Kudai Israeli ni Taifa la Mungu huku Wayahudi wakimkaata Yesu, ni ushahidi hizi dini zimejaa uongo mwingi

hilo ni swala la uelewa tu,si kila mkristo ana uelewa mdogo kama wake.
sisi wakristo wengine tunajua kabisa kwamba Yesu aliondoa kabisa huo uteule wa israel baada ya kumkataa,na akaawahidi kuwakabidhi urithi huo watu wengine wa ulimwengu.
 
Kwa hiyo Ukristo ni Jina la hiyo Imani!
Katika rank za viumbe wa mungu aliwatumia duniani kufikisha ujumbe kuna mitume,manabii na masihi(kristo). Yesu aliwaambia watu yeye sio mtume kama mitume waliotangulia kabla yake na wala sio nabii kama waliokuwepo kabla yake,bali yeye ni kristo yaani masihi yaani hakuwepo mwingne kabla yake na hatafika mwingne baada ya yeye.
Mungu aliupenda ulimwengu hadi akamtoa mwanae wa pekee. Yesu ni wa pekee kwakuwa ni kristo i.e masihi. Mitume na manabii ni watu miongoni mwetu na wanachaguliwa na mungu ili kuifanya kazi yake. Maseh i.e kristo ni daraja la juu baada ya malaika. 1 angels 2 maseh 3 messangers 4 apostle 5 believers(ndo sisi duniani hapa). Na wewe mkorinto umenielewa ninaposema kristo ni jina?
 
Israle ni taifa teule, maandiko hayajadanganya, ndio maana limebarikiwa kwenye kila nyanja, wapo mbele kwa vingi, hii sio bahati mbaya, Mungu aliweka kitu maalum kwenye vichwa vya wale jamaa, hili sina shaka nalo.
 
Fix
 

Steven,

Rudi shuleni tena kusoma Historia......Inaonekana ni kipofu na maamuma kabisa na historia ya Middle East.....Hujui hata Zionism ni nini....Labda soma maandishi ya msingi ya akina Theodor Herzl na wenzie ndio utajua maana ya Zionism.

Kama unasema hawa Wayahudi ni Wayahudi Wakwavi......Vipi Kuhusu Wapalesina Hujui hata Waarabu wenzao wanaona ni Waarabu koko tu.....Ndio Maana Jordan iliwafukuza....Egpty inashindwa kabisa kutaka waingie kwao...Hakuna nchi ya Waarabu kiundani inawakubali 100% .Kinachowaunganisha ni imani ya Kiislamu, hasa Uadui wa Uislamu ambao una mizizi ndani ya Quuran na lugha tu Hakuna kingine! .....Hebu tueleze taifa la Wapelestine limewahi kuwepo lini? Nani amewahi kuwa kiongozi wa taifa hilo kihistoria....maybe urudi hadi 1948.....Liko kinadharia tu.....Jiulize Yasser Arafat alianzisha PLO lini.....na maisha yake mengi kaishi Tunisia na alizaliwa Egpty..nadhani alirudi Gaza 1994! Hata kufia amefia France......ambako alikuwa anaishi muda mwingi......na akiwa na pesa kama $1 to 3 Billion kwenye accounts zake alizozichota kwa kuwazuga Waarabu na Western World anapigania taifa ambalo liko kwenye makabrasha.....!

Na unajua ushenzi wa Hamas wewe? Sisemi Ushenzi wa Hamas dhidi ya Wayahudi, bali ushenzi wa Hamas dhidi ya Wapelestine wenzao....! Unajua utajiri wa akina Ismael Haniyeh, Mousa Abu Marzuk na Khaleed Mashal....Hawa ni viongozi wa Hamas na Hawakai Gaza......Utajiri wao unakadiriwa ni $ 11 Billion.....Wanatumbua Qatar.....Pesa ikipelekwa Gaza ni kuchimba Mahandaki......na wakianzisha Uchokozi dhidi ya Israel, wakipigwa kidogo pesa zinamiminika mifukoni mwao toka Iran na Warabu wenye mrengo wa Jihad, na Humanitarian organizations.......Gaza ingelikuwa Singapore kama sio ushenzi wa viongozi wa Palestine kwa wenzao.....Huu ni mradi......Tafakari kidogo kabla kuandika, usijiingize kwenye bandwagon ya watu wengi ambao wamekuwa brainwashed.....
 
Sasa wewe inakuhusu nini? Fanya yako kwenye dini yako muache mtu aamini anachokiamini

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
Wazungu wenyewe waliotuletea Ukristo, hata makanisani hawaendi na Wayahudi alikozaliwa Yesu, nao wamekataa kumpokea Yesu kama mwana wa Mungu. Je, mpaka hapa huoni kuna shida tena kubwa tu??
 

Mkuu ukristo uislam na dini nyingine uijuayo, ni ngonjera ya kulainisha watu ili watawaliwe vizuri.

Imani ya kweli ni inayozingatia misingi ifuataayo:

1. Kuipenda, kuitunza na kuilinda familia yako vizuri.

2. Kuwaheshimu, kuwapenda na kuwaenzi wazazi wako pamoja na wakubwa wenzao.

3. Kutenda wema kwa binadamu wenzako bila kujali jinsia, rika, umri, rangi, tamaduni, imani, mazingira au kipato!

4. Kuzingatia, kuenzi, kusimamia na kulinda misingi, taratibu, miongozo, mila, desturi, kanuni, sheria na tamaduni za jamii yako.

Waisrael sio taifa la Mungu, kwa sababu tulitegemea tuone special treatment ya kutoka kwa Mungu tofauti na jamii zingine.

1. Je wanavuta hewa tofauti na wengine?

2. Je hawaishi kwa chakula kama wengine.

3. Je hawazaliwi, kukua na kuzeeka kama wengi?

4. Je hawafi kama wengine?

5. Je hawajishughulishi kuishi kama wengine.

6. Je hawajitawali kama wengine?

7. Je wanakutana na huyo Mungu wao ana kwa ana, bila kutumia maandishi ya historia?

8. Je huyo Mungu wao anawaondelea changamoto, shida, matatizo yao mubashara tofauti na wengine?

9. Je walivyo kuwa wanauawa kipindi cha Hitler huyo Mungu wao hakuona, ashughulike na Hitler.

10. Je bila msaada wa Marekani na ulaya wanaweza kuzichapa na majirani kwa nguvu ya Mungu wao wakashinda?

11. Huyo Mungu kwa nini asiwanyakue na kuwa peleka kwenye ardhi isiyo na ukame, mawe, vita na majirani Visiwani?

12. Huyo Mungu wao kwanini asiwabadilishe majirani zao wapalestina au kuwa ondoa kabisa?

Mkuu nikijibiwa maswali hayo, bila ngonjera na maneno mengi nitaamini kweli hawa jamaa ni wateule au watu wa Mungu!
 
Israle ni taifa teule, maandiko hayajadanganya, ndio maana limebarikiwa kwenye kila nyanja, wapo mbele kwa vingi, hii sio bahati mbaya, Mungu aliweka kitu maalum kwenye vichwa vya wale jamaa, hili sina shaka nalo.
Wamebarikiwa halafu wanaishi katika vita isiyoisha?!
 
Enyi mlioamini! Msiwafanye mayahudi na wakirsto kuwa marafiki – wao kwa wao ni marafiki – na yeyote atakayewafanya marafiki basi yeye ni katika wao. Hakika Allaah haongoi watu madhalimu.” (05:51)
 
Wakristo wanao sema israel bado ni tsifa la mungu akili hawana yesu mwenyewe anasema na kuililia Israel...anasema nyumba yako imeachwa ukiwa maana yake yale ya kusema ni tsifa la mungu kwisha habali yake
 
Una maswali fikirishi na magumu

Unachotakiwa ni kuamini tu Israel ni Taifa teule bila kijali kuwa sio wakristo na hawamkubali Yesu
Mkuu hapo kwenye 'kuamini' ndipo penye mushkeli! Hapo ndipo unapo muingiza mwenzio kwenye chaka na tope ulilozama wewe!
 
Imani inafanya watu wasihoji, na ndio maana hata Wafuasi wa Kibwetere hawakuhoji matokeo yake wakaangamia.

Imani ni kutokuhoji kile ambacho kinapaswa kuhojiwa.

Kitendo Cha Kumfanya mtu mzima mwenye midevu yake na uwezo mkubwa wa kureason kushindwa kuhoji Yale ambayo yanapaswa kuhojiwa ni ujuha wa kiwango Cha PhD.

Waafrika wako shimoni, wataandelea tu kuhangaika na kuomba omba misaada kutoka kwenye hizi agency za kidini za Western na mashariki ya kati kwa sababu ya ujinga uliotukuka walionao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…