KISUTU: Jamhuri kuleta mashahidi 24, vielelezo 19 kesi ya Mbowe na wenzake

KISUTU: Jamhuri kuleta mashahidi 24, vielelezo 19 kesi ya Mbowe na wenzake

Kufadhili ugaidi kwa 600,000?
Au kafadhili udokozi?
Kuna kesi ya ugaidi kweli hapa?
 
Mbowe akishinda hii kesi itakuwa ni aibu kubwa sana na anguko kubwa la kisiasa kwa Madam SSH.

Binafsi sina chama na sipendi vurugu za kisiasa lakini naomba sana Mbowe ashinde.

Msiniulize sababu.
Em soma tena jina lako..
 
Sabaya mlifurahia alivyopewa kesi ya uporaji wa laki tatu ila Mbowe kufadhili laki sita ila magaidi wakachome vituo vya mafuta ni ajabu.
 
Mama anaupiga mwingi Sana.... Hii nchi Bana, serekasi hazitaishaga mpk CCM imezikwa kaburi la sahau
 
Sabaya mlifurahia alivyopewa kesi ya uporaji wa laki tatu ila Mbowe kufadhili laki sita ila magaidi wakachome vituo vya mafuta ni ajabu.
Unaweza kupora elfu tano lakini huwezi kufadhili UGAIDI kwa elfu tano. Elewa uzito wa jambo katika kutendwa! Sabaya anaweza weka watu chini ya ulinzi na akawasachi na kuchukua mali /pesa.

Ndiyo maana Serikali imeweka ujanja ujanja kwamba mashtaka ya UHUJUMU UCHUMI yenye UGAIDI ndani yake!
 
Unaweza kupora elfu tano lakini huwezi kufadhili UGAIDI kwa elfu tano. Elewa uzito wa jambo katika kutendwa! Sabaya anaweza weka watu chini ya ulinzi na akawasachi na kuchukua mali /pesa.

Ndiyo maana Serikali imeweka ujanja ujanja kwamba mashtaka ya UHUJUMU UCHUMI yenye UGAIDI ndani yake!
Tunayo haki ya kusema sema na kuandika andika chochote on this issue lakini uamuzi wa mwisho ni wa Mahakama jamani. Tuwe wavumilivu kwa hili ili tuvuke nalo tukiwa kitu kimoja!
 
Tunayo haki ya kusema sema na kuandika andika chochote on this issue lakini uamuzi wa mwisho ni wa Mahakama jamani. Tuwe wavumilivu kwa hili ili tuvuke nalo tukiwa kitu kimoja!
Tunaelewa uamuzi ni wa Mahakama ila haituzii kujadili, kuchokonoa na kuja na nadhalia.
 
Dar es Salaam.

Mashahidi 24 na vielelezo 19, wanatarajia kutoa ushahidi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu.

Miongoni mwa mashahidi hao, yupo aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Boaz.

Hayo yameelezwa leo, Agosti 23, 2021 na upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga akisaidiana na Ester Martin, wakati wakiwasomea maelezo ya mashaidi na vielelezo (Commital Proceedings) washtakiwa hao, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba.
 
Safi kabisa. Moyoni mwake anajua ukweli wote juu ya vitendo hivyo vya ugaidi. Mbowe ni mtu hatari sana siyo tu kwa taifa lakini hata kwa Chadema. Polisi waimarishe ulinzi Nguvu ya Chadema imekwisha mahakamani na imekwisha Twitter Republic. Sasa mahakama ifanye kazi yake kwa utulivu na mambo yote yawekwe wazi. Mbowe si malaika.
600,000 Tzs kufadhili ugaidi sio Jambo dogo, kumbe ugaidi sio garama
 
Tunaelewa uamuzi ni wa Mahakama ila haituzii kujadili, kuchokonoa na kuja na nadhalia.
Elewa nilicho sema! Sijasema "msiandike au msijadili" nilichosema ni kuwa tunaweza "kuandika andika na kusema sema" chochote! Sijazuia watu kusema jamani! Ninyi semeni semeni na adikeni andikeni chochote ILA uamuzi wa mwisho ni wa Mahakama! Huo ni msisitizo tu na hicho ndicho nilicho sema.
 
Elewa nilicho sema! Sijasema "msiandike au msijadili" nilichosema ni kuwa tunaweza "kuandika andika na kusema sema" chochote! Sijazuia watu kusema jamani! Ninyi semeni semeni na adikeni andikeni chochote ILA uamuzi wa mwisho ni wa Mahakama! Huo ni msisitizo tu na hicho ndicho nilicho sema.
Asante kwa kunielewa Kayamba Moses. Tuko pamoja.
 
Mwenyekiti wa chama taifa Mhe. Freeman Mbowe amewasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo leo Agosti 23, 2021 kesi Na.63/2020 ya Uhujumu Uchumi yenye mashtaka ya Ugaidi ndani yake itaanza kusomwa kwa hati ya mashtaka na ushahidi kwa hatua ya awali.

UPDATE: Mashtaka
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam wamesomewa maelezo ya mashtaka mbalimbali yanayowakabili ikiwemo la kutaka kudhuru viongozi wa Serikali akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.


Upande wa mashitaka unasoma mashitaka kwa kusema kuwa; Halfan Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa, Mohamed Abdallah Ling'wenya na Mhe. Freeman Mbowe wanatuhumiwa;

1. Freeman Mbowe anatuhumiwa kufadhili vitendo vya Ugaidi kwa kutoa shilingi za kitanzania laki sita ( 600,000).

2. Kula njama na kusabisha majeraha kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya

3. Watuhumiwa wote ambapo wanatuhumiwa kushiriki vikao na Kula Njama za kutenda Ugaidi

4. Mshtakiwa wa pili anashitakiwa kumiliki bastola yenye risasi tatu kwa ajili ya kutenda kosa la ugaidi.

5. Mshtakiwa wa tatu anatuhumiwa kumiliki nguo, begi na koti za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWT) na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT.)

-
UPDATE: Mashahidi 24 vielelezo 19 kesi ya Mbowe na wenzake

Mashahidi 24 na vielelezo 19, wanatarajia kutoa ushahidi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu.

Miongoni mwa mashahidi hao, yupo aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Boaz.

Hayo yameelezwa leo, Agosti 23, 2021 na upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga akisaidiana na Ester Martin, wakati wakiwasomea maelezo ya mashaidi na vielelezo (Commital Proceedings) washtakiwa hao, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba.

Credit: Mwananchi
Eee Mola; mlinde Freeman.
 
niwaoga hao acha kabisa lakini ni mashujaa kwenye simu hao hata wakimuona mende wanakimbia
Poleni, Nimepiga magoti nikiwaombea ili shetani akiishamalizana nanyi, mtubu na kurudi kwa Mungu. Sisi pia tutawapokea.
 
Kiongozi wa chadema ( Chama cha democrasia na maendeelo) FREEMAN MBOWE . Amesomewa mashtaka yake leo.

Chakushangaza charge sheet inasema bwana mbowe anatuhumiwa kufadhili u
UGAIDI kwa kiasi cha shi $ 297 ( kama Tsh 600,000)

Je UGAIDI UPI unafadhiliwa kwa kiasi hicho cha fedha?


Its crazy that @freemanmbowetz is charged with terrorism by 'funding' US Dollar 297.54 sponsoring terrorists. What kind of terrorism can $297 do?
#hisisnotaterrorist


Uzi tayari.
 
KAMANDA_WOTE_MASHUJAA,_WAPENDA_HAKI,_WAFIA_CHAMA__tukutane_KIsutu_leo_mapema_kwenye_kesi_ya_mw...jpg


Gharama ya Ugaidi wa Mbowe imenifanya nishangae mno na wakati huo huo niogope , ikiwa kama mtu anaweza kutumia pesa ndogo kiasi hicho kufanya ugaidi basi dunia iko matatani hasa ! badala ya kusikitika nimejikuta nacheka !

Nadhani kuna haja ya watunga kesi kujiongeza ili angalau dunia iwaamini hata kidogo basi , kiwango cha uongo walioweka humu ni duni mno !
 
Mwenyekiti wa chama taifa Mhe. Freeman Mbowe amewasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo leo Agosti 23, 2021 kesi Na.63/2020 ya Uhujumu Uchumi yenye mashtaka ya Ugaidi ndani yake itaanza kusomwa kwa hati ya mashtaka na ushahidi kwa hatua ya awali.

UPDATE: Mashtaka
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam wamesomewa maelezo ya mashtaka mbalimbali yanayowakabili ikiwemo la kutaka kudhuru viongozi wa Serikali akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.


Upande wa mashitaka unasoma mashitaka kwa kusema kuwa; Halfan Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa, Mohamed Abdallah Ling'wenya na Mhe. Freeman Mbowe wanatuhumiwa;

1. Freeman Mbowe anatuhumiwa kufadhili vitendo vya Ugaidi kwa kutoa shilingi za kitanzania laki sita ( 600,000).

2. Kula njama na kusabisha majeraha kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya

3. Watuhumiwa wote ambapo wanatuhumiwa kushiriki vikao na Kula Njama za kutenda Ugaidi

4. Mshtakiwa wa pili anashitakiwa kumiliki bastola yenye risasi tatu kwa ajili ya kutenda kosa la ugaidi.

5. Mshtakiwa wa tatu anatuhumiwa kumiliki nguo, begi na koti za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWT) na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT.)

-
UPDATE: Mashahidi 24 vielelezo 19 kesi ya Mbowe na wenzake

Mashahidi 24 na vielelezo 19, wanatarajia kutoa ushahidi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu.

Miongoni mwa mashahidi hao, yupo aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Boaz.

Hayo yameelezwa leo, Agosti 23, 2021 na upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga akisaidiana na Ester Martin, wakati wakiwasomea maelezo ya mashaidi na vielelezo (Commital Proceedings) washtakiwa hao, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba.

Credit: Mwananchi
Yaani Laki 6 ndiyo inafadhiri mauaji ya Sabaya.

Na huo mpango wa kuuwa viongozi unamuhusu kiongozi moja tu, Sabaya ambaye naye anatuhumiwa kwa makosa yanayofanana na ya mtuhumiwa. I can smell fishy.....!!

Anyway, makosa yote yaliyoorodhehwa yako very diluted tofauti na ukubwa wa hiyo kesi yenyewe.
 
Back
Top Bottom