Kishindo cha BAVICHA chatikisa Kigoma, wawatembelea Wazazi wa Azory Gwanda

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ile Taasisi ya vijana inayoongoza kwa Ubora barani Africa , na ya tatu kwa ubora duniani , BAVICHA , Imekwishaingia Mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi ya Kusambaza moto wa Katiba mpya Mkoani humo .

Kabla ya kuanza operesheni ya KATIBA MPYA vijana hao wamefika kijiji cha MSIMBA kwa lengo la kuwasalimia na kuwajulia hali Bi Eva Mpurumba na Bw Obadia Gwanda ambao ni wazazi wa AZORY GWANDA aliyepotezwa nchini Tanzania tangu 2017 , Azory alikuwa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi aliyekuwa anafuatilia habari za mauaji ya Kibiti .

Kwa niaba ya Watanzania wazalendo nachukua nafasi hii kuipongeza BAVICHA kwa moyo wa kibinadamu na kuwaamua kuwatembelea wazee hawa ambao sasa umri umewatupa mkono sana .

Mungu ibariki Bavicha .



 
Bi. Eva Mpurumba, mama mzazi wa Azory Gwanda, akibubujikwa machozi baada ya kutembelewa na viongozi wa @bavicha_taifa leo Februari 03, 2022. Walienda kutoa pole ya kupotelewa na mtoto wao mwaka 2017. Bavicha wapo Kigoma katika n Operesheni #KatibaMpya Kanda ya Magharibi https://t.co/3Z0ZYgyWTu
 
Kama mlikuwa na misaada isinge ngojea siku hiyo mmewadhalilisha tu hao watu kwa mazingira ya picha!
 
Magufuli. Daaah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…