Kitendo cha kuwakatalia Wakurugenzi wa Kenya na kuruhusu wengine ni ubaguzi

Kitendo cha kuwakatalia Wakurugenzi wa Kenya na kuruhusu wengine ni ubaguzi

Wao wanatusakama kila wakati hamsemi wao kubanwa kidogo midomo juu
 
AMKENI AMKENI AMKENI📢📢📢📢📢📢📢

RIPOTI YA UFISADI NA UTOROSHWAJI MKUBWA WA FEDHA NA FEDHA HIZO KUFICHWA HUKO UGHAIBUNI KUNAKODAIWA KUMILIKIWA NA WANASIASA WA NCHINI KENYA.

Wanasiasa wa KENYA wametajwa kutorosha KILAGHAI na kuficha zaidi ya DOLA BILIONI 300 huko ULAYA kwa miaka 20 iliyopita.

👆👆👆

Hilo LINASADIFU yale maneno aliyosema mh.Uhuru Kenyatta kuwa "NDUGU ZANGU WAKENYA MMEZIDI KWA WIZI UBADHIRIFU KUTOAMINIKA ULAGHAI NA JINAI ZA HOVYOHOVYO"🤣🤣

Huwa siwashangai WAKENYA wengi WA KAWAIDA kumpenda MAGUFULI.

Huwa simshangai Prof.Lumumba kumpenda sana MAGUFULI.


Tanzania yangu NINAKUPENDA
Wewe Tanzania utaendelea kuwa BORA zaidi ya WENGI WAKUZUNGUKAO leo kesho na hata milele,aaamin aaamin.




MAENDELEO HAYANA VYAMA.
 
Una maana gani? Una maana wakenya ni bora kuliko wamisri? Una maana ni lazima wakenya wawe considered kwanza kabla ya watu wa mataifa mengine? Una maana hatuna uhuru wa kumpa mtu mwingine kabla ya wakenya? Huu ni ujinga wa aina fulani. Tanzania is a sovereign state.
Kuna wakati mtu una kasirika kwa sababu tu mchangiaji wa mada iliyomezani anajifanya hamnazo kwa makusudi
Mimi nimemuelewa vema mleta mada kuwa kama tunaamua kuwakataa wageni kufanya kazi Fulani kazi hizo wapewe wazawa
Kwa mantiki yake ukienda mbali ni kuwa Kenya na Misri Kenya ni jirani yetu na mwanajumuia mwenzetu wa EAC na kwa vyovyote vile na haki kuliko mmisri vinginevyo kuwe na kitokuelewa.
 
Tatizo wakenya mwanzo walikua wanajiona superior..


#Mkuki_kwa_ngurue...
Asaiv wao wanajiona watakuq inferior mbaka mnaanza kuwaombea #pooo!!
 
Na Mwandishi wetu.

Mkurugenzi mtendaji wa Coca-Cola kwanza ndugu. Andrew Musingo aliyeteuliwa na wamiliki wa kampuni ya Coca-Cola kwanza ambao ni Coca-Cola beverages Africa kutoka nchini Afrika ya Kusini amenyimwa kibali na mamlaka ya nchi ya Tanzania kwa kile wasemacho kuwa watanzania wanauwezo wa kufanya hivyo.

Katika mazingira ya mwendelezo wa ushindani wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania na kenya kwa mara nyingine kiongozi mkuu wa taasisi binafsi kutoka nchi ya kenya anakataliwa kibali cha kufanya kazi katika taifa la Tanzania baada wa yule wa VODACOM (sylivia Mulinge) kukataliwa kutokana na sababu ambazo mamlaka imeziweka kwa ufupi kama watanzania wanauwezo wa kufanya kazi hizo.

Imeelezwa na mwandishi wetu kuwa miezi kadhaa nyuma kampuni ya cocacola beverages Afrika ilimtanganaza Andrew Musingo raia wa kenya kama mkurugenzi mpya wa kampuni yao kwa tawi la Tanzania ifahamikayo kama Coca-Cola Kwanza. Hii ni baaada ya raia wa Afrika kusini Ndugu Basil Gadzios kumaliza muda wake nchini Tanzania na kuhamia Zambia kwa majukumu mengine.

Kwa maelezo ya watu wa ndani baada ya kutangazwa, kumekuwa na maombi ya vibali vya kufanya kazi nchini yaliotumwa na kampuni hiyo kwa wizara na Zaidi ya mara 4 wizara imekataa maombi hayo na kusema haiwezi kumpa kibali kwani watanzania wanaweza kufanya kazi hizo.

Tangu kunyimwa kwake vibali vya kufanya kazi katika taifa la Tanzania amekuwa akija kwa visa ya kibiashara na kufanya kazi kwa muda mfupi mpaka pale mamlaka ya uhamiaji ilipofika na kumkamata kwenye ofisi na kumtoa kwa nguvu na kumrudisha kenya.

Mnamo tarehe 23/11/2020 akitokea Nairobi kenya na shirika la ndege la Kenya Airways Mkurugenzi mpya wa Coca-Cola kwanza Andrew Musingo amekataliwa na mamlaka uhamiaji ya Tanzania kuingia nchini kutekeleza majuku yake mapya kwa maelezo kuwa anapaswa kupata kibali cha kufanya kazi nchini ndipo aweze kuja nchi, hivyo Raia huyo wa kenya amelazimika kuondoka tena nchini kurudi kwako kutokana na kukataliwa kuingia taifa la Tanzania.
 
Kwani nyinyi wakenya ni lazima muajiriwe bongo?
 
Wakenya wanasahau kauli za mbunge Jaguar? Kuchukuliwa vibarua tu wakataka kufukuza watanzania na ule sio msimamo wa Jaguar kama walivyosema ni mawazo ya serikali yao na ndio mawazo ya wakenya wote

Lakini wao kukataliwa nafasi mbili tu wanalalamika
Wanajihesabia haki kupewa fursa huku sio sisi kupewa fursa kwao

Hawa huwa wanatuona wa hovyo
 
Nikiangalia Marekani walivo na diversity ya watu jinsi nchi yao ilivoendelea nabaki nasikitika tu
 
Waende na viwandani
Kuna wahindi weng wameshikilia nafasi ambazo watanzania wanaweza fanyia kazi
Waende na Pepsi kuna wahindi ndio mabosi wahindi wenyewe vilaza tu tenda zote wanwapa wahindi wenzao
 
na kweli watanzania wanaweza kufanya shughuli hii!
 
Lakini Kuna viwanda vingine na tasisi zingine wamejaza wabongo tu kwa kuwekana tu , ambao hawana uwezo wa kufanya izo kazi.
 
Back
Top Bottom