Uchaguzi 2020 Kishindo: Sheikh Ponda atoa neno kwenye mkutano wa Lissu Dodoma, Uwanja walipuka kwa shangwe

Uchaguzi 2020 Kishindo: Sheikh Ponda atoa neno kwenye mkutano wa Lissu Dodoma, Uwanja walipuka kwa shangwe

9 July 2020

HAPO AWALI KABISA MWEZI JULAI TAREHE 29 2020 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU, WAMUIBUA SHEIKH PONDA / ATOA WARAKA HUU MZITO / ATAJA SIFA ZA RAIS ANAYEPASWA KUCHAGULIWA



Waislamu Tanzania wataka uchaguzi huru na wa haki, wataja sifa za wagombea​

Jul 09, 2020 15:32 UTC
  • Waislamu Tanzania wataka uchaguzi huru na wa haki, wataja sifa za wagombea
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania ametoa mwito wa kufanyika uchaguzi huru na wa haki mwezi Oktoba mwaka huu nchini humo.

Sheikh Ponda Issa Ponda ametoa mwito huo leo Alkhamisi katika kikao na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kusisitiza kuwa, vyombo husika vinapaswa kuhakikisha kuwa uchaguzi huo mkuu unafanyika katika mazingira ya amani, uhuru na haki.

Kuhusu sifa za wagombea wa uchaguzi mkuu, Sheikh Ponda amesema waraka uliotolewa na taasisi hiyo imeorodhesha baadhi ya sifa hizo kama ifuatavyo: mgombea awe mkweli na mwenye utu, awe mwenye kuheshimu kiapo, awe mwenye sifa ya kupiga vita ubaguzi wa aina zote na awe mwenye maarifa ya kutosha ya kuongoza watu na serikali.

Sifa zingine zilizoainishwa kwenye waraka huo wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania ni mgombea awe mwenye kuheshimu uhuru na mawazo ya watu wengine, mbali na kuzijua na kuziheshimu haki za binadamu. Kadhalika taasisi hiyo ya Waislamu wa Tanzania imetaka wananchi wasiwachague watu madikteta na wadhalilishaji katika uchaguzi huo wa Oktoba 28, 2020.
 
"Tulitamani kuwa na Kiongozi kama Dr.Magufuli,Tumempata, tunaendelea nae.
KURA YANGU KWA MAGUFULI "

#TulipotokaTunapokwenda
#MagufuliNiMafanikio
#Magufuli5Tena
#ChaguaMagufuli #ChaguaMagufuli #ChaguaMagufuli
Ulitamani sio tulitamni,Mimi sikumtani.
Kura yangu kwa Lissu,Mke wangu ananibembeleza nisimsaliti kutokumchagua Lisu.
Kwa maana hiyo Nina uhakika kura yangu na mke wangu Ni kwa Lissu.
 
Ponda hanunuliki sio kama yule mamluki wa bakwata
Kuudanganya moyo ni kosa kubwa, kwani hata viongozi wa dini, nao ni binadamu kama sisi, wanauamuzi mioyoni mwao, nani wamshabikie na nani wasimshabikie, hivyo, Sena kwamba, inawapasa viongozi wote Wa dini hawapaswi kugawika kuhusu vyama, hawapaswi kuegemea chama chochote zaidi ya kuhubiri haki na amani pia kukemea inapobidi

Kwa sababu, dunuiani kila kitu kinawezekana, Watawala wa Dunia wote si wema, kwa kuwa huangalia mambo yao na si ya Mungu

Wachache mno wenye hofu ya Mungu, na huenda tokea utawala ule wa kifalme uliokuwa ukitumika Israeli uishe, tokea hapo, pengine hakujawahi kuwepo mtawala mwenye kutenda kwa hofu na kukubali kuongozwa na Mungu

Fikiri kwa kina, Embu kiongozi yeyote wa kidini, aegemee upande mmoja wa chama, halafu chama hicho kije kianguke kisishike dola, unadhani atakuwa na amani afanyapo kazi zake??

Kalaga bao....
 
Mungu mwongoze vema kiongozi wetu dini Sheikh Ponda, na ni muda muafaka sasa kwa viongozi wote wa dini kuja pamoja kwa ajili ya Tanzania mpya ya wote na kiongozi wetu ni Lissu
 
Na safari hii wakijaribu kuiba kura watakoma, Lissu hataki ujinga, wafadhili/mabeberu nao hawataki ujinga na wanaomuunga mkono wote nao hawataki ujinga, CCM itabidi wajue wataibaje hizo kura kwa akili vinginevyo kazi wanayo.
Tusijipe moyo kamanda,Chadema haikubaliki kama zamani, hakuna wizi wa kura, tuwe wapole makamanda.
 
Tusije moyo kamanda,Chadema haikubaliki kama zamani,hakuna wizi wa kura,tuwe wapole makamanda.
Kama haki zingine za kawaida tu inashindikana kuona zinaheshimiwa , kweli kunyimwa ugali , mtakubali bila kusimamiwa kwa bakora.
 
Haki tunazotaka waislamu hazpo Kwenye hizi siasa.

Huyo shkh ni shehena,mchumia tumbo asie jua kutofautisha tui na maziwa, tena Ponda ni mjinga asiejitambua Allah amuongoze
Sasa Kama hata wenzake mnawanyima haki za msingi asiwaambie.
 
Back
Top Bottom