Uchaguzi 2020 Kishindo: Sheikh Ponda atoa neno kwenye mkutano wa Lissu Dodoma, Uwanja walipuka kwa shangwe


..Magufuli na ccm wamekuwa wanaitumia kamati ya amani ya viongozi wa dini kumshambulia Tundu Lissu na Cdm.

..kwa upande wangu naona ni jambo la kheri kwamba Sheikh Ponda amejitokeza kumpa " tafu " Tundu Lissu.

..tena natamani sasa wajitokeze na Maaskofu nao wajitokeze kumuunga mkono Lissu.
 
Ponda ameamua kushirikiana na damu ya kunguni Shauri yake
Mponda juzi tu katoka mahabusu, anajua machungu ya huu uongozi usimchukulie poa sana.

Ni mtu wa haki na atasimamia haki sikuzote.

Ww kaa kwa shemeji tu
 
Kwa akili yako fupi nilikuwa natokwa POVU lakini Kikwete alikuwa DHAIFU na historia itamuandika hivyo. Kikwete alifikia hadi kuambiwa na Kinana kwamba kuna Mawaziri mizigo awafute kazi. Kikwete alilidanganya Taifa kwamba pesa za Escrow si za Watanzania leo hii Ruge na yule baniani wako ndani mwaka wa nne. Na huyo DHAIFU yuko kimya kabisa. Cha kushangaza pesa zile za Watanzania walizifaidi wengi sana lakini huyo MNAFIKI waliokuwa ndani ya maccm na Serikali kaogopa kuwagusa.

Haihusu kitu Mkapa alitaka Tume huru lini lakini hakuogopa kuongea hadharani kuhusu umuhimu wa uwepo wa Tume huru. Hakuna hata mmoja ndani ya maccm alimpinga au kumuunga mkono kutokana na UNAFIKI wao mkubwa.

 
Labda waibe kama walivyozoea,ila NEC wakitenda haki Ccm kwisha.
CCM wataiba nini kwa Lissu wakati hana kura za kuibwa? Robo tatu ya wapiga kura ni CCM, kuna haja ya kuiba kura?
 
17 October 2020
Makao Makuu Dodoma
Tanzania

Mapokezi ya Tundu Lissu 17/10/2020 TunduLissu2020
Ripoti yawekwa hadharani baada ya miezi miwili ya kampeni za CHADEMA nchi nzima , na habari nzuri ni kuwa nchi ipo tayari kwa mabadiliko ya kumuondoa John Pombe Joseph Mafuguli na chama chake cha CCM 'Mpya' hapo 28 October 2020
 
Your browser is not able to display this video.

Mh. Tundu Antiphas Lissu, baraka za wapenda amani na haki unazo. Mwisho wa madikteta uchwara ni tarehe 28/10/2020!​
 
Sisi wanachadema wenye akili tunapinga kumtumia Ponda,maana ana asili ya ugaidi.
Eti sisi chedema, sema sisi sisiem tunaotumika kama ndomu. Unafikili kuweka profile ya bendera ndo kuwa chadema? Acha ufala wewe Lumumba waambie na wenzio.. wakusanye makopo yao zimebakia siku 10 tu watupishe Ikulu
 
Bila samahani Mkuu wewe si wa kutumia lugha hizi lakini bila ya shaka UMECHEFUKWA na wala si kulaumu Mkuu. Tuko pamoja.
..samahani sana mkuu.


..wakati mwingine uvumilivu unafika kikomo.
 
wasalimie ifakara usaliti unakutesa sana UMETUMIKA kazi kwisha....
Ivi ndo lijualikali uyu etii

Daaah kamanda kaza aisee kazi ni kazi ata kudeki ofsi ya chakubanga ni kazi pia.
 
Akae mbali na mbeligiji lissu, anadamu ya kunguni atamuingiza matatizoni ponda
Mponda juzi tu katoka mahabusu, anajua machungu ya huu uongozi usimchukulie poa sana.

Ni mtu wa haki na atasimamia haki sikuzote.

Ww kaa kwa shemeji tu
 
Huyu ndio amekuja kuharibu kabisa, maana huwa ana itikadi za kutokupenda amani ya nchi yetu, kwa ujumla Chadema tumebugi sana.
Kwanza ww hujawahi kuwa chadema pili wale mashehe ubwabwa wa bakwata kwa akili yako ndio wanahubiri amani?

Wale kutwa wanashinda ikulu tu kula tende na halua hamna kitu pale, wale ni ccm wenzenu.
 
Kawe Tanganyika Parkers patawaka moto, hapo ndipo Gwajiboy atakapoolewa na Halima Mdee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…