siwezi kujua jibu hili si sahihi, wakati natafuta jibu sahihi, bila kujua jibu sahihi?

Mbona unafanya logical non sequitur fallacy?
Kama kujua origin ya watu kumekutoa jasho, nilitegemea uamini uwepo wa nguvu kubwa zaidi ambayo inaweza kuhusika na origin ya watu ambayo huijui, ambayo ndo tunaita Mungu......naona mdogo mdogo umeanza kuelewa.
 
Kama kujua origin ya watu kumekutoa jasho, nilitegemea uamini uwepo wa nguvu kubwa zaidi ambayo inaweza kuhusika na origin ya watu ambayo huijui, ambayo ndo tunaita Mungu......naona mdogo mdogo umeanza kuelewa.
Hapana,

Unachanganya mambo.

Inawezekana kujua origin ya watu kunanitoa jasho kwa sababu Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwapo, angempa kila mtu jibu la kila swali analolipata.

Angekuwapo, kwa sifa zake hizo, kusingekuwa na swali lolote ambalo watu wanajiuliza na kukosa jibu lake.

Nimekuuliza, unajua Epicurean Paradox ni nini?

Hujajibu.

Kwa nini hujajibu?
 
Sorry kwa kuwa nje ya Mada..huwa natamani siku moja nionane uso kwa uso na hawa watu
1.Nguruvi3
2.Kiranga
 
Back
Top Bottom