Kitendo cha Rais kusimamisha hotuba kisa Adhana ya waislam imakaaje hii kitaifa?

Kitendo cha Rais kusimamisha hotuba kisa Adhana ya waislam imakaaje hii kitaifa?

R. I. P Jamiiforums servers...

Keyboard warriors wanaandika tu bila thinking.
 
Leo tarehe 1/5/2022 Rais akiwa anawahutubia wafanyakazi Dodoma katika siku muhimu ya wafanyakazi duniani, ilitokea kusitishwa hotuba Kwa dk kama 3 na Rais pale Adhana ya mchana ilipokuwa ikisika kutokea msikitini karibu na uwanja wa Dodoma.

Hivi wadau wa utaifa hili lilipaswa kufanywa na Rais kiongozi mkuu wa Serikali ambaye tuna amini anaongoza SERIKALI ISIYO NA DINI?

Wananchi wakristo inabidi tuendelee kuvumilia tu kama msingi wa dini yetu.
Wacha uzombie wewe! Usiingize udini hapo, hizo ndizo taratibu na zipo enzi na enzi!
 
Mleta mada ALIDHANI angefanikiwa KUZUA TAHARUKI! [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwani mkuu na wewe kafiri una kitu cha kuheshimu katika imani yako?
 
Jambo la kiungwana sana hili

Nakumbuka hata uhuru kenyatta pia alifanya hivyo pale dodoma
Na uwanja ulikuwa ni huo huo wa Jamhuri wakati adhana ilipoungurumishwa ndani ya msikiti wa Ghadafi siku viongozi wanatoa heshima za mwisho kwa hayati JPM.
 
Mtoa mada pokea mikuki, ulialika mwenyewe. Wafia dini wenzako naona wamemute kimya kuna masuapa mengine sio ya kuhoji mkuu.
 
Tambua tu kunakuwa na mwingiliano wa sauti, hivyo anapaswa asubiri jambo la adhana lipite ili aweze endelea na kusikika vyema!
 
Leo tarehe 1/5/2022 Rais akiwa anawahutubia wafanyakazi Dodoma katika siku muhimu ya wafanyakazi duniani, ilitokea kusitishwa hotuba Kwa dk kama 3 na Rais pale Adhana ya mchana ilipokuwa ikisika kutokea msikitini karibu na uwanja wa Dodoma.

Hivi wadau wa utaifa hili lilipaswa kufanywa na Rais kiongozi mkuu wa Serikali ambaye tuna amini anaongoza SERIKALI ISIYO NA DINI?

Wananchi wakristo inabidi tuendelee kuvumilia tu kama msingi wa dini yetu.
Hii Jamii Forums very soon itakufa kwani kuna hoja zingine za kijinga sana na chuki hata za kidini zinaruhusiwa kuletwa humu. Hii hatuwezi kuita ni uhuru wa kutoa maoni bali tutaita uhuru wa kuonyesha tunawanachama wangapi wana IQ 0 kwenye kichwa
 
Mtoa Hoja ni mtu mwenye akili ndogo na isiyoona mbali. Asubiri na Waislamu walalamike kwamba nchi hii ilitawaliwa na Wakiristu na hadi leo inaendeshwa Kikristu.

Waislamu watadai siku ya Mapumziko kwao iwe Ijumaa, Wasabato Jumamosi na Wakiristu Jumapili. Waislamu pia watadai Fidia kwa uonevu na ukandamizaji wote waliopata kuanzia Wamisinari kuja na kutawala Kikiristu hadi kuondoka.

Hapa ndiyo suala la Udini litakapoeleweka vizuri
Nyinyi wazee wa Madrasa! Endeleeni kuvaa madera tu! Ulishawahi kukuta darasa la chup huku Tanzania bara wana funzi wengi ni waislam? Nitajie chup hata kama kiko huku pwani!? Mnapoteza mda kusoma hadithi badala ya kufanya vitu vya msingi!
 
Leo tarehe 1/5/2022 Rais akiwa anawahutubia wafanyakazi Dodoma katika siku muhimu ya wafanyakazi duniani, ilitokea kusitishwa hotuba Kwa dk kama 3 na Rais pale Adhana ya mchana ilipokuwa ikisika kutokea msikitini karibu na uwanja wa Dodoma.

Hivi wadau wa utaifa hili lilipaswa kufanywa na Rais kiongozi mkuu wa Serikali ambaye tuna amini anaongoza SERIKALI ISIYO NA DINI?

Wananchi wakristo inabidi tuendelee kuvumilia tu kama msingi wa dini yetu.
Jana hata nilikuwa Rufiji ndani huko kwenye mbio za mwenge wa Uhuru, Kuna Adhana ilipigwa mida ya saa kumi kasoro hivi mkimbiza mwengi akiwa anahutubia akasimama kuhutubia kisha akaendelea baada ya kumaliza Adhana, sikuona kama watu walikereka.

Lakini kama hasingefanya hivyo kwa kuwa wote wanatumia vipaza sauti kungekuwa na mwingiliano wa sauti (chaos) na kupelekea upande mmoja kutoelewa. Kwa hiyo mtoa mada kama si kuwa na emotions angefikiria kwanza ili asingepata taabu.
 
Huyu mzee kaanza mambo yake
Babu...
Huwa mara nyingi nasoma huu utambulisho wangu wa ''mzee.''
Hakika mimi ni mzee.

Mwezi Februari nimefikisha miaka 70.

Lakini hapa hoja si umri wangu.

Kunitambulisha kwa ,''Huyu mzee,'' wewe unadhani unanikebehi na kunifanyia kejeli.

Mimi sihamaki kwa kuitwa mzee.

Nikifanya hivyo nitakuwa mpuuzi kwani kuishi hadi unafikia uzeeni ni jambo la kushukuru vinginevyo Allah angenichukua kijana na nisingefika umri huu wa uzee.

Nilikuwa kijana na kijana khasa.

Alhamdulilah pengine wewe hujapitia hata kwa mbali ujana niliopitia mimi.

Tuje sasa kwenye maudhui.

Nimeeleza kuwa huu Uislam unaokughadhibisha wewe hii leo kwa kusikia Adhana ndiyo ilikuwa silaha iliyomtoa mkoloni Tanganyika.

Ilikuwa kila tatizo lililokumba harakati za kudai uhuru TANU ilikuwa ikirejea kwa Allah kutafuta msaada.

Nyerere kafariki akilijua hili na akishiriki kwa kila dua iliyofanywa.

Kuna dua aliyofanyiwa Rashid Ali Meli 1955.

Rashid Ali Meli alitoa fedha za Dar es Salaam Municipal Council (DMC) kuwakopesha TANU ili Nyerere awahi safari ya kwanza UNO 1955.

Rashid Ali Meli alikuwa Bwana Fedha wa DMC.

Historia ya Ali Meli iko hapa JF fanya search utaiona.

Kuna dua aliyofanyiwa Abdul Sykes 1955.

Abdul Sykes alishutumiwa kwa kutumia ofisi yake ya Market Master Kariakoo Market kuuza kadi za TANU.

Kisa hiki kipo hapa JF fanya search.

Kuna dua alifanyiwa Nyerere Lindi na Sheikh Yusuf Badi 1956.

Kisa kipo hapa kitafute.

Kuna dua aliyofanyiwa Nyerere Mnyanjani, Tanga 1958.

TANU ilikuwa imezongwa na tatizo la Kura Tatu.

Kisa kipo hapa JF.

Yote haya yakifanywa na Waislam ndani ya TANU na Wakristo hawakulalamika kwa nini Waislam wanamtukuza Mungu katika kutafuta uhuru?

Haya ndiyo mimi nakuomba utoe majibu.

Haya ndiyo mapenzi yaliyokuwapo nchini petu.

Tusiuvuruge udugu huu kwa chokochoko.

Historia hii ingesomeshwa na ikafahamika watu kama wewe wangeelimika.

1651465680127.png

Mtaa wa Muhammad Yusuf Badi Lindi
 
Back
Top Bottom